Makamo wa Rais Mama Samia Suluhu kumuwakilisha Rais Magufuli mkutano AU - Kigali

koryo

JF-Expert Member
Jun 21, 2010
639
276
Nimesoma kwenye magazeti kuwa Mhe. Makamu wa Rais,Mama yetu Samia atamuakilisha Mhe. Rais wetu kwenye Mkutano huo. Mimi binafsi nina mawazo tofauti kuhusiana na uwakilishi huo. Mimi ninashauri Mhe. Rais ahudhurie hicho kikao binafsi kutokana na sababu zifuatazo:-
  • Kwanza juzi ndiyo kachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri wa Tanzania, ni vema akajumuika na wenzake ili wamfahamu.
  • Pale watahudhuria wawakilishi kutoka mashirika mengi ya Kimataifa, ni fursa adimu kukutana na viongozi kama hawa na kuweza kupata hata msaada.
  • Ni fursa kubwa kujitambulisha mbele ya wenzake na kuitambuisha TANZANIA.
  • Kigali siyo mbali na hivyo suala la gharama na uchovu kwa Mhe.Rais haupo.
Huu ni ushauri wangu na hata siku za usoni anaweza kuufanyia kazi.
 
Nimesoma kwenye magazeti kuwa Mhe. Makamu wa Rais,Mama yetu Samia atamuakilisha Mhe. Rais wetu kwenye Mkutano huo. Mimi binafsi nina mawazo tofauti kuhusiana na uwakilishi huo. Mimi ninashauri Mhe. Rais ahudhurie hicho kikao binafsi kutokana na sababu zifuatazo:-
  • Kwanza juzi ndiyo kachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri wa Tanzania, ni vema akajumuika na wenzake ili wamfahamu.
  • Pale watahudhuria wawakilishi kutoka mashirika mengi ya Kimataifa, ni fursa adimu kukutana na viongozi kama hawa na kuweza kupata hata msaada.
  • Ni fursa kubwa kujitambulisha mbele ya wenzake na kuitambuisha TANZANIA.
  • Kigali siyo mbali na hivyo suala la gharama na uchovu kwa Mhe.Rais haupo.
Huu ni ushauri wangu na hata siku za usoni anaweza kuufanyia kazi.


Namuunga mkono Raisi wangu kwa kutokudhuria huwo Mkutano, Viongozi wote wa Kiafrika wanaojitambau na wenye akili walishaipotezea AU, Ian Khan wa Botswana haudhurii, Moroko, Algeria, Tunisia hawahudhurii kwa maana wanajua kwamba AU ni tofauti na OAU!

AU ni muundo wa Wazungu ulio na lengo la kututawala, ni kama EU mabapo Uingereza wameishtukia na kujitoa, NAFTA muungano wa USA, Kanada na Mexiko ambapo D.Trump ameapa kuuvunja, na sasa hivi wanataka kuanzia electronic African passport na Wazungu ndiyo wanaotoa fedha kwa na kuna siri kubwa sana nyuma ya electronic African Passport Wazungu wanataka kuiba data kufanya Biashara, sasa hivi Big data ni biashara kubwa sana Duniani!


Say no to ,,electronic African Passport"!
 
Nimesoma kwenye magazeti kuwa Mhe. Makamu wa Rais,Mama yetu Samia atamuakilisha Mhe. Rais wetu kwenye Mkutano huo. Mimi binafsi nina mawazo tofauti kuhusiana na uwakilishi huo. Mimi ninashauri Mhe. Rais ahudhurie hicho kikao binafsi kutokana na sababu zifuatazo:-
  • Kwanza juzi ndiyo kachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri wa Tanzania, ni vema akajumuika na wenzake ili wamfahamu.
  • Pale watahudhuria wawakilishi kutoka mashirika mengi ya Kimataifa, ni fursa adimu kukutana na viongozi kama hawa na kuweza kupata hata msaada.
  • Ni fursa kubwa kujitambulisha mbele ya wenzake na kuitambuisha TANZANIA.
  • Kigali siyo mbali na hivyo suala la gharama na uchovu kwa Mhe.Rais haupo.
Huu ni ushauri wangu na hata siku za usoni anaweza kuufanyia kazi.
ww akili yako bado inaamini kwny kupata msaada, msaada wa nini?? aende kwny mkutano sababu wapo watu wa kuwaomba msaada..? ushauri wako c mzr. acha kufikiria habari za msaada, jifunze kujitegemea na kuwa huru kufanya yale unaona yana faida kwako na kwa jamii yako! misaada haiwezi kukutatulia changamoto zako!!!
 
Mwache mh. Raisi afanye kazi, akisafiri sana kwa ajili ya kujitambulisha mtaanza maneno
 
Nimesoma kwenye magazeti kuwa Mhe. Makamu wa Rais,Mama yetu Samia atamuakilisha Mhe. Rais wetu kwenye Mkutano huo. Mimi binafsi nina mawazo tofauti kuhusiana na uwakilishi huo. Mimi ninashauri Mhe. Rais ahudhurie hicho kikao binafsi kutokana na sababu zifuatazo:-
  • Kwanza juzi ndiyo kachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri wa Tanzania, ni vema akajumuika na wenzake ili wamfahamu.
  • Pale watahudhuria wawakilishi kutoka mashirika mengi ya Kimataifa, ni fursa adimu kukutana na viongozi kama hawa na kuweza kupata hata msaada.
  • Ni fursa kubwa kujitambulisha mbele ya wenzake na kuitambuisha TANZANIA.
  • Kigali siyo mbali na hivyo suala la gharama na uchovu kwa Mhe.Rais haupo.
Huu ni ushauri wangu na hata siku za usoni anaweza kuufanyia kazi.

Acha maneno ya jumla jumla, sema mama yako diyo mama yetu. Usiwajumuishe wengine
 
Tulishashauri alipokosa mkutano wa AU kule Addis Ababa mwezi January.

Hayupo strategic kimataifa.Yupoyupo tu na siamini kama lugha ndio Tatizo hapana mimi siamini hivyo kabisa bali kuna tatizo kubwa zaidi la uelewa katika siasa za kimataifa.

He's too Local !
 
  • Kwanza juzi ndiyo kachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri wa Tanzania, ni vema akajumuika na wenzake ili wamfahamu.
  • Pale watahudhuria wawakilishi kutoka mashirika mengi ya Kimataifa, ni fursa adimu kukutana na viongozi kama hawa na kuweza kupata hata msaada.

Misaada wakati hapa bongo watu wanapiga mamilioni ya EFD?
 
Ila sasa kuwakilishwa kunazidi. Wakuu wakikutana mkuu hatakiwi kuwakilishwa. Hivi kweli ni kwa nini asiende mwenye? Ana nini cha kumzuia ambacho makamu, waziri mkuu au mawaziri wake au hawawezi kufanya. Hebu tuwe wakweli; mkuu apunguze kuwakilishwa.
 
MTUKUFU YUKO BUSY ANA MECHI YA YANGA NA MADEAMA HATAWEZA KWENDA HUKO
 
Tulishashauri alipokosa mkutano wa AU kule Addis Ababa mwezi January.

Hayupo strategic kimataifa.Yupoyupo tu na siamini kama lugha ndio Tatizo hapana mimi siamini hivyo kabisa bali kuna tatizo kubwa zaidi la uelewa katika siasa za kimataifa.

He's too Local !
Huwa siwaelewi mnasimamia nini?

Nikuulize swali , hivi ni lazima kwenda? Na kama sio lazima je anaruhusiwa kutuma mwakilishi?


Wakati mwingine elimu zenu haziwasaidii

Eti. He is too local ?

Nina was was sana na elimu zenu na kushindwa kutambua Majukumu ya Rais
 
Huwa siwaelewi mnasimamia nini?

Nikuulize swali , hivi ni lazima kwenda? Na kama sio lazima je anaruhusiwa kutuma mwakilishi?


Wakati mwingine elimu zenu haziwasaidii

Eti. He is too local ?

Nina was was sana na elimu zenu na kushindwa kutambua Majukumu ya Rais
Eti Majukumu.Kwani hana wasaidizi?Kwa nini anawakimbia wenzake?
 
He is too local indeed! in fact angekuwa tu chief wa kijijini kwao maana exposure ni nill kabisaaa.
 
MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuondoka nchini kesho kwenda Kigali nchini Rwanda, kuhudhuria Mkutano wa 27 wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika (AU).

Makamu wa Rais atamwakilisha Rais John Magufuli katika mkutano huo wa siku mbili unaotarajiwa kuanza kesho na kumalizika keshokutwa.

Katika msafara wake, Makamu wa Rais atafuatana na Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustine Mahiga na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Zanzibar, Issa Haji Ussi.

Mkutano huo utakaohudhuriwa na Makamu wa Rais, utaanza kwa vikao vya ndani ambapo viongozi watajikita kujadili masuala ya kimkakati, ikiwemo umuhimu wa kuunganisha Bara la Afrika kibiashara. Umuhimu huo unalenga kuwa na soko la biashara huria ifikapo mwaka 2017.

Suala lingine litakalojadiliwa kimkakati ni mageuzi katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Wajumbe wa mkutano huo wa 27 wa AU, pia watachagua Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika pamoja na Makamu wake, makamishina wanane wa sekta mbalimbali na majaji wanne wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu.

Lingine litakalopitishwa ni mapendekezo kuhusu gharama za uendeshaji wa umoja huo na bajeti ya fedha kwa mwaka 2017. Makamu wa Rais na ujumbe wake wanatarajia kurejea nchini Julai 19 mwaka huu, baada ya kumalizika kwa mkutano huo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom