Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,886
- 6,883
Mungi watu hawataki kwenda Dar es Salaam makao makuu! Huko kila mtu ni mkubwa. Wewe kwa mfano utoke kuwa RPC mwanza (yaani IGP wa Mwanza) halafu uhamishiwe sijui kuwa mkuu wa kitengo makao makuu! Nani anataka hiyo ukiamka IGP huyu hapa, ukigeuka DCI huyu hujakaa sawa Waziri huyu kabla hujajipanga sijui Mkurugenzi gani huyu; nani anataka hiyo?
Ukiwa mkoani wewe na mkuu wa mkoa tu basi hakuna kingine. Budget ya mkoa yako kama mkoa una madini kesi zinaanzia kwako na makandokando mengine kibaaaao.
Wachache wetu ndio wenye kuwa na uelewa wa kiwango chako, wengine wanaangalia majina ya vyeo bila kuangalia nafasi zipi zinazompa mtu mafao na heshima zaidi kwa kiwango ambacho anaonekana ndiye mkuu wa juu kabisa katika himaya yake.
Pale mkoani alikuwa ndiye mwenye maamuzi na mtendaji mkuu katika mambo ya usalama katika mkoa mzima. Niambieni huko Dar atamwamrisha nani maana ofisi yake imezungukwa na wazito zaidi yake ambao anatakiwa kuwapigia saluti na shikamoo kulinda kitumbua chake.
Pale makao makuu kila anachofanya anatazamwa na kufuatiliwa tofauti na mkoani yeye ndiye yeye, na mkoani ni mmojawapo wa wakuu wa juu mkoani kama Mkuu wa mkoa, Mkurugenzi wa Maendeleo wa Mkoa na RPC. Huko nani atampa nafasi hiyo wakati vizito akina Mwema wapo?
Wasiojua maana ya demotion by promotion tuwaache na utetezi wao, vinginevyo ni kumpigia mbuzi gitaa.