Vawulence
JF-Expert Member
- Jan 4, 2009
- 1,928
- 2,101
Imekuwa ni kawaida kwa makampuni mbalimbali ya simu kujinadi kuwa wao peke ndio waliofika kila kona ya nchi. Nilifunga safari ya kwenda Semunge kwa babu ila katika siku 3 nilizoishi kule sikufanikiwa kupata mawasiliano ya mtandao wowote ule. Hii ni sehemu moja tu kati ya nyingi tusizozifahamu kuwa na shida ya namna hii. Kujinadi ni jambo moja ila kujinadi kitapeli ni jambo lingine. Hakuna jinsi yoyote ile ya kujinadi bila kudanganya wajeja wenu? Uongo wenu unatugharimu sana kwani unatukwamisha mambo mengi ya msingi. Kuna mambo mengi ya kitapeli kama vile makato ya muda wa maongezi yasiyoeleweka bila maelezo.