Makamba, Umeme umekushinda utaweza bodaboda?

Mjomba wa taifa

JF-Expert Member
Apr 20, 2012
231
161
Nimesikitishwa na kitendo cha January Makamba kwenda Mwanza kushughulikia Bima ya afya kwa waendesha bodabpda. Makamba amekwenda kama nani? Kwa gharama ipi? Ni wizara gani inashughulikia suala hili?

Hivi hawa mawaziri hawana Job Descriptions? Waziri wa afya akilia kuingiliwa majukumu anaonewa?

Sitoona ajabu kesho nikimuona makamba kasimama barabarani akifanya ukaguzi wa driving license, maana sasa kila kitengo yupo. Muda wa kujipanga kwa urais ameshachelewa ndo maana anakurupuka kila kitengo.

Umeme umemshinda ya bodaboda atayaweza?
 
Muache yeye na mamvi wake wahangaike hawa vijana ni smart sana watajilia vyao halafu kwenye boc wanajua nani wa kumchagua
 
Umeme ni janga...
Swala la kufanya shughuli zingine sidhani kama ni tatizo..
Haya ya kua umekaa tu mezani hadi kazi zinazo lingana na position uliyopo ndio uzifanye nalo ni tatizo...
 
huyu kajipanga urais wa Tanganyika,lowassa anajipanga muungano washasoma majira,akina membe,sita na sumaye nyota zao zimefifia wanangoja kuoteshwa ndoto,wataisoma namba ridhiwani na wapwani wenzie kuwa rais hatoki kaskazini
 
Serikali ya CCM haina tofauti na bwawa la kambale kila mmoja ana sharubu. Wazee wetu wanaishi ktk mazingira magumu hawaoni akawatengenezea hiyo bima, mpaka apeleke kwa vijana? hiyo ndiyo risk assessment aliyofanya, vipi swala la usalama barabarani?
 
kama umechukia sana kwanini usimeze wembe au usage chupa unywe ili tukuone kweli mwanaume kakasirika
 
Nimesikitishwa na kitendo cha January Makamba kwenda Mwanza kushughulikia Bima ya afya kwa waendesha bodabpda. Makamba amekwenda kama nani? Kwa gharama ipi? Ni wizara gani inashughulikia suala hili?


Hivi hawa mawaziri hawana Job Descriptions? Waziri wa afya akilia kuingiliwa majukumu anaonewa?

Sitoona ajabu kesho nikimuona makamba kasimama barabarani akifanya ukaguzi wa driving license, maana sasa kila kitengo yupo. Muda wa kujipanga kwa urais ameshachelewa ndo maana anakurupuka kila kitengo.

Umeme umemshinda ya bodaboda atayaweza?
Urais 2015 unawatesa watanzania wenzetu. Angekuwa anayafanya hayo huko Bumburi, tungejua anahangaika na wapiga kura wake. Hata hivyo pia Soho hashughuliki na umeme bali Sayansi,teknolojia na Mawasiliano.
 
Huyu Makamba akiwa Rais wa tanganyika mie nahama nchi aisee.
Ntaukana huu uraia for real
 
Back
Top Bottom