Makala ya Mwanahalisi kuhusu SS, kusababisha kufungiwa tena...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Vyanzo vya ndani toka Wizara ya Habari, Michezo na Utamaduni ambayo ndiyo inasimamia tasnia ya habari vinadokeza kuwa Serikali imechukizwa sana na makala iliyoandikwa na gazeti la Mwanahalisi toleo la 195 lenye kichwa cha habari "Akili ya Sofia haiwezi kuwaza zaidi ya ngono" ambapo makala imetumia kejeli (sarcasm) kuelezea maoni ya Waziri Simba.

Sehemu ambayo inaonekana kuwatibua kabisa ni sehemu ya mwisho ya makalah hiyo:

Sofia kila anapomwaangalia wanawake wenzake anamwangalia kama mashine ya kumtuliza mwanaume; fikra zake kuhusu wanawake ni ngono.


Kwake, haoni nguvu nyingine yoyote ya wanawake ambayo inaweza kutumiwa kuleta mabadiliko katika jamii yetu; kwake mwanamke ni kiungo chake cha uzazi basi.
Katika dunia ya watu wanaowaza sawasawa siku Sofia alipotoa kauli ya kuwataka wanawake wawanyime waume zao unyumba, tungeona taharuki kubwa serikalini na hata bosi wake angemkemea kama si kumweka pembeni.


Lakini kwa kuwa nafasi za uwaziri zilikwisha kurahisishwa siku nyingi, bado ataendelea kutesa na kutesa, kwani ana shida gani wakati akili yake imeganda kwenye ngono na hicho ndicho kilichompa uwaziri?
Gazeti toleo na. 195

Maneno hayo yaliyokolezwa rangi ndiyo yanaonekana kuwatibua wakuu kiasi cha kuandika barua ya kutaka maelezo toka kwa Mwanahalisi ya kwanini wasifungiwe.

Hata hivyo hilo la kutaka maelezo ni formality tu kwani wenye nchi wameshatoa agizo kuwa Mwanahalisi lifunguwe na safari hii kwa muda mrefu zaidi ili lisiwepo kuelekea uchaguzi mkuu.
 
Mwanahalisi halipo above responsible journalism. Wakiambiwa ku back up sentensi hiyo ya Waziri kupata uwaziri kwa sababu ya ngono wanaweza?
 
Mwanahalisi halipo above responsible journalism. Wakiambiwa ku back up sentensi hiyo ya Waziri kupata uwaziri kwa sababu ya ngono wanaweza?

ndicho walichoambiwa kufanya.. lakini katika fasihi yawezekana wametumia msemo fulani hivi wenye kuhitaji ufafanuzi tu.
 
ndicho walichoambiwa kufanya.. lakini katika fasihi yawezekana wametumia msemo fulani hivi wenye kuhitaji ufafanuzi tu.

Kuna maneno ya fasihi na mengine ni libel and defamation case. Huwezi kuispin hiyo sentensi kwamba ni fasihi. Wamesema she slept her way to the cabinet, now they have to prove that. Hamna cha fasihi hapo. Huwezi kutoa kashfa directly na kusingizia fasihi.
 
Mmh kwani wawahukumu kwa sentenis moja tu wakati ujumbe mzima umeeleweka?wajenge hoja kuanzia mwanzo wa makala wasiegemee kwenye kipengele kimoja tu.
 
Kuna maneno ya fasihi na mengine ni libel and defamation case. Huwezi kuispin hiyo sentensi kwamba ni fasihi. Wamesema she slept her way to the cabinet, now they have to prove that. Hamna cha fasihi hapo. Huwezi kutoa kashfa directly na kusingizia fasihi.

Hapana bwana hawakusema hivyo..
 
Hapana bwana hawakusema hivyo..

kwani ana shida gani wakati akili yake imeganda kwenye ngono na hicho ndicho kilichompa uwaziri?

However you spin this, serious accusation kwamba either ngono au akili yake kuwa kwenye ngono ndicho kilichompa uwaziri. Both are salacious accusations.Now they have to prove either or face a legitimate disciplinary action.
 
:amen:niliwahi kunukuu sehemu ya makala hiyo hapa nikionesha wasi wasi kuhusu uwezekano wa hatua kama hii ya sasa.
 
Mmh kwani wawahukumu kwa sentenis moja tu wakati ujumbe mzima umeeleweka?wajenge hoja kuanzia mwanzo wa makala wasiegemee kwenye kipengele kimoja tu.

Ukiandika kitabu cha kurasa 1000 na kunitukana matusi ya defamation katika sentensi moja, watu hawataangalia kurasa 1000, bali ukurasa mmoja, particularly hiyo sentensi moja.Kwa hiyo hii point ya kusema waangalie larger context hapa ni moot.Ukimtukana ina adefamatory way mtu katika sentensi moja, wakati umeandika yote vizuri, watu wataangalia ulipotukana.

Ingekuwa sivyo watu wangekuwa wana accumulate mazuri kila siku ili siku moja watende baya na kupata defence ya balance of actions.
 
However you spin this, serious accusation kwamba either ngono au akili yake kuwa kwenye ngono ndicho kilichompa uwaziri. Both are salacious accusations.Now they have to prove either or face a legitimate disciplinary action.

kweli kabisa.. na labda watajifunza kuwa waangalifu.. nasubiri kusikia maelezo yao ni yepi hasa.
 
Kwani utaratibu wa kuchagua waziri ukoje?Ni Rais pamoja na waziri mkuu ama kuna influence mbali mbali?Mathalan flani alimpigia debe nk...
 
kweli kabisa.. na labda watajifunza kuwa waangalifu.. nasubiri kusikia maelezo yao ni yepi hasa.

The sad thing ni kwamba, these things are not decided by the actual facts. As lawyers say, it is not what you know, it is what you can prove. Kwa kutokuwa waangalifu wanawapa msemo watu wa SS na kuharibu credibility ya waandishi.

Halafu CCM naona kama hawako consistent deliberately, inakuwa kama wanawaachia makusudi ili waandishi wajisikie wana uhuru, waandishi wanajisahau, halafu BAAM, wanawa hit na disciplinary action.

Wenzetu washajifunza zamani sana, habari hazina tamthiliya.Ukisoma New York Times unaona kabisa hawa watu walikuwa wana struggle kuielezea habari as accurately as possible bila ku overstep boundaries ya wanachoweza ku prove.

Mara nyingine magazeti yanakalia scoops kubwa kabisa kwa sababu hawana proof 100% labda wana 90% tu, editor anakataa kwa sababu anajua wakiambiwa wa prove beyond doubt atashindwa. Hii ndiyo approach tunayotakiwa kuwa nayo, labda waandishi wetu wangejifunza hili.Ukisoma sentensi kama hiyo NYT ujue wana picha na documents nyingine za ku prove kwa kiasi cha kutosheleza madai hayo.I hope these Mwanahalisi peeps have something concrete, otherwise wanaweza kupigwa suit ya mamia ya mamilioni ya shilingi.
 
Ukiandika kitabu cha kurasa 1000 na kunitukana matusi ya defamation katika sentensi moja, watu hawataangalia kurasa 1000, bali ukurasa mmoja, particularly hiyo sentensi moja.Kwa hiyo hii point ya kusema waangalie larger context hapa ni moot.Ukimtukana ina adefamatory way mtu katika sentensi moja, wakati umeandika yote vizuri, watu wataangalia ulipotukana.

Ingekuwa sivyo watu wangekuwa wana accumulate mazuri kila siku ili siku moja watende baya na kupata defence ya balance of actions.

Asante kwa shule nilikuwa sifahamu hili..
 
The sad thing ni kwamba, these things are not decided by the actual facts. As lawyers say, it is not what you know, it is what you can prove. Kwa kutokuwa waangalifu wanawapa msemo watu wa SS na kuharibu credibility ya waandishi.

Halafu CCM naona kama hawako consistent deliberately, inakuwa kama wanawaachia makusudi ili waandishi wajisikie wana uhuru, waandishi wanajisahau, halafu BAAM, wanawa hit na disciplinary action.

Wenzetu washajifunza zamani sana, habari hazina tamthiliya.Ukisoma New York Times unaona kabisa hawa watu walikuwa wana struggle kuielezea habari as accurately as possible bila ku overstep boundaries ya wanachoweza ku prove.

Mara nyingine magazeti yanakalia scoops kubwa kabisa kwa sababu hawana proof 100% labda wana 90% tu, editor anakataa kwa sababu anajua wakiambiwa wa prove beyond doubt atashindwa. Hii ndiyo approach tunayotakiwa kuwa nayo, labda waandishi wetu wangejifunza hili.Ukisoma sentensi kama hiyo NYT ujue wana picha na documents nyingine za ku prove kwa kiasi cha kutosheleza madai hayo.I hope these Mwanahalisi peeps have something concrete, otherwise wanaweza kupigwa suit ya mamia ya mamilioni ya shilingi.


haiwezekani wajiamini kiasi hicho bila shaka wana proof. everything shall be made manifest, lets just wait and see.
 
Ile alama ya kuuliza mwishoni mwa sentensi inaweza kuwa ni kinga. Kitu ambacho mwandishi anatakiwa kuki-prove, ni kwamba je mawazo ya huyo mama yameganda kwenye ngono? Kauli ya Waziri inaonyesha ufinyu wake wa kufikiri na hivyo kwa kutamka hayo maneno, ni dalili tosha kuwa mama anachowaza ni ngono. Kwani alikosa maneno mengine ya kutumia ili kuwaambiwa wanawake wenzake namna ya kuwashawishi waume zao kujiunga na CCM?

Waziri mzima huwezi kwenda kutamka maneno ya kumnyima ngono mume kisa ni kwa kuwa yuko upinzani. Hapo alipochemsha na kuonyesha kwamba mawazo yake yanafikiria nini, au anaona ngono ni muhimu sana kiasi kwamba inaweza kutumika kama chambo ili kuongeza wanachama kwenye chama chake. Hivi kweli ngono ni muhimu kiasi hicho?

Mwanamke mwelewa na mwenye busara angewaambia wanawake wenzake wawashawishi waume zao kujiunga na chama chake kwa kutumia ushawishi wa sera ama ahadi za kwamba watawapa mambo mazuri hata kama ni ahadi za uongo.

Kipengele cha pili cha hiyo sentensi, ni mwandishi anajiuliza ama anauliza swali, ina maana kilichompa uwaziri ni hicho? Kuna tofauti kati ya swali na kauli. Kauli lazima mtu anakuwa na uhakika nayo, but swali inaweza kuwa ni sehemu ya kufikiri na kutafakari kwa kina ukiwa unajaribu kutafuta jibu.

Kama serikali itaamua kulifungia hilo gazeti watakuwa na agenda yao. Lakini question mark iliyo mwishoni mwa sentensi inamlinda aliyeandika makala hiyo.
 
Tanzania judicial system imekaa kwa mfumo wa military courts.
Yaani wakishakusomea mashtaka subiri hukumu yao hata kama una utetezi hawataukonsider wakiwa wanadetermine hukumu
damn
 
Ile alama ya kuuliza mwishoni mwa sentensi inaweza kuwa ni kinga. Kitu ambacho mwandishi anatakiwa kuki-prove, ni kwamba je mawazo ya huyo mama yameganda kwenye ngono? Kauli ya Waziri inaonyesha ufinyu wake wa kufikiri na hivyo kwa kutamka hayo maneno, ni dalili tosha kuwa mama anachowaza ni ngono. Kwani alikosa maneno mengine ya kutumia ili kuwaambiwa wanawake wenzake namna ya kuwashawishi waume zao kujiunga na CCM?

Waziri mzima huwezi kwenda kutamka maneno ya kumnyima ngono mume kisa ni kwa kuwa yuko upinzani. Hapo alipochemsha na kuonyesha kwamba mawazo yake yanafikiria nini, au anaona ngono ni muhimu sana kiasi kwamba inaweza kutumika kama chambo ili kuongeza wanachama kwenye chama chake. Hivi kweli ngono ni muhimu kiasi hicho?

Mwanamke mwelewa na mwenye busara angewaambia wanawake wenzake wawashawishi waume zao kujiunga na chama chake kwa kutumia ushawishi wa sera ama ahadi za kwamba watawapa mambo mazuri hata kama ni ahadi za uongo.

Kipengele cha pili cha hiyo sentensi, ni mwandishi anajiuliza ama anauliza swali, ina maana kilichompa uwaziri ni hicho? Kuna tofauti kati ya swali na kauli. Kauli lazima mtu anakuwa na uhakika nayo, but swali inaweza kuwa ni sehemu ya kufikiri na kutafakari kwa kina ukiwa unajaribu kutafuta jibu.

Kama serikali itaamua kulifungia hilo gazeti watakuwa na agenda yao. Lakini question mark iliyo mwishoni mwa sentensi inamlinda aliyeandika makala hiyo.

Keil,

I see where you are coming from.Lakini katika societies zilizo na high accountability hata maswali unayouliza ni lazima yawe justifiable.Unaweza kuulizwa evidence unayo base swali lako.

Lawrence Summers alipata kasheshe kwa ku pose a suggestive question kwamba "Are women as good as men in science and math?" and this was in an academic setting. Watu wakamuita sexist, kwa sababu ukiuliza swali kama hilo watu watakuuliza umelitoa katika research gani? Unalibase wapi? Ukishindwa kujieleza utakuwa sexist.

Vivyo hivyo kwa Mwanahalisi, wanatakiwa kuwa so accountable hata maswali yao yanatakiwa kuwa based on a realistic frame. Ama sivyo kila mtu anaweza kumtukana kila mtu, si unaweka question mark tu mwisho wa sentensi.
 
Ile alama ya kuuliza mwishoni mwa sentensi inaweza kuwa ni kinga. Kitu ambacho mwandishi anatakiwa kuki-prove, ni kwamba je mawazo ya huyo mama yameganda kwenye ngono? Kauli ya Waziri inaonyesha ufinyu wake wa kufikiri na hivyo kwa kutamka hayo maneno, ni dalili tosha kuwa mama anachowaza ni ngono. Kwani alikosa maneno mengine ya kutumia ili kuwaambiwa wanawake wenzake namna ya kuwashawishi waume zao kujiunga na CCM?

Waziri mzima huwezi kwenda kutamka maneno ya kumnyima ngono mume kisa ni kwa kuwa yuko upinzani. Hapo alipochemsha na kuonyesha kwamba mawazo yake yanafikiria nini, au anaona ngono ni muhimu sana kiasi kwamba inaweza kutumika kama chambo ili kuongeza wanachama kwenye chama chake. Hivi kweli ngono ni muhimu kiasi hicho?

Mwanamke mwelewa na mwenye busara angewaambia wanawake wenzake wawashawishi waume zao kujiunga na chama chake kwa kutumia ushawishi wa sera ama ahadi za kwamba watawapa mambo mazuri hata kama ni ahadi za uongo.

Kipengele cha pili cha hiyo sentensi, ni mwandishi anajiuliza ama anauliza swali, ina maana kilichompa uwaziri ni hicho? Kuna tofauti kati ya swali na kauli. Kauli lazima mtu anakuwa na uhakika nayo, but swali inaweza kuwa ni sehemu ya kufikiri na kutafakari kwa kina ukiwa unajaribu kutafuta jibu.

Kama serikali itaamua kulifungia hilo gazeti watakuwa na agenda yao. Lakini question mark iliyo mwishoni mwa sentensi inamlinda aliyeandika makala hiyo.

Ahsante Keil kwa ufafanuzi. Nilipoisoma hiyo makala siku gazeti lilipotoka niliongoea na mwansheria mmoja...nae alikuwa na maoni hayo hayo...
 
Je SS alikuewa sahihi kusema kauli kama ile? Je kama wanawake wangefuata kauli yake wakaachika then wakampleelka mahakamani si angekuwa answarable! Kwanu mimi mwandishi hajakosea chochote, swali kama hilo linasaidia kuonyesha rais alivyozungukwa na wavivu wa kufikiria. Zaidi ya hapo huyo mama ni kweli mawazo yake yamekaa kingonongono kwa sababu kuna kupindi alishawahi kusema EL ni mwanamme wa shuka (rejea tume ya mwinyi).
 
hawa walishakosa kazi hata siwashangai akili zao zinatakiwa kukua na kushugulikia matatizo ya nchi hii wanachanganywa na nn mbona habari yenyewe inaeleweka
 
Back
Top Bottom