Elections 2010 Makamba: Watanzania Watasahau .... Watatupa tena!

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
10,827
4,172
Akihojiwa na BBC kwamba watawafanyia nini Watanzania kiasi cha kukifanya Chama chake kionekane cha maana tena mbele ya umma na hivyo Watz wakipigie kura 2015, Makamba(Yusuf) alisema:

" tutatekeleza yaliyo kwenye ilani yetu na Watanzania watasahau haya (akimaanisha wizi, ufisadi na uchakachuaji wa kura), halafu watatupa (akimaanisha sisi Watz tutakipa kura chama chake 2015)".

Eti Watz wenzangu. Kweli tutasahau?
 
Kinachosikitisha Watanzania wengi ni mambumbumbu mno, wagumu kuelewa na wepesi kusahau.
Trend imeonekana katika uchaguzi huu. Mikoa ambayo wana uelewa wa mambo na shauku ya mabadiliko ya maisha wameibwaga CCM na walikua tayari kulinda ushindi wao, Lakini mikoa mingine ambayo bado wamelala, sidhani kawa wataamka katika kipindi hiki.

Labda watakaponunua Sukari kwa SHS 2,500/- Mchele shs 3,000/- Cement Shs 20,000/- Bati SHs 20,000/- na 1 USD = Tshs 3,000/- ndipo watakaposhika akili vichwani mwao, But then it will be too late.

Lets wait and see hii miaka mitano italeta nini maana Mkataa Jema, Baya humsubiri.
 
Mzee keshaanza pumba tena!! Ila kuna watanzania ambao hapa duniani wapo kama mizingo. Wanaamini umasikini walionao ni laana ya haki kwao!!
 
Alichoongea Makamba ni ukweli mtupu.
Historia inaonyesha hivyo hata CCM wakifanya mabaya gani lakini siku ya uchaguzi wartanzania wanayasahau na kuwapigia kura CCM.
So, jamaa amaeongea ukweli mtupu.
 
Lazima tukiri kila mmoja kwa nafsi yake ni kweli sisi watz ni mambumbu ndio maana tunayaruhusu hayo yote kutokea hata huyo makamba japo ni msema ovyo statement yake inaonyesha uhalisia wetu.Mpaka inafikia wanaanza kujiaminisha hivyo manaake tumewakubalia.Njia za kuwakataa tunazijua lakini hatuzifuati.Na hiyo ndiyo reward ya ujinga wetu.
 
Si kweli..hatusahau kitu hapa...Ategemee upinzani na ushindi wa wapinzani, hata kama watahonga kila kiendacho juu ya ardhi!
 
Ati tutasahau???!!! Miaka hii 5 ni ya kuwafumbua wengine macho. Silali hata nikiamsha ndg zangu 10 tu kwa miaka hii 5 toka usingizini inatosha na wao kuamsha wengine 10 kila mmoja usingizini huko huko waliko. Hakuna kulala!!:A S angry:
 
Kweli comrade,yaani WTZ wengi kama vile wamelogwa na ccm.hawakumbuki kuwa ukiumwa na nyoka hata uonyasi ukikuguza hunabudi kushtuka.wao hilo halipo na hutamani waumwe tena na nyoka ndo wakumbuke kuwa kumbe yule nyoka bado yupo.
 
" tutatekeleza yaliyo kwenye ilani yetu na Watanzania watasahau haya (akimaanisha wizi, ufisadi na uchakachuaji wa kura), halafu watatupa (akimaanisha sisi Watz tutakipa kura chama chake 2015)".

Eti Watz wenzangu. Kweli tutasahau?
CCM hawahitaji tusahau........hata tukikumbuka haisaidii...kwa sababu hawaongozi nchi kwa ridhaa ya wapigakura ila kwa ridhaa yao wenyewe kupitia NEC ya CCM..................labda muundo wa NEC ubadilishwe.....vinginevyo hatuna bao..................
 
Huyo vuvuzela hana mawazo akili zake zimeshachoka kufanya kazi. Hadi kufika 2015 hakutakuwa na chama kinaitwa CCM, ngoja tu wampe huyo Jambazi wa kisukuma aka mzee wa vijisenti USPIKA wa bunge ndiyo kaburi lao. USHAURI KWA MZEE MAKAMBA: KWANINI USIPUMZKE NA WAJUKUU ZAKO KULIKO KUTOA PUMBA KILA UCHAO?
 
Huyo vuvuzela hana mawazo akili zake zimeshachoka kufanya kazi. Hadi kufika 2015 hakutakuwa na chama kinaitwa CCM, ngoja tu wampe huyo Jambazi wa kisukuma aka mzee wa vijisenti USPIKA wa bunge ndiyo kaburi lao. USHAURI KWA MZEE MAKAMBA: KWANINI USIPUMZKE NA WAJUKUU ZAKO KULIKO KUTOA PUMBA KILA UCHAO?

Lakini kasema ukweli pamoja na uvuvuzela wake mkuu!!! WaTZ tunajulikana kwa kusahau...:A S angry:
 
umefika wakati baadhi ya mikoa iwe na kura ya veto kwenye uchaguzi, enzi za mwalimu ilikuwa mwanafunzi wa lindi akipata 60% na wa mwanza akapata 75% hapa wa lindi ndio alikuwa anapewa hiyo nafasi ya kwenda secondary. Sasa kwa stlyle ya mikoa ambayo ni maskini wa kutupwa halafu mikoa hiyohiyo ndio ccm wanavuna kura nyingi, mimi nadhani baadhi ya mikoa ipewe kura ya veto, kama ukipiga kura moja ihesabike kuwa ni kura tatu, maana nina wasiwasi nchi inaweza ikwa tunachaguliwa rais na wajinga miaka nenda miaka rudi, ili linafanyika marekani sio wajinga wale, walilitambuwa hili mapema. Mwenye ufahamu mpana kuhusu collegeu votes kule marekani hebu tuelimishane.
 
Akihojiwa na BBC kwamba watawafanyia nini Watanzania kiasi cha kukifanya Chama chake kionekane cha maana tena mbele ya umma na hivyo Watz wakipigie kura 2015, Makamba(Yusuf) alisema:

" tutatekeleza yaliyo kwenye ilani yetu na Watanzania watasahau haya (akimaanisha wizi, ufisadi na uchakachuaji wa kura), halafu watatupa (akimaanisha sisi Watz tutakipa kura chama chake 2015)".

Eti Watz wenzangu. Kweli tutasahau?

kwana hatukumpa .... waliiba
 
Nimeona uchaguzi huu kituo kimoja cha polisi kimempa kura tatu cand. wa sisiem kwenye uprezidaa. Dr.Slaa ilisoma 100 kadhaa hivi! Achilia mbali wakati wanatupasua na mabomu ya machozi walikuwa wakitusihi tutafute maji. Dalili hizi si nuru njema kwa sisiemu pale 2015. Wasitoneshe vidonda.
 
nawashauri chadema, wanajf, na wapenda maendeleo, TUTENGENEZE DVD, VCD, AU CASSETTE, na tuweke huu, upuuzi hawa jamaa wanaosema alafu this can work as very good for chadema campaign 2015
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom