Makamba: Msinihukumu kwa mabaya, I love you

KadaMpinzani

JF-Expert Member
Jan 31, 2007
3,715
86
Makamba: Msinihukumu kwa mabaya, I love you

2007-11-06 08:33:34
Na Beatrice Bandawe, Dodoma


Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusuf Makamba, (pichani kulia) juzi alilazimika kuwaomba wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM kura kwa kutomhukumu kwa mabaya yake na kuwaambia: `Ilove you`.

Bw. Makamba ambaye mara baada ya kuwaambia wajumbe hao `I love you` (nawapenda), waliripuka kwa mayowe ya vicheko, alisema kuwa binadamu yuko mara tatu.

Alifafanua kwamba upande wa kwanza wa binadamu ni vile anavyojifahamu mwenyewe, anavyofahamika na wenzake na anavyofamika na Mungu.

Alisema kwa jinsi anavyojifahamu yeye, anafaa kuchaguliwa katika uchaguzi huo.

Bw. Makamba ambaye aligombea kundi la viti 20 la NEC Taifa, hata hivyo, alichaguliwa kwa ushindi mnono.

`Chonde chonde wajumbe nichagueni I Love you,` alisema kwa kuweka msisitizo.

Aliwataka wanachama hao kutomhukumu kwa mabaya yake kwani hata Mungu aliwasamehe waliomkosea.

`Nawaombeni mninusuru na chama chetu,` alisema na kuongeza kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu aliochaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, amepambana na kuwagaragaza wapinzani.

Alisema kama wajumbe watamuangusha, hata wapinzani watafurahi na kusema CCM wameangusha Katibu Mkuu wao.

Aidha, alisema vyombo vya habari pia vitapata ya kuandika na kuweka kwenye vichwa vya habari kwamba Makamba agaragazwa na wana-CCM wenzake.

Bw. Makamba ambaye alikuwa akitoa kauli hiyo wakati aliposimama kwenye jukwaa la kuombea kura, mara baada ya kumaliza kujinadi, Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete, alimjibu kwa kumwambia: `We love you too,` na kusababisha ukumbi mzima kushangilia.

SOURCE: Nipashe
 
hapo ndio utaamini kwamba CCM ni wasanii si mchezo,huyu ni msanii namba mbili.anashindwa kuwaeleza wapiga kura wake amefanya mambo gani ya maendeleo,anakazania kuwagalagaza wapinzani,je hiyo ndiyo sera ya maisha bora kwa kila mtanzania?
 
Chama cha mapinduzi si mama yangu na wala si dini yangu,siwezi kuabudu usanii..
Naomba kuungana na Mwanakijiji kuacha kuwaombea viongozi hawa..
toka makamba ameingia haya yametokea.

1.Suala la Muafaka limekosa mwelekeo ulio thabiti,rejea ilifikia kipindi ukataka kuvunjika.

2.amewatusi viongozi wa CCM wa Tanga,na nina uhakika hata baada ya kuwaambia I Love you hawakumchagua sababu sio kipenzi chao..

Mie naona imetosha,Tafakari
 
Usishangae, CCM ni waoga wa mabadiliko/mapinduzi. Nilishanga style ya kuunda ya JK ya kishamba ya kuunda tume ya madini ikiingiza hata mashehe na mapdri. Hivi ikitokea sekta nyingine ya kiuchumi ina matatizo ataunda tume nyingine kuongoza. Ina maana mawaziri 60 alionao hawatoshi au ni "compitency issue"?. Kuunda tume ni upuuzi, kama anaona hawezi kusimamia vizuri apishe watu waendelee.

Nimekasirishwa.
 
I am not quite sure if Lt, Makamba is really representative of sisiemu's views, vision, mission and legacy. I have been making a close follow-up of what he has been promulgating since he was a regional commissioner in Dar, he seems to be more than a partisan, calling 'wapinzani' mapaka.
He has constantly been blaspheming opposition and anyone who is against his views. Do we all deserve this blasphemy and insults simply because we do not belong to sisiemu?
 
Usishangae, CCM ni waoga wa mabadiliko/mapinduzi. Nilishanga style ya kuunda ya JK ya kishamba ya kuunda tume ya madini ikiingiza hata mashehe na mapdri. Hivi ikitokea sekta nyingine ya kiuchumi ina matatizo ataunda tume nyingine kuongoza. Ina maana mawaziri 60 alionao hawatoshi au ni "compitency issue"?. Kuunda tume ni upuuzi, kama anaona hawezi kusimamia vizuri apishe watu waendelee.

Nimekasirishwa.

babu, sio ccm inayoogopa mapinduzi, ukizingatia kikaitwa chama cha mapinduzi, hivi unataka kuniambia wewe ulipokuja hapo ulipo haikuwa vigumu kuadapti mazingira ? je ulikuwa muoga, usiye na uhakika na mafanikio ya nia zako au ulikuwa na uhakika ? ccm KAMWE HAIOGOPI MAPINDUZI HENCE CHAMA CHA MAPINDUZI !
 
Back
Top Bottom