Makampuni barani Afrika yatumie CIIE kufungua soko la China kwa ajili ya bidhaa zao

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
Na Caroline Nassoro

Maonyesho ya 4 ya Kimataifa ya Uagizaji Bidhaa Nje ya China (CIIE) yamefunguliwa rasmi Novemba 5, 2021. Ikiwa ni awamu ya nne, Maonyesho haya yameendelea kuandaliwa kwa ufanisi zaidi, kitaalamu zaidi, na pia kwa njia ya kidijitali zaidi.

Maonyesho haya yamevutia washiriki 3,000 kutoka nchi na sehemu 127 duniani, ambao wataonyesha bidhaa zao nje ya mtandao, na mashirika matatu ya kimataifa na nchi 58 kutoka mabara manne duniani, hususan zile zilizosaini Pendekezo la Ukanda Mmoja na Njia Moja (BRI) zitashiriki kupitia mtandao.

Nchi nyingi za Afrika zinashiriki maonyesho hayo aidha moja kwa moja ama kwa kupitia mtandao wa Internet, zikionyesha bidhaa zao bora na kutafuta ushawishi wa kuingia katika soko kubwa la China.

Ni kwa kupitia Maonyesho haya, bidhaa nyingi zinazotoka nchi za Afrika ikiwemo kahawa, parachichi, korosho, pilipili na nyingine nyingi zimeweza kuingia kwenye soko la China na kupokelewa vizuri na wateja wa China.

Bidhaa kama kahawa kutoka Tanzania, Parachichi za Kenya, Kahawa ya Rwanda na Ethiopia, chai ya Afrika Kusini na asali ya Zambia na bidhaa nyingine zimepokelewa vyema katika soko la China.

Lakini pamoja na kwamba bidhaa za Afrika zinaweza kuingia kwenye soko la China, kuna changamoto kubwa ya upatikanaji wa bidhaa hizo kwa watu wa kawaida nchini China, na ni kwa kutokana na hilo, nchi nyingi za Afrika, licha ya kushiriki kwenye Maonyesho ya Kimataifa ya Uagizaji Bidhaa Nje ya China, pia zimeingia makubaliano na kampuni za biashara kupitia mtandao kama vile Alibaba na Jd.com ili kuweza kukidhi mahitaji ya bidhaa hizo. Hivi karibuni, Ubalozi wa Tanzania nchini China uliingia mkataba na kampuni ya JD.com ya China ambayo inashughulika na mauzo ya bidhaa kupitia mtandao wa internet, ambapo kupitia jukwaa kampuni hiyo la Maduka ya Kimataifa, bidhaa mbalimbali kutoka Tanzania ikiwemo korosho, kahawa na nyinginezo zinatweza kuuzwa kwa watumiaji wa China kwa urahisi zaidi.

Nchi za Afrika na China zimekuwa ni nchi zinazosaidiana na kushirikiana kwa kina ili kujipatia maendeleo kwa pamoja, na CIIE ni moja ya majukwaa muhimu yanayotumika na nchi hizi katika kutimiza lengo hilo. Takwimu za Wizara ya Biashara ya China zinaonyesha kuwa, biashara kati ya China na nchi za Afrika iliongezeka kwa asilimia 40.5 katika miezi saba ya kwanza ya mwaka huu, na kufikia rekodi ya juu ya dola bilioni 139.1.

Nchi za Afrika zinapaswa kutumia vizuri fursa kama hii ya Maonyesho ya Kimataifa ya Uagizaji Bidhaa Nje ya China kujitangaza na kutangaza bidhaa zao, ikiwemo vivutio vya utalii katika nchi husika, ili kuliteka soko kubwa la China na pia soko la kimataifa.

Hatua ya China kufungua mlango wake zaidi kwa nchi nyingine zinazoendelea zikiwemo za Afrika, ni ishara ya nia ya dhati ya China ya kujenga jamii ya binadamu yenye hatma ya pamoja, kunufaishana, na kusaidiana ili kutimiza ustawi wa pamoja.

VCG111258465498.jpg
 
Back
Top Bottom