Makala za Mohamed Said Katika Mwananchi: Miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika

Na miye niweke 50 cents zangu.

Alichoandika Bw. Said kwenye simulizi la kila ambacho anakiita "historia" kwa kweli siyo historia kwa maana ambayo inakubalika. Ndio maana toka mwanzo wa mnakasha huu nimekuwa nikiuliza maswali ambayo yanahusiana na ukusanyaji wa taarifa mbalimbali. Napenda zaidi maana ya neno "history" inavyotolewa kwenye wikipedia - History (from Greek ἱστορία - historia, meaning "inquiry, knowledge acquired by investigation"[SUP][2][/SUP]) is the discovery, collection, organization, and presentation of information about past events. History can also mean the period of time after writing was invented.

Kamuni ya "The Pocket Webster School & Office Dictionary" inasema kuwa "history" ni a. A narration or description of facts and events arranged chronologically with their causes and effects. b. A knowledge of facts c. all of the known past and d. A scientific study of the past.

Kumbe historia siyo simulizi kama hadithi. La hasha! Historia ni somo linaloongowa na kanuni za kisayansi na kanuni ya kwanza kabisa ni kuwa objective. Manake nini? Maana yake ni kwamba unapoenda kuangalia matukio ya nyuma unakuwa huru kutoka katika biases zako, stereotypes zako na kwa hakika kabisa kuzigundua hivyo vikwazo vya kuwa objective. Hapa ndipo tunapokutana na kosa kuu kabisa la mzee wetu.

Bw. Said hakuisogelea historia katika mwanga wa mtu ambaye ni objective. Alisimuliwa maneno na wazazi wake, aliyaona mambo kadha wa kadha akiwa na umri mdogo, na kwa bahati mbaya sana alikulia na kufundishwa chini ya wale ambao waliamini kabisa kuwa Nyerere alikuwa ni mdini toka siku ya kwanza anaingia Dar. Hivyo anapokua na kupata Ilimu tayari ameshajengewa hisia hii kutokana na masimulizi mbalimbali. Mara kwa mara hurudia kutuambia jinsi alivyosimuliwa na "wazee" wake. Hilo lilikuwa kosa lake la kwanza.


Kosa lake la pili mzee wetu ni kuwa alipoanza kufanya utafiti hakuwa anafanya utafiti ili kuwathibitisha wazee wake au kuwakanusha. Hakuwa anafanya utafiti ili kujua ukweli wote kabla ya kujenga maoni yake. Badala yake yeye alienda kuangalia historia ili kuthibitisha kile ambacho alishaaminishwa tangu akiwa kijana mdogo hadi leo hii. Hivyo, chochote ambacho angekutana nacho kinyume na kile alichosimuliwa alikiweka pembeni. Na matokeo yake ni kuwa simulizi zima halihusiani na historia hata kidogo linahusiana na MAJINA YA WAISLAMU.

Umenisoma vizuri.

Bw. Said kwa kweli hajali kabisa kama hao wanaoitwa "waislamu" wa wakati ule walikuwa kweli wanashika dini au wanaitwa tu kwa majina. Hilo kwake si hoja hata kidogo. Alipofanya utafiti alipoona jina la Kiislamu alihitimisha ni "MUislamu" na hivyo hata kama watu hao kihistoria walikuwa hawashiki dini au hata kufuata imani ilivyo yeye kwake haikuwa hoja alimradi tu wale walijiita "Waislamu" sasa hiki ukiangalia ni kigezo kidogo sana kukifikia. Nguruvi ameonesha mahali fulani hapa - kwamba Bw. Said anatumia majina ya Waislamu kuwapa watu "Uislamu" lakini ikija kwenye BAKWATA au mtu mwingine yeyote anayempinga ambaye anajina la Kiislamu kipimo chake hicho hukitupa mbali. Anaingiza kipimo kingine kabisa nacho ni "kukubaliana nasi". Yaani, Muislamu ambaye anaampinga si Muislamu ila yule wanayekubaliana naye. Matokeo yake kwake BAKWATA haiwezi kuwakilisha maslahi ya Waislamu kwa sababu hata kama wote waliomo mle wanaamini katika Uislamu; wanamuamini Mwenyezi Mungu Mmoja asiye na Mshirika na wanaamini kuwa ni Mtume Mohammed (SAW) ni mjumbe wake.

Hili linashangaza. Hakuna kipimo chochote kingine cha Muislamu zaidi ya imani yake katika mambo haya mawili ya msingi na mengine yanayotokana na hayo. Hakuna siasa, hakuna rangi, hakuna uanachama wa chama fulani n.k

Hata hivyo kosa la tatu ambalo linavunja kabisa hii dhana kuwa anachosimulia ni historia ni kuwa haandiki ili kuwaleta watu pamoja kuweza kufahamu ukweli . Nina bahati kuwa nimesoma maandishi yake mengi sana na katika yote yeye anazungumzia ugomvi kati ya Waislamu na Wakristu au kati ya Uislamu na Kanisa. Na katika hili kwa kweli amefanikiwa sana. Siyo kuwaamsha Waislamu bali kuwapotosha watu kuamini kuwa adui yao ni Kanisa! Hazungumzii umaskini, magonjwa na ujinga uliokithiri kati ya watu wetu - Waislamu, Wakristu na Wapagani; hazungumzii matumizi mabaya ya fedha za umma ambazo zinatokana na kodi za walio BAKWATA NA wale walio nje ya BAKWATA; hazungumzii haja ya mabadiliko ya kisiasa ambayo yatawaleta wananchi wetu pamoja kuubomoa na kuuvunjilia mbali mfumo wa utawala wa kifisadi. Anachofanya yeye ni kuwafanya baadhi ya Waislamu - na inasikitisha wapo ambao wanamini -kuwa adui yao ni Kanisa!

Matokeo yake ni kweli wapo watu wanalichukia kanisa katoliki; wapo watu ambao wanachukia hata Wakristu kwa sababu ya mafundisho ya Bw. Mohammed. Ndio nikaonesha juzi kwamba anachofanya ni kinyume hata na mafundisho ya Qurani. Analeta faraka siyo tu kati ya Waislamu na Waislamu (wale wa BAKWATA NA WALE NJE YAKE) bali pia faraka kati ya wanadamu tulioumbwa na Mwenyezi Mungu ili "tujuane" siyo tuchikiane, tuogopane au hata tudhulumiane. Angekuwa kweli kabisa lengo lake ni kutafuta umoja na ukweli asingedai kuwa ameandika kwa ajili ya "kuwatuhumu" watu fulani.

Na hata kama angetaka kutuhumu watu basi tungeona kweli kabisa angejiunga na wengine na kuleta mashtaka Mahakamani.

Bw. SAid na wale wanaoamini kuna mfumo Kristu wangeweza kabisa kuleta hata kesi mahakamani. Kushtaki Baraza la Maaskofu Katoliki kwa kuwa wanafanya ubaguzi. Wangeweza kufungua mashtaka dhidi ya Wizara ya Elimu ili kuonesha kuwa inafanya kazi kibaguzi. Hadi leo hii hakuna kesi hata moja iliyowahi kufunguliwa dhidi ya kanisa au serikali au hata mtu yeyote mwingine kudai kuwa kuna watu wanabaguliwa. Nilimuambia mtu mmoja juzi humu humu ambaye alidai kuwa kuna ubaguzi wa kidini NSSF - nikasema kama yeye ni mwathirika leteni mashtaka.

Sitaraji kama kuna mtu yeyote upande wa Bw. Said ambaye anaweza kuleta mshtaka nchini ya kudai kuwa Waislamu wanadhulumiwa. Hakuna ushahidi unaoweza kusimama mahakamani wa jambo hilo. NONE. Wapo ambao wanapenda uwepo ushahidi ili waweze kusema "tuliwaambia" lakini kwamba kuna ushahidi unaoweza kuoneshwa wa mfumo rasmi wa kibaguzi wenye kupendelewa Wakristu (mfumo kristu) haupo.

Kwa hiyo, kwa ufupi mjadala huu unatuonesha tu hatari tuliyonayo kama taifa. Hasa uwepo wa watu ambao wanaamini yanayodaiwa bila kuuliza. Mwanahistoria wa Kiarabu aliyeishi 1337 Ibn Khaldun - ambaye anatajwa kama Baba wa Sayansi ya Historia na mmoja wanafalsafa wa hali ya juu toka katika Ulimwengu wa Kiislamu - aliandika kuhusu makosa saba ambayo waandishi wa historia wanayafanya. Lakini kwa sehemu hii itoshe kunukuu maneno yake ni kukosoa kile aliachokiita "idle superstition and uncritical acceptance of historical data" kama mojawapo ya makosa ya wanahistoria.

Tumeona humu wapo watu ambao hawataki kuuliza maswali sahihi kwa sababu majibu yake yanavunja hoja zao. Matokeo yake ni kuwa watu wanakubali bila kupatiwa uhakika na hasa vijana ambao huenda kumsikiliza nawaonea huruma kwa sababu wengi wanajikuta wanaamini kile lisemwalo kwa sababu aliyelisema anatumia authority ya kuwa amezungumza sehemu nyingi duniani, anakubalika na majarida mbalimballi duniani. For untrained minds hii ni authority tosha. It is sad that some people among "great thinkers" wako hivyo hivyo. Wanakubali kitu wanachoambiwa bila kukihoji kwa sababu tayari wanakiamini.

Kwa hiyo, tafuteni kazi za Bw. Said mzisome lakini mkae mkijua hamsomi historia bali masimulizi ya kijana kuhusu wazazi na wazee wake. Mtu anayesoma akiamini anasoma historia hatuna jinsi ya kumsaidia bali kumuonea huruma.

Mwanakijiji,

Sitanii hii ni kweli.

Katika hii "critique" yako nakiona kitabu kileeee kinakuja.

Usipuuze ushauri wangu.

Wewe una uwezo wa kuandika hebu tazama ulivyosimama na mimi "toe to toe" kama Waingereza wasemavyo unadhani ni kitu kidogo.

Matani ya nondo zote nilizokushushia hukufa bado unakuja tu.

Hilo si mchezo si unaona rafiki yako Mag3 kakimbia karudi leo anauliza hivi mnakasha bado unaendelea?

Andika kitabu unitoe makosa na dunia nzima ijue Mohamed Said kakutana na saizi yake.

Bila kitabu bado ushindi uko kwangu.

Mohamed
 
Mwanakijiji,

Sitanii hii ni kweli.

Katika hii "critique" yako nakiona kitabu kileeee kinakuja.

Usipuuze ushauri wangu.

Wewe una uwezo wa kuandika hebu tazama ulivyosimama na mimi "toe to toe" kama Waingereza wasemavyo unadhani ni kitu kidogo.

Matani ya nondo zote nilizokushushia hukufa bado unakuja tu.

Hilo si mchezo si unaona rafiki yako Mag3 kakimbia karudi leo anauliza hivi mnakasha bado unaendelea?

Andika kitabu unitoe makosa na dunia nzima ijue Mohamed Said kakutana na saizi yake.

Bila kitabu bado ushindi uko kwangu.

Mohamed

Najisikia kuheshimiwa mzee, ila kwa kweli kitabu ambacho nilikuwa nakifiria ni kutumia kitabu chako peke yake kuangalia vile vile ulivyoangalia wewe na kuvipa tafsiri nyingine.
 
Najisikia kuheshimiwa mzee, ila kwa kweli kitabu ambacho nilikuwa nakifiria ni kutumia kitabu chako peke yake kuangalia vile vile ulivyoangalia wewe na kuvipa tafsiri nyingine.

Plagiarism.

Andika chako usitafute pakutokea. Mohamed Said kisha weka msingi, kwa hilo tunamsifu, wewe ubaki kuwa "critique" na kuandika vijarida vya uchochezi, kuandika historia huwezi kabisa. Na Mohamed Said kawa "diplomatic" tu.

Mimi nakupa "open challenge" huwezi kuandika kitabu kikapata hata hata 5% ya "academical response" kama cha Mohamed Said. Uandishi wa vijarida ni tofauti kabisa na uandishi wa historia.

Huwezi, ikiwa hata vitabu vya imani za watu unavi "quote" isivyo na unashindwa hata kuomba msamaha unapostukiwa. Utaweza kuandikia historia? Aahhh, hilo si rahisi.

"Fumbo hufumbiwa mjinga, mwerevu huling'amua" nimeona nikusaidie kwa uliyoambiwa na Mohamed Said kwani nakuona huna uwerevu huo.
 
BREAKING NEWS!

An Nuur la leo Ijumaa (Dhul Hajj 1432, 28 Oktoba, 2011) limeandika "Waislam Waliojenga Chuo Kikuu Watupwa.
Yupo Abbas Sykes, Bibi Majaliwa, Salum Athuma, Ibrahim Bofu...
Hawakualikwa wala kutajwa miaka 50 ya Chuo Kikuu UDSM...90% waliochangia ni Waislam wameorodhesha majina 9
  1. P.A. Makwaia 500.00
  2. Julius K. Nyerere 200.00
  3. Salum Athumani 500.00
  4. Ibrahim Bofu 150.00
  5. Schneider Abdillah Plantan 100.00
  6. Abdallah Said 100.00
  7. Kondo Salum 100.00
  8. Abbas Sykes 100.00
  9. Bibi Panya Majaliwa 500.00
Gazeti linalaumu mfumokristo kwa kusahauliwa wazalendo hawa na wengine.

Mohamed
Walichanga kwa kuwa ni WAISLAMU au mioyo na uwezo wao uliwatuma kufanya hivo? Mohamed, kwako DINI ni gamba la nguvu. Na kwa umri wako kulivua hauwezi.
 
Walichanga kwa kuwa ni WAISLAMU au mioyo na uwezo wao uliwatuma kufanya hivo? Mohamed, kwako DINI ni gamba la nguvu. Na kwa umri wako kulivua hauwezi.

WC,

Kweli hawa watu walichanga kwa NIA moja,UWEZO na MIOYO yao misafi,sasa kinachotufanya sisi tushindwe KUWAPA TUNU nini?? au majina yao hayataleta UTAMU kwenye kuyatamka??? kama yale mingine ambayo juzi tu tumyapa vitivo pale Mlimani
 
Mwanakijiji,

Sitanii hii ni kweli.

Katika hii "critique" yako nakiona kitabu kileeee kinakuja.

Usipuuze ushauri wangu.

Wewe una uwezo wa kuandika hebu tazama ulivyosimama na mimi "toe to toe" kama Waingereza wasemavyo unadhani ni kitu kidogo.

Matani ya nondo zote nilizokushushia hukufa bado unakuja tu.

Hilo si mchezo si unaona rafiki yako Mag3 kakimbia karudi leo anauliza hivi mnakasha bado unaendelea?

Andika kitabu unitoe makosa na dunia nzima ijue Mohamed Said kakutana na saizi yake.

Bila kitabu bado ushindi uko kwangu.

Mohamed

Wakati mwingine tunajiburudisha.

1971 Muhammad Ali kafunguliwa kupigana na kamkuta Joe Frazier ndiyo "World Heavy Weight Champion."

Ali katoa changamoto, Frazier kapokea sasa wanakutana Guy Madison Square Garden, New York.

Mpamabano ukapewa jina "Fight of the Century."

Kwenye kitabu chake "The Greatest My Own Story" Ali anamsifia Frazier anasema nimeshusha kila aina ya kipigo kwa Frazier, Frazier anakuja tu yuko na mimi haniachii..."

Frazier akamshinda Ali kwa "points"

Ukiingia Guy Madison Square Garden utakuta bango kubwa sana la mpambano ule wa Ali na Frazier limepamba lango kuu.


Mohamed
 

Wakati mwingine tunajiburudisha.

1971 Muhammad Ali kafunguliwa kupigana na kamkuta Joe Frazier ndiyo "World Heavy Weight Champion."

Ali katoa changamoto, Frazier kapokea sasa wanakutana Guy Madison Square Garden, New York.

Mpamabano ukapewa jina "Fight of the Century."

Kwenye kitabu chake "The Greatest My Own Story" Ali anamsifia Frazier anasema nimeshusha kila aina ya kipigo kwa Frazier, Frazier anakuja tu yuko na mimi haniachii..."

Frazier akamshinda Ali kwa "points"

Ukiingia Guy Madison Square Garden utakuta bango kubwa sana la mpambano ule wa Ali na Frazier limepamba lango kuu.


Mohamed

Sheikh Mohamed,

Nachukulia bandiko hili kama wewe ndiye Muhamad Ali na Mwanakijiji ndiye Frazier!! au sivyo ulikusudia?
 
WC,

Kweli hawa watu walichanga kwa NIA moja,UWEZO na MIOYO yao misafi,sasa kinachotufanya sisi tushindwe KUWAPA TUNU nini?? au majina yao hayataleta UTAMU kwenye kuyatamka??? kama yale mingine ambayo juzi tu tumyapa vitivo pale Mlimani
TUNU wamepewa sana. Mitaa mingi tu hapa Dar ina majina yao. Ukitoa mchango wa harusi wanandoa wakizaa mtoto ni lazima wamwite JINA lako au la mkeo? Watu tunaielewa vibaya dhana ya michango.
 
Plagiarism.

Andika chako usitafute pakutokea. Mohamed Said kisha weka msingi, kwa hilo tunamsifu, wewe ubaki kuwa "critique" na kuandika vijarida vya uchochezi, kuandika historia huwezi kabisa. Na Mohamed Said kawa "diplomatic" tu.

Mimi nakupa "open challenge" huwezi kuandika kitabu kikapata hata hata 5% ya "academical response" kama cha Mohamed Said. Uandishi wa vijarida ni tofauti kabisa na uandishi wa historia.

Huwezi, ikiwa hata vitabu vya imani za watu unavi "quote" isivyo na unashindwa hata kuomba msamaha unapostukiwa. Utaweza kuandikia historia? Aahhh, hilo si rahisi.

"Fumbo hufumbiwa mjinga, mwerevu huling'amua" nimeona nikusaidie kwa uliyoambiwa na Mohamed Said kwani nakuona huna uwerevu huo.

Hal yangu.
Ulichoongea hapo kitu kizito sana. Kwani kunatofauti kubwa sana katika uadishi wa makala za kiucgunguzi na vijalida.

Hakka mwadishi anayediriki kuthubutu kuandika makala za kiuchunguzi siku zote ni mwandishi makini kwani hapo zinahitajika busara zan atka uuatilia mambo kuahata kufaya mahojiano mengi na watu mbalimbali kisha kuiweka mezani hiyo makala yako.

Mwanakijij hiyo ni chalenge kubwa sana kwako kwani pamoja na kutumia muda mwingi lakini pia unahitaji uwe na pesa za kufuatilia habari husika. Ok all in all tunasubiri makala yako.

Kila lenye kheir
 

Wakati mwingine tunajiburudisha.

1971 Muhammad Ali kafunguliwa kupigana na kamkuta Joe Frazier ndiyo "World Heavy Weight Champion."

Ali katoa changamoto, Frazier kapokea sasa wanakutana Guy Madison Square Garden, New York.

Mpamabano ukapewa jina "Fight of the Century."

Kwenye kitabu chake "The Greatest My Own Story" Ali anamsifia Frazier anasema nimeshusha kila aina ya kipigo kwa Frazier, Frazier anakuja tu yuko na mimi haniachii..."

Frazier akamshinda Ali kwa "points"

Ukiingia Guy Madison Square Garden utakuta bango kubwa sana la mpambano ule wa Ali na Frazier limepamba lango kuu.


Mohamed
Baadae wakakutana Zaire ya Mobutu na Mohamed Ali akashinda mwaka 1973?
 
Jasusi nikuulize,

Historia lazima muikubali nyie ndio iwe historia???? Kwani msikubali tu kuwa mmekosea na hivyo historia iandikwe kwa pande zote hata kama nyie hamuikubali??

Nafikiri ahali yangu hujaelew somo.

Hakuna hata ha kubadiisha historia yaTanganyka hapa bali alichoandika Sheikh Mohamed ni kuandika yale yaiyo sahaulika au kufichwa katika histori a Tanganyika. Kusaahulika huko au kufichwa huko iwe kwa makusudio maalum au bahati mbaya, Bw Mohamed ameamua kufanyika utafiti na kutuwekea makala yake hapa.
 
Mwanakijiji,

Sitanii hii ni kweli.

Katika hii "critique" yako nakiona kitabu kileeee kinakuja.

Usipuuze ushauri wangu.

Wewe una uwezo wa kuandika hebu tazama ulivyosimama na mimi "toe to toe" kama Waingereza wasemavyo unadhani ni kitu kidogo.

Matani ya nondo zote nilizokushushia hukufa bado unakuja tu.

Hilo si mchezo si unaona rafiki yako Mag3 kakimbia karudi leo anauliza hivi mnakasha bado unaendelea?

Andika kitabu unitoe makosa na dunia nzima ijue Mohamed Said kakutana na saizi yake.

Bila kitabu bado ushindi uko kwangu.

Mohamed

Shk Mohammed nilikuonya juu ya huyu mtu anayejiita Mwanakijiji. Huyu jamaa ni mbishi sana..utapoteza muda wako bureee! kuna mada humu ya NSSF na Dr Masau au NSSF na Vifo vya watoto Tabora ndipo utakapo mjuwa huyu mtu. Hebu fuatilia mijadala yake na Game Theory ndipo utakapo mjuwa.

Anathubutu kukudhihaki ilihali wasomi wa Ulaya na Marikani wanaafiki kama ulichoandika ni Historia.. mpaka reviews zake zikawekwa kenye ma jono ya historia '' Journal of Africa History''. Huyu jamaa licha ya kumpa rejea zoote na nyashaahid zote yeye bado haelewi, basi ni dhaahir ana ajenda yake huyu.
 
To imply that the struggle for Uhuru wa Tanganyika was solely initiated or even spear-headed by those mentioned by Mohamed Said is a distortion of history.

Tanganyika being a Trust Territory of the British, the United Nations Organization received Tanganyika representatives as early as 1945. The Trusteeship Council was addressed by Tanganyika personalities like Japhet Kirillo on the Meru Corridor dispute in the late 1940s triggering the fight for freedom and the right to own our land. Personalities like John Rupia, Cliest Sykes and Dossa Aziz and those who initiated TAA (Tanganyika African Association), stressing the inclusion of country-wide leaders like Adam Sapi Mkwawa, Abdallah Fundikira, Humbi Ziota, Kidaha Makwaiya of Shinyanga, Elias Sarwatt of Mbulu and Chief Patrick Kunambi of Morogoro.

What I am trying to say is that the struggle for Uhuru was not purely a Dar es Salaam Kisutu affair. There were many players.

Kilasara,

With due respect... please read my book and you will see that we are of the same mind. There is no place in my work where even by far I hinted that the struggle for independence was a monopoly of Dar es Salaam.

But the chiefs were not forthcoming in supporting, TAA, TANU or the struggle.

If you have any new information contrary to what I have stated ukumbi will be glad to hear you.

But to give you the state of affairs obtabing at that time please go through this:

"Ilikuwa katika kipindi cha uongozi waAbdulwahid ndipo alipomwendea Chifu Kidaha Makwaia na kumuomba achukue uongoziwa chama kama rais. Abdulwahid alimwambia Chifu Kidaha kuwa endapo atachukuauongozi wa TAA, kwa kuchukua kwake uongozi wa Waafrika, angekua amefungua dimbala mageuzi Tanganyika kwa sababu machifu wengine wangemfuata. Kidaha alikuwachifu aliyependwa mno na serikali ya kikoloni, kwa ajili hiyo hakuweza kwawakati ule kuona busara ya kukubali ombi hilo. Pamoja na kauli aliyotoa kuhusuwatumishi Waafrika serikalini waruhusiwe kushiriki katika siasa, kauli ambayohuenda ndiyo iliyofanya uongozi wa TAA kumuomba achukuwe uongozi, Chifu Kidahaaliuamini uchifu na ushirikiano wa karibu na serikali ya Kiingereza kwa kupitiaindirect rule. Chifu Kidaha hakuwa tayari kuweka rehani nafsi yake na namaslahi ya watu wake kwa kukiunga mkono chama kilichokuwa kinapinga ukoloni.Baadaye mambo yalipowiva ndipo alipotanabahi kuwa alikuwa amepoteza nafasi yapekee ambayo ingemwezesha kuwa rais wa chama cha kwanza cha siasa (TANU)na labda kuwaWaziri Mkuu wa kwanza Tanganyika ililopata uhuru mwaka 1961."

Kilasara sasa huyu Nyerere mwaka 1957 yuko Mtaa wa Mvita, Dar es Salaam katika taarab ya TANU anahutubia. Hebu msikilize madongo yake kwa machifu:

"Katikahafla hiyo waheshimiwa, wageni waalikwa walipewa vitafunio, vinywaji baridi nachai. Nyerere katika kutoa shukrani kwa wanachama wa TANU alikamata kikombe chachai na kukionyesha juu kwa wasikilizaji wake. Aliwaambia watu kwamba wasidhanikitendo cha kumpa mtu kikombe cha chaini kitu kidogo. Nyerere aliendelea kusema kuwa watu wameiuza nchi hii kwakupewa kikombe cha chai na wakoloni. Nyerere alikuwa akitoa maneno hayo akiwaanawapigia vijembe watu maalum. Nyerere kwa maneno yake alikuwa akiwakusudia machifu. Baadhi yaowalikuwa pale pale katika meza kuu wakinywa chai na yeye. Wakati huo baadhi ya machifu walikuwa wakishirikianana Gavana Twining na UTP katika hila za kuipiga vita TANU ishindwekuikomboa Tanganyika kutoka makucha yaukoloni. Ilikuwa dhahiri kuwa makombo waliyokuwa wakipata machifu kutoka kwaMwingereza hayakuwa hata na thamani ya kikombe cha chai. Maneno ya Nyererehayakuwa fumbo kwa wale machifu. Yalikuwa maneno ya wazi ambayo waliyaelewa.Machifu walitambua kuwa wao ndiyo walikuwa wakisemwa katika hotuba ile yashukurani."

Karibu kwenye jamvi Bwana Kilasara.

Mohamed


Mohamed
 
Shk Mohammed nilikuonya juu ya huyu mtu anayejiita Mwanakijiji. Huyu jamaa ni mbishi sana..utapoteza muda wako bureee! kuna mada humu ya NSSF na Dr Masau au NSSF na Vifo vya watoto Tabora ndipo utakapo mjuwa huyu mtu. Hebu fuatilia mijadala yake na Game Theory ndipo utakapo mjuwa.

Anathubutu kukudhihaki ilihali wasomi wa Ulaya na Marikani wanaafiki kama ulichoandika ni Historia.. mpaka reviews zake zikawekwa kenye ma jono ya historia '' Journal of Africa History''. Huyu jamaa licha ya kumpa rejea zoote na nyashaahid zote yeye bado haelewi, basi ni dhaahir ana ajenda yake huyu.

Nimekusika Shk Yahya lakini nifanyeje nami nina amana ya Allah? Sheikh Mohamed Ayoub akisema ilm ni amana mwenyewe akija kuitaka ni wajib wako umpatie.

Sasa huyu mtu yarabi ndiyo kama unavyomwelezea mbishi lakini wajibu wa sie kumsomesha hauondoki.

Hivyo hivyo twende nae taratibu.

Mohamed
 
Sheikh Mohamed,

Nachukulia bandiko hili kama wewe ndiye Muhamad Ali na Mwanakijiji ndiye Frazier!! au sivyo ulikusudia?

MM,

Nakupa mji chukua New York kama hujafika nenda Guy Madison Garden tena iwe Jumamosi maana ndiyo kuna mambo hapo.
Umepatia.

Mwanakijiji kiboko bwana usifanye maskhara mie nikimsikia kwa vijana wangu wananieleza khabari zake.
Kataka kuniongeza mvi...huyu mtu.

Mohamed
 
TUNU wamepewa sana. Mitaa mingi tu hapa Dar ina majina yao. Ukitoa mchango wa harusi wanandoa wakizaa mtoto ni lazima wamwite JINA lako au la mkeo? Watu tunaielewa vibaya dhana ya michango.

Ilishindikana nini kuwa -acknowldged UDSM katika sherehe ya miaka 50? majina yao au dini zao? au ndio mfumo kristo at work
 
Kilasara,

With due respect... please read my book and you will see that we are of the same mind. There is no place in my work where even by far I hinted that the struggle for independence was a monopoly of Dar es Salaam.

But the chiefs were not forthcoming in supporting, TAA, TANU or the struggle.

If you have any new information contrary to what I have stated ukumbi will be glad to hear you.

But to give you the state of affairs obtabing at that time please go through this:

"Ilikuwa katika kipindi cha uongozi waAbdulwahid ndipo alipomwendea Chifu Kidaha Makwaia na kumuomba achukue uongoziwa chama kama rais. Abdulwahid alimwambia Chifu Kidaha kuwa endapo atachukuauongozi wa TAA, kwa kuchukua kwake uongozi wa Waafrika, angekua amefungua dimbala mageuzi Tanganyika kwa sababu machifu wengine wangemfuata. Kidaha alikuwachifu aliyependwa mno na serikali ya kikoloni, kwa ajili hiyo hakuweza kwawakati ule kuona busara ya kukubali ombi hilo. Pamoja na kauli aliyotoa kuhusuwatumishi Waafrika serikalini waruhusiwe kushiriki katika siasa, kauli ambayohuenda ndiyo iliyofanya uongozi wa TAA kumuomba achukuwe uongozi, Chifu Kidahaaliuamini uchifu na ushirikiano wa karibu na serikali ya Kiingereza kwa kupitiaindirect rule. Chifu Kidaha hakuwa tayari kuweka rehani nafsi yake na namaslahi ya watu wake kwa kukiunga mkono chama kilichokuwa kinapinga ukoloni.Baadaye mambo yalipowiva ndipo alipotanabahi kuwa alikuwa amepoteza nafasi yapekee ambayo ingemwezesha kuwa rais wa chama cha kwanza cha siasa (TANU)na labda kuwaWaziri Mkuu wa kwanza Tanganyika ililopata uhuru mwaka 1961."

Kilasara sasa huyu Nyerere mwaka 1957 yuko Mtaa wa Mvita, Dar es Salaam katika taarab ya TANU anahutubia. Hebu msikilize madongo yake kwa machifu:

"Katikahafla hiyo waheshimiwa, wageni waalikwa walipewa vitafunio, vinywaji baridi nachai. Nyerere katika kutoa shukrani kwa wanachama wa TANU alikamata kikombe chachai na kukionyesha juu kwa wasikilizaji wake. Aliwaambia watu kwamba wasidhanikitendo cha kumpa mtu kikombe cha chaini kitu kidogo. Nyerere aliendelea kusema kuwa watu wameiuza nchi hii kwakupewa kikombe cha chai na wakoloni. Nyerere alikuwa akitoa maneno hayo akiwaanawapigia vijembe watu maalum. Nyerere kwa maneno yake alikuwa akiwakusudia machifu. Baadhi yaowalikuwa pale pale katika meza kuu wakinywa chai na yeye. Wakati huo baadhi ya machifu walikuwa wakishirikianana Gavana Twining na UTP katika hila za kuipiga vita TANU ishindwekuikomboa Tanganyika kutoka makucha yaukoloni. Ilikuwa dhahiri kuwa makombo waliyokuwa wakipata machifu kutoka kwaMwingereza hayakuwa hata na thamani ya kikombe cha chai. Maneno ya Nyererehayakuwa fumbo kwa wale machifu. Yalikuwa maneno ya wazi ambayo waliyaelewa.Machifu walitambua kuwa wao ndiyo walikuwa wakisemwa katika hotuba ile yashukurani."

Karibu kwenye jamvi Bwana Kilasara.

Mohamed


Mohamed

Mohamed,'
This is another face of Nyerere, no? Kuna mahali umetuambia kuwa Nyerere hakuweza kukabiliana na mtu uso kwa uso, mbona hapa anawamwagia machifu waziwazi bila kumung'unya maneno?
 
Shukran sana kwa mjadala wenye maana na ndio sababu napenda sana kujadiliana na wewe kwa sababu unatafuta suluhu ya tatizo unaloliona na sii kutafuta mchawi kumtangaza hali anaendelea na uchawi...

Ningependa sana kuelewa wewe ulikosa vipi elimu na umeweza vipi kuipata maanake tupo waislaam wengi sana tulosoma enzi ya mwalimu na tumefaidika na mabadiliko aliyoyafanya. pengine elimu yako umeikosa wakati wa Mwinyi au Mkapa na hi sintoshangaa isipokuwa kwa uhakika nimekufahamisha huko nyuma matatizo ya kielimu aliyopambana nayo mwalimu. Na kati ya wazee wako wlaiopata taabu nimesema mimini mmoja wapo na hakika nimefaidika na kutaifishwa kwa shule, lakini nimetukanwa kwa sababu nilikuwa nilitumia jina la Kikristu kuweza kusoma ktk shule za kikatoliki..Sikujibu nimekaa kimya kwa sababu mtukanaji hakutaka kujadili isipokuwa matusi yamemkaa kinywani na hana haya...

Mkuu wangu, ni vigumu sana kuchukua kati ya wananfunzi wote asilimia 5 kuendelea na masomo ya form 1 kutokana na uchache wa shule na walimu halafu ni gumu zaidi kuchukua wananfunzi asilimia 1 kuendelea ma masomo ya vyuo vikuu bila shaka kwa mtu yeyote unaweza kusema lolote lile. Binafsi naelewa mfduko kristu ulikuwepo kabla ya Uhuru na hakuuanzisha mwalimu isipokuwa mwalimu aliupiga vita na ndio maana tukataifisha mashule yote ya taasisi za kidini.. Kwa hilo wengi waliliona kosa kwa sababu elimu zao zinawafundisha kwamba ubepari ni pamoja na kuweka elimu mikononi mwa watu na sio serikali... Hii sio kweli na haijawa ubepari isipokuwa ni upotoshaji kuifanya elimu sii haki ya mwananchi isipokuwa ni previlege..

Sasa unapoondoa serikali ktk mamlaka ya kusimamia elimu na uendeshaji wake ukaviweka mikononi mwa serikali kwa mtazamo ule ue wa biashara ina maana hata elimu haihitaji regulations zinazowabana waendesha biashara. Na huwezi kumlazimisha mtoa elimu a target watu gani isipokuwa yeye anatazama biashara yake itauzika wapi zaidi na ktk standard iliyowekwa..Na matokeo ya mfumo huu utawapa nafasi zaidi wale wenye kipato kupata elimu bora zaidi ya wale wasiokuwa na kipato.

Na kwa bahati mbaya waislaam ndio wengi maskini kuliko wakristu ktk mikoa ya Pwani lakini kwa ujumla mimi nadhani Wakristu maskini ni wengio zaidi ya Waislaam kwa sababu wengi takwimu zinaonesha wazi kwamba umaskini upo zaidi vijijini ambako kuna asilimia kubwa ya wananchi na mara nyingi waislaam hawaishi vijijini.. Hivyo, tunapozungumzia umaskini nadhani swala hili siii la waislaam pekee isipokuwa Taifa zima wote tunanyimwa elimu bora kwa kutokana na hizo shule za kata ambazo hazina walimu na vifaa vya kufundishia. Unjust society sii ya waislaam pekee ni kwa wananchi wote kutokana na hivyo unapata lawless society...

Sheria zipo kuwa favor wenye kipato, haijalishi wewe mkristu au Muislaam kwa sababu leo hii huwezi kusoma na mtoto wa JK, Lowassa, Mwinyi au Mkapa, Rostam na wengineo wakubwa ndani ya chama CCM, hawa wote wanapewa special treaties hata hospital zao ni nje ya nchi tofauti na wewe au mMwanakijiji.. Kwa hiyo unapotumia lugha ya Udini na advantage wanazopewa Wakristu wakati Mwanakijiji au Jasusi wanaelewa kwamba they struggle hard to get education wakati ni wakristu ndio maana hawawezi kukubaliana na mawazo yako. Kama wao wangekuwa mfanoi wa madai yetu ingeweza kabisa kuobnekana lakini sote tunasota!.. inakuwaje Mkristu aliyependelewa na serikali ya Nyerere leo hii awe na maisha duni sana na yako wakati yeye anaona wazi kabisa kwamba watoto wa viongozi wa CCM wote waislaam kwa Wakristu wakila bata..


Na ndio maana nikasema Unjust ipo ktk uongozi wa serikali ya CCM na nakubaliana sana na mawazo yako isipokuwa unayatazama kwa viatu ulovaa wewe muislaam bila wewe pia kuvaa viatu vya mkristu ambaye hana refa CCM. Na maadam sisi sote tumeishi na tunaendelea kuishi tanzania kwa nini hatutaki kukubali kwamba CCM ndiye mgonvi wetu, kwa nini tunataka sana kulaumiana sisi ambao wote ni victim wa mfuko huo huo Kristu ambao hakika unawapendelea ndugu na watoto wa viongozi wetu kiasi kwamba leo hii wamepangana kupokezana madaraka ndani ya chama hicho. Na pengine hata hiyo mikataba ya MoU na AghaKhan ni kwa sababu ya watoto wao wapate elimu bora ama walichukua asilimia 10 kuwezeshwa..

Mkandara,

Ndugu yangu tosheka na kwamba wengine tulikosa nafasi kwa sababu ya majina yetu. Kuna mzee wangu moja alipelekwa kusoma shule ya kikatoliki kwasababu ya uhaba wa shule zengine na ikabidi abadilishe jina lake ili aweze kuingia humo ndani. But tuachane na suala hilo pengine kuna sababu zengine zilichangia because I do not like to mourn the past.

Unapoyazungumza haya ya sasa na sheria kuwalinda wenye nazo source ya matatizo haya ni Nyerere. Kwanini mfumo aliouanzisha wa ujamaa ulipelekea jamii ya wateule nchini na wasiokuwa watawala. Tulikuwa tunasikia familia za kiteule tu Kuanzia Nyerere, Rupia, Bomani etc familia zengine za kimaskini zikawa hazisikiki. Mfumo wa utopia uliokuwapo madarakani ulipelekea kila kitu kikawa centralized na hatukuweza kuuliza kwanini imekuwa hivi badala ya vile. Isitoshe idara ya usalama wa taifa ilikuwa haifanyi kazi kwa interest ya taifa bali ikifanya kwa interest ya mfumo wa nchi. Ndio sababu watu kama akina Oscar Kambona, Mtei , Babu na wengineo wengi walikimbia nchi kwasababu waliyaonamapungufu wakaamua kuondoka nchini kuokoa maisha yao. Mfumo huo sasa ukaja ukarithiwa na mabepari wa nchi na wanautumia kulinda maslahi yao. Hivyo kabla hujaulalamikia mfumo pengine tuuliza mfumo huu ulianzia vp hadi ukafikia ulivyo sasa hivi.

HIVYO BASI KABLA HUJAANZA KUZUNGUMZIA MFUMO ULIOPO ULIZIA MFUMO HUO ULIANZIA WAPI? Anyway hiyo sioni jambo la msingi suala la msingi ni kwanini kuna imbalance katika education and social development between Muslims and Christians. Umesema sana kuhusu wakristo kuendeleza shule zao na jamii zao hata hivyo nimekuuliza swali msingi kabisa JE SERIKALI INAWAPA HELA WAISLAMU KAMA INAVYOWAPA WAKRISTO???? Hili swali haulijibu badala yake unakimbilia kujustify kwanini wakristo wanapewa hela. Labda nikuongezee swali jengine hivi unafahamu kuna taasisi na shule za waislamu zilichukuliwa before independence na viwanja vingi vya waislamu vilichukuliwa baada ya kutangazwa kwa azimio la arusha. Je viwanja hivyo wenye navyo walirudishiwa kihalali?

Mkandara usiyaguse ya sasa kwanza kabla hatujamaliza ya zamani ndugu yangu. Sifa moja ya usomi is to know how ask the right question at the right time and place sio vyenginevyo.
 
23 Reactions
Reply
Back
Top Bottom