MwanaDiwani
JF-Expert Member
- Mar 22, 2013
- 5,536
- 2,264
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), January Makamba, amesema chama hicho hakijatengwa na vijana wa elimu ya vyuo vikuu kama inavyosemwa na wapinzani. Makamba, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, alitoa kauli hiyo wakati akifungua kongamano la vijana ambao ni wanachama wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) wa vyuo vikuu.
Alisema tofauti na hoja zinazoenezwa na wapinzani kwamba vijana wengi, hususani wa vyuo vikuu hawaiungi mkono CCM, hawawezi kutishwa na maneno hayo ya mtaani.
CCM bado kinawathamini vijana na ndiyo maana wanaendelea kukiunga mkono, umati huu unadhihirisha kwamba hatujapoteza umaarufu wetu katika vyuo vikuu nchini, wenzetu wanaoeneza propaganda hii wamepotoka.
Wenzetu wanawatafuta na kuwajenga vijana katika dhana ya kuhatarisha amani, CCM tunataka vijana washiriki na kujadili siasa ya nchi yao nje ya vyuo, alisema Makamba.
Alisema CCM ndiyo msingi wa amani ya nchi kwa sababu kimejenga msingi huo kuanzia kwa vijana wa chipukizi ambapo vijana wadogo wanafundwa uzalendo kwa nchi yao.
Katika kongamano hilo, makada mbalimbali wa CCM waliwakumbusha vijana hao wasomi kutobweteka na kuwaachia wenzao wa upinzani kutamba katika mitandao ya kijamii kwa kutoa hoja za kuupotosha umma kuhusu Serikali inayoongozwa na CCM.
Katika hatua nyingine, Kamanda mteule wa Umoja wa Vijana, Kata ya Kitunda, Godfrey Obonyo, alitoa msaada wa samani mbalimbali kwa ajili ya ofisi hiyo.
Katika makabidhiano hayo, Obonyo, aliwaasa vijana kuvitumia vifaa hivyo kwa ajili ya maendeleo ya chama na si vinginevyo.
Aidha, aliahidi kuwaunganisha vijana katika kampuni mbalimbali waweze kupata miradi ya kujitegemea na kuepuka na adha ya kutokuwa na ajira za kuaminika.
habari Mtanzania Jumapili.
baadhi ya picha za mkutano.
Alisema tofauti na hoja zinazoenezwa na wapinzani kwamba vijana wengi, hususani wa vyuo vikuu hawaiungi mkono CCM, hawawezi kutishwa na maneno hayo ya mtaani.
CCM bado kinawathamini vijana na ndiyo maana wanaendelea kukiunga mkono, umati huu unadhihirisha kwamba hatujapoteza umaarufu wetu katika vyuo vikuu nchini, wenzetu wanaoeneza propaganda hii wamepotoka.
Wenzetu wanawatafuta na kuwajenga vijana katika dhana ya kuhatarisha amani, CCM tunataka vijana washiriki na kujadili siasa ya nchi yao nje ya vyuo, alisema Makamba.
Alisema CCM ndiyo msingi wa amani ya nchi kwa sababu kimejenga msingi huo kuanzia kwa vijana wa chipukizi ambapo vijana wadogo wanafundwa uzalendo kwa nchi yao.
Katika kongamano hilo, makada mbalimbali wa CCM waliwakumbusha vijana hao wasomi kutobweteka na kuwaachia wenzao wa upinzani kutamba katika mitandao ya kijamii kwa kutoa hoja za kuupotosha umma kuhusu Serikali inayoongozwa na CCM.
Katika hatua nyingine, Kamanda mteule wa Umoja wa Vijana, Kata ya Kitunda, Godfrey Obonyo, alitoa msaada wa samani mbalimbali kwa ajili ya ofisi hiyo.
Katika makabidhiano hayo, Obonyo, aliwaasa vijana kuvitumia vifaa hivyo kwa ajili ya maendeleo ya chama na si vinginevyo.
Aidha, aliahidi kuwaunganisha vijana katika kampuni mbalimbali waweze kupata miradi ya kujitegemea na kuepuka na adha ya kutokuwa na ajira za kuaminika.
habari Mtanzania Jumapili.
baadhi ya picha za mkutano.