Makamba azungumza kwa mara ya Kwanza Bungeni.

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Feb 27, 2007
4,132
1,571
Kwa mujibu wa Tangazo la Spika mchana wa leo ni kuwa jioni hii mbunge wa Viti maalum MH.Yusuph Rajabu Makamba ,na kwa mujibu wa tangazo hilo spika alisema kuwa kuna wabunge watatakiwa kusafisha njia na Makamba atakuwa mtu wa tano kuchangia.


Sasa kuna haja ya kujua mbunge huyu wa viti maalum atachangia nini kwa mara ya kwanza tangu aingie kwenye Bunge .

Leo ni siku ya hotuba ya kilimo hivyo huenda anakuja kutueleza kuwa ILANI iliposema kuwa kilimo kitakuwa kwa asilimia 20 ifikapo 2010 ilikuwa na maana gani.

Nawatakia kulifuatilia bunge kwa umakini ili kujua huyu atachangia kitu gani.

Atasema kuwa Zanzibar ni nchi?
Atasema kuwa Nnape alichemka?
 
Last edited by a moderator:
Jamani jueni kuwa huyu ni mteuliwa wa Rais sasa kama mnaona hana lolote je?kumpa mpaka ukatibu mkuu ina maana kuwa alikosea ama ndio alimuona anafaa?


Ila pia ni aibu kwa huyu katibu mkuu wa chama kinachotawala kukaa ndani ya bunge kwa zaidi ya miaka miwili kukaa bila hata kuchangia huku akiwa ndio mwenye jukumu la kuhakikisha kuwa ilani ya chama chake inafuatwa na serikali iliyopo madarakani.

Tunasubiri kuona kama atailinda ilani juu ya kilimo ama atasema ya kwake.

Nawawekea ilani ilisema nini kuhusu kilimo punde.
 
Makamba is simply senile, ataishia kuimba pambio tu humo, figuratively or even literally.
 
Kwa mujibu wa Tangazo la Spika mchana wa leo ni kuwa jioni hii mbunge wa Viti maalum MH.Yusuph Rajabu Makamba ,na kwa mujibu wa tangazo hilo spika alisema kuwa kuna wabunge watatakiwa kusafisha njia na Makamba atakuwa mtu wa tano kuchangia.


Sasa kuna haja ya kujua mbunge huyu wa viti maalum atachangia nini kwa mara ya kwanza tangu aingie kwenye Bunge .

Leo ni siku ya hotuba ya kilimo hivyo huenda anakuja kutueleza kuwa ILANI iliposema kuwa kilimo kitakuwa kwa asilimia 20 ifikapo 2010 ilikuwa na maana gani.

Nawatakia kulifuatilia bunge kwa umakini ili kujua huyu atachangia kitu gani.

Atasema kuwa Zanzibar ni nchi?
Atasema kuwa Nnape alichemka?

Kieleweke Mbowe aliwahi jusema hayo hapo chini....

Bunge linapokuwa mchezo wa kuigiza

na
Freeman Aikaeli Mbowe



Naam, hatimaye Bunge wiki hii linamaliza mkutano wake wa nane ambao pamoja na mambo mengine umepitisha bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2002 - 2003. Mimi pamoja na Waheshimiwa wenzangu tunafungasha kurudi majimboni mwetu.

Kwa takriban miezi miwili mimi na Waheshimiwa wenzangu tumebebeshwa makabrasha mbalimbali yenye taarifa kadhaa za serikali na asasi zake. Lengo (angalao) ni kujua kilichofanyika katika mwaka wa fedha uliopita na kadhalika mipango ya Serikali katika mwaka ujao wa fedha. Kwa mzigo huu wa makabrasha, hata mikono imeshupaa kidogo!

Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Nina hakika asilimia 75 ya makabrasha haya hayafunguliwi achilia mbali kusomwa. Yote haya husababishwa na kupewa pengine kwa makusudi makabrasha haya siku hiyohiyo ya Waziri kuwasilisha hoja yake. Wabunge wachache hupata nafasi ya dakika zisizozidi 15 kuchangia Wizara hiyo kwa siku hiyo hiyo moja.

Gharama ya kuchapisha na "kubind" makabrasha haya ni mzigo mkubwa kwa Serikali na hivyo mlipa kodi! Si unajua tena! "Mnoko" mkabidhi lundo la makabrasha dakika za majeruhi na lazima atalewa.

Mada yangu ya leo inalenga kwenye kujadili kama miezi miwili tuliyolipwa (labda tuliyojilipa) posho kwa kutumia kodi za wananchi tumefanya kazi waliyotutuma au tumekuwa tunaigiza mchezo wa luninga.

Kabla sijaingia kwenye uchambuzi wa kina wa ni kwanini naamini kuwa bunge letu leo ni "Talk Show" nitapenda kuainisha majukumu ya nguzo tatu za utawala wa nchi yetu kama ilivyo kwa nchi nyingine zenye kuamini dhana ya utawala bora na demokrasia. Ikumbukwe kuwa kuamini ni suala moja na kutekeleza ni jingine.

Napenda kunukuu vifungu viwili vya kwanza vya utangulizi wa Katiba yetu vinavyoainisha misingi yake:

"...Kwa kuwa sisi wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, undugu na amani:

Na kwa kuwa misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi, na pia yenye mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote..."
Kwa tafsiri hii basi, bunge lina wajibu mkubwa kwa niaba ya Watanzania wa kutunga sheria na hatimaye kisimamia Serikali katika utendaji wake wote. Sura ya tatu , Sehemu ya kwanza Ibara ya 62 mpaka 65 ya katiba yetu inaainisha waziwazi madaraka haya ya Bunge juu ya Serikali. Aidha, Rais kama kiongozi mkuu wa Nchi ni sehemu ya Bunge.

Serikali nayo ina wajibu wa kusimamia na kutekeleza pamoja na mambo mengine maagizo ya Bunge. Aidha ina wajibu wa kusimamia ulinzi na Usalama wa nchi, raia wake na mali zao.

Kwa upande wake, Mahakama ina wajibu wa kusimamia haki kwa mujibu wa sheria zilizotungwa na Bunge chini ya Sheria Mama ambayo ni Katiba ya Nchi.

Naam, kinachoendelea leo ndani ya Bunge letu ni kinyume na msingi wote wa Katiba na dhana nzima ya Bunge kusimamia Serikali.

Shughuli za kila siku za Bunge husimamiwa na kanuni ambazo Bunge linajitungia lenyewe. Kanuni za Bunge letu leo ndiyo chimbuko (naamini la makusudi) la kupoka madaraka ya Bunge na hatimaye kugeuza Bunge kuwa mchezo wa kuigiza.

Kanuni ya 13 (1), (2) na (3) ya kanuni za Bunge inatambua uwepo wa Kamati za wabunge za vyama. Kimsingi, sina tatizo na uwepo wa kamati za vyama. Usongo wangu ni pale vikao hivi vinapotumika vibaya kupoka maslahi ya Umma kwa dhamira ya kudumisha maslahi ya "Status Quo." Ni katika vikao hivi wanasiasa wenzetu hawa wanadhihirisha Siasa Si Hasa. Wakileta "fyoko", huitwa kwenye vikao hivi na wakitoka ndani huwa kama wamemwagiwa maji ya barafu na ukiwasalimia pengine hata majibu wasikupe kwani wakionekana watahusishwa na wapinzani!

Tunachoambiwa ni kuwa Bunge letu limeiga utaratibu huu wa kisekta kutoka Bunge la India. Aidha, kanuni zetu nyingine zinatokana na kanuni za mabunge mengine ya Jumuiya ya Madola (Commonwealth) ikiwemo Bunge la Uingereza. Spika wetu ni Mwenyekiti wa Mabunge ya Jumuia ya Madola. Spika wetu ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM vilevile. Utajazia mwenyewe!

Ndiyo, tunaweza kudai kuwa Bunge letu linaongozwa na mfumo unaoitwa "Three Line Whip". Utaratibu huu unawezesha vyama vyenye wabunge kusimamia wabunge wake. Ni vyema ieleweke kuwa kwa wenzetu waliokomaa kidemokrasia huwathibiti Wabunge wao kwenye masuala ya sera tu na sio Uhuru na Haki yao kuhoji mienendo ya uendeshaji wa Serikali. Kwa Bunge letu, utaratibu huu unatumiwa kuwafunga Wabunge midomo. Hivyo, la msingi hapa ni Je? Mfumo huu wa Bunge una maslahi kwa Taifa letu au unang'ang'aniwa kudumisha maslahi na matakwa ya viongozi wakuu?

Pamoja na Bunge kuwa na mamlaka ya kujitungia kanuni zake yenyewe kwa mujibu wa kifungu namba 89(1) na (2) cha katiba ya nchi; kanuni hizi hazistahili kupoka uhuru wa msingi wa Kikatiba wa Bunge kusimamia Serikali. Wakati huo huo Kanuni hazistahili kupoka Uhuru na Haki za msingi za Kikatiba za Wabunge kutoa mawazo yao kwa uhuru bila kuathiriwa na mizengwe ya kamati za wabunge kama vyama vya siasa. Kadhalika hata vyama vyenyewe ambavyo tiketi zake zimewawezesha wabunge kuingia Bungeni havina haki kikatiba kupoka Uhuru wa kutoa mawazo wa wabunge wao.

Bila kujali msimamo wangu au ule wa Waheshimiwa Wabunge wenzangu wa Vyama vyetu vya Mageuzi (ambao kiukweli tunaburuzwa Bungeni kutokana na uchache wetu) wote tunastahili lawama labda kwa kutokazana kuwaambia Watanzania kwa kina jinsi Bunge letu leo lilivyofanywa mchezo wa Luninga.

Aidha, baada ya kutafakari kwa kina mwenendo wa Bunge tangu niingizwe na wale wapenzi wangu wa Hai (Mungu awabariki sana), leo nadiriki kusema kuwa ADUI namba moja wa maslahi ya Watanzania sio Serikali yao bali ni Wabunge wa Chama cha Mapinduzi ambao kwa udhaifu, woga na labda ubinafsi wao wanaruhusu Serikali yao iburuze Bunge wao wakiwamo!

Nasema hivyo kwa sababu wao ndio wengi bungeni na Katiba ya nchi imewapa Wabunge mamlaka yote ya kudhibiti Serikali. Aidha, kanuni hizi za Bunge zinazopoka madaraka yake zinapitishwa na wabunge hawa hawa wa CCM walio wengi Bungeni.

Kwa udhaifu huu wa Wabunge wa CCM, leo kimsingi Bunge haliwezi kubadilisha mipango yeyote ya Serikali. Uhuru kidogo wa mawazo na mapendekezo hutolewa katika kamati za Kisekta. Bunge letu leo lina Kamati Nane za Kisekta. Kila Mbunge anakuwa kwenye kamati mojawapo ya kisekta. Kamati hizi zina wastani wa wabunge 30 kila moja. Kwa mantiki hii basi anapata wasaa wa kunusa angalao kidogo moja ya nane ya shughuli za Serikali! We fikiria, Wataalam "waliobobea" wa Serikali hutayarisha bajeti zao kwa miezi kadhaa na kutayarisha "misaafu" ya maelezo. Kamati ya Kisekta ya Bunge hupitia "misaafu" hii kwa siku moja kwa kila Wizara na kisha utasikia "...Ipiteee!!!" Hapo utawaona wataalam wa wizara wakiangaliana na wakati mwingine kama kuonyeshana ishara kuwa Waheshimiwa hawa hawajui wafanyalo. Hata wakijua, Muda uko wapi?

Kundi hili la wabunge 30 likishapitisha bajeti ya Wizara Fulani kundi lingine lote la Wabunge zaidi ya 250 halina tena mamlaka ya kubadilisha chochote ila hubakia kuigiza mchezo wa luninga ambao hauna tofauti na porojo. Piga kelele hata upasuke koo; unafurahisha genge!

Hali hii imepelekea kuua ari ya wabunge ya kuchambua kwa kina mwenendo mzima wa Bajeti ya Serikali. Aidha hali hii imegeuza Bunge letu chanzo cha ajira na posho kuliko kufanya kwa dhamira yale umma wa Watanzania wangetegemea Bunge lao lifanye.

Kwa upande mwingine, Serikali kwa kujua Bunge lina meno ambayo yamegeuzwa ya plastiki hali heshimu tena Bunge. Inadhubutu kufanya maamuzi na kuletea Bunge kama taarifa. Aidha, hii inapelekea hata baadhi ya Mawaziri kujibu hoja za wabunge kwa dharau na kejeli wakati wa majumuisho ya wizara zao wakijua fika kuwa wabunge wanafanya kazi ya upambe na hawawezi kubadilisha chochote.

Serikali haikuomba Bunge ruhusa ya kununua ndege wala rada. Sio nia yangu kuingia kwenye hoja ya kama kweli ni kipaumbele sahihi kununua vifaa hivi vya bei mbaya kwa kuzingatia umaskini wetu. Ni nia yangu kuonyesha jeuri ya Serikali kudharau Bunge.

Suala la ndege limeletwa Bungeni kama taarifa kuwa Serikali ina mpango wa kununua ndege ya Rais na tayari imeshatenga fedha zake za ndani kiasi cha Tshs 7,000,000,000.00 kama malipo ya awali.

Wapinzani tulikataa katakata mpango huu na hata kutoka nje ya ukumbi wa Bunge. Wenzetu wa CCM walituzomea na hatimaye kuipitisha bajeti nzima ikiwepo mpango huu wa ndege kwa mbwembwe bila hata kuhoji masuala ya msingi kama thamani ya jumla ya ndege, aina ya ndege, itokako na inatakiwa kulipiwa kwa muda gani! Watanzania hili ndilo Bunge lenu mnalodaiwa kulipa ushindi wa kishindo kwa bao la kisigino.

Naomba niweke rekodi sawa. Ninaposema Wabunge wa CCM Watanzania wasifikiri hawa ni watu wasiwasi!

Hili ni kundi kubwa lenye wasomi wengi waliobobea kwenye fani mbalimbali. Vilevile linajumuisha Wazee kadhaa ambao wanaheshimika na jamii ya Watanzania kwani kwa nyakati kadhaa wamekuwa viongozi waandamizi katika Serikali yetu, CCM na Mashirika kadhaa ya Umma bila kusahau taasisi za kimataifa.

Ingekuwa wanakuja Bungeni na vyeti vyao basi ingehitajika masjala kubwa kuliko Bunge lenyewe kizihifadhi. Pamoja na taaluma zao na ukweli kuwa wanatoka miongoni mwa Watanzania ambao ni masikini sana, wenzetu hawa wamekubali kusindikiza hoja za Serikali kwa msemo wao wenyewe; nanukuu "mia kwa mia". Hebu fikiria: Anasimama mtu msomi aliyebobea anapongeza kwa dakika tano, kisha analalamika kwa dakika kumi na mwishowe anaunga mkono hoja asilimia mia kwa mia! Wenzake wanamshangilia! Kasheshe tupu! Hii ndiyo dhana nzima ya Bunge kuwa mchezo wa luninga.

Inaumiza na kusikitisha hali hii inapoendelea kila siku katika Bunge. Hoja za msingi hazionekani. Bunge letu leo linapenda kung'ang'ania vitu "trivial." Hivi kweli sakata la IGP Mahita lilihitaji kuwa hoja ya nguvu kiasi hicho kuliko hata suala la ndege na rada?

Hata wale watani zangu wanaojifanya wao ni wakereketwa sana; mnajua Chama Chenu cha CCM kinapata ruzuku zaidi ya milioni 750 kwa mwezi? Hii ni zaidi ya Shilingi za Kitanzania Bilioni Tisa! Yaani kwa tarakimu ni: Tshs 9,000,000,000.00 kwa mwaka. Je? Mlikwisha ona mapato na matumizi ya Chama chenu? Je? Ruzuku hii inawafikia huko Wilayani na Mikoani?

Nawauliza watani zangu hawa kwani wao ndio wenyewe wa kuomba na hata kulazimisha michango wakati Chama chao kikizoa mamilioni kila mwezi kwenye hazina ya nchi kwa kigezo cha ruzuku ya vyama vya siasa. Hapo ni bila kuongezea "Michango ya Hiari" kutoka kwa wafanyabiashara na asasi mbalimbali zinazobembeleza fadhila kwa gharama za walalahoi!

Kwa sisi Wabunge wa upinzani (bila kuwasahau wachache ndani ya CCM - ambao kamwe hawatajionyesha) kinachoendelea bungeni kinaweza kufananishwa na hali katika eneo la ajali. Katika maeneo ya ajali unaweza kumkuta mtu anakata roho na huna uwezo wa kumsaidia. Aidha, unachanganyikiwa unapomwona kibaka akijaribu kumpora mtu aliyezimia! Mengine utajaza mwenyewe.

Laiti wanamageuzi tena "Viongozi" na "wapenzi wa ruzuku" wangelijua ni mabilioni mangapi yanapotea nchi hii na upinzani ukishuhudia bungeni bila kuwa na uwezo wa kuzuia. Laiti wangejua hiyo chambo ya karoti wanayopewa ya vimilioni wastani wa 20 ni tone la maji baridi ndani ya bahari ya chumvi ili kuhalalisha "Wenzao" kuzoa mabilioni! Ndugu zangu wapinzani njaa isitupe ukomo wa kuona. Tusisahau kuna msemo usemao "Ukimwona adui akililia wembe ameze, mpe ni bwege"

Bunge leo linatumika kuhalalisha jeuri ya Serikali. Kila mara najiuliza : Inawezekanaje wasomi wa nchi hii wakawa "so timid"?

Napenda kuamini kuwa wengi wa wabunge wetu wa CCM wanajaribu kulipa fadhila ya kubebwa na Serikali wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2000. Aidha, sasa naamini adabu hii ya woga (kwa gharama ya Watanzania masikini) inatokana na tumaini la kurushiwa angalao kamkate kadogo kupitia kuteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali ikiwemo Uwaziri, wajumbe wa bodi na kadhalika!

Ni ukweli usiofichika kuwa wabunge wenzetu wa CCM wanathibitiwa vilivyo. Mkikutana pembeni hawaishi kulalamika kama vile hawajui upeo wa mamlaka yao waliyopewa na katiba ya nchi. Wanachoamini, Wanachoongea mtaani na wanachofanya Bungeni ni mbingu mbili tofauti.

Siku zote huwa nasema na ninajua msemo huu hauwafurahishi wahusika. "Penye udhia tia Rupia" Kwa vyama vya upinzani ni ruzuku kwa wabunge, ni nyongeza ya mishahara na posho, na kwa wananchi ni Takrima, mashati, fulana na kofia za kijani. Tusidanganyane na kibwagizo cha sera bwana! Kwa mtaji huu lazima watu wapete! Kweli umaskini huzaa umaskini na kujiondoa katika mzunguko huu kunahitaji kazi ya ziada na kujitoa mhanga kwa hali ya juu.

Bunge linafungwa wiki hii na Watanzania walio wengi wanajua kuwa hoja kubwa ya Bunge hili ilikuwa Mahita, Ukarabati wa Ikulu, Rada na Ndege! Sina hakika ni wangapi wanajua kuwa pamoja na majitapo yote ya serikali na jeuri yake ya kulazimisha matumizi ya ajabu ajabu bado kwa kiasi kikubwa inategemea misaada hata kwa kujilipa mishahara!

Sina hakika ni wangapi wanajua kuwa katika mwaka huu wa fedha Serikali yao itatumia zaidi ya shillingi Trillioni 2.2 kujiendesha? Kwa kuweka kwenye tarakimu ni sawa na: Tshs 2,219,212,000,000.00. Katika fedha zote hizi Shilingi bilioni 720 tu ndizo zitatumika kwa matumizi ya maendeleo ambapo kati yake Serikali yetu imechangia Shilingi bilioni 95.662 na wafadhili wamechangia Shilingi bilioni 624.465 kwa njia ya mikopo na misaada.

Hebu wenzetu wa vyombo vya habari sasa wasaidieni Watanzania kwa kuchambua kwa kina undani wa bajeti ya kila idara na Wizara za Serikali badala ya kuendeleza utamaduni uliozoeleka wa kuripoti "Mchezo wa Luninga."

Sasa niwarudie Watanzania na kwa maana hii Watanzania wote bila kujali itikadi zao za kisiasa. Ni lini tutajua kuwa tuna wajibu wa kushiriki "process" nzima ya kukomboa nchi yetu?

Ni lini mtajua kuwa kazi ya kujikomboa kutoka kwenye umaskini sio kazi ya wanamageuzi bali ya Watanzania wote wenye usongo kwa njaa na umaskini unaotukabili?

Ni lini tutajua kuwa Bunge letu ni Mchezo wa Luninga na kamwe kwa uwiano uliopo halitaweza kutetea maslahi ya wanyonge?

Ni lini ndugu zangu wapenzi wa ruzuku mtajua kuwa nguvu ya umma (People's Power) inashinda nguvu ya pesa, jeshi au dola?

Ni lini viongozi wetu watajua kuwa Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu?

Viongozi wa Serikali na CCM wanastahili kujua kuwa nchi hii imemwagiwa mafuta ya umaskini na majuto. Wananchi walio wengi sasa wanakosa tumaini. Mtu aliyekosa tumaini ni mbaya kuliko Simba aliyejeruhiwa.

Siku masikini hawa wa Tanzania tunaowadhihaki kila siku kwa propaganda ya amani na utulivu (wakati hawana amani ya aina yeyote kwenye kaya zao) watasema basi - mjue hakuna cha mswalie mtume.

Burundi, Rwanda, Siera Leone, Congo na hata Somalia yalianza kidogo kidogo viongozi wakaambiwa na wapambe wao kuwa wasijali, wamevaa suti za hariri na jeshi lina vifaa vya kisasa.

Nimalizie kwa Salaam kwa Mheshimiwa Rais. Ninakupongeza kwa mengi mazuri uliyofanya. Tumia muda wako uliobaki kuweka mazingira ya wewe kuingizwa katika vitabu vya historia ya nchi hii, Africa na Dunia nzima kama "Stateman" na sio "President."

Andaa mazingira mazuri ya kuwezesha uchaguzi ujao kuwa huru na haki kwa kuridhia mabadiliko ya msingi katika katiba yetu ambayo pamoja na mengine yatahusisha Tume huru ya Uchaguzi. Mhe. Rais hakikisha wagombea binafsi wanaruhusiwa ili nchi yetu ipate watu makini wa kushiriki utawala badala ya dhana potofu kuwa wanatakiwa wawe makada na watoke kwenye vyama vya siasa pekee!

Mhe. Rais, achia bunge lako madaraka ya kuthibiti Serikali. Kama Bunge litaachiwa Uhuru wake lifanye kazi bila mizengwe, nakuhakikishia ufanisi wa Serikali yako utaufurahia pamoja na wale wote wenye nia njema na nchi hii. Wasaidizi na wapambe wako wasikuchuuze. Wananchi wako tunataabika sana pamoja na matumaini lukuki yatokanayo na sera zako za kuboresha uchumi.

Maadam wewe ni sehemu ya Bunge, shauri uwepo wa kamati ya Bunge ya kushughulika na Rushwa na hii isimamiwe na wabunge wa vyama vya upinzani kama ilivyo Kamati ya Bunge ya Mahesabu ya Serikali. Tutakusaidia kazi hii ambayo inaonekana nzito sana kwako na wasaidizi wako.

Nawatakia Watanzania wote kila la Heri

Je mawazo yamebadilika?

Kweli Makamba ategemewe kusema nini?

Nini ambacho hakijulikani hadi sasa hapa tulipo kuhusu ufisadi wa ccm?

Nilipoona heading ya Thread nikadhani anakuja kuchangia hapa jf...Kumbe ni bungeni?

Sasa kama ni bungeni unapingana na mawazo ya awali kuwa bunge ni mchezo wa kuigiza.
 
Sura ya tatu.
Sekta ya uzalishaji.

31.Ili uchumi wa nchi yetu ukue kwa kiwango cha asilimia 10 ifikapo mwaka 2010 lazima angalau kilimo kifikie ukuaji wa angalau asilimia 20 ifikapo mwaka huo.Kwa lengo la kufikia kiwango hicho cha ukuaji wa kilimo ifikapo mwaka 2010 CCM itachukua hatua zifuatazo;

c)kwa utengenezaji na upatikanaji wa mikokoteni ya kuvutwa na wanyama na vinu vya kisasa vya kukobolea na kusagia nafaka.

Ntaendelea kuweka ilani juu ya kilimo.
 
Jmushi sijaelewa maswali yako hata kidogo, umeweka hiyo makala ya Mbowe na kunuliza maswali kana kwamba unawasiliana na aliyeandika makala husika.

Kwa taarifa zaidi ni kuwa sasa anachangia Nsanzuguanko na atafuatiwa na Mama Malecela then Makamba atafuata kuchangia kwa kina.
 
Hata wale watani zangu wanaojifanya wao ni wakereketwa sana; mnajua Chama Chenu cha CCM kinapata ruzuku zaidi ya milioni 750 kwa mwezi? Hii ni zaidi ya Shilingi za Kitanzania Bilioni Tisa! Yaani kwa tarakimu ni: Tshs 9,000,000,000.00 kwa mwaka. Je? Mlikwisha ona mapato na matumizi ya Chama chenu? Je? Ruzuku hii inawafikia huko Wilayani na Mikoani?

Jamani kama ni kweli ccm inapata bilioni tisa kwa mwaka(tena kwasasa inaweza kuwa zaidi)
Naomba yule mwenye data aweke hapa ili tujuwe ccm ina wanachama wangapi na tulinganishe na pesa hizo!
Hizo ni pesa nyingi sana...Halfu na maendeleo hakuna na huku serikali yenyewe ikiwa haifanyi kitu zaidi ya ufisadi.
Tunaomba namba ya wanachama wa ccm halafu tuangalie ni wananchama wangapi wamenufaika na ruzuku hiyo na pia tujuwe wananchi wasiokuwa na vyama walinufaika vipi na pesa zao hizo walizopewa ccm.
 
Jmushi sijaelewa maswali yako hata kidogo, umeweka hiyo makala ya Mbowe na kunuliza maswali kana kwamba unawasiliana na aliyeandika makala husika.

Kwa taarifa zaidi ni kuwa sasa anachangia Nsanzuguanko na atafuatiwa na Mama Malecela then Makamba atafuata kuchangia kwa kina.

Hapana..Ni makosa ya kiusomaji ama ya kimaandishi.
Nita verify...Nilikuwa namaanisha kusema hivi...Kieleweke eeh! Mbowe alishawahi kusema Bunge ni kama mchezo wa kuigiza na hivyo wewe kama kieleweke unapingana na kauli ya Mwenyekiti wako kuwa bunge halina mpango na hivyo haina maana sana kuwa Makamba atasema nini kwani yeye kama kada wa ccm ataifagilia tu!

Umesahahu hata bajeti ya kifisadi ilipitishwa na watu kama kina Killango na Chenge?

Sasa kama kimaamuzi ni kitu kimoja huko bungeni na kikauli kwenye press ni tofauti na za kiukali tutafika kweli?

Inawezekana kabisa wabunge wa ccm wameamuwa kutumia tactics nyingine kwa kujidai wako tofauti kwa kauli zao tata!

Lakini at the end of the day bajeti husika inapitishwa!

Hivyo kama tunajuwa uamuzi upi ni right..Then watakochesema hakitajalisha bali watakachoamuwa kwa kupiga kura zao huko bungeni.

Ni mawazo yangu tu..Ila pia tutaendelea kumsubiri kwani hapa ni jf na awe makini na kauli zake kwani tushamjuwa.

Cha muhimu ni..Je at the end of the day ni mwananchi MNUFAIKA?
 
Jmushi mbona hapa tunazungumzia tendo la kihistoria la mbunge wa viti maalum kuzungumza kwa mara ya kwanza tangu alipoteuliwa wewe unahamisha mjadala?

Umewahi kusoma espionage of writting?
Umewahi kupata elimu ya Mosad?

Mama Kilango anachangia na kutaka kujua ni kwanini kilimo chetu kipo butu ,anasema kuwa ni kukosekana kwa mbegu,mbolea,teknolojia. ila yeye atajikita zaidi kwenye kuunganisha kilimo na viwanda vya usindikaji na hilo ndio linatufanya tunakuwa nyuma kiasi hicho.

Kuna haja ya kujua huyu atasema nini kwani ilani yao imejipanga kukuza kilimo kwa asilimia 20 ifikapo 2010 sasa hiki ni kilimo kitakachokuwa kimekuwa kuliko popote pale duniani , kweli CCM kwa ilani hii wataweza kutufikisha nchi ya neema.
 
Jmushi mbona hapa tunazungumzia tendo la kihistoria la mbunge wa viti maalum kuzungumza kwa mara ya kwanza tangu alipoteuliwa wewe unahamisha mjadala?

Umewahi kusoma espionage of writting?
Umewahi kupata elimu ya Mosad?

Mama Kilango anachangia na kutaka kujua ni kwanini kilimo chetu kipo butu ,anasema kuwa ni kukosekana kwa mbegu,mbolea,teknolojia. ila yeye atajikita zaidi kwenye kuunganisha kilimo na viwanda vya usindikaji na hilo ndio linatufanya tunakuwa nyuma kiasi hicho.

Kuna haja ya kujua huyu atasema nini kwani ilani yao imejipanga kukuza kilimo kwa asilimia 20 ifikapo 2010 sasa hiki ni kilimo kitakachokuwa kimekuwa kuliko popote pale duniani , kweli CCM kwa ilani hii wataweza kutufikisha nchi ya neema.
 
Hana lolote huyu
atakaa kunukuu vifungu vya biblia na msaafu mahali ambapo apatakiwi references tena kwa makosa

Huyu ndio anaprove failure ya Kikwete, Mimi sijui Kikwete alikuwa akifikilia nini eti kumpa mpaka ubunge mtu kama huyu.

Nadhani Kikwete haelewi maana na umuhimu wa nafasi za ubunge wa kuteuliwa na ndio maana anatoa tu kwa watu ambao hawafanyi mambo yanayotakiwa kutokana na kuteuliwa kwao

Babah, hata hivyo vifungu vya Biblia na Kuran havijui ni mbabaishaji tu. Yeye na JK aliyekuwa mbele hajulikani.
 
Jamani jueni kuwa huyu ni mteuliwa wa Rais sasa kama mnaona hana lolote je?kumpa mpaka ukatibu mkuu ina maana kuwa alikosea ama ndio alimuona anafaa?


Ila pia ni aibu kwa huyu katibu mkuu wa chama kinachotawala kukaa ndani ya bunge kwa zaidi ya miaka miwili kukaa bila hata kuchangia huku akiwa ndio mwenye jukumu la kuhakikisha kuwa ilani ya chama chake inafuatwa na serikali iliyopo madarakani.

Tunasubiri kuona kama atailinda ilani juu ya kilimo ama atasema ya kwake.

Nawawekea ilani ilisema nini kuhusu kilimo punde.

Unashangaa, Rais mwenyewe ni bomu sasa unategemea nini. Enzi za Mkapa watu hatukuwa tunajadili jinsi gani kazi inamshinda bali ni jinsi gani mikataba anyoingia na the so called wawekezaji itatuaffact vipi. Lakini sasa kwa JK swala hilo sio periority tena kwa vile hata mwelekeo wa nchi hatuujui. Imagine Katibu wa CCM kuwa Makamba, kuna jipya hapo au ni kutafutiana mlo tu??????
 
Jmushi mbona hapa tunazungumzia tendo la kihistoria la mbunge wa viti maalum kuzungumza kwa mara ya kwanza tangu alipoteuliwa wewe unahamisha mjadala?

Umewahi kusoma espionage of writting?
Umewahi kupata elimu ya Mosad?

Mama Kilango anachangia na kutaka kujua ni kwanini kilimo chetu kipo butu ,anasema kuwa ni kukosekana kwa mbegu,mbolea,teknolojia. ila yeye atajikita zaidi kwenye kuunganisha kilimo na viwanda vya usindikaji na hilo ndio linatufanya tunakuwa nyuma kiasi hicho.

Kuna haja ya kujua huyu atasema nini kwani ilani yao imejipanga kukuza kilimo kwa asilimia 20 ifikapo 2010 sasa hiki ni kilimo kitakachokuwa kimekuwa kuliko popote pale duniani , kweli CCM kwa ilani hii wataweza kutufikisha nchi ya neema.

Haya tuone kama hilo tendo la kihistoria litaweza kubadili maigizo hayo ya bunge la ccm.

Tena makamba!

Tunasubiri kwa hamu kwasababu ni kweli issue ya kilimo na viwanda ni muhimu kupita kiasi...Just kama madini na utalii.

Sisi Watanzania ni matajiri na hivyo hapo ndipo kwenye pointi na kufikiri kuwa Makamba atatuletea neema ni ndoto!

Huyu mtu alimbusu Manji mnasema ana akili nzuri huyu?

Huyu ndiye Yusufu yule yule aliyejipatia umaarufu kwa kupenda kutowa mifano ya Biblia!

Ama kweli wajinga ndio waliwao.
 
Makamba ameanza kwa kusema kuwa amekaa kwa muda mrefu sana bila kusema kwani alikuwa shuleni, na kwa kuwa yeye amezoea kukaa kwenye mikutano ya pasua baba akifanya hivyo huko ataaibika.

Leo ndio anamshukuru rais kwa kumteua na anasema kuwa deni la fadhila ni kulipa fadhila, uteuzi wake ulikuwa ni fadhila za rais.

Anasema kuwa amesoma maandiko matakatifu kutoka kwenye biblia kuwa anayetamani uasikofu anatamani kazi njema ,na anayetamani usipika anatamani kazi njjema.

Anampongeza waziri mkuu ,anasema kuwa siku njema huanza mapema ,ameanza vizuri.ila anasema kuwa pengo la jino la dhahabu limezibwa kwa dhahabu.

Nabii Yeremia aliogopa sana ila akaambiwa kuwa atapewa maneno ya kusema na hivyo pinda hana sababu za kuogopa .

Anawapongeza wabunge kwa kuwa wanatekeleza ilani ya chama na anataka kuwatoa hofu kuwa wakiendelea namna wanavyoendelea sasa kazi yao 2010 ni rahisi sana.

Anasema kuwa atasema machache na sio makubwa sana, anaomba radhi kuwa mzee Ngombale alipokuwa anachangia alisema kuwa anampongeza rais kwa kuwa anasimamia ilani ya ccm.

Siku mbili baadae alisimama mbunge mwingine kwa staili ya waandishi na kusema kuwa haya tunayosema tunayaona,tuanayasikia, na tunayafanyia kazi ila kesho yake magazeti yaakaandika mzee Ngombale kitanzini.
unaweza ukawa na masikio lakini ukayaziba ukayatia hata na pamba ili usiyasikie mambo mazuri ambayo yanafanywa na ccm ,hata ukaambiwa kuwa pale dodoma panajengwa chuo kikuuu ukaweka kisogo wala usitake kuona, unaweza kukiona kitabu kizuri cha ilani ila usisikie, anachotaka kusema ni kuwa ukijua kulaumu sharti ujue kusifu ili wenzako wasikuone kuwa ni kilema kwani hata kwenye jimbo lako yapo ambayo yanafanyika .

baada ya kusema haya naona nimpongeze rafiki yangu wassira na naunga mkono hoja.

Humu ndani tuna mzee Ngombale aliandika maandiko mwaka 1972 kuwa siasa ni kilimo, kuna sera mbalimbali na azimio la iringa, atalitazama zaidi azimio la iringa la mwaka 1972, linasema kuwa watumishi wa kilimo hawawezi kuwepo kila kijiji wakati ulele wanapokuwa wanahitajika ila wanapaswa kuelekeza teknolojia ya kilimo.

Anasema kuwa kazi ya kwanza ya kiongozi ni kujifunza kanuni za kilimo hana uhakika wassira anajua vipi kilimo, ni rafiki yangu hatanipeleka popote.

Ukisoma hotuba ukurasa wa 20 anatuambia kuwa mwaka 2007 wataalamu wa kilimo waliajiriwa 337 ila lengo lilikuwa ni kuajiri 2500, ila anasema kuwa namna nziuri ya kufanya ni kuwa nchi hii ina viongozi wengi sana kuanzia shina,n.k, hivi ukilitazama shamaba la Lowassa linakuwa mfano?shamba la kapuya ni mfano? wabunge wenzangu tunaandika sana tunasema sana ila tatizo ni kuwa ugumu upo kwenye kutekeleza , tunakuwa kama mafarisayo ananukuu biblia na kuraan, enyi mlioamini mbona mnasema maneno ambayo hamtendi?wananchi wanatusikiliza hapa .

Sera za CCM zinasema kuwa serikali inapaswa kuwatambua wakulima kwa kuanzisha mashindano ya kilimo hivi yapo? tunawaenzi wakulima wetu?kila mtu akiandika anayasema ila wa kuyatekeleza hakuna?

Ilani ya uchaguzi 2005 inazungumzia tuzo ,zawadi kimikoa ...ananukuu ilani 31(b) .......
sura ya 9 ibara ya 132, anasema ipo mikoa ambayo imeonyesha mifano ila hawajapewa tija na zawadi.

amemaliza muda wake.
 
Anamhoji Waziri wa Kilimo mikoa iliyoongoza kwa uzalishaji wa mahindi imeopata tuzo gani wakati chama chake ndicho kinachounda serikali iliyopaswa kuyafikiria hayo. anataka nani amjibu? Kama anaona serikali iliyoundwa na chama chake haifanyi kazi inavyostahili si ivunjiliwe mbali?!
 
Makamba ameanza kwa kusema kuwa amekaa kwa muda mrefu sana bila kusema kwani alikuwa shuleni, na kwa kuwa yeye amezoea kukaa kwenye mikutano ya pasua baba akifanya hivyo huko ataaibika.

Leo ndio anamshukuru rais kwa kumteua na anasema kuwa deni la fadhila ni kulipa fadhila, uteuzi wake ulikuwa ni fadhila za rais.

Anasema kuwa amesoma maandiko matakatifu kutoka kwenye biblia kuwa anayetamani uasikofu anatamani kazi njema ,na anayetamani usipika anatamani kazi njjema.

Anampongeza waziri mkuu ,anasema kuwa siku njema huanza mapema ,ameanza vizuri.ila anasema kuwa pengo la jino la dhahabu limezibwa kwa dhahabu.

Nabii Yeremia aliogopa sana ila akaambiwa kuwa atapewa maneno ya kusema na hivyo pinda hana sababu za kuogopa .

Anawapongeza wabunge kwa kuwa wanatekeleza ilani ya chama na anataka kuwatoa hofu kuwa wakiendelea namna wanavyoendelea sasa kazi yao 2010 ni rahisi sana.

Anasema kuwa atasema machache na sio makubwa sana, anaomba radhi kuwa mzee Ngombale alipokuwa anachangia alisema kuwa anampongeza rais kwa kuwa anasimamia ilani ya ccm.

Siku mbili baadae alisimama mbunge mwingine kwa staili ya waandishi na kusema kuwa haya tunayosema tunayaona,tuanayasikia, na tunayafanyia kazi ila kesho yake magazeti yaakaandika mzee Ngombale kitanzini.
unaweza ukawa na masikio lakini ukayaziba ukayatia hata na pamba ili usiyasikie mambo mazuri ambayo yanafanywa na ccm ,hata ukaambiwa kuwa pale dodoma panajengwa chuo kikuuu ukaweka kisogo wala usitake kuona, unaweza kukiona kitabu kizuri cha ilani ila usisikie, anachotaka kusema ni kuwa ukijua kulaumu sharti ujue kusifu ili wenzako wasikuone kuwa ni kilema kwani hata kwenye jimbo lako yapo ambayo yanafanyika .

baada ya kusema haya naona nimpongeze rafiki yangu wassira na naunga mkono hoja.

Humu ndani tuna mzee Ngombale aliandika maandiko mwaka 1972 kuwa siasa ni kilimo, kuna sera mbalimbali na azimio la iringa, atalitazama zaidi azimio la iringa la mwaka 1972, linasema kuwa watumishi wa kilimo hawawezi kuwepo kila kijiji wakati ulele wanapokuwa wanahitajika ila wanapaswa kuelekeza teknolojia ya kilimo.

Anasema kuwa kazi ya kwanza ya kiongozi ni kujifunza kanuni za kilimo hana uhakika wassira anajua vipi kilimo, ni rafiki yangu hatanipeleka popote.

Ukisoma hotuba ukurasa wa 20 anatuambia kuwa mwaka 2007 wataalamu wa kilimo waliajiriwa 337 ila lengo lilikuwa ni kuajiri 2500, ila anasema kuwa namna nziuri ya kufanya ni kuwa nchi hii ina viongozi wengi sana kuanzia shina,n.k, hivi ukilitazama shamaba la Lowassa linakuwa mfano?shamba la kapuya ni mfano? wabunge wenzangu tunaandika sana tunasema sana ila tatizo ni kuwa ugumu upo kwenye kutekeleza , tunakuwa kama mafarisayo ananukuu biblia na kuraan, enyi mlioamini mbona mnasema maneno ambayo hamtendi?wananchi wanatusikiliza hapa .

Sera za CCM zinasema kuwa serikali inapaswa kuwatambua wakulima kwa kuanzisha mashindano ya kilimo hivi yapo? tunawaenzi wakulima wetu?kila mtu akiandika anayasema ila wa kuyatekeleza hakuna?

Ilani ya uchaguzi 2005 inazungumzia tuzo ,zawadi kimikoa ...ananukuu ilani 31(b) .......
sura ya 9 ibara ya 132, anasema ipo mikoa ambayo imeonyesha mifano ila hawajapewa tija na zawadi.

amemaliza muda wake.

Kwa hiyo hiyo alert yako ya Makamba ndiyo hiyo hapo juu?

Na maneno niliyoyasema dakika chache zilizopita si ndiyo hayo hapo juu!

Tena kwa ku NAKSHI kabisa....YUSUFU KWA MARA NYINGINE AMETOWA MFANO WA YEREMIA!

Hivi huyu jamaa ni mkristo ama msilam?

Maana matendo yake na maneno yake vinatofautiana!

Nadhani huyu ndiye aliyewajaza viongozi wa dini ujinga kuwa JK ni mpango wa Mungu.

Huu ni utapeli mtupu kwani makanisa hayo hayo yashamwalika RA na wachungaji pia kupokea RUSHWA!

Jamii imegeuza mwelekeo...Sasa ni Utanzania kwanza kabla ya dini wala kabila.

Na ujumbe wangu ni huu kwa viongozi wadini..Kama haki isipopatikana na JK akarudi madarakani..Basi nyie ni wasaliti MANABII WA UWONGO NA TUTAWACHOMA MOTO KABLA YA SHETANI MWENYEWE KUFANYA HIVYO HUKO JEHANAM!

Mlikuwa na ushawishi mkubwa sana na ndio maana ushindi ukawa wa Tsunami kwa sababu ya RUSHWA na unajuwa WACHUNGAJI NA MAASKOFU WENGI WENU NI MATUMBO TU NA THIS TIME YATAPASUKA KAMA JK AKIRUDI MADARAKANI NA UFISADI USIPOPATIWA UFUMBUZI NA HAKI KUTENDEKA!

Sasa hivi naandaa tu namna ya kuwamalizia mbali manabii wa Uwongo waliolifikisha Taifa letu hapa kwa unafiki na TAMAA!

VIONGOZI WA DINI WAMETUMIKA SANA KUIANGAMIZA TANZANIA HILO WAJUWE NA MAPINDUZI HAYATAWAACHA KAMA WASIPOFANYA KAZI INAVYOTAKIWA!

Kabla ya kujidai kwenda kuyaombea mapepo huko bungeni wengi wenu ni wa kuombewa hayo mapepo ya unabii wenu wa uongo yatolewe!

Taifa litafikiaje mahali kama hapa na sisi tuseme ETI TUNA VIONGOZI WA DINI?

Kungekuwa na viongozi hao wa dini wa kweli wenye kuijali jamii na wala si manyapara wa wakoloni wa kila aina...Basi Taifa lisingekuwa hapa lilipo!

NA PIA HILO BUNGE NALO KAMA LINGEKUWA LA MAANA LISINGEPITISHA HAYA MAAMUZI YOTE YA KIFISADI na sheria za kifisadi zilizovunja KATIBA YETU!

sHERIA ZILIZOAMULIWA NA bunge hilo mnalotaka tulisikilize!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom