Makamba usipotoshe Nyanda za Juu Kusini hakuna ukame

Ileje

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,796
12,239
Jana katika ziara ya Makamba alipotembelea mabwawa ya kuzalisha umeme alitoa taarifa akitaka kuaminisha umma kuwa tatizo la upungufu wa umeme nchini na kwa sababu ya ukame! Hii si kweli hata kidogo.

Kwa macho yake mwenyewe ameona bwawa la Mtera lina maji ya kutosha, na kwa kuthibitisha hilo meneja wa bwawa amemwambia maji yaliyopo yanatosha kuzalisha umeme kwa full capacity ya megawatt 80 kwa miezi 7 hata kama hakuna hata tone moja la mvua litanyesha.

Kama bwawa la Mtera limejaa maji, iweje bwawa la Kidatu likose maji? Kwa sababu moja ya sababu ya kujenga bwawa la Mtera ilikuwa kuhifadhi maji kwa ajili ya bwawa la Kidatu.

Aidha kwa taarifa zilizopo bwawa la Kihansi linatapika maji. Kwa maana hiyo mabwawa yote ya Mtera, Kidatu na Kihansi yana maji ya kutosha kuzalisha umeme kwa full capacity yao.

Kuhusu mvua ni kuwa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ina msimu mmoja wa mvua kuanzia Novemba/Disemba hadi April/Mei. Kwa hiyo huu ndiyo mwanzo wa msimu wa mvua, sasa huo ukame ni wa lini?

Hivyo namuomba Makamba afanye homework yake atafute nini chanzo cha upungufu wa umeme na siyo kusingizia maji. Maji yapo!
 
Kama watu wanamhujumu na kumpa taarifa za uongo si apeleke kwenye baraza la mawaziri Ili watu wa intelligence wafanye Kazi?
 
Kama watu wanamhujumu na kumpa taarifa za uongo si apeleke kwenye baraza la mawaziri Ili watu wa intelligence wafanye Kazi?
Makamba amekuwa katika wizara ya mazingira kwa muda na amefanya kazi kwa ukaribu na wizara ya maji ambayo ndiyo inahusika na utunzaji na usimamizi wa vyanzo vya maji, kwa nini asitafute ukweli huko?
 
Jana katika ziara ya Makamba alipotembelea mabwawa ya kuzalisha umeme alitoa taarifa akitaka kuaminisha umma kuwa tatizo la upungufu wa umeme nchini na kwa sababu ya ukame! Hii si kweli hata kidogo.
Kalemanii anawalipa sh. Ngapi mumchafue Makamba
 
Wahindi wanamlipa ili waendelee kuuza generator..
Hato dumu hapo kama anafanya hivyo kumbuka umeme ni jambo la maslah ya taifa usipotolewa na wenye mamlaka kelele za raia zitakutoa. Na ukigoma basi jiandae kupanda mahakamani siku moja
 
Wimbo wa Taifa ile sehemu ya ..."wabariki viongozi wetu"..... inabidi ibadilishwe kidogo.
Haaaa tuimbeje huo wimbo.

Hata nyumba za ibada nako kuangaliwe,iwe tuwaombee wagonjwa,yatima,wagonjwa na wenye mahitaji maalumu.

Viongozi wakihitaji huduma za maombezi wamfuate Gwaji boy
 
Niseme tu kama kelele zimepigwa sana juu ya mambo anayofanya Makamba toka siku ya kwanza ateuliwe kushika nafasi hiyo wizarani.
LAKINI aliyemteua yupo kimya kama hasikii.

Itoshe kusema haya anayofanya anatekeleza maagizo ya ALIYEMTEUA.

Tuna katiba mbovu sana.
 
Back
Top Bottom