Makada wa CCM hawazomewi

LUCAS KISIMIR

Member
Sep 11, 2012
29
4
Makada wa CCM hawazomewi na watu wastaarabu baliwatu walioandaliwa kwa kumezeshwa viroba (Pombe kali), ili wapoteze viwango vyautu na utashi wao, hali inayowawezesha kuvamia vikao vya CCM na kupiga mayowekunakopunguza utulivu na masikilizano. Wazomeaji hao ni vijana wadogowaliopotoka kimaadili kwani huwazomea viongozi ambao kiumri wako sawa na wazaziwao au hata kuwazaidi. Hizo ndizo Siasa za baadhi ya wapinzani ambaohawana hoja mbadala za kuwasilisha mbele ya umma bali kuvuruga Chama chenye SERAdhahiri na ILANI inayotekelezwa kwa kulenga mahitaji halisi ya umma kupitia Serikaliza Mitaa. Wapinzani hawawezi kuwasilisha mipango yao ya maendeleo bali lao ni kutoaporojo za kukichonganisha CCM na Umma. Hawana jipya.

Generali Ulimwengu kama Mtanzania mzalendo, alikuwana nia njema katika kuasisi mitandao ya kijamii. Kwa uzalendo wake aliamuakuweka mfumo wa kimawasiliano ili WaTanzania wenzake wapate fursa yakubadilishana mawazo ili kuboreshana kifikra. Mchango wake sasa umewamiwa nawatu ambao wanachukulia ubunifu huo kama fursa ya kutukanana na kukashifiana nakupotosha kila jambo kama kwamba wanapo pengine pa kuhamia wakipachafua palipopao. Watumiaji wengine wa mitandao ya kijamii hawajitofautishi na bomba ambalokwa asili yake halichagui kati ya kupitisha maji-taka au maji safi!

Hawachujihabari na ikiwa wamebahatika kuzifahamu chembechembe za ukweli wanakosauungwana wa kuisawazisha habari ili kuiweka katika mwanga bora ili watu waijuekweli iliyo kweli.
Kumbukeni kwamba watoto wa Tanzania wanasoma hayomnayoyaandika na hivyo mnawapa uridhi mchafu nao hubaki kwenye giza tatanishi wakidhanikwamba hayo yasemwayo ni kweli na hivyo kubakia katika wingu la dhana potofu!! Siouungwana mtu kushupalia jambo asilolijua kwa ushabiki tu na kwa kuwa kalionakwenye mtandao na kujiweka katika nafasi kama kwamba analifahamu lisemwalo!Wapo watu wanajiofanya wanajua wasichokijua kumbe hawajui wajuacho!

Ikumbukwe kwamba Waziri Professor Maghembe alikuwana ziara maalum ya kitaifa kuzindua Miradi ya ya maji katika Vijiji 10 kwenyekila Halmashauri nchini. Uzinduzi huu ulifanyikia KITAIFA katika kijiji cha Endagilleambapo maji yatatosheleza kwa 246%. Hili lilikuwa tukio la shukrani kwa Mungukwa ufanisi huo wa kupatikana kwa maji yatakayotumika kwa binadamu na mifugoyao. Maji hayo yataboresha kipato katika ngazi ya kaya, kwa watu kuanzishabustani na hivyo kuuza mazao yao. Kwa mantiki hiyo, mzunguko wa fedha kijijiniutaboreka. Sasa, katika mazingira hayo, ni binadamu gani mtimilifuambaye anaweza kukosa moyo wa shukrani kwa Mungu hadi kumzomea Kiongozialiyekuja kuwaondolea adha ya muda mrefu ya ukosefu wa maji?

Kazi ya kipaumbele(aliyoijia) Professor kaifanya kwenye kata ya jirani (Mamire) na baada ya hapo akaombwakufika kwenye Kata ya Gallapo, ambayo, wala haikuwa kwenye ratiba ya shughulizake za siku! Kutokana na tabia yake ya upendo, upole, utu na uungwana, alikubaliombi la viongozi na kuchepusha ratiba na muda wake ili apate fursa ya kuwaonawana Gallapo wanaokabiliwa na adha ya upungufu wa maji kwa muda mrefu.

Alikubali! Kwa watu wanaomjua Mungu, wananchi haowalipata "Bahati ya Mtende"
Waziri Maghembe hakuzomewa na wananchi wa Gallapo.Waziri huyo alitoa maelekezo ya njia za utatuzi wa kero ya upungufu wa maji-akiwaWaziri mwenye dhamana. Aliahidi KISIMA kipya cha MAJI ambacho kitakamilika kablaya mwisho wa Mwaka wa Fedha, mradi wa maji uliopo uboreshwe na masualayanayolalamikiwa na wananchi ambayo Mkuu wa Mkoa aliyatolea maagizo namaelekezo yatekelezwe haraka sana. Je, huyo ndiye kiongozi wa kuzomewa?

Ukweli wa hali halisi ni kwamba Vijana waliandaliwakufanya vurugu kwa kuwa Zito Kabwe amepanga kufanya ziara yake Gallapo. Walichobainini kwamba hawatakuwa na hoja yenye mashiko kwa kuwa Serikali imeshapataufumbuzi wa tatizo lililokuwa likiwakabili wanaGallapo. Sasa, hoja na agendainayosikilizika kwa wananchi wangeipata wapi kwa ufanisi huo wa kudumu waSerikali ya CCM?Akina mama wa Gallapo pamoja na wananchi wenyemapenzi mema wanaishukuru Serikali kwa utekelezaji wake mahiri. Madhaifu yakiutekelezaji yatashughulikiwa na Mkuu wa Mkoa kwa hatua za ufuatiliaji. Wakati huo, muda ulikuwa Saa 10 jioni, alimbidi MheshimiwaMaghembe kwa heshima aombe ruhusa ya kuondoka mkutanoni kwenda Arusha nahatimaye KIA ambako atapanda ndege kwenda Dar-es-salaam na ndiyo sababu yakuomba asiulizwe maswali kwa mambo muhimu yafuatayo;

1.
Mudaulikwisha na hivyo asingeweza kuyajibu maswali ya wananchi kikamilifu na kwaufanisi. Hakutaka kulipua,
2. Aliwapawataalamu maelekezo ya mambo ya kufanya kwa kuwa watu wanahitaji huduma ya majina wala sio maneno matupu,
3.
Taarifaya mgogoro wa maji Gallapo ilikwisha-kuwasilishwa kwake kwa maandishi,
4. Maelekezoya Mkuu wa Mkoa yatatekelezwa mara arudipo kutoka msibani,
5. Alitakiwakwenda Arusha na hatimaye KIA atakaporuka kwenda Dar. Ndege haisubiri pindimuda unapowadia,
6. AliwaagizaWataalamu aliofuatana nao warudi kufanya uchunguzi wa tatizo la maji Gallapo kuanziasiku ya tatu na taarifa iwasilishwe kwake kabla ya ziara yake ya Gallapo,
7.
AlitoaAhadi ya kurudi tena Gallapo ndani ya Mwezi Desemba ili ashiriki katika uchambuziwa tatizo hadi ufumbuzi wa kudumu uapatikane huku tukiendea kipindi chautekelezaji wa mradi.
Hakuna jambo la kuzomea hapa ila tu athari yamaandalizi ya vijana kwa ajili ya ziara ya Zitto Kabwe anayezuru Gallapo.

Kwa mantikihii, hata wewe mwenyewe utajua kwamba tatizo hilo la maji ndiyo uhai na kiinicha ziara ya wapinzani Gallapo. Mtu kama Kabwe akiyajua haya, bila shakaatapuuza ziara hiyo na kwenda kwingineko! Mungu anatuelekeza kuijua kweliitakayotuweka huru na tukiitumia kweli tutakuwa huru kweli kweli.
 
Ni kweli kabisa wanawanunulia viroba na ndumu kwa akili timamtu huwezi zomea kama taahira kuna chama wanavaa kama mgambo ndo zao hao ni watu wa fujo sana
 
Wanajizomea woooooooo!! halafu wanashuka jukwaaani. Kamuulize Pinda pale uwanja wa sahara Mwanza, WAsara pale Bunda na Pinda huyu huyu pale Mkendo Musoma. Utapata kufyatuka ubungo wako maana uko gandamana na magamba.
 
Jipeni moyo, wale kina mama wa UWT waliomzomea Shyrose baada ya kumtwanga Sofia Simba swali walikua wamemezeshwa viroba???
Vipi wanaCCM waliotwangana kwa viti na makonde kwenye chaguzi za ccm za ndani ni wapinzani? je walikua wamemezeshwa viroba??

NB: Jifunze kuweka paragraph hata kama hii ni post yako ya 3 tangu ujiunge JF.

HATARI:
Weka mbali na Tembo.

 
Ningependa wachapane badala ya kuzomea maana maneno matupu hayavunji mfupa. Unadhani bangi mchezo? Wameanza na kuzomea mwishowe watafanya kweli.
 
Jipeni moyo, wale kina mama wa UWT waliomzomea Shyrose baada ya kumtwanga Sofia Simba swali walikua wamemezeshwa viroba???
Vipi wanaCCM waliotwangana kwa viti na makonde kwenye chaguzi za ccm za ndani ni wapinzani? je walikua wamemezeshwa viroba??

NB: Jifunze kuweka paragraph hata kama hii ni post yako ya 3 tangu ujiunge JF.

HATARI:
Weka mbali na Tembo.


Hawa hapa ni viroba oclock.....

ImageUploadedByJamiiForums1353683518.663461.jpg

ImageUploadedByJamiiForums1353683566.165302.jpg
 
Mheshimiwa mleta mada una uhakika na unachosema kwamba wananunuliwa viroba ili wawazomee viongozi wa CCM?

Nina wasiwasi na hilo hitimisho lako, nadhani washauri hao viongozi wako wafanye utafiti wajue sababu a wao kuzomewa badala ya kufikiria tu na kuropoka!
 
Ninafahamu kwa uhakika kwamba ukweli haupendezi kwa wahalifu kuwa unawashughulisha! Uongo ni nja nyepesi ya kukwepa uwajibikaji. Tulikwishafunzwa kupitia biblia kwamba njia ya maanguko ni pana, nyepesi na haraka. Ikiwa UONGO na UKWELI vitashindanishwa mbio vitoke Moro kwenda Dar Saa 1:30, wakati UKWELI unavaa track suit yake ili uingie mbioni, UONGO wenyewe utakuwa ukivua suti yake Dar ili uoge kuondoa jasho! Umefika zamani sana! Ni jambo la ajabu watu wazima wakitaka kulazimisha wenzao kukubaliana na uongo wa kiajabu kwamba duniani kuna kizazi malum cha watu wabaya. Sisi CCM hatuwahi kusema kamba kwenye upinzani wapo wabwia viroba tu kama ninyi mnavyowaita wanaCCM wote jina moja la mafisadi. Nyumbani kwenu, ndugu zako wote wako kama ulivyo wewe? Je, duniani kunawat wa kurudufishwa? Haiwezekani ikatokea kwamba udhaifu wa mtu moja umegeuka kuwa wa jamii nzima wala kwamba wanaCCM wote ni wa kurudufishwa? CCM ni chama chenye historia isiyofutika kwa kuwa tu wewe unakuwadia na kuiga siasa za ughaibuni zilizobomoa dola zote zilizokuwa maarufu ulimwenguni. Achana na siasa za maji taka.
 
Jipeni moyo, wale kina mama wa UWT waliomzomea Shyrose baada ya kumtwanga Sofia Simba swali walikua wamemezeshwa viroba???
Vipi wanaCCM waliotwangana kwa viti na makonde kwenye chaguzi za ccm za ndani ni wapinzani? je walikua wamemezeshwa viroba??

NB: Jifunze kuweka paragraph hata kama hii ni post yako ya 3 tangu ujiunge JF.

HATARI:
Weka mbali na Tembo.


Tehe tehe tehe. Hii imekaa vyema mkuu Daudi. Wanakimbizana na kivuli chao. Vipi wale vijana waliovuana nguo pale barabarani wakatwangana ngumi za ridhaa, mbele ya jengo la UVCCM wakimpokea kijeba!

Sijui kwa nini hawatambui, watu hawataki mabadiliko ya sura, wanataka maisha bora mliyoahidi badala yake yamekuwa maisha magumu. Wanataka kuona rasilimali zikitumika kwa manufaa ya Watanzania wote badala ya mnavyofanya sasa kuhamishia nje ya nchi. Hata Twiga wanapanda ndege kwenda Qatar, do!
 
Mwanzo mlipendekeza wafuasi wenu waulize maswali magumu, mlivyoona yanajibiwa mkapendekeza zomeazomea

Mtwara waliuliza kwa nini hawafaidiki na gesi ambayo inasafirishwa tu kwenda DSM huku Mtwara ikiachwa maskini! Kuna kada wa magamba aliyeweza kujibu swali hilo zaidi ya kudai eti wanasomesha vijana bure? Magamba wajue kwamba mikoa mingine nayo inahitaji maendeleo sio kurundika kila kitu DSM! Kwa namna hii ya kudhani kuwa wanawahonga watu kwa scholarship hewa wataona ziara zao kuwa chungu na badala yake wataanza ziara za kushtukiza!
 
Ninafahamu kwa uhakika kwamba ukweli haupendezi kwa wahalifu kuwa unawashughulisha! Uongo ni nja nyepesi ya kukwepa uwajibikaji. Tulikwishafunzwa kupitia biblia kwamba njia ya maanguko ni pana, nyepesi na haraka. Ikiwa UONGO na UKWELI vitashindanishwa mbio vitoke Moro kwenda Dar Saa 1:30, wakati UKWELI unavaa track suit yake ili uingie mbioni, UONGO wenyewe utakuwa ukivua suti yake Dar ili uoge kuondoa jasho! Umefika zamani sana! Ni jambo la ajabu watu wazima wakitaka kulazimisha wenzao kukubaliana na uongo wa kiajabu kwamba duniani kuna kizazi malum cha watu wabaya. Sisi CCM hatuwahi kusema kamba kwenye upinzani wapo wabwia viroba tu kama ninyi mnavyowaita wanaCCM wote jina moja la mafisadi. Nyumbani kwenu, ndugu zako wote wako kama ulivyo wewe? Je, duniani kunawat wa kurudufishwa? Haiwezekani ikatokea kwamba udhaifu wa mtu moja umegeuka kuwa wa jamii nzima wala kwamba wanaCCM wote ni wa kurudufishwa? CCM ni chama chenye historia isiyofutika kwa kuwa tu wewe unakuwadia na kuiga siasa za ughaibuni zilizobomoa dola zote zilizokuwa maarufu ulimwenguni. Achana na siasa za maji taka.

kiswahili nacho ni kiingereza, communication skill hakuna hapa
 
kama kuna vijana wahuni wanaoweza kuwazomea top ya ccm mpaka mkutano unavunjika basi ujue hapo hakuna tena chama.
kwa hiyo akitokea lowasa akinunu kontena la viroba akawamwagia vijana kwenye uchaguzi mkuu anakuwa rais wa nchi hii.
mbona kipindi cha nyerere hata ununue bia na nyama wanakuzomea wewe uliyenunua.

CCM INAYUMBAYUMBA NA KUWAYAWAYA.
 
Nnaona kila panapokucha 2015 mnaiona ipo karibu,mpo tarari kuua ili mmbaki madarakani,hivi hichi ulichokiandika hapa umetoa moyoni mwako kweli au pana jambo linakusukuma kwa nyuma ndani ya fikra zako?Uongo siku zote utajitenga na ukweli kwanini nyie kama ni chama tawala hamtaki changamoto?(ikiwapo kuzomewa).hauoni matangazo ya kukatika kwa umeme nchini yalivyotawala kwa sasa hivi ktk vyombo vya habari?,hilo dogo pekee hauoni mnapaswa kuondolewa madarakani kwa nguvu?
 
Mwanzo mlipendekeza wafuasi wenu waulize maswali magumu, mlivyoona yanajibiwa mkapendekeza zomeazomea
Mkuu mbona wazomeaji walikuwa na mavazi ya kijani na Swaga za kiCCM halafu walikuwa wengi zaidi.
 
Huu uandishi haufai kabisa, yaani hakuna paragraph halafu maneno yanaunganaungana tu.

Halafu mwandishi tuweke sawa haya ni maneno ya kinana wewe anareport tu au ni maoni yako, au maelezo ya Prof.Maghembe.

Wewe ni nani ndani ya Serikali mpaka uje na details za ziara ya Prof.Maghembe
 
Ni kweli kabisa wanawanunulia viroba na ndumu kwa akili timamtu huwezi zomea kama taahira kuna chama wanavaa kama mgambo ndo zao hao ni watu wa fujo sana

Toto laini khanga mokomoko ndo mavazi yenu, du maana Mr Dhaifu alisema ktk mkutano na wazee Dar ya kuwa Rais wa Walimu anakihelehele sana huku akinyanjua vidole kinamama wasutanapo.Mwanaume huvaa nguo ngumu hivi weye wawezavaa baibui, jitambua as man not she.
 
Back
Top Bottom