KING COBRA
JF-Expert Member
- Nov 10, 2011
- 2,782
- 864
WAHISANI KUZUIA MISAADA: MTAZAMO TOFAUTI
Maggid MjengwaToleo la 379 12 Nov 2014
NIANZE kwa kuungana na kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, aliyotoa bungeni Dodoma, Alhamisi, Novemba 6, 2014, kuonyesha masikitiko yake na ya nchi yetu kwa ujumla kwa kitendo cha wahisani kuzuia misaada ya Jumuiya ya Ulaya zikiwamo pia Norway, Canada, Japan, Benki ya Dunia na hata Benki ya Maendeleo ya Afrika.
Kama ilivyo kwa mwanadamu, hakuna duniani taifa timilifu.
Sakata la tuhuma za wizi wa fedha za IPTL/ Escrow ni 'msiba' wetu Watanzania.
Lakini, kama nchi, Serikali yetu haijakunja mikono na kusema ni 'kazi ya Mungu tu'.
Watanzania tunaona na wahisani pia wanaona, labda kama hawataki kuona, kuwa Serikali iliagiza CAG na Takukuru kulifanyia uchunguzi suala hilo.
Sasa kabla ripoti hazijawekwa mezani na kuona hatua gani wahusika wanachukuliwa, tunashuhudia wahisani wakisitisha kutoa kwenye Bajeti Kuu, kiasi cha dola za Marekani 558 sawa na shilingi bilioni 937.
Hizo ni fedha nyingi mno kwa nchi kuwa na nakisi nazo. Kuwa muhisani ni pamoja na kumheshimu unayemuhisani. Kwamba naye ana wanaomtegemea ili nao waishi na waendeshe mambo yao ya msingi ya kila siku.
Inavyoonekana, wahisani wao wanaamua bila kufanya mazungumzo ya kina na wanaowahisani. Laiti wahisani wangekaa chini na Serikali kuzungumzia azma yao ya kusitisha misaada yao kwa bajeti kuu, naamini, kuwa wangepata ufahamu mkubwa juu ya mchakato wa sakata hilo ulivyo, na kwamba wangevuta subira kusubiri matokeo ya mchakato huo.
Na katika kipindi hicho bado wangetoa fedha walizotuahidi kama nchi ili ziweze kuchangia kwenye kuhakikisha watu wetu wanaendelea kupata huduma za afya na pia watoto wetu wanaendelea kupata elimu.
Hakika, unapotembea vijijini leo unakutana na watoto wa wanyonge wa Tanzania wengine wakiwa wameamka alfajiri kuwahi shuleni, pengine bila kupata hata kikombe cha chai nyumbani, basi, unajiwa na fikra, kuwa ni kwanini makosa yenye kutendwa na wachache katika nchi yafanye wahisani kufanya maamuzi yenye kuwaumiza wengi wasio na hatia, na hata kuharibu mustakabali wao kimaisha, kwa kuwakosesha huduma bora za afya na elimu bora.
Hivyo, naungana na Waziri Mkuu wetu, Pinda katika kukosoa hatua ya wahisani ya kusitisha msaada wao kwenye Bajeti Kuu ya Serikali kwa sababu za kutaka kwanza kuona hatua za Serikali juu ya sakata la IPTL/Escrow.
Kimsingi hatua za awali zimeshachukuliwa, ikiwa ni pamoja na CAG na PCCB kupewa jukumu la kufanya uchunguzi. Kinachosubiriwa sasa ni taarifa hizo za kiuchunguzi ambazo wabunge watazijadili wiki ijayo na hata kutoa mapendekezo ya hatua mujarab za Serikali kuchukua.
Hivyo basi, ni mtazamo wangu kuwa wahisani wangesubiri tuifikie hatua hiyo ndipo nao wapime juu ya hizo hatua zilizochukuliwa, na hata kama hawataridhika nazo, diplomasia inawataka waheshimiwa wahisani wakae na Serikali yetu kujadiliana juu ya hatua wanazoazimia kuchukua. Hiyo ndiyo maana halisi ya ushirikiano wa kimaendeleo.
Maana, sakata hili ni kubwa, limehitaji uchunguzi mkubwa na wenye umakini, na maamuzi ya hatua zitakazochukuliwa bila shaka yatalitikisa Taifa. Tulikofikia tumeshakula ng'ombe mzima na umebaki mkia. Wahisani wangetusubiri tu badala ya kukimbilia kukata misaada yao.
Na kwa vile wahisani ni washirika wetu katika maendeleo, ifahamike pia, kuwa moja ya changamoto za maendeleo ni ufisadi wa baadhi ya viongozi. Wahisani watusaidie katika kupambana na ufisadi, lakini si kwa kukimbilia kusitisha misaada ya bajeti yenye kulenga kumsaidia mwananchi wa kawaida.
Hatua hii ya wahisani, inatukumbusha umuhimu wa kujitegemea kama nchi. Tupambane na mafisadi wetu kuhakikisha kuwa hawaendelei kutafuna vya kwenye hazina yetu.
HISTORIA YA MAGGID MJENGWA
Maggid ni Msangu wa kutoka Kijiji cha Nyeregete, Madibira wilayani Mbalari katika Mkoa wa Mbeya. Ni mtoto wa kaka yake Kanali Edmund Mjengwa, ambaye alipata kuwa Mbunge wa Mbalari kati ya mwaka 1995-2005.
Alizaliwa Machi 11, 1966 jijini Dar es Salaam. Akasoma shule mbalimbali ikiwemo Tambaza Sekondari alikohitimu kidato cha nne Novemba 1987 na baadaye Sangu Sekondari jijini Mbeya alikohitimu kidato cha sita Mei 1989.
Baadaye akajiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa Sheria kwa mwaka mmoja ambapo alipangwa katika Kambi ya Itende JKT mjini Mbeya.
Ni wakati akiwa sekondari pale Sangu ndipo alipokutana na Mia Berghdal, binti wa Kiswedi ambaye sasa ndiye mkewe na mama wa watoto wake wanne wa kiume wote Olle (17), John (15) na mapacha Gustav na Manfred (12). Wakati huo binti huyo alikuwa akifanya kazi za kujitolea katika mashirika kutoka nchi za Scandinavia.
Bahati ya mtende ya kupendwa na binti wa Kizungu na mapenzi motomoto hatimaye vikampa tiketi ya kwenda Sweden mwaka 1992 baada ya binti huyo kumaliza mkataba wake na kurejea kwao, ambako ndiko walikoanza maisha ya ndoa na kuzaa watoto wao wawili wa kwanza.
Baada ya kukaa huko kwa takriban miaka kumi, ndipo Agosti 2001 akajiunga na Chuo Kikuu cha Linkoping (inatamkwa Linchoping) ambako alichukua shahada ya Elimu, akiwa amechepua katika Elimu ya Masafa. Alihitimu Aprili 2004, mwaka ambao ndio walirudi Tanzania baada ya mkewe kupata kazi katika Shirika la Karibu Tanzania Association (KTA) ambalo ni tawi la shirika la Karibu Sweden Association (KSA). Walirejea mwezi Juni 2004.
Maggid naye akapata kazi kwenye shirika hilo akiwa ameajiriwa kama Mshauri wa Ufundi akishughulika na program za Elimu ya Masafa kwa ngazi ya Stashahada kwenye Programu ya Taifa ambayo ilikuwa ya majaribio. Shirika hilo linafanya kazi kwenye Vyuo vya Maendeleo ya Jamii/Wananchi, hivyo linaangaliwa kwa karibu na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto.
Kwa kuwa aliomba kujiunga na chuo akiwa Sweden na akasomeshwa huko huko, basi hata ajira yake ndani ya KTA aliipata moja kwa moja kutoka Sweden kupitia shirika la ForumSyd kama ilivyo kwa mkewe.
Kwa sasa Maggid Mjengwa ndiye Mkurugenzi Mtendaji wa KTA na ameajiriwa akiwa Tanzania. Nitawaeleza ilikuwaje mpaka akapata ukurugenzi huo na lini.
MAGGID MJENGWA ANAWATUMIKIA MAFISADI ANGALIAHAPA
maggid mjengwa <mjengwamaggid@gmail.com> 15/04/2009
to Asha-Rose Migiro <migiro@un.org>
Mama Mpendwa,
Salaam nyingi na pole na kazi zako nyingi. Bila shaka, ulihitaji retreat kama ulivyoandika. Kazi na safari zako ni nyingi lakini nina imani unaona na kujifunza mengi pia.
Naandika alfajiri hii nikiwa Dar Es Salaam. Pasaka imepita salama na kazi zetu zinaendelea. Jana nilikuwa Wizarani katika maandalizi yetu ya kozi ile ya Diploma kwa Wakufunzi wa Vyuo Vya Maendeleo ya Wananchi. Leo nitarudi tena huko kukutana na Bwana Msimbe, huyu ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii (bila shaka unamkumbuka).
Tuje kwenye yangu binafsi, harakati zangu za kuisaidia jamii kupitia gazeti la ' KWANZA JAMII' nilizianza rasmi majuma matatu yaliyopita.
Juma lijalo tunaingia toleo la nne. Nitapenda nikutumie matoleo yote kwa njia ya posta kila yanapofikia matoleo manne. Naam. Tumeanza vema ingawa mwanzo siku zote ni mgumu. Wasomaji wameanza kutukubali. Tunasambaza nchi nzima. Tumeanza na nakala elfu sita.
Utakumbuka kuna wakati nilikugusia kuhusu Msaidizi wa Muheshimiwa kuwasiliana nami kutaka niwasaidie kupitia media. Wazo la kuanzisha 'KWANZA JAMII' nilikuwa nalo. Sikutaka kusaidiwa kifedha kuendesha gazeti bali matangazo maana kimsingi nami nilikuwa na bado nina nia njema kabisa ya kuisaidia Serikali na jamii kwa ujumla. Nikagundua kuwa aliyetumwa kuongea nami alikuwa akitanguliza maslahi binafsi (anaitwa bwana Luwavi). Yeye si mtu wa habari, ni msaidizi wa Mheshimiwa katika masuala ya siasa. Nikaona ni heri nikutane na Salva Rweyemamu (Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu). Huyu tunafahamiana kwa miaka mingi. Nilikutana naye majuma matatu yaliyopita. Salva alinielewa kwa dakika kumi tu, kuwa nilichohitaji si fedha za Ikulu au mfanyabiashara ili niendeshe gazeti bali matangazo ili nibaki na uhuru wangu. Bahati mbaya, siku hiyo tuliyokutana na Salva pale Palm Beach Hotel, naye alikuwa anaanza likizo yake ambayo ingempeleka kwao Kagera na kwa familia yake, London.
Kilichopo sasa, nisingependa kuweka mayai yangu yote kwenye kikapu kimoja. Naliona ' KWANZA JAMII' kama gazeti la miaka zaidi ya ishirini ijayo, si la uchaguzi au kukidhi maslahi ya wakati uliopo kwa kikundi kidogo cha watu. Siwezi kumtegemea Salva Rweyemamu arudi, anisaidie na matangazo ndio gazeti liende. Nahitaji kwenda na matoleo 20 ya 'KWANZA JAMII' bila kukosa kila juma na kuanzia sasa ili gazeti hili liweze kusimama kwa nguvu za mauzo kwa wasomaji na matangazo yatakayopatikana. Kwa sasa naingia toleo la nne juma lijalo. Gharama za uendeshaji ni kubwa, mke wangu na mimi tulikubaliana mwezi uliopita tuuze kiwanja chetu kilichopo Bagamoyo, block E, eneo la Magambani karibu kabisa na pwani ya bahari ya Hindi. Kina ukubwa wa M. 70 upana na M. 100 urefu (Ni viwanja viwili kwa pamoja). Nilitangaza kinauzwa kupitia blogu yangu, sikupata hata simu moja, juma hili nitatangaza pia kupitia Daily News na Habari Leo. Bei ya kiwanja hiki tumeipanga kuwa ni shilingi milioni 80. Kimepimwa na kina ofa. Anayetaka anaweza ku-process kupata hati ya kiwanja Idara ya Ardhi, Bagamoyo au Dar Es Salaam.
Ninachokuomba, ingawa naandika hili kwa ugumu sana kwa kuwa nisingependa kabisa nikusumbue kwa issue kama hizi. Kama una interest nacho, naweza kukiuza kwako kwa punguzo la shilingi za Kitanzania milioni 20 kwa maana naweza kukubali kupokea Shilingi za Kitanzania milioni 60. Na kama itakuwa vigumu kunilipa fedha taslimu, naweza kukubali kukumilikisha kiwanja na kupokea shilingi milioni mbili kila wiki hadi deni litakapomalizika. Ni kiasi hicho cha fedha ninachohitaji kwa sasa, na kwa kila wiki kwa matoleo 20 kutoka sasa ili ' KWANZA JAMII' kama gazeti liweze kuwafikia wanajamii, mijini na vijijini. Mama huo ndio mtihani nilio nao mwanao kwa sasa, inahusu kulinda uhuru wangu, maana nafahamu kuna walio tayari kunichangia kiasi hicho cha fedha kwa wiki lakini kwa gharama ya uhuru wangu.
Hilo la mwisho nisingependa linitokee na ndio maana ya kujikaza huku kukuomba msaada na hata ushauri wako.
Mwisho, kama wewe binafsi hutakuwa na haja kwa sasa ya kununua kiwanja hicho, basi, kama kuna rafiki, au jamaa yako hapo ulipo na mwenye haja hiyo naomba uniunganishe naye. Nitakuwa tayari naye anunue kwa taratibu nilizokupa wewe alimradi unamwamini kuwa atanimalizia deni langu.
Nikutakie kazi na afya njema.
Mwanao,
Maggid
Maggid MjengwaToleo la 379 12 Nov 2014
NIANZE kwa kuungana na kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, aliyotoa bungeni Dodoma, Alhamisi, Novemba 6, 2014, kuonyesha masikitiko yake na ya nchi yetu kwa ujumla kwa kitendo cha wahisani kuzuia misaada ya Jumuiya ya Ulaya zikiwamo pia Norway, Canada, Japan, Benki ya Dunia na hata Benki ya Maendeleo ya Afrika.
Kama ilivyo kwa mwanadamu, hakuna duniani taifa timilifu.
Sakata la tuhuma za wizi wa fedha za IPTL/ Escrow ni 'msiba' wetu Watanzania.
Lakini, kama nchi, Serikali yetu haijakunja mikono na kusema ni 'kazi ya Mungu tu'.
Watanzania tunaona na wahisani pia wanaona, labda kama hawataki kuona, kuwa Serikali iliagiza CAG na Takukuru kulifanyia uchunguzi suala hilo.
Sasa kabla ripoti hazijawekwa mezani na kuona hatua gani wahusika wanachukuliwa, tunashuhudia wahisani wakisitisha kutoa kwenye Bajeti Kuu, kiasi cha dola za Marekani 558 sawa na shilingi bilioni 937.
Hizo ni fedha nyingi mno kwa nchi kuwa na nakisi nazo. Kuwa muhisani ni pamoja na kumheshimu unayemuhisani. Kwamba naye ana wanaomtegemea ili nao waishi na waendeshe mambo yao ya msingi ya kila siku.
Inavyoonekana, wahisani wao wanaamua bila kufanya mazungumzo ya kina na wanaowahisani. Laiti wahisani wangekaa chini na Serikali kuzungumzia azma yao ya kusitisha misaada yao kwa bajeti kuu, naamini, kuwa wangepata ufahamu mkubwa juu ya mchakato wa sakata hilo ulivyo, na kwamba wangevuta subira kusubiri matokeo ya mchakato huo.
Na katika kipindi hicho bado wangetoa fedha walizotuahidi kama nchi ili ziweze kuchangia kwenye kuhakikisha watu wetu wanaendelea kupata huduma za afya na pia watoto wetu wanaendelea kupata elimu.
Hakika, unapotembea vijijini leo unakutana na watoto wa wanyonge wa Tanzania wengine wakiwa wameamka alfajiri kuwahi shuleni, pengine bila kupata hata kikombe cha chai nyumbani, basi, unajiwa na fikra, kuwa ni kwanini makosa yenye kutendwa na wachache katika nchi yafanye wahisani kufanya maamuzi yenye kuwaumiza wengi wasio na hatia, na hata kuharibu mustakabali wao kimaisha, kwa kuwakosesha huduma bora za afya na elimu bora.
Hivyo, naungana na Waziri Mkuu wetu, Pinda katika kukosoa hatua ya wahisani ya kusitisha msaada wao kwenye Bajeti Kuu ya Serikali kwa sababu za kutaka kwanza kuona hatua za Serikali juu ya sakata la IPTL/Escrow.
Kimsingi hatua za awali zimeshachukuliwa, ikiwa ni pamoja na CAG na PCCB kupewa jukumu la kufanya uchunguzi. Kinachosubiriwa sasa ni taarifa hizo za kiuchunguzi ambazo wabunge watazijadili wiki ijayo na hata kutoa mapendekezo ya hatua mujarab za Serikali kuchukua.
Hivyo basi, ni mtazamo wangu kuwa wahisani wangesubiri tuifikie hatua hiyo ndipo nao wapime juu ya hizo hatua zilizochukuliwa, na hata kama hawataridhika nazo, diplomasia inawataka waheshimiwa wahisani wakae na Serikali yetu kujadiliana juu ya hatua wanazoazimia kuchukua. Hiyo ndiyo maana halisi ya ushirikiano wa kimaendeleo.
Maana, sakata hili ni kubwa, limehitaji uchunguzi mkubwa na wenye umakini, na maamuzi ya hatua zitakazochukuliwa bila shaka yatalitikisa Taifa. Tulikofikia tumeshakula ng'ombe mzima na umebaki mkia. Wahisani wangetusubiri tu badala ya kukimbilia kukata misaada yao.
Na kwa vile wahisani ni washirika wetu katika maendeleo, ifahamike pia, kuwa moja ya changamoto za maendeleo ni ufisadi wa baadhi ya viongozi. Wahisani watusaidie katika kupambana na ufisadi, lakini si kwa kukimbilia kusitisha misaada ya bajeti yenye kulenga kumsaidia mwananchi wa kawaida.
Hatua hii ya wahisani, inatukumbusha umuhimu wa kujitegemea kama nchi. Tupambane na mafisadi wetu kuhakikisha kuwa hawaendelei kutafuna vya kwenye hazina yetu.
HISTORIA YA MAGGID MJENGWA
Maggid ni Msangu wa kutoka Kijiji cha Nyeregete, Madibira wilayani Mbalari katika Mkoa wa Mbeya. Ni mtoto wa kaka yake Kanali Edmund Mjengwa, ambaye alipata kuwa Mbunge wa Mbalari kati ya mwaka 1995-2005.
Alizaliwa Machi 11, 1966 jijini Dar es Salaam. Akasoma shule mbalimbali ikiwemo Tambaza Sekondari alikohitimu kidato cha nne Novemba 1987 na baadaye Sangu Sekondari jijini Mbeya alikohitimu kidato cha sita Mei 1989.
Baadaye akajiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa Sheria kwa mwaka mmoja ambapo alipangwa katika Kambi ya Itende JKT mjini Mbeya.
Ni wakati akiwa sekondari pale Sangu ndipo alipokutana na Mia Berghdal, binti wa Kiswedi ambaye sasa ndiye mkewe na mama wa watoto wake wanne wa kiume wote Olle (17), John (15) na mapacha Gustav na Manfred (12). Wakati huo binti huyo alikuwa akifanya kazi za kujitolea katika mashirika kutoka nchi za Scandinavia.
Bahati ya mtende ya kupendwa na binti wa Kizungu na mapenzi motomoto hatimaye vikampa tiketi ya kwenda Sweden mwaka 1992 baada ya binti huyo kumaliza mkataba wake na kurejea kwao, ambako ndiko walikoanza maisha ya ndoa na kuzaa watoto wao wawili wa kwanza.
Baada ya kukaa huko kwa takriban miaka kumi, ndipo Agosti 2001 akajiunga na Chuo Kikuu cha Linkoping (inatamkwa Linchoping) ambako alichukua shahada ya Elimu, akiwa amechepua katika Elimu ya Masafa. Alihitimu Aprili 2004, mwaka ambao ndio walirudi Tanzania baada ya mkewe kupata kazi katika Shirika la Karibu Tanzania Association (KTA) ambalo ni tawi la shirika la Karibu Sweden Association (KSA). Walirejea mwezi Juni 2004.
Maggid naye akapata kazi kwenye shirika hilo akiwa ameajiriwa kama Mshauri wa Ufundi akishughulika na program za Elimu ya Masafa kwa ngazi ya Stashahada kwenye Programu ya Taifa ambayo ilikuwa ya majaribio. Shirika hilo linafanya kazi kwenye Vyuo vya Maendeleo ya Jamii/Wananchi, hivyo linaangaliwa kwa karibu na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto.
Kwa kuwa aliomba kujiunga na chuo akiwa Sweden na akasomeshwa huko huko, basi hata ajira yake ndani ya KTA aliipata moja kwa moja kutoka Sweden kupitia shirika la ForumSyd kama ilivyo kwa mkewe.
Kwa sasa Maggid Mjengwa ndiye Mkurugenzi Mtendaji wa KTA na ameajiriwa akiwa Tanzania. Nitawaeleza ilikuwaje mpaka akapata ukurugenzi huo na lini.
MAGGID MJENGWA ANAWATUMIKIA MAFISADI ANGALIAHAPA
maggid mjengwa <mjengwamaggid@gmail.com> 15/04/2009
to Asha-Rose Migiro <migiro@un.org>
Mama Mpendwa,
Salaam nyingi na pole na kazi zako nyingi. Bila shaka, ulihitaji retreat kama ulivyoandika. Kazi na safari zako ni nyingi lakini nina imani unaona na kujifunza mengi pia.
Naandika alfajiri hii nikiwa Dar Es Salaam. Pasaka imepita salama na kazi zetu zinaendelea. Jana nilikuwa Wizarani katika maandalizi yetu ya kozi ile ya Diploma kwa Wakufunzi wa Vyuo Vya Maendeleo ya Wananchi. Leo nitarudi tena huko kukutana na Bwana Msimbe, huyu ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii (bila shaka unamkumbuka).
Tuje kwenye yangu binafsi, harakati zangu za kuisaidia jamii kupitia gazeti la ' KWANZA JAMII' nilizianza rasmi majuma matatu yaliyopita.
Juma lijalo tunaingia toleo la nne. Nitapenda nikutumie matoleo yote kwa njia ya posta kila yanapofikia matoleo manne. Naam. Tumeanza vema ingawa mwanzo siku zote ni mgumu. Wasomaji wameanza kutukubali. Tunasambaza nchi nzima. Tumeanza na nakala elfu sita.
Utakumbuka kuna wakati nilikugusia kuhusu Msaidizi wa Muheshimiwa kuwasiliana nami kutaka niwasaidie kupitia media. Wazo la kuanzisha 'KWANZA JAMII' nilikuwa nalo. Sikutaka kusaidiwa kifedha kuendesha gazeti bali matangazo maana kimsingi nami nilikuwa na bado nina nia njema kabisa ya kuisaidia Serikali na jamii kwa ujumla. Nikagundua kuwa aliyetumwa kuongea nami alikuwa akitanguliza maslahi binafsi (anaitwa bwana Luwavi). Yeye si mtu wa habari, ni msaidizi wa Mheshimiwa katika masuala ya siasa. Nikaona ni heri nikutane na Salva Rweyemamu (Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu). Huyu tunafahamiana kwa miaka mingi. Nilikutana naye majuma matatu yaliyopita. Salva alinielewa kwa dakika kumi tu, kuwa nilichohitaji si fedha za Ikulu au mfanyabiashara ili niendeshe gazeti bali matangazo ili nibaki na uhuru wangu. Bahati mbaya, siku hiyo tuliyokutana na Salva pale Palm Beach Hotel, naye alikuwa anaanza likizo yake ambayo ingempeleka kwao Kagera na kwa familia yake, London.
Kilichopo sasa, nisingependa kuweka mayai yangu yote kwenye kikapu kimoja. Naliona ' KWANZA JAMII' kama gazeti la miaka zaidi ya ishirini ijayo, si la uchaguzi au kukidhi maslahi ya wakati uliopo kwa kikundi kidogo cha watu. Siwezi kumtegemea Salva Rweyemamu arudi, anisaidie na matangazo ndio gazeti liende. Nahitaji kwenda na matoleo 20 ya 'KWANZA JAMII' bila kukosa kila juma na kuanzia sasa ili gazeti hili liweze kusimama kwa nguvu za mauzo kwa wasomaji na matangazo yatakayopatikana. Kwa sasa naingia toleo la nne juma lijalo. Gharama za uendeshaji ni kubwa, mke wangu na mimi tulikubaliana mwezi uliopita tuuze kiwanja chetu kilichopo Bagamoyo, block E, eneo la Magambani karibu kabisa na pwani ya bahari ya Hindi. Kina ukubwa wa M. 70 upana na M. 100 urefu (Ni viwanja viwili kwa pamoja). Nilitangaza kinauzwa kupitia blogu yangu, sikupata hata simu moja, juma hili nitatangaza pia kupitia Daily News na Habari Leo. Bei ya kiwanja hiki tumeipanga kuwa ni shilingi milioni 80. Kimepimwa na kina ofa. Anayetaka anaweza ku-process kupata hati ya kiwanja Idara ya Ardhi, Bagamoyo au Dar Es Salaam.
Ninachokuomba, ingawa naandika hili kwa ugumu sana kwa kuwa nisingependa kabisa nikusumbue kwa issue kama hizi. Kama una interest nacho, naweza kukiuza kwako kwa punguzo la shilingi za Kitanzania milioni 20 kwa maana naweza kukubali kupokea Shilingi za Kitanzania milioni 60. Na kama itakuwa vigumu kunilipa fedha taslimu, naweza kukubali kukumilikisha kiwanja na kupokea shilingi milioni mbili kila wiki hadi deni litakapomalizika. Ni kiasi hicho cha fedha ninachohitaji kwa sasa, na kwa kila wiki kwa matoleo 20 kutoka sasa ili ' KWANZA JAMII' kama gazeti liweze kuwafikia wanajamii, mijini na vijijini. Mama huo ndio mtihani nilio nao mwanao kwa sasa, inahusu kulinda uhuru wangu, maana nafahamu kuna walio tayari kunichangia kiasi hicho cha fedha kwa wiki lakini kwa gharama ya uhuru wangu.
Hilo la mwisho nisingependa linitokee na ndio maana ya kujikaza huku kukuomba msaada na hata ushauri wako.
Mwisho, kama wewe binafsi hutakuwa na haja kwa sasa ya kununua kiwanja hicho, basi, kama kuna rafiki, au jamaa yako hapo ulipo na mwenye haja hiyo naomba uniunganishe naye. Nitakuwa tayari naye anunue kwa taratibu nilizokupa wewe alimradi unamwamini kuwa atanimalizia deni langu.
Nikutakie kazi na afya njema.
Mwanao,
Maggid