Makamanda Polisi Mikoa Arusha na Mbeya wateremshwa vyeo

Mungi watu hawataki kwenda Dar es Salaam makao makuu! Huko kila mtu ni mkubwa. Wewe kwa mfano utoke kuwa RPC mwanza (yaani IGP wa Mwanza) halafu uhamishiwe sijui kuwa mkuu wa kitengo makao makuu! Nani anataka hiyo ukiamka IGP huyu hapa, ukigeuka DCI huyu hujakaa sawa Waziri huyu kabla hujajipanga sijui Mkurugenzi gani huyu; nani anataka hiyo?

Ukiwa mkoani wewe na mkuu wa mkoa tu basi hakuna kingine. Budget ya mkoa yako kama mkoa una madini kesi zinaanzia kwako na makandokando mengine kibaaaao.

Wachache wetu ndio wenye kuwa na uelewa wa kiwango chako, wengine wanaangalia majina ya vyeo bila kuangalia nafasi zipi zinazompa mtu mafao na heshima zaidi kwa kiwango ambacho anaonekana ndiye mkuu wa juu kabisa katika himaya yake.

Pale mkoani alikuwa ndiye mwenye maamuzi na mtendaji mkuu katika mambo ya usalama katika mkoa mzima. Niambieni huko Dar atamwamrisha nani maana ofisi yake imezungukwa na wazito zaidi yake ambao anatakiwa kuwapigia saluti na shikamoo kulinda kitumbua chake.

Pale makao makuu kila anachofanya anatazamwa na kufuatiliwa tofauti na mkoani yeye ndiye yeye, na mkoani ni mmojawapo wa wakuu wa juu mkoani kama Mkuu wa mkoa, Mkurugenzi wa Maendeleo wa Mkoa na RPC. Huko nani atampa nafasi hiyo wakati vizito akina Mwema wapo?

Wasiojua maana ya demotion by promotion tuwaache na utetezi wao, vinginevyo ni kumpigia mbuzi gitaa.
 
Venance Tossi amestaafu kazi ya polisi. Sasahivi ameajiriwa kwa mkataba na Tanapa akiongoza kikosi cha Rangers (askari wa wanyamapori).
Mwita Maranya yaani Tossi ameajiriwa tena baada ya kulitumikia Taifa miaka yote hiyo? Ina maana hakuinuliwa mgongo kiasi kwamba akapumzike na kusubiri kukutana na mola wake? Miminilifikiri baada ya kutupatia utumishi uliotukuka basi huyu Kamanda angekuwa anakula pension yake kwa mbwembwe bila tena kutakiwa kutoa report kwa mtu yeyote. Kumbe bado anapambana na majangiri waliomuua George?

Kuna siku nimemuona kwwenye taarifa ya habari nikadhani alipelekwa tu na Polisi kwa kazi maalumu kumbe anatumika. Lakini mimi kama nilimuona NCA (Ngorongoro Conconservation Area) kumbe yupo TANAPA?
 
Last edited by a moderator:
Kwa uelewa wangu mdogo cheo cha Mkuu wa Utawala na Rasilomali watu ktk Jeshi letu la Polisi siyo kikubwa kwa madaraka tu bali hata rushwa anayopokea mwenye hiki cheo ni kubwa kulinganisha na RPC wa mikoa! Huyu ni mungu mtu ktk jeshi la polisi! Nadhani amechukua nafasi ya kamishina Mtweve kama sikosei. Acheni mchezo na hiyo nafasi!

Asante sana Mkuu timbilimu...........

unajua watu wapenda udaku.......na story za gogovivu ndio huja na maneno kama haya............

.............Pale mkoani alikuwa ndiye mwenye maamuzi na mtendaji mkuu katika mambo ya usalama katika mkoa mzima. Niambieni huko Dar atamwamrisha nani maana ofisi yake imezungukwa na wazito zaidi yake ambao anatakiwa kuwapigia saluti na shikamoo kulinda kitumbua chake.

Pale makao makuu kila anachofanya anatazamwa na kufuatiliwa tofauti na mkoani yeye ndiye yeye, na mkoani ni mmojawapo wa wakuu wa juu mkoani kama Mkuu wa mkoa, Mkurugenzi wa Maendeleo wa Mkoa na RPC. Huko nani atampa nafasi hiyo wakati vizito akina Mwema wapo?

......hizi ni story za kusimuliwa.........halafu wanakurupuka kutumia misemo sehemu ambayo haihusiki kama......eti...

.............. demotion by promotion.......

not relevant......at all kwa kesi ya akina Kamanda Andengenye............

..........unajifanya unajua wakati hajui kuwa hajui..........ni bora ukafanya kuuliza/utafiti ili ueleweshwe....na sio kuudanganya umma kupitia JF.........

......Mkuu kuliko kujiweka wazi na ujinga hapo juu.....ni bora ukafanya your homework kidogo.....
 
Last edited by a moderator:
Kwenye hii thread watu wanaongelea dhuluma za polisi dhidi ya raia na hapo hapo wanaongelea kuwa RPC ni deal kwasababu kuna ulaji.

Hizi contradiction katika fikra zetu ndio zinatishia ile Tanzania bora ambayo wote tunaitaka.

Tatizo la TZ sio mtu mmoja mmoja bali mfumo mzima na culture ya sisi wananchi ya kufikiria deals badala ya kufikiria kazi na uwajibikaji.

Bila kuzingatia hayo tutaondoa Andengenye mmoja na kuleta Andengenye mwingine na tofauti pekee itakuwa sura na utii kwa wanasiasa tofauti.

Hii ni kweli mkuu mindset za watanzania ndiyo kiini cha matatizo yote haya.Imetokea mara nyingi tunawaheshimu watu wa deal na kudharau waadilifu.Fikra huru pekee ndio zitatuweka huru, yaani kujua haki zetu za msingi na kujitambua hapo ufisadi utakuwa umefikia kikomo.Ninaamini kabisa tukijua haki zetu, vyombo vya ulinzi na usalama vitafanya kazi kwake kwa weledi.
 
Ngoja nimsubiri,nitaenda kumpa salamu.Karibu sana.

Mama

Sijaikubali hiyo response yako....
Nakuita MAMA, behave like one....2015 ni karibu mno.....unatakiwa kujipima kwenye mambo madogo kama haya...

JIFUNZE KUSAMEHE....wengine bado tunaikumbuka ile picha yako...ukiwa unavuja damu kwenye paji la uso...
hivyo......HATUJASAHAU...
USITUANGUSHE.....
FANYA MAANDALIZI.........
 
Andengenye is the most compitent RPC in Tanzania,ana busara sana ,na hana upolisi wa kizamani kama kina Diwani Athumani ambaye ni kijana lakini ana upolisi wa mwaka 47.
 
Heee' zile mil 10 alitoa ahad za kukamatwa kwa waliomuua mwenyekiti wa CDM usa ndo bas tena na hata ufatiliaji wa wahusika wa kifo hicho utakua hafifu sana coz huyo aliyekuja atasema hajui au kakuta file mezani lililoachwa na mtangulizi wake Andengenye so atakuwa hana nguvu ya ufatiliaji wa mauaji hayo.
Hapo kwa ma-analyst wazuri ndipo point ilipo, Mnajua huyu jamaa hana tatizo na mtu na ni mtu wa logic na haki sana niliwahi kukutana ama kushuhudia kashkash zake Moro alipokuwa IGP pale. Anyway nataka kusema kumuhamisha huyu jamaa inaweza ikahusiana na mauaji ya Mwenyekiti wa CDM kwani alikuja na strategy nzuri sana hadi akaahidi 10M sio masihara na inawezekana wauaji walitumwa na WAKUBWA na watu walioko kwenye SYSTEM sasa jamaa (Andengenye) inaonekana angeweza kuwabainisha wahusika wote so ikabidi wamhamishe fasta kufunika kombe mwanaharamu apite wakampa na cheo cha kuzugia. Hebu fikirieni kidogo ni kwanini wamhamishe sasa na kama mnakumbuka maandamano mengine ya CDM Arsh aliyaachia yafanywe freely baada ya yale ya mwanzo sababu yeye kama IGP lazima ashrkshwe, Mi naamini kuna kitu hapo...
 
Niwaibie siri moja. Wachache sana wameteuliwa kuwa ma-IGP kutokea hapo makao makuu ya jeshi la polisi. Andengenye hawezi tena kuteuliwa kuwa IGP. Hebu nasi tutafute raia msomi mzuri aliongoze jeshi hili la polisi. South Africa walifanya hivo na hata Kenya walifikiria kufanya hivo. Katiba yao ya sasa inawaruhusu kuteua raia mzuri kiuongozi kuongoza njagu hawa ambao wamebobea kwa rushwa na kuua bila kukusudia.
 
Mungi,
Taarifa za Andengenye kuandaliwa kuwa IGP zimezagaa sana mitaani hata kabla ya uteuzi huu. Lakini atambue kwamba hata kama atakuwa ameteuliwa kuwa IGP siku tukipandisha juu bendera ya ukombozi kwa mara ya pili basi hapo ni kama alivyofanya Rais Joyce Banda wa Malawi.

Kabla ya Saidi Mwema kuitwa kutoka Interpol Nairobi, redio mbao zilikuwa zinasema IGP angekuwa Abdallah Msika, lakini hola.
 
Mi kuna kamanda namtafuta anaitwa Venance Tossi..........

Yuko TANAPA anafanyishwa kazi za mgambo. Polisi muwafikirie wastaafu wenu jamani, wengine wanatia aibu kabisa. Wastaafu wengine wanashikishwa virungu kwenye vikampuni uchwara vya ulinzi hadi aibu!
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom