Mathanzua
JF-Expert Member
- Jan 4, 2017
- 15,848
- 20,697
Mzee Tupatupa kama binadamu mengine yanauma.Hivi Jokate awe boss wa Mkurugenzi na DAS kweli,mh,hapana,hii haijakaa vizuri.Tangu Jumamosi niliporejea Dar es Salaam nikitokea mkoani Iringa, nimekuwa nikipokea simu za makada kindakindaki wenzangu wa CCM za kunilalamikia kana kwamba nina mkono wangu katika teuzi zilizofanywa kwa ujuzi za juzi. Teuzi za Makatibu Wakuu wa Wizara; Makatibu Tawala wa Mikoa; Wakuu wa Mikoa na Wilaya.
Makada wamefikia hatua ya kunisema kwa kuhema kuwa nilikuwa Iringa kumng'oa dada yangu Masenza. Ukweli ni kuwa dada Masenza amestaafu na mwanangu Hapi anakwenda kumpokea kijiti akiwa fiti kutokea jijini Dar es Salaam, wilayani Kinondoni. Makada wanalalamika na kununa kuwa wao hawaonekani. Wanaonekana wale 'wapya' chamani au watumiaji wa mitandao na vuombo vya habari vinginevyo.
Makada wananung'unika na kuhuzunika. Wanakumbuka mbali. Wananisimulia walivyojiunga na CCM kupitia UVCCM na kukulia humo. Wakakitetea chama na kukipigania. Kampenini, wakakinadi bila kusita kwa nguvu zao zote hadi ushindi ukapatikana. Ingawa wanakwepa kuniambia, najua kuwa walitegemea kuwa baada ya uchaguzi 'wangefutwa jasho' hata kama ingekuwa kwa muda mfupi.
Makada wenzangu, hakika, wanaonekana kuguswa na 'kuanza kununa'. Nawasihi makada wenzangu wote kindakindaki wa CCM ambao bado 'hamjafutwa jasho' muheshimu maamuzi ya Rais na Mwenyekiti wetu wa Taifa, Daktari John Pombe Magufuli. Tumuunge mkono Zaidi na Zaidi. Tumpe nguvu na kumuombea. Hakuna haja ya kununa. Hakuna haja ya kujisikia vibaya. Hakuna haja ya kurudi nyuma kwenye harakati za kichama.
CCM hoyeeeeeeeeeeeee!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam