Asha Abdala
JF-Expert Member
- Mar 21, 2007
- 1,130
- 44
Makamba aingizwa mjini CCM Tanga
Na Maingwa Mohamedi, Tanga
Na Maingwa Mohamedi, Tanga
WAASISI wa Chama cha Mapinduzi (CCM) jijini hapa wameeleza kusikitishwa kwao na kitendo cha Katibu Mkuu Yusuph Makamba kuwapokea na kuwaapisha wanachama hewa alipofanya ziara mkoani wa Tanga hivi karibuni.
Wamesema wamegundua kuwa viongozi wa chama hicho kutoka wilaya mbalimbali walilazimika kutumia mbinu za udanganyifu ili kumridhisha Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga Idd Amme ambaye aliwaagiza kuleta wanachama wapya.
Wazee hao walitoa madai hayo jana walipokuwa wakizungumza na mwaandishi wa habari hizi mara baada ya kumalizika kwa mkutano na ziara ya Katibu Mkuu wa CCM mkoani hapa.
Wazee hao walidai kuwa wanachama waliyopokelewa na Makamba katika uwanja wa Tangamano jijini hapa kuwa kwanatoka upinzani ni hewa.
Wanasiasa hao walisema hayo wakati wakiichambua taarifa iliyotolewa kwamba wanachama 12,000 kutoka vyama vya upinzani wamejiunga na CCM na kumtaka Makamba kuwapokea na kuwakabidhi kadi mpya za uanachama.
Walisema kitendo alichofanyiwa Makamba ni utapeli wa kisiasa kutokana na ukweli kwamba hakuna kazi ya siasa iliyofanywa na viongozi hao na kuwawezesha kupata wananchama wapya 12,000 waliojiunga kutoka vyama vya upinzani kujiunga na Chama hicho.