Makachero wa Special Branch ndani ya harakati za uhuru wa Tanganyika

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,912
30,253


Katika maziko ya Mzee Kitwana Kondo niliombwa nizungumze.

Sikiliza video hii kuna historia muhimu sana kueleza kuundwa kwa TANU.

Nilizungumza kuhusu kikao cha watu watatu nyumbani kwa Hamza Mwapachu, wengine wakiwa Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe agenda ikiwa namna ya kumuingiza Julius Nyerere katika uongozi wa TAA katika uchaguzi uliokuwa mbele yao April 1953 na baada ya hapo 1954 TANU iundwe.

Nazungumza mbele ya viongozi wa CCM na serikali waliokuwepo hapo mazikoni.

Wote waliokuwapo pale walipigwa na mshangao mkubwa sana na kisa nilichoeleza.

Naamini kikubwa kilichowashangazwa wengi pale mazikoni ni ile kusema kuwa Abdul Sykes na Hamza Mwapachu wakifanya mipango ya kuunda TANU.

Waingereza walikuwa wanaijua mpango hii na walichuua hatua madhubuti kuzuia TANU isiundwe.

Waliwatumia makachero kupata taarifa zote.

Haujafanywa utafiti wa kuwajua makachero wa Special Branch ndani ya TANU wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kachero niliyekutananae wakati wa utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes ni mmoja tu, Alexander Tobias na huyu jina lake nilitajiwa na Mzee Germano Pacha nilipokwenda Tabora kufanyanae mahojiano.

Hassan Upeka ambae yeye mwenyewe alikuwa kachero wa TANU kuanzia mwaka wa 1956 na baada ya uhuru akawa Usalama wa Taifa katika mazungumzo niliyofanyanae miaka ya 1980 alinisisitizia sana nizungumze na Mzee Germano Pacha.

Mzee Pacha alinifahamisha kuwa agenda ya kwanza ya mkutano wa TAA wa 1954 uliounda TANU ilikuwa kuthibitisha kufukuzwa kazi kwa Alexander Tobias kwa kosa la kuwapa Specal Branch mafaili ya TAA.

Alexander Tobias aliajiriwa kama Executive Secretary wa TANU mwaka wa 1951 au 1952 baada ya Abdul Sykes kurejea Dar es Salaam kutoka Nansio Ukerewe.

Abdul Sykes alikwenda Nansio kushauriana na Hamza Mwapachu kuhusu matatizo yaliyokuwa yanaikabili TAA HQ baada karibu vongozi wake wote kuondolewa Dar es Salaam na kupelekwa majimboni kufuatia mapendekezo ya katiba yaliyowasilishwa TAA kwa Gavana Twining ambayo yaliwataka Waingereza waruhusu uchaguzi kuchagua Wajumbe wa LEGCO na baada ya miaka 13 waipe Tanganyika uhuru wake.

President wa TAA Dr. Vedasto Kyaruzi akahamishiwa Kingolwira.

Waingereza walighadhibishwa sana na mapendekezo haya na wakaamua kuwaondoa viongozi wa TAA Dar es Salaam ili wapate kupumua.

Hamza Mwapachu akapelekwa kisiwani Nansio.

Hamza Mwapachu akamshauri Abdul Sykes ambae alikuwa Act. President na Secretary kuwa TAA HQ iajiri Executive Secretary.

Hivi ndivyo Alexander Tobias alivyokuja kuajiriwa na TAA.

1654403024065.png

Alexander Tobias​
 


Katika maziko ya Mzee Kitwana Kondo niliombwa nizungumze.

Sikiliza video hii kuna historia muhimu sana kueleza kuundwa kwa TANU.

Nilizungumza kuhusu kikao cha watu watatu nyumbani kwa Hamza Mwapachu, wengine wakiwa Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe agenda ikiwa namna ya kumuingiza Julius Nyerere katika uongozi wa TAA katika uchaguzi uliokuwa mbele yao April 1953 na baada ya hapo 1954 TANU iundwe.

Nazungumza mbele ya viongozi wa CCM na serikali waliokuwepo hapo mazikoni.

Wote waliokuwapo pale walipigwa na mshangao mkubwa sana na kisa nilichoeleza.

Naamini kikubwa kilichowashangazwa wengi pale mazikoni ni ile kusema kuwa Abdul Sykes na Hamza Mwapachu wakifanya mipango ya kuunda TANU.

Waingereza walikuwa wanaijua mpango hii na walichuua hatua madhubuti kuzuia TANU isiundwe.

Waliwatumia makachero kupata taarifa zote.

Haujafanywa utafiti wa kuwajua makachero wa Special Branch ndani ya TANU wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kachero niliyekutananae wakati wa utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes ni mmoja tu, Alexander Tobias na huyu jina lake nilitajiwa na Mzee Germano Pacha nilipokwenda Tabora kufanyanae mahojiano.

Hassan Upeka ambae yeye mwenyewe alikuwa kachero wa TANU kuanzia mwaka wa 1956 na baada ya uhuru akawa Usalama wa Taifa katika mazungumzo niliyofanyanae miaka ya 1980 alinisisitizia sana nizungumze na Mzee Germano Pacha.

Mzee Pacha alinifahamisha kuwa agenda ya kwanza ya mkutano wa TAA wa 1954 uliounda TANU ilikuwa kuthibitisha kufukuzwa kazi kwa Alexander Tobias kwa kosa la kuwapa Specal Branch mafaili ya TAA.

Alexander Tobias aliajiriwa kama Executive Secretary wa TANU mwaka wa 1951 au 1952 baada ya Abdul Sykes kurejea Dar es Salaam kutoka Nansio Ukerewe.

Abdul Sykes alikwenda Nansio kushauriana na Hamza Mwapachu kuhusu matatizo yaliyokuwa yanaikabili TAA HQ baada karibu vongozi wake wote kuondolewa Dar es Salaam na kupelekwa majimboni kufuatia mapendekezo ya katiba yaliyowasilishwa TAA kwa Gavana Twining ambayo yaliwataka Waingereza waruhusu uchaguzi kuchagua Wajumbe wa LEGCO na baada ya miaka 13 waipe Tanganyika uhuru wake.

President wa TAA Dr. Vedasto Kyaruzi akahamishiwa Kingolwira.

Waingereza walighadhibishwa sana na mapendekezo haya na wakaamua kuwaondoa viongozi wa TAA Dar es Salaam ili wapate kupumua.

Hamza Mwapachu akapelekwa kisiwani Nansio.

Hamza Mwapachu akamshauri Abdul Sykes ambae alikuwa Act. President na Secretary kuwa TAA HQ iajiri Executive Secretary.

Hivi ndivyo Alexander Tobias alivyokuja kuajiriwa na TAA.

View attachment 2250770
Alexander Tobias​
Hadithi za kusadikika.
 
Hadithi za kusadikika.
Ntemii,
Sikulaumu.

Kitabu cha Abdul Sykes kilipoingia nchini 1998 na watu kusoma yaliyokuwamo wengi walitaabika.

Lakini hawakusema niliyoandika ni ya "kusadikika," na sababu ni yale maelezo na ushahidi wa nyaraka na picha.

Naelewa kwa nini na wewe unapata tabu kuamini.

Akili inakataa na sababu ni kuwa umeaminishwa sicho.

Kwani unajua kuwa kadi ya TANU ya Julius Nyerere ni No. 1 kama President wa TANU na aliandikiwa na Ally Sykes na ndiye aliyechapa kadi 1000 za kwanza kutoka mfukoni kwake?

Unajua kuwa kadi No. 2 ni yake Ally Sykes na kadi No. 3 ni ya kaka yake Abdul Sykes?

Jiulize imekuwaje kadi hizo za hawa ndugu wawili ziwe za mwanzo pamoja na Nyerere zikifuatana?

Yako mengi usiyoyajua na nikikueleza utazidi kushangaa.

1654425213987.jpeg
 
Ntemii,
Sikulaumu.

Kitabu cha Abdul Sykes kilipoingia nchini 1998 na watu kusoma yaliyokuwamo wengi walitaabika.

Lakini hawakusema niliyoandika ni ya "kusadikika," na sababu ni yale maelezo na ushahidi wa nyaraka na picha.

Naelewa kwa nini na wewe unapata tabu kuamini.

Akili inakataa na sababu ni kuwa umeaminishwa sicho.

Kwani unajua kuwa kadi ya TANU ya Julius Nyerere ni No. 1 kama President wa TANU na aliandikiwa na Ally Sykes na ndiye aliyechapa kadi 1000 za kwanza kutoka mfukoni kwake?

Unajua kuwa kadi No. 2 ni yake Ally Sykes na kadi No. 3 ni ya kaka yake Abdul Sykes?

Jiulize imekuwaje kadi hizo za hawa ndugu wawili ziwe za mwanzo pamoja na Nyerere zikifuatana?

Yako mengi usiyoyajua na nikikueleza utazidi kushangaa.

View attachment 2251174
hivi hawa wapendwa wako Ally na Abdul Sykes walifanya kosa gani TANU mpaka wakawekwa pembeni?
 
hivi hawa wapendwa wako Ally na Abdul Sykes walifanya kosa gani TANU mpaka wakawekwa pembeni?
Vito...
Kwa nini unatumia hili neno ''wapendwa.''
Mimi hawa ni baba zangu.

Nikugusie kitu kimoja upate kujua.

Mtaa wa Kipata No. 69 alikuwa akiishi Kleist Sykes na mkewe Bi. Mluguru bint Mussa.

Mtaa wa Kipata No. 68 alikuwa akiishi babu yangu Salum Abdallah na mkewe Bi. Zena bint Farijalla.

Wake zao walikuwa marafiki wakubwa

Watoto wao wakicheza pamoja hapo mtaani na wakisoma shule moja Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Musim School.

Hii ni miaka ya mwanzoni 1920s na wote hawa walikuwa wakifanyakazi Tanganyika Railways.

Hawa watoto wao wametuzaa sisi katika mitaa hii na sisi tukacheza pamoja toka udogo wetu hadi leo.

Sisi tumepata watoto wetu udugu huu bado ungalipo kwa mapenzi yale yale tuliyoyakuta na tukarithi kutoka kwa wazee wetu.

Ujamaa huu sasa una historia ya miaka 100.

Nakusihi usinifanyie kejeli kwa wazee wangu ninawaheshimu sana kama inavyotakiwa.

Nataka nikupe mfano mdogo.

Siku moja bint Abdul Sykes yeye kafiwa na mumewe miaka mingi basi kaja kwangu mke wangu akawa anamtania anamwambia, ''Mohamed akuoe.''

Dada yangu akamjibu mke wangu, ''Mohamed hawezi kunioa mimi huyu mimi kaka yangu.''

Hii ndiyo staha, heshma na mapenzi tuliyorithi kwa wazee wetu ingawa udugu wetu si wa damu.

Haya ndiyo mafunzo na mila zetu.

Sasa tuendelee.

Sidhani kama kulikuwako na suala la kuwekwa pembeni kwa Abdul na mdogo wake Ally.

Kuwekwa pembeni kwa vipi?
Uhuru ilipatikana salama na kila mtu alikuwa kafurahi nchi imekombolewa.

Tatizo nadhani lilikuja katika kuwatambua wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika.

Nasema hivi kwa kuwa zipo tarifa kuwa ilipokuwa sasa n dhahiri kuwa uhuru unapatikana waliingia watu wapya katika TANU na hapa yakaanza maneno ya chinichini kuhusu historia ya mapambano.

Inaelekea kulikuwa na watu ndani ya chama na wengine viongozi wa juu TANU HQ wakitaabishwa na historia iliyokuwako kuwa Waislam walitoa mchango mkubwa katika kuunda kwanza African Association kisha TANU na wanafahamika kwa majina.

Ukoo wa Sykes kuanzia Kleist Sykes na wanae ndiyo waliokuwamo katika harakati hizi kuanzia baba AA 1929 kisha watoto wakachukua chama TAA 1950 baada ya baba yao kufa 1949 na wakawa siku zote mstari wa mbele wakaunda TANU 1954 hadi uhuru ulpopatikana 1961.

Hapakuwa na mtu ambae angeweza kupinga ukweli huu.

Julius Nyerere alikuwa shahidi wa haya kuanzia 1952 alipofahamiana na Abdul Sykes hiki kisa ni maarufu sasa wengi mnakifahamu.

Tatizo ninaoliona miimi si kuwekwa pembeni wale waliopigania uhuru kwa maana labda ya watu kupewa vyeo.

Tatizo nililoliona ni kuikataa historia ya TANU kama ilivyokuwa na kuleta historia mpya.

Kwa kuhitimisha ndipo mimi niliponyanyua kalamu kuandika historia ya TANU nikitumia Nyaraka za Sykes.

1654448160237.jpeg

Abbas Sykes nyumbani kwake Sea View kushoto Mwandishi.
 
Vito...
Kwa nini unatumia hili neno ''wapendwa.''
Mimi hawa ni baba zangu.

Nikugusie kitu kimoja upate kujua.

Mtaa wa Kipata No. 69 alikuwa akiishi Kleist Sykes na mkewe Bi. Mluguru bint Mussa.

Mtaa wa Kipata No. 68 alikuwa akiishi babu yangu Salum Abdallah na mkewe Bi. Zena bint Farijalla.

Wake zao walikuwa marafiki wakubwa

Watoto wao wakicheza pamoja hapo mtaani na wakisoma shule moja Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Musim School.

Hii ni miaka ya mwanzoni 1920s na wote hawa walikuwa wakifanyakazi Tanganyika Railways.

Hawa watoto wao wametuzaa sisi katika mitaa hii na sisi tukacheza pamoja toka udogo wetu hadi leo.

Sisi tumepata watoto wetu udugu huu bado ungalipo kwa mapenzi yale yale tuliyoyakuta na tukarithi kutoka kwa wazee wetu.

Ujamaa huu sasa una historia ya miaka 100.

Nakusihi usinifanyie kejeli kwa wazee wangu ninawaheshimu sana kama inavyotakiwa.

Nataka nikupe mfano mdogo.

Siku moja bint Abdul Sykes yeye kafiwa na mumewe miaka mingi basi kaja kwangu mke wangu akawa anamtania anamwambia, ''Mohamed akuoe.''

Dada yangu akamjibu mke wangu, ''Mohamed hawezi kunioa mimi huyu mimi kaka yangu.''

Hii ndiyo staha, heshma na mapenzi tuliyorithi kwa wazee wetu ingawa udugu wetu si wa damu.

Haya ndiyo mafunzo na mila zetu.

Sasa tuendelee.

Sidhani kama kulikuwako na suala la kuwekwa pembeni kwa Abdul na mdogo wake Ally.

Kuwekwa pembeni kwa vipi?
Uhuru ilipatikana salama na kila mtu alikuwa kafurahi nchi imekombolewa.

Tatizo nadhani lilikuja katika kuwatambua wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika.

Nasema hivi kwa kuwa zipo tarifa kuwa ilipokuwa sasa n dhahiri kuwa uhuru unapatikana waliingia watu wapya katika TANU na hapa yakaanza maneno ya chinichini kuhusu historia ya mapambano.

Inaelekea kulikuwa na watu ndani ya chama na wengine viongozi wa juu TANU HQ wakitaabishwa na historia iliyokuwako kuwa Waislam walitoa mchango mkubwa katika kuunda kwanza African Association kisha TANU na wanafahamika kwa majina.

Ukoo wa Sykes kuanzia Kleist Sykes na wanae ndiyo waliokuwamo katika harakati hizi kuanzia baba AA 1929 kisha watoto wakachukua chama TAA 1950 baada ya baba yao kufa 1949 na wakawa siku zote mstari wa mbele wakaunda TANU 1954 hadi uhuru ulpopatikana 1961.

Hapakuwa na mtu ambae angeweza kupinga ukweli huu.

Julius Nyerere alikuwa shahidi wa haya kuanzia 1952 alipofahamiana na Abdul Sykes hiki kisa ni maarufu sasa wengi mnakifahamu.

Tatizo ninaoliona miimi si kuwekwa pembeni wale waliopigania uhuru kwa maana labda ya watu kupewa vyeo.

Tatizo nililoliona ni kuikataa historia ya TANU kama ilivyokuwa na kuleta historia mpya.

Kwa kuhitimisha ndipo mimi niliponyanyua kalamu kuandika historia ya TANU nikitumia Nyaraza za Sykes.

View attachment 2251519
Abbas Sykes nyumbani kwake Sea View kushoto Mwandishi.
Mzee Mohamed naomba unijuze kulingana na tafiti ulizofanya kwa miaka mingi .. Nini kilipelekea historia hii kupindishwa baada ya uhuru?

Kwanini haikuwa hivyo kabla ya uhuru? Ni kina nani walipindisha kwa maslahi ya nani?

Katika maisha ya kila siku huku mtaani mbona hizi hisia za pande mbili ni kidogo sana yaani tunashirikiana kwa mambo mengi na hatuoni shida.
 
Mzee Mohamed naomba unijuze kulingana na tafiti ulizofanya kwa miaka mingi .. Nini kilipelekea historia hii kupindishwa baada ya uhuru?

Kwanini haikuwa hivyo kabla ya uhuru? Ni kina nani walipindisha kwa maslahi ya nani?

Katika maisha ya kila siku huku mtaani mbona hizi hisia za pande mbili ni kidogo sana yaani tunashirikiana kwa mambo mengi na hatuoni shida.
SMC...
Unaniuliza nini kilipelekea historia ya kweli ya TANU kufutwa na kuwekwa nyingine.
Kwa nni haikuwa kabla na akna nani walipindisha.

Soma kitabu cha Abdul Sykes kuna historia nzima ya uhuru wa Tanganyika kuanzia 1929 ilipoundwa African Association hadi uhuru ulipotatikana 1961.

Soma historia ya miaka hii ya karibuni hadi kufikia kuandikwa kitabu ''Mwembechai Killings...'' na Hamza Njozi na serikali kukipiga marufuku.

Njia bora ya kukabiliana na tatizo lolote si vurugu ni mazungumzo.
Serikali inatambua tatizo lililopo hasa hili la 20:80.
 
Mzee yuko na kitu tatizo ni UDINI, watu wanachukia machapisho yake sababu yanaadvoketi UDINI.
Ally...
Udini si kusahihisha historia iliyokosewa.

Udini ni kula njama ya kukandamiza imani isiyo yako na kunufaisha watu wa imani yako.

Huu ndiyo udini.
Hakuna anaechukia machapisho yangu.

Ungekuwa wewe unachukia kalamu yangu usingenisoma na kunandika kuhusu mimi.

Kitabu cha Abdul Sykes kinakwenda toleo la tano.
Hii si dalili kuwa wasomaji hawapendi kalamu yangu.

1654459516274.jpeg
 
Nadhani wa mlengo wako ndio watasoma hizo fiction stories zako.
 
Nadhani wa mlengo wako ndio watasoma hizo fiction stories zako.
Ntemii...
''Mrengo'' si ''Mlengo.''
Prof. Haroub Othman aliposoma kitabu changu alifadhaika sana.

Historia aliyosoma ilikuwa tofauti na ile ambayo yeye ingawa alikuwa mwalimu wa Chuo Kikuu hakupatapo kuifahamu.

Haya kanieleza mwenyewe uso kwa macho.
Akapita kwa jamaa wa Ki-Dar es Salaam kuuliza.

Majibu aliyopewa yalizidi kumtaabisha.

Prof. Haroub akaenda kumuona Mwalimu na kitabu changu kutaka kujua ukweli ni upi.

Mwalimu alikuwa ameshakisoma kitabu.
Nimealikwa vyuo vingi ndani na nje ya mipaka yetu kuzungumza.

Nimezungumza Northwestern University, Chicago hawa ndiyo mabingwa wa African History ulimwenguni.

Walitaka kunisikia na kuniuliza maswali.
Nimezungumza Zentrum Moderner Orient, Berlin, University of Johannesburg etc.

Nilingizwa katika mradi wa kuandika Dictonary of African Biography (DAB).

Huu ulikuwa mradi wa Harvard na Oxford University Press New York na wamechapa historia ya Kleist Sykes na wanae katika kamusi hili.

Nakupa haya machache lakini yapo mengi.

Bado unaamini kuwa naandika ''fiction'' na nasomwa na wasomaji wa mrengo wangu?

1654460902962.png
 
Historia imefichwa sana.nilipata nafasi ya kuongea mara nyingi na marehemu mzee Haruna Taratibu wa Dodoma,Kuna mengi sana yaliwekwa kapuni
 
Historia imefichwa sana.nilipata nafasi ya kuongea mara nyingi na marehemu mzee Haruna Taratibu wa Dodoma,Kuna mengi sana yaliwekwa kapuni
Jimmy,
Katika kitabu cha Abdul Sykes historia ya TANU Central Province niliipata kwake na kwa Mzee Omar Suleiman.

1654626222331.jpeg

Kulia: Haruna Iddi Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Nyerere, Sheikh Mohamed Ramia na Iddi Faiz Mafungo, Dodoma 1955/56.
 
Vito...
Kwa nini unatumia hili neno ''wapendwa.''
Mimi hawa ni baba zangu.

Nikugusie kitu kimoja upate kujua.

Mtaa wa Kipata No. 69 alikuwa akiishi Kleist Sykes na mkewe Bi. Mluguru bint Mussa.

Mtaa wa Kipata No. 68 alikuwa akiishi babu yangu Salum Abdallah na mkewe Bi. Zena bint Farijalla.

Wake zao walikuwa marafiki wakubwa

Watoto wao wakicheza pamoja hapo mtaani na wakisoma shule moja Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Musim School.

Hii ni miaka ya mwanzoni 1920s na wote hawa walikuwa wakifanyakazi Tanganyika Railways.

Hawa watoto wao wametuzaa sisi katika mitaa hii na sisi tukacheza pamoja toka udogo wetu hadi leo.

Sisi tumepata watoto wetu udugu huu bado ungalipo kwa mapenzi yale yale tuliyoyakuta na tukarithi kutoka kwa wazee wetu.

Ujamaa huu sasa una historia ya miaka 100.

Nakusihi usinifanyie kejeli kwa wazee wangu ninawaheshimu sana kama inavyotakiwa.

Nataka nikupe mfano mdogo.

Siku moja bint Abdul Sykes yeye kafiwa na mumewe miaka mingi basi kaja kwangu mke wangu akawa anamtania anamwambia, ''Mohamed akuoe.''

Dada yangu akamjibu mke wangu, ''Mohamed hawezi kunioa mimi huyu mimi kaka yangu.''

Hii ndiyo staha, heshma na mapenzi tuliyorithi kwa wazee wetu ingawa udugu wetu si wa damu.

Haya ndiyo mafunzo na mila zetu.

Sasa tuendelee.

Sidhani kama kulikuwako na suala la kuwekwa pembeni kwa Abdul na mdogo wake Ally.

Kuwekwa pembeni kwa vipi?
Uhuru ilipatikana salama na kila mtu alikuwa kafurahi nchi imekombolewa.

Tatizo nadhani lilikuja katika kuwatambua wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika.

Nasema hivi kwa kuwa zipo tarifa kuwa ilipokuwa sasa n dhahiri kuwa uhuru unapatikana waliingia watu wapya katika TANU na hapa yakaanza maneno ya chinichini kuhusu historia ya mapambano.

Inaelekea kulikuwa na watu ndani ya chama na wengine viongozi wa juu TANU HQ wakitaabishwa na historia iliyokuwako kuwa Waislam walitoa mchango mkubwa katika kuunda kwanza African Association kisha TANU na wanafahamika kwa majina.

Ukoo wa Sykes kuanzia Kleist Sykes na wanae ndiyo waliokuwamo katika harakati hizi kuanzia baba AA 1929 kisha watoto wakachukua chama TAA 1950 baada ya baba yao kufa 1949 na wakawa siku zote mstari wa mbele wakaunda TANU 1954 hadi uhuru ulpopatikana 1961.

Hapakuwa na mtu ambae angeweza kupinga ukweli huu.

Julius Nyerere alikuwa shahidi wa haya kuanzia 1952 alipofahamiana na Abdul Sykes hiki kisa ni maarufu sasa wengi mnakifahamu.

Tatizo ninaoliona miimi si kuwekwa pembeni wale waliopigania uhuru kwa maana labda ya watu kupewa vyeo.

Tatizo nililoliona ni kuikataa historia ya TANU kama ilivyokuwa na kuleta historia mpya.

Kwa kuhitimisha ndipo mimi niliponyanyua kalamu kuandika historia ya TANU nikitumia Nyaraka za Sykes.

View attachment 2251519
Abbas Sykes nyumbani kwake Sea View kushoto Mwandishi.
Mwandishi

Ambaye niwewe father muddy
 
Sheikh kwanini hao watu wakitoka huko wengi wao wakistaafu huomba maghufira sana ina wezekana hufanyia watu na ummah dhulma kubwa au ? Maana zimenitoka sana kazi hizo tangu bosome vitabu.
 
Sheikh kwanini hao watu wakitoka huko wengi wao wakistaafu huomba maghufira sana ina wezekana hufanyia watu na ummah dhulma kubwa au ? Maana zimenitoka sana kazi hizo tangu bosome vitabu.
Mbogo...
Mimi hukaa nikajiuliza ilikuwaje?
Hawa walikuwa kama watu waliorogwa.

Naam wakitoka akili zinarejea.
 
..lakini Waingereza walikuwa na utu kuzidi Ccm.

..kwa mfano, ktk uchaguzi mkuu wa mwaka 1958 hakuna mgombea wa Tanu aliyeenguliwa kwa sababu zozote zile.

..uchaguzi wa mwaka 2020 uliosimamiwa na Ccm wagombea udiwani 700 wa Cdm walienguliwa.

..sijui kama kina wazee waliounda Tanu na kudai uhuru lengo lao lilikuwa tujitawale na chama chao kigeuke kuwa cha kidhalimu kama Ccm.
 
Back
Top Bottom