Makamba atamba, mtoto wake lazima awe waziri....

ChingaMzalendo

Senior Member
Nov 9, 2008
192
3
Kama kawaida yake, katibu mkuu wa CCM mzee Yusuf Makamba amewaacha hoi viongozi wengine wa ngazi za juu wa chama hicho baada ya kusema kwamba yeye hazai wala halei mtoto asiye na akili. Akatoa mfano wa kijana wake January ambaye hakuwa na mpinzani.

Mzee huyo aliendela kusema kwamba, atashangaa sana iwapo mwanae hatapewa uwaziri kwani kijani huyo alikosa mpinzani kutokana na uwezo wake. Wanajamvini, ni kweli uyu mzee anaitendea nchi haki kwa matamshi kama haya?

Kwanini mtoto wake lazima awe waziri?
 
Huyu ni mzee wa majigambo. Nasikia mwanae alipooa Uchagani akaseme sasa na sisi tunatambulika kama watu tulioendelea.
 
JK akishinda, hiyo sitashangaa kwani nategemea hata First lady naye ataukwaa uwaziri wa watoto na .............., bado kinana anaweza kuwa waziri mkuu kwa akili za JK subirini muone.
 
Anachanganya akili na upendeleo + kununua wagombea wa upinzani + kulamba miguu ya mafisadi aka RA hajui kwamba political career if any ya mwanae ni very short lived? inaweza ikaingia kaburini october 31. .

Kuwa na akili kwa track record gani? ya kubeba mifuko ya JK? ingekua tofauti angekua ana experience ya kufanya kazi na watu wenye akili leo hii ndio maana waziri pinda yuko pale angekua karani wa JK mnadhania angekua wapi? walitaka ku joy ride kwa Kamuhambwa speech aandike Seth sifa wampe mwanao tunamjua tangu Galanos hana kitu ni wa kawaida tu sana wata ji fool kwa muda mfupi labda kwa vile baba yao na elimu duni kadumu hapo hureey witch cfraftship!
 
Mpaka makamba kafikia hatua ya kusema haya then this was a long term plan, hawa jamaa wanataka kuimilikisha hii nchi, wana kauli za kukinzana sana, Rais alisema bashe si raia, Waziri anayeriport kwa rais akasema bashe raia, hatujui wa kumuamini so far, si rais wala mawaziri. Hawako organized, wanapeana vyeo pasi na kuangalia utendaji wao wa kazi ila kujuana na kufahamiana zaidi, wengi wao wana elimu za junction of disjunctionctions.

Koz kasema hatashangaa so am sure kama JK ataukwaa urais for the next 5 years then January atakua waziri na hata kama sio waziri then naibu waziri, ila sio kwamba anaweza kiutendaji ila basi tu nae apate KULA, na aendelee kulinda Maslahi yao. Tusipokua makini kizazi kijacho kitakua hakina pa kushika. hakutakua na uwezo wa kubridge gap kati ya masikini na matajiri. nchi kuongozwa kwa kufuata ma ukoo ya viongozi ni upuuzi mtupu.......

mwisho wa yote sijui utakuwa vp?????.......mungu atusaidie sisi na vizazi vyetu........
 
Kama kawaida yake, katibu mkuu wa CCM mzee Yusuf Makamba amewaacha hoi viongozi wengine wa ngazi za juu wa chama hicho baada ya kusema kwamba yeye hazai wala halei mtoto asiye na akili. Akatoa mfano wa kijana wake January ambaye hakuwa na mpinzani.

Mzee huyo aliendela kusema kwamba, atashangaa sana iwapo mwanae hatapewa uwaziri kwani kijani huyo alikosa mpinzani kutokana na uwezo wake. Wanajamvini, ni kweli uyu mzee anaitendea nchi haki kwa matamshi kama haya?

Kwanini mtoto wake lazima awe waziri?

Makamba ni mgonjwa tena karibia anaanza kuokota makopo. Mtu mzima anaropoka utafikiri mwenda wazimu. Sasa January kilaza awe waziri wa nini? waziri wa Clouds FM? atakuwa kama dada na baba yake mpayukaji? kwanza mwamvita si alikuwaga mnenguaji, kwa sababu alikuwa akizurura sana na watu wa mabendi! mara kawa mkurugenzi Vodacom na uzoefu gani wa kazi? January pia Ikulu kwa uwezo gani alonao? Hili kundi la kikwete na Makamba waondoe familia zao kwenye uongozi wa nchi. Miraji anavuta unga yeye hana mambo mengi. Tatizo ni Salma Kikwete, Ridhiwani na January Makamba.

Heri ya Ridhiwani, kwa sababu anajua fika kwamba akili hana na anatumiwa ilhali hajui. Hau hawa watu wanaogopa Slaa akichukua nchi wataingiwa lupango? basi wasubiri waanze kupigwa mawe

January hana uwezo wa kuwa waziri. Speeches (Hotuba) za kikwete zilivyombovu uwezo wa kuongoza wizara atoe wapi, au kwa sababu nchi ni mali ya baba na kikwete ndo kila kitu apewe? jimboni baada ya kufanyiwa ufisadi na kuwannunua upinzani ulitosha siyo uwaziri. Akijaribu tu, nchi kwisha. Kikwete asituchezee kabisa sisi siyo watoto na nchi siyo mali yake. Kuna vijana makini mno kuliko January, Wakina Mwanakijiji, Nyani Ngabu, Dr. Hildebrand Shayo, John Mashaka na wengine wengi makini wapo wametulia, ambao wana uwezo mkubwa wa kuongoza bila shida lakini siyo January.

Blog yake aliiba articles za watu akadai zake, speeches za kikwete anadesa iwe kuongoza wizara? huyu mzee makamba kalewa. Madhambi yake yaliyomfanya afukuzwe uwalimu ukuu asilete kwenye uongozi wa nchi. Haki ya nani, Kikwete na Makamba wakiendeleza kuingiza familia zao kwenye uongozi wa nchi, nchi itapasuka kesho. hii ndio dalili ambayo tunaiona sasa hivi
 
Atakuwa waziri kivuli wa nishati na madini Bungeni kwenye kambi ya upinzani itakayo onngozwa na chama kikuu cha upinzani Bungeni CCM.
 
mh!Hiki ni kituko cha mwaka,mbona kuna wana CCM competent wengi sana,kwani kuna ulazima gani Januari Makamba awe waziri?Na kwa kuwa JK si mtu makini basi haya yatatokea,nyinyi subirini tu!
 
Kama kawaida yake, katibu mkuu wa CCM mzee Yusuf Makamba amewaacha hoi viongozi wengine wa ngazi za juu wa chama hicho baada ya kusema kwamba yeye hazai wala halei mtoto asiye na akili. Akatoa mfano wa kijana wake January ambaye hakuwa na mpinzani.

Mzee huyo aliendela kusema kwamba, atashangaa sana iwapo mwanae hatapewa uwaziri kwani kijani huyo alikosa mpinzani kutokana na uwezo wake. Wanajamvini, ni kweli uyu mzee anaitendea nchi haki kwa matamshi kama haya?

Kwanini mtoto wake lazima awe waziri?

Nimefurahishwa na hizo bold &/red,
Kwanza huyu mzee ni "Prophet of doom" kama kawaida hasemi yale ambayo hayapo japo ni mropokaji. Pili huyu Kijana wake wamemwandaa wenyewe (CCM)achukue jimbo la Mzee shelukindo maana huyu jamaa alishakuwa si "Mwenzetu"
Suala la mwanaye kuwa waziri japokuwa hana uzoefu, hii ndo hali ya Tanmzania ya leo na tutegemee hayo na vituko vingi zaidi. Kwa kifupi anapiga ndogondogo. Na huyu Dr. wa heshima JK atamsikiliza tu maana yeye Yusuf alimsikiliza pale aliposema "Mzee unikumbuke katika ufalme wako" na akampa hicho kiti.

Kwa suala la kuitendea hhaki nchi, Mtazamo wangu kama mwana jamvi ni kwamba JK pamoja na wafuasi wake wote na mashabiki na wapenzi wake wote HAWAITENDEI HAKI NCHI HII KABISA.
Na kama Yusuf yeye anacheza mziki kutokana na beat zilizopo hawezi kucheza reggae wakati iliyopo ni bongo fleva.

Mbona Mwalim Salma, wakili Ridhiwan na wengine pia wapo hivyo hivyo

TUHAMASISHE WATU WAKAPIGE KURA! HASA WENYE MTAZAMO WA KIMAENDELEO!!
TUTAZAMA NCHI HII SIKU ZIJAZO:smow:
 
Kikwete ndiye kiongozi mpuuzi Tanzania imewahi kupata, kwa hiyo msishange huyu January akipewa uwaziri. Hii nchi inaendeshwa na kichwa cha mwenda wazimu.

Yaani sijui mtu mppuuzi kama yule alipatapateje urais, nashindwa kabisa kuelewa, hadi wakina ridhiwani , makamba, salma na hata mvuta unga miraji ndio waendeshe nchi
 
Polepole wandugu, nini kupoteza nguvu kumjadili Pwagu? subirini na Pwaguzi naye atatoka na lake
 
Nje ya mada kidogo:

Huyu mleta thread (ambaye huenda amechangia kwene thread hii kwa ID tofauti) naona amegombana na January huko kwene mishemishe zao sasa anataka kulipizia JF..lakini hii ndio spirit mpya ya JF, uwongo, upuuzi na hoja legelege. Kuna kipindi hapa alikuwa akiwatetea kwa nguvu zote akina Shayo, Makamba,Michuzi na Mashaka et al (huenda ni mmojawao hapo) kuwa ni watu makini blah blah blah, lakini sasa all over sudden ati January ni kilaza! lol

Mie yangu macho..
 
Mzee huyo aliendela kusema kwamba, atashangaa sana iwapo mwanae hatapewa uwaziri kwani kijani huyo alikosa mpinzani kutokana na uwezo wake. Wanajamvini, ni kweli uyu mzee anaitendea nchi haki kwa matamshi kama haya? Kwanini mtoto wake lazima awe waziri?


Usiwe na shaka kwa sababu january makamba atakuwa waziri kivuli kwenye serikali ya CCM ndani ya upinzani itakayoundwa na Mheshimiwa Peter Pinda
 
Back
Top Bottom