Makamba: Tanzania inahitaji TSh. Bilioni 345 kukabili Tabia Nchi

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,355
8,042
Waziri wa Nishati, January Makamba amesema Tanzania inahitaji dola 150 milioni za Marekani (Sh345 bilioni) kwa mwaka kujenga uwezo wa kukabiliana na athari za mabadili-ko ya tabianchi.

Makamba amesema fedha hizo zinatakiwa kutumika kujenga uwezo katika sekta ya kilimo, afya, miundombinu, nishati na maji hivyo kuziomba nchi zilizoendelea na wabia wa maendeleo kufadhili mchakato huo.

Waziri amesema hayo leo Jumatatu, Septemba 5, 2022 katika mkutano wa viongozi wa dunia unaojadili Programu ya Afrika ya Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Africa Adaption Summit) unaofanyika Rotterdam nchini Uholanzi.

“Nina furaha kuwa Kituo cha Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia nchi Duniani (GCA) na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) zimeungana kuiendeleza Programu ya Kuharakisha Afrika Ina-kabiliana na Majanga (AAAP) ya mabadiliko ya ta-bianchi ukiwamo Uviko-19, ukame, ukosefu wa ajira na mafuriko,” amesema.

Katika mkutano huo ulioongozwa na Rais wa Sen-egal, Macky Sally na Mwenyekiti wa GCA ambaye ni Katibu Mkuu smtaafu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon, Waziri Makamba alimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan.

Lengo kuu la mkutano huo ni kuwashawishi washirika wa maendeleo, taasisi za fedha na sekta binafsi kuchangia dola 25 bilioni zinazohitajika mpaka mwaka 2025 kufanikisha kuitekeleza pro-gramu hiyo.

Mbali na hilo, Makamba amesema Tanzania inahitaji dola 14 bilioni kugharimia utekelezaji wa mpango wa Taifa wa kupunguza athari za maba-diliko ya tabianchi kiasi kinachotarajiwa kupanda hadi dola 30 bilioni mwaka 2030.

Mkutano huo umefanyika kabla ya mkutano wa 27 nchi Wananchama wa Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi utakaofanyika Misri hapo Novemba.
 
Daah! Baada ya Makamba kutumwa kumuwakilisha mh kwenye maswala ya mazingira na wakati Jafo yupo; Sijui Jafo atakuwa katika hali gani!
Jafo ambaye kwa wakati fulani alionekana kuandaliwa kuja kuwa 'in charge' inaonekana madawa yake yameisha nguvu!
 
Bilioni 345 ili kukabiliana na tatizo ambalo linaikumba dunia yote, anamaanisha akipewa hizo pesa ndio tatizo la ukame nk yatakwisha Tanzania?
 
Bilioni 345 ili kukabiliana na tatizo ambalo linaikumba dunia yote, anamaanisha akipewa hizo pesa ndio tatizo la ukame nk yatakwisha Tanzania?

Hayo ni baadhi ya maswali najiuliza hapa. Kama ni kweli tumefanikiwa kufanya utafiti Kwa ufasaha na kubaini tatizo letu ni hizo pesa kulimaliza itakua tumepiga hatua kubwa sana.

Ikumbukwe Tanzania sio kisiwa, na haya madhara kama ulivyosema yanaikumba dunia yote na vyanzo vya tatizo sio lazima viwe Tanzania. Swali ni Je, mikakati ipi inahitaji hizo pesa kukabiliana na hayo madhara?

Hiyo pesa inahisisha namna ya kuzuia kupotea Kwa theluji kwenye kilele Cha mlima wetu Kilimanjaro?
 
Hayo ni baadhi ya maswali najiuliza hapa. Kama ni kweli tumefanikiwa kufanya utafiti Kwa ufasaha na kubaini tatizo letu ni hizo pesa kulimaliza itakua tumepiga hatua kubwa sana.

Ikumbukwe Tanzania sio kisiwa, na haya madhara kama ulivyosema yanaikumba dunia yote na vyanzo vya tatizo sio lazima viwe Tanzania. Swali ni Je, mikakati ipi inahitaji hizo pesa kukabiliana na hayo madhara?

Hiyo pesa inahisisha namna ya kuzuia kupotea Kwa theluji kwenye kilele Cha mlima wetu Kilimanjaro?
Tunakata miti mamilioni kujenga bwawa ambalo haliishi huku tunaomba pesa ya kuhifadhi mazingira
 
Bilioni 345 ili kukabiliana na tatizo ambalo linaikumba dunia yote, anamaanisha akipewa hizo pesa ndio tatizo la ukame nk yatakwisha Tanzania?

..wakati kila mwaka Tz inatumia billion 500+ kununua ma-V8 ya vigogo serikalini.
 
Bwawa la umeme ndiyo lilikuwa jibu la tabia nchi maana lingekamilika na kushushwa kwa bei ya umeme kufikia Tsh 1000 unit 4 basi miti isinge katwa ovyo.
 
Back
Top Bottom