Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha ,Mrisho Gambo,Mfanyabiashara Maarufu jijini Arusha,Philemoni Mollel(Monaban),Meya mstaafu Kalist Lazaro na Mfanyabiashara wa Madini Thomas Munis Ni miongoni mwa Makada 46 wa ccm waliojitokeza leo kuchukua fomu kugombea ubunge jimbo la Arusha mjini.
Idadi hiyo inatajwa huenda ikaongezeka katika siku za usoni hadi kufikia julai 17 ambayo ndiyo siku ya mwisho na kuvunja rekodi za wagombea wa kiti hicho katika miaka ya nyuma.
Katibu wa ccm wilaya ya Arusha, Denis Mwita ameeleza kuwa Idadi hiyo inaonyesha jinsi gani chama hicho kime kubalika kwa wananchi na wanatazamia Idadi hiyo huenda ikafikia watu 60 Idadi ambayo haikuwahi kutokea katika.kinyang'anyiro hicho
Idadi hiyo inatajwa huenda ikaongezeka katika siku za usoni hadi kufikia julai 17 ambayo ndiyo siku ya mwisho na kuvunja rekodi za wagombea wa kiti hicho katika miaka ya nyuma.
Katibu wa ccm wilaya ya Arusha, Denis Mwita ameeleza kuwa Idadi hiyo inaonyesha jinsi gani chama hicho kime kubalika kwa wananchi na wanatazamia Idadi hiyo huenda ikafikia watu 60 Idadi ambayo haikuwahi kutokea katika.kinyang'anyiro hicho