Nimesoma kwenye magazeti kuwa Mhe. Makamu wa Rais,Mama yetu Samia atamuakilisha Mhe. Rais wetu kwenye Mkutano huo. Mimi binafsi nina mawazo tofauti kuhusiana na uwakilishi huo. Mimi ninashauri Mhe. Rais ahudhurie hicho kikao binafsi kutokana na sababu zifuatazo:-
- Kwanza juzi ndiyo kachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri wa Tanzania, ni vema akajumuika na wenzake ili wamfahamu.
- Pale watahudhuria wawakilishi kutoka mashirika mengi ya Kimataifa, ni fursa adimu kukutana na viongozi kama hawa na kuweza kupata hata msaada.
- Ni fursa kubwa kujitambulisha mbele ya wenzake na kuitambuisha TANZANIA.
- Kigali siyo mbali na hivyo suala la gharama na uchovu kwa Mhe.Rais haupo.