Makamba: Mjadala wa EPA ufungwe

Hii ni sawa na Mchawi kumpigiqa kelele za mchawi kila kukicha, akishindwa kuwanyamazisha atawaroga, ndio haya ya Makamba, Huyu ni Fisadi na kelele za ufisadi zina mkera, hana jinsi na nadhani iongekuwa yeye ndo JK angeshautekeleza Mpabngo wa Masha wa Kum fleece Mengi. Huyu ni chiriku tu ndo maana hata kwenye chama anawaingiza machriku wenzake kwani wakikaa pamoja stori zinapanda. Huyu hawezi kukaa meza moja na akina Mwakyembe, Seleli, Kilango, Mpendazoe, Zambi nk. Huyu anaweza kaa meza moja na kina Komba Cpt, Chitalilo a.k.a Kikojozi, Rostam, Masha et al.

Hii ni sawa ni Mbweko usio na Mbwa, teh... tehe. kho,
 
hii ni sawa na mchawi kumpigiqa kelele za mchawi kila kukicha, akishindwa kuwanyamazisha atawaroga, ndio haya ya makamba, huyu ni fisadi na kelele za ufisadi zina mkera, hana jinsi na nadhani iongekuwa yeye ndo jk angeshautekeleza mpabngo wa masha wa kum fleece mengi. Huyu ni chiriku tu ndo maana hata kwenye chama anawaingiza machriku wenzake kwani wakikaa pamoja stori zinapanda. Huyu hawezi kukaa meza moja na akina mwakyembe, seleli, kilango, mpendazoe, zambi nk. Huyu anaweza kaa meza moja na kina komba cpt, chitalilo a.k.a kikojozi, rostam, masha et al.

Hii ni sawa ni mbweko usio na mbwa, teh... Tehe. Kho,
mzee mzee mzee taratibu basi
 
kawaida uzee huja na busara ila Tanzania wazee wengi ndani ya serikali na chama tawala huwa wapumbavu wezi na hawana hekima. Wana zeeka na kufa na laana za wananchi ndio maana hawajui waseme nini wapi na wakati gani.
Kwa mtaji huu nchi inaenda shimoni.
makamba mpiga debe wa mafisadi unategemea aseme nini???? mwizi ni mwizi tu na kizazi chake hutoa wezi.....
 
I wish also to express my doubt to Mwenyekiti wa Chama Chetu Cha Mapinduzi Chajenga Nchi, did he found this to be the right person to hold that position of Secretary General in a frustrating party. Tusimlaumu Makamba, nadhani JK Mwenyewe ndiye wa kuangaliwa kwa Macho yote b'se of the type of people anaowachagua wamsadie. Makamba, Masha, Chenge, Karamagi, kwenye CC ana Rostam, Kingunge, Is he serious or he really knows what is he supposed to do?

Nachelea kusema kwamba, Tatizo sio Uzezeta wa Mgosi, bali ni yule aliyemchagua, kwani yeye anaona anayoyafanya ni safi kabisa, he wants now to halt the ufisadi dialogue, au ndio janja ya kuwapeleka mahakamani ili kutunyamazisha.

Wewe Mgosi wewe acha utoto wewe .... hii nchi ni yetu na hizo hela alizoiba Rostam ni zetu sio za CCM please, Ukome kutoa kauli zisizo na akili..... next time you will be hanged naked.....
 
Acha baadhi ya Wabunge wa CCM watake huyu jamaa aondolewe kwenye nafasi hiyo. Anaropoka kila kukicha vitu visivyokuwa na kichwa wala miguu. JK inabidi amtafute mtu mwingine katika nafasi hiyo maana kuwepo kwake kunazidi kuiharibia CCM.

Weeeee.. Bubu acha usiseme kabisa, Makamba muache abaki hapo hapo, kwa maana huyu anatusaidia sana kusafisha njia yetu ya kutuondolea chama cha mafisadi kilicho tufikisha hapa tulipo!
 
Kwakweli inatia uchungu kusikia kiongozi mwenye dhamana kubwa kama yake anacheza wimbo tofauti na wakuu wenzake. Hata kama kinachofanyika sasa cha kushikilia dagaa wa ufisadi ni kiini macho, Makamba alipaswa asome alama za nyakati na kufahamu viongozi wenzake na wananchi kwa ujumla wana mtazamo gani?

Hapa anatuletea hoja ya kitoto kuwa wapinzani wameshupalia ufisadi na EPA na inamkera, hivyo anajisahau na kuamua kujiropokea. Hajui etiquette za uongozi na anajidhalilisha mno kwani hata hao waliomchagua yaelekea wamepigwa na butwaa kwa kauli yake hii.

Pia hata kama kesi ya watuhumiwa ipo mahakamani, na pia hata kama hao waliopatikana hadi sasa ndio wote waliopaswa kushitakiwa; suala hili hili ndio kwanza lipo katika hatua za mwanzo za kimahakama... hivyo mjadala wake hauta acha kusikika.. kwani yanayotokea yenyewe ni mjadala tosha. Mfano, Mramba na Yona kujidhamini kwa Mabilioni ya shilingi, ilihali wao walikuwa ni watumishi wa Serikali.. ni mjadala tosha na pia ni suala linalohitaji nguvu ya ziada kulielewa.

Kwa vyovyote vile Makamba hawezi kutufungia mjadala wa Ufisadi kwa porojo zake. na akome kabisa kwani si yeye aliouanzisha.
 
wewe Babu funga DOMO LAKO !!!OMBA MUNGU UMALIZE SALAMA HILO LA FISADI ALIKUSAIDII KUTOONDOLEWA N WABUNGE SUBIRI WANARUDI UPYA KUJIPANGA ATUTAKI USHENZI KWENYE CHAMA CHETU!!!1
 
Katibu mkuu wa CCM bwana Yusuph Makamba amedai Mjadala wa EPA ufungwe kwa kuwa watuhumiwa wote wameshafikishwa mahakamani. Je ni kweli watuhumiwa wa EPA wote wameisha fikishwa mahakamani?


Hapa ndipo tunajua ukweli kuhusu Kagoda unavyopiganiwa kufichwa! Huyu Mzee anataka kutuaminisha kuwa watuhumiwa wa EPA ndo hao na wote wameshafikishwa Mahakamani, na hapa ndo tunaweza kuhisi kwa nini Kagoda inafichwa na yale madai ya EPA kutumika kuifikisha CCM kwenye utawala ndo yanaelekea kuwa dhahiri.
 
Makamba EPA haiwezi kunyamazishwa mpaka pale yule swahiba wako aliyekumegea fungu toka EPA amepandishwa kizimbani; lazima unamkumbuka yule jamaa uliyekuwa unampigia debe awe mbunge wa Kigamboni!! Pia huyo aliyekuwa mweka hazina wako kabla ya Makalla nae lazima apandishwe kizimbani; baada ya hapo hao wakishakwenda Ukonga ndio uje ulete porojo zako za kufunga mjadala.
 
Yote yanayozungumzwa kwenye thread hii kuhusu Mzee Makamba yalizungumzwa kwenye thread nyingi zilizopita. Wana JF waliowengi wanajua kuwa Mzee anatakiwa kupumzika baada ya kazi kubwa aliyoifanya kwa ajili ya chama.
 
Wanasema 'uzee (utu uzima) dawa', lakini kwa huyu mgosi inakua kinyume!
Au wamemnukuu vibaya....can someone confirm this please?
Nahisi alisema 'watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani'.
 
CCM yamtetea Makamba kuhusu EPA

na Esther Mbussi
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimemtetea Katibu Mkuu wake, Yusuph Makamba, kutokana na kauli yake aliyoitoa kuhusu suala la Akaunti ya Malipo ya Madeni ya nje (EPA) kutafsiriwa vibaya na baadhi ya wanasiasa nchini.

Taarifa iliyotolewa jana na Kaimu Mkuu wa Propaganda wa chama hicho, Hizza Tambwe, ilieleza inawezekana wanasiasa hao hawakumuelewa au hawakupata taarifa kamili kuhusiana na aliyoyasema Makamba.

Taarifa hiyo ilieleza katika kuweka mambo sawa juu ya upotoshaji huo, CCM imechukua fursa hiyo kufafanua alichokisema Makamba ni kuwa, Bunge limetimiza wajibu wake katika suala hili na serikali pia kwa kuajiri kampuni iliyofanya ukaguzi (Ernst & Young) kupitia kwa mkaguzi mkuu, ambayo ilichunguza na kugundua mapungufu.

Taarifa hiyo iliongeza kuwa baada ya rais kupata taarifa hiyo alichukua hatua za haraka kwa kufanya mabadiliko katika uongozi wa juu wa Benki Kuu na kuunda kamati ya wataalam wa masuala ya sheria kushughulikia suala hilo kisheria, ambapo baada ya kumaliza kazi yake ilimpatia ripoti ikiwa ni pamoja na kufanikisha upatikanaji wa baadhi ya fedha zilizochukuliwa.

“Watuhumiwa wamefikishwa mahakamani, kwa wale waliobaki jeshi letu la polisi linashirikiana na vyombo vingine vya kimataifa kuupata ukweli kama mchunguzi alivyopendekeza, kwa hiyo suala hili sasa lisiwe wimbo, aachiwe Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali, mahakama na vyombo vingine vya sheria vitimize wajibu wake kwa mujibu wa sheria za nchi yetu.” Ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Kutokana na hali hiyo, chama hicho kilisema, Makamba aliyasema hayo kwa nia njema akiamini kwamba suala la EPA sasa si la kutumiwa na wanasiasa kuwapotosha wananchi, kama ambavyo wale wasioitakia mema nchi walivyojaribu kufanya kwa muda mrefu bila mafanikio pamoja na kuihusisha CCM huku wakijua haiusiki kwa namna yoyote ile.

Katika ufafanuzi huo, taarifa iliongeza kuwa, katika kauli yake Makamba alisisitiza kuwa serikali inastahili pongezi kubwa kwa hatua ilizochukua na zinazoendelea kuchukuliwa na vyombo vyake na si kulaumiwa, na kwamba haoni sababu ya wanasiasa wasiokubalika na umma wa Watanzania kuendelea kuwakatisha wananchi tamaa, na kuwataka watulie na kuwa na subira badala ya kuingilia kati utendaji wa vyombo vya sheria.

Hivi karibuni, akiwa ziarani mkoani Arusha, Makamba alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema mjadala kuhusu suala la EPA ufungwe kwani watuhumiwa wote wameshafikishwa mahakamani, jambo lililopingwa vikali na baadhi ya wananchi na wanasiasa wakitaka mmiliki wa Kagoda naye afikishwe mahakamani kabla mjadala huo haujafungwa rasmi.
 
SISIEMU ina wanasisasa uchwara wengi ambao mara nyingi huropoka upupu, halafu baadaye wakigundua kuwa wameboa, basi ndipo hutumia muda mrefu na raslimali kuspini ili "kufafanua." Hata jakaya mwenyewe ana upungufu wa namna hiyo.
 
Kuna watu ha JF walikataa kumhusisha Makamba na watoto wake. Ila sitashangaa nikisikia kati yao 2010 kuna anayegombea ubunge CCM au viti maalum Tanga. Tanzania ni nchi ya kifalme ndio maana Makamba anaweza kuongea upupu kama huu na bado akaonekana yuko sawa. Harakati zao zimeanza tutaziona shadidi muda mfupi ujao
 
Back
Top Bottom