Elections 2010 Makamba aanza zogo jipya

nickname

JF-Expert Member
Dec 20, 2009
544
147
Makamba2%286%29.jpg

Yusuf Makamba
Baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupoteza majimbo 53 ya ubunge katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu, Katibu Mkuu wake, Yusuf Makamba sasa ameamua kila mgombea ubunge na udiwani aliyeshindwa afungue kesi ya kupinga matokeo.


Hatua hii inayotafsiriwa kama kukutaa kutambua matokeo ya uchaguzi wa wabunge na madiwani, inathibitisha mtikisiko ndani ya chama hicho na wagombea wote walioshindwa wa ubunge na udiwani wametakiwa kufungua kesi mahakamani katika kipindi cha siku 30 kuanzia kutangazwa kwa matokeo hayo.

NIPASHE ina taarifa za barua ya siri iliyoandikwa na Makamba kwenda kwa Makatibu wote wa CCM nchini ikiwataka wagombea wote wa CCM walioshindwa uchaguzi, kufungua kesi mahakamani.

Barua hiyo ambayo NIPASHE imeiona yenye kumbukumbu namba CCM/OND/636/VOL.11/122 iliyoandikwa Novemba 9, 2010, ikiwa imesainiwa na Makamba na inaonyesha kuwa ilipokewa na makatibu wa CCM wa mikoa.

Katika barua hiyo, Makamba anawataka wagombea wa ubunge kufungua kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania huku wagombea udiwani walioangushwa kwenda kufungua kesi katika mahakama za mahakimu wakazi ndani ya siku 30, tangu ulipofanyika uchaguzi huo Oktoba 31, mwaka huu.

Makamba anawaagiza makatibu wa CCM wa mikoa kwa kushirikiana na makatibu wa CCM wa wilaya na kata kuwasaidia wagombea hao walioshindwa kwenye uchaguzi kuandaa hoja za malalamiko na vielelezo kwa ajili ya kupeleka mahakamani.

Aidha, Makamba ameagiza kuwa baada ya hoja hizo za malalamiko kukamilika zipelekwe katika ofisi ndogo ya CCM jijini Dar es Salaam au kuwasiliana moja kwa moja kwa mawakili ambao ni makada wa CCM ili kuandaa hati za malalamiko ndani ya muda huo.
“Kwa barua hii, mshirikiane na makatibu wa CCM wilaya/kata na wagombea husika kuandaa hoja za malalamiko na vielelezo/ushahidi na kuwasilisha CCM ofisi ndogo Dar es Salaam au kuwasiliana na mawakili ambao ni makada wetu moja kwa moja ili kuandaa hati za malalamiko ndani ya muda huo,” ilisema sehemu ya barua hiyo ya Makamba.
Katika barua hizo, Makamba pia amewaahidi wagombea wasiokuwa na uwezo wa kifedha kuwa chama kitachangia gharama za mawakili ili kuwasaidia kufanikisha azma hiyo.
“Chama Cha Mapinduzi Makao Makuu kitachangia gharama za mawakili kwa wagombea ambao hawana uwezo wa kifedha,” ilisema sehemu ya barua hiyo.

Katibu huyo wa CCM Taifa anahitimisha barua yake kwa kuwataka makatibu wa CCM wa mikoa kusimamia ipasavyo maagizo hayo ili kuhakikisha kuwa kesi hizo zinafunguliwa mahakamani.

Akizungumzia barua hiyo,Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilaya ya Mbeya Mjini, John Mwambigija, alisema shinikizo hilo la CCM kwa wagombea wake kukimbilia mahakamani linaonyesha kuwa chama hicho kinataka ushindi wa nguvu badala ya kuridhika na maamuzi ya wananchi.

Alisema kwa kuwa chama hicho kina fedha nyingi, kinataka kuzitumia kuzima demokrasia, na ndiyo sababu kubwa ya kuwataka wagombea wake walioangushwa kwenye uchaguzi kukimbilia mahakamani huku kikiwaahidi kuwasaidia gharama za kuendesha kesi.
Uchunguzi umebainisha kuwa baada ya agizo hilo kuwafikia mmoja wa viongozi wa CCM wa Wilaya ya Mbeya Mjini, ameonekana akiwaita wagombea wa udiwani walioshindwa akiwataka wakafungue kesi mahakamani....

Source : NIPASHE 20th Novemba 2010
 
Janja ya nyani iyo wanataka dissolve move ya CDM ili kuwe na mikesi mingi alafu mahakama ianze fanya madudu,kama mna evidence then wakafungue kesi
 
Changamoto kubwa kwa nchi yetu ni kwamba na mahakama nazo ni kama mbwa wa polisi anayefanya kazi kulingana na maagizo ya bosi wake bila kujali impact ya maagizo hayo anayopewa na bosi. Kama Makamba amefikia uamuzi wa kutumia hela ya chama kuwasaidia wagombea kufungua kesi, basi si ajabu tayari keshawasiliana na mahakimu wote kuhakikisha kwamba angalau nusu ya wabunge walioshindwa wanaingia bungeni. Hapa ndipo watu watakapoona ni bora kufa kuliko kuishi maisha yenye mashaka kutokana na ujambazi huu wa CCM.
 
Makamba ni mwehu hata CCM wanajua hilo anataka kuibua mgogoro mwingine na wananchi kama CCM wana pesa nyingi kiasi hicho wazielekeze kwawananchi masikini ziwaletee maendeleo badala ya kuzitumia kwa mambo ya hovyo kama hayo
 
kwa kiasi fulani au chote, kuchukiwa kwa JK na wana-ccm wenzake na wananchi wengine kunachangiwa na huyu mzee. Kauli zake zimekuwa za kukera kila wakati.
 
Hizi ni dalili za udikteta na zinadhihirisha kwamba CCM haikukubali kwa dhati mfumo wa vyama vingi. Hata kwa Tume ya Uchaguzi kulazimishwa na Serikali iliyoiteua, kuchakachua matokeo ya uchaguzi na kura zilizopigwa na Watanzania, kuhakikisha Mgombea wa u-Rais wa CCM anaibuka mshindi ni dalili kwamba hawa watu bado hawakubali demokrasia ya dhati.

Ubaya zaidi ni kwamba wengi wa majaji na mahakimu wanajali kazi zao zaidi ya haki kwa wananchi, kwa hiyo watakubali kutengua uchaguzi ili waendelee na mwajiri wao Kikwete/Makamba. This is traversty of justice and democracy. There is a curse on Tanzania, by the fact that cadres like Makamba are tolerated and paid from public funds.

Imagine the flood of cases in the courts of all madiwani (councillors) in Mwanza, Arusha, Moshi, Mbeya, Dar es Salaam and other areas where CCM lost to opposition parties. Imagine the number of cases to be started by the CCM cadres who were defeated in the parliamentary constituencies; about 80. Makamba promises financial assistance to pay lawyers for all these, out of funds acquired from EPA and illegal moneys in the accounts of CCM. I repeat this is traversty of justice and democracy. Shame on us all if Tanzanians accept this willy nilly.

I have never heard of a ruling party agreeing to an election in which other parties take part, and then afterwards decides to challenge all those who defeated their candidates. This may be a suitable case to submit to the International Court of Justice.
 
Chadema na cuf na wao wafungue kesi mahakamani ktk baadhi ya majimbo ambayo ccm ni dhahiri ilichakachua.
 
Makamba2%286%29.jpg

Yusuf Makamba
Baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupoteza majimbo 53 ya ubunge katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu, Katibu Mkuu wake, Yusuf Makamba sasa ameamua kila mgombea ubunge na udiwani aliyeshindwa afungue kesi ya kupinga matokeo.


Hatua hii inayotafsiriwa kama kukutaa kutambua matokeo ya uchaguzi wa wabunge na madiwani, inathibitisha mtikisiko ndani ya chama hicho na wagombea wote walioshindwa wa ubunge na udiwani wametakiwa kufungua kesi mahakamani katika kipindi cha siku 30 kuanzia kutangazwa kwa matokeo hayo.

NIPASHE ina taarifa za barua ya siri iliyoandikwa na Makamba kwenda kwa Makatibu wote wa CCM nchini ikiwataka wagombea wote wa CCM walioshindwa uchaguzi, kufungua kesi mahakamani.

Barua hiyo ambayo NIPASHE imeiona yenye kumbukumbu namba CCM/OND/636/VOL.11/122 iliyoandikwa Novemba 9, 2010, ikiwa imesainiwa na Makamba na inaonyesha kuwa ilipokewa na makatibu wa CCM wa mikoa.

Katika barua hiyo, Makamba anawataka wagombea wa ubunge kufungua kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania huku wagombea udiwani walioangushwa kwenda kufungua kesi katika mahakama za mahakimu wakazi ndani ya siku 30, tangu ulipofanyika uchaguzi huo Oktoba 31, mwaka huu.

Makamba anawaagiza makatibu wa CCM wa mikoa kwa kushirikiana na makatibu wa CCM wa wilaya na kata kuwasaidia wagombea hao walioshindwa kwenye uchaguzi kuandaa hoja za malalamiko na vielelezo kwa ajili ya kupeleka mahakamani.

Aidha, Makamba ameagiza kuwa baada ya hoja hizo za malalamiko kukamilika zipelekwe katika ofisi ndogo ya CCM jijini Dar es Salaam au kuwasiliana moja kwa moja kwa mawakili ambao ni makada wa CCM ili kuandaa hati za malalamiko ndani ya muda huo.
"Kwa barua hii, mshirikiane na makatibu wa CCM wilaya/kata na wagombea husika kuandaa hoja za malalamiko na vielelezo/ushahidi na kuwasilisha CCM ofisi ndogo Dar es Salaam au kuwasiliana na mawakili ambao ni makada wetu moja kwa moja ili kuandaa hati za malalamiko ndani ya muda huo," ilisema sehemu ya barua hiyo ya Makamba.
Katika barua hizo, Makamba pia amewaahidi wagombea wasiokuwa na uwezo wa kifedha kuwa chama kitachangia gharama za mawakili ili kuwasaidia kufanikisha azma hiyo.
"Chama Cha Mapinduzi Makao Makuu kitachangia gharama za mawakili kwa wagombea ambao hawana uwezo wa kifedha," ilisema sehemu ya barua hiyo.

Katibu huyo wa CCM Taifa anahitimisha barua yake kwa kuwataka makatibu wa CCM wa mikoa kusimamia ipasavyo maagizo hayo ili kuhakikisha kuwa kesi hizo zinafunguliwa mahakamani.

Akizungumzia barua hiyo,Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilaya ya Mbeya Mjini, John Mwambigija, alisema shinikizo hilo la CCM kwa wagombea wake kukimbilia mahakamani linaonyesha kuwa chama hicho kinataka ushindi wa nguvu badala ya kuridhika na maamuzi ya wananchi.

Alisema kwa kuwa chama hicho kina fedha nyingi, kinataka kuzitumia kuzima demokrasia, na ndiyo sababu kubwa ya kuwataka wagombea wake walioangushwa kwenye uchaguzi kukimbilia mahakamani huku kikiwaahidi kuwasaidia gharama za kuendesha kesi.
Uchunguzi umebainisha kuwa baada ya agizo hilo kuwafikia mmoja wa viongozi wa CCM wa Wilaya ya Mbeya Mjini, ameonekana akiwaita wagombea wa udiwani walioshindwa akiwataka wakafungue kesi mahakamani....

Source : NIPASHE 20th Novemba 2010


Huyu mzee Makamba mimi nina wasiwasi na halmashauri yake ya ubongo naona heri akapimwe akili.
 
Kama CCM ina fedha nyingi kwa nini wasitumie hizo fedha kuwavutia wananchi wakipende? Simple logic...ningekuwa mimi ni katibu mkuu wa CCM ningekaa na wenzangu tukajadili kuhusu miradi itakayowasaidia wananchi moja kwa moja.Tukaandika Project Plan tofauti na Ilani ya chama,hiyo project plan ni kuhusu kuanzisha miradi nchi nzima inayowagusa wananchi moja kwa moja ikawapatia vijana na wakinamama ajira na kuweza inua vipato vya wananchi.

Moja ya malengo ya miradi hiyo ni kuongeza pato la chama,kuwapatia ajira wanawake na vijana ambao ndio wapiga kura wengi na kuongeza imani ya wananchi kwa CCM.

CCM ina fedha nyingi, Project Plan ikishapitishwa na Kamati Kuu basi ;miradi ya chama inaanza mara moja.Baada ya miaka 2 hadi mitatu maisha ya wananchi yanainuka na wananchi wengi wanaanza kuipenda CCM na hata hao wabunge walioshindwa watashinda kiulaini uchaguzi unaofuata.


Lakini kwa sababu cheo cha Ukatibu na vyeo vingi ndani ya CCM na serikali ni vya kupeana basi hata walio na akili pungufu wanapata uongozi na ni hao kina Ma kamba watakaoleta machafuko hapa Tanzania Makaamba hafai kabisa ubongo wake zero kabisa
 
Makamba bado utakuna kichwa zaidi; hapo ni mwanzo tu; kumbe mkuki mtamu kwa nguruwe...losers
 
Back
Top Bottom