Makabila ya Tanzania: Tamaduni zao na Historia yao

Bowbow

JF-Expert Member
Oct 20, 2007
541
31
Hi wana JF.

Nimeona nilete mada hii hapa mbele yenu baada ya kukutana na mtanzania mwenzangu na kusema kabila lake ni moja wapo ya "endangred species" maana yake wapo labda chini ya 1,000.

So nimeona nije na mada HIi ambayo lengo lake ni kujadili kabila moja hadi jingine katika mtiririko ufuatao

1.Jina la kabila na asili yao
2. Organisation yao kwa maana mfumo wao wa utawala ulikuaje au ukoje kwa sasa
3. Idadi yao, sehemu wanakopatikana ni mtawanyiko katika nchi
4. Mila na desturi zao
5. Mafanikio waliyowahi kuyafikia
5. Pamoja na mambo mengine muhimu yanayohusu jamii husika, prominent figures kama zipo.


Kwanza nitaanza kwa kutoa list ya makabila yote yanayopatikana Tanzania then kila siku nitakuwa naweka walau kabila moja
 
Hii ni orodha ya makabila ya Tanzania.
Kuna matatizo kwenye majina kadhaa katika orodha hii, kwasababu mbalimbali. Orodha hii inatokana na orodha ya Ethnologue ya lugha za Tanzania, pamoja na tovuti nyingine. Inawezekana kwamba baadhi ya majina ya makabila ni majina ya lugha au lahaja badala ya makabila, na labda majina mengine yaliandikwa vibaya. Juu ya hivyo, hakuna ufafanuzi wa wazi kusema kwamba kikundi fulani ni kabila au siyo. Vikundi kadhaa katika orodha hii vina wenyeji mamia tu, lakini vikundi vingine vinavyo mamilioni ya watu; labda kila kikundi kinaitwa "kabila," lakini ni jamii za aina tofauti kabisa. Vikundi katika ukurasa huu vimeorodheshwa kuwa vikundi tofauti kutokana na ushahidi kutoka Ethnologue kutofautisha lugha zao.
Hii ni orodha ya makabila ya watu ambao wamekuwa wanaishi tangu zamani katika eneo ambalo sasa linaitwa Tanzania, pamoja na makabila yaliyogawiwa na mipaka baina ya Tanzania na nchi za jirani. Orodha hii haizingatii makabila yanayoishi katika Tanzania kama wakimbizi kutoka vita katika nchi za jirani. Ukurasa huu hauorodheshi vikundi vya wahamiaji kutoka nchi za kigeni, kama wahamiaji au wazao wao kutoka Arabia au Uhindi.
Retrieved from "http://sw.wikipedia.org/wiki/Orodha_ya_makabila_ya_Tanzania"
 
Tunaanza na wachaga

Early history
Early migration patterns of the Niger-Congo Bantu's led the Chagga to settle in the North Pare Mountains. This is the Home of the ancestral chagga. The population growth by about eleventh or twelve century led a number of people to begin looking for a new land on which to live.

They found it on the nearby and, in those days, still heavily forested southern and eastern slopes of Mount Kilimanjaro. The movement of the early chagga banana farmers to Kilimanjaro set off a period of rapid and extensive cultural amalgamation, in which large numbers of the Ongamo people and the Rift Southern Cushites were assimilated into the newly expanding chaga communities.

Though apparently growing in numbers and territory, the chaga remained organised in the seventeenth and eighteenth centuries into a great many very small and very local social and political units, whose histories are still largely unstudied by Western scholars.

But if the Maasai settled in the open plains around much of the chaga country, they presently cannot be credited with great influence on chaga affairs during this period, another people, the Ongamo or Ngasa who were closely related in language to the Maasai, did have much influence in chaga history
 
Interactions with the Pare and the Outside world

The Pare had been the chief suppliers of iron to the inhabitants of the mountain regions of north-eastern Tanzania. The demand for Pare iron, increased from the beginning of the nineteenth century. The cause of the increase was the military rivalry among the rulers of the chaga. It is likely that there was a connection between this rivalry and the development of long distance trade from the coast to the interior of the Pangani river basin, suggesting that the chaga made contacts with the coast may have dated to about the end of the eighteenth century.

The rivalry among chagga rulers was probably the result of competition among them for the control of the trade with people from the coast. Raids and counter raids characterised the chagga rivalry, as observed and understood by European colonisers. Subsequently there was an increase in demand for pare Iron to forge military weapons to equip the armies of the chaga rulers
 
Kabla ya Ukristu na Uislam walikua na Dini?


Early religion
In religion a thoroughgoing syncretism took place. The importance of ancestors, a Niger-Congo feature, was strongly maintained by the chagga to this day, they had an idea of Divinity, identified with the majestic sun as life giving, a faith also seen in the Rift Southern Cushitic version of the Sudanic religion, with the creator god concept of the Niger-Congo belief. Later on they became victims of forced Christianity and Islam that destroyed their religious system
 
Wachagga ni kabila la watu wenye asili ya Kibantu wanaoishi kaskazini mwa Tanzania chini ya mlima Kilimanjaro, mkoani Kilimanjaro. Shughuli kubwa ya Wachagga ni biashara na kilimo.
Wachagga ni kabila la tatu kwa ukubwa nchini Tanzania. Takwimu za mwaka 2003 zinaonyesha kuwa idadi ya Wachagga mkoani Kilimanjaro ni 2,000,000
 
Majina ya Kichagga
Familia maarufu za Kichagga nchini Tanzania ni kama Kimaro, Swai, Massawe, Mushi, Moshi, Lema, Urassa, Nkya, Temu, Mlaki, Mlay, Lyimo, Moshiro, Mselle, Kileo, Tesha, Mariki, Tarimo, Laswai, Ndosi, Mallya, Kimambo, Sawe, Usiri,Shayo na kadhalika.
Pia inasemekana kuwa, Wachagga wengi hupenda kurudi nyumbani kipindi cha Krismasi, ikiwa ni kuwatembelea wazazi wao, rafiki, au ndugu. Ingawa wengi hudhani kwamba Wachagga wameathiriwa sana na dini ya Kikristo, inaaminika pia kuwa kurudi kwao Uchaggani wakati wa Krismasi ni pamoja na kutembelea au kuomba baraka za mizimu yao.
 
Mbege
Mbege ni pombe ya asili ya Wachagga, wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro. Mbege hutengenezwa na ndizi mbivu, ulezi, na maji. Mara nyingi mbege hutengenezwa na wanawake na hutumika katika sherehe na matukio mbalimbali kama vile harusi, misiba, ubarikio, kuzaliwa kwa mtoto, n.k. Mbege hutumiwa pia kama faini kwenye mahakama za jadi. Utengenezaji wa mbege hufanywa pia kama shughuli ya kibiashara. Mbege huuzwa katika vilabu vya pombe na pia majumbani.

Pombe hii hutengenezwa kwa kuchemsha ndizi mbivu kama vile ndizi songea, ndizi uganda,kibungara,kisukari(kama zinapatikana kwa sana) n.k. Ndizi hizo zikishachemshwa huachwa kwa kipindi cha kama tatu au zaidi ili zichache. Baada ya hapo unga wa ulezi hupikwa na kuachwa upoe. Ndizi zilizochemshwa na kuchacha huchanganywa na maji kisha kukamuliwa ili kupata juisi yake. Juisi hiyo huchanganywa na unga wa ulezi uliopikwa na tunapata (kivuo, kifue, togwa) na kuachwa usiku mzima. Kesho yake mbege huwa tayari kwa kunywewa.

pombe hii kama haitanyewa na kumalizika cku huiyo bac ikilala tunapata kitu kinachooitwa ngera, ambayo ni chachu sana, ila ngera pia huweza kuzimuliwa na kuwa pombe ifaayo tena kwa kuchanganya na unga uliopikwa na unga kidogo usiopikwa, ila ngera ikilala tena humwagwa kwani haitafaa kunywea tena
Watengenezaji wengi wa pombe huwa wanaweka gamba la mti wa msesewe (Rauvolfia Caffra), hasa maeneo ya kibosho,machame na rombo ili kuongeza ladha ya uchachu na kupunguza kasi ya mbege kuchacha.

Chombo maalum kiitwacho kata hutumiwa kunywea mbege, ila mara nyingi sehemu za mijini hutumia vyombo vya plastiki, vikiwa na ujazo tofauti navyo huitwa chubuku na kitochi. Katika maeneo ya vijijini mbege hunywewa kijamaa kwa kupokezana kata. Mtu mmoja anakunywa kisha anampatia mwingine anayekunywa na kumpa mwingine.
 
Nataka kwenye hii topic kuanza kujadili suala hili, wahaya walitoka wapi?Je mila zao na dini yao ya asili ni ipi?Je koo (oluganda) zilianza vipi na ziko ngapi?

Baada ya wahaya nitajadili makabila mengine, labda kuanzia yale ya great lakes, kwa mfano wasukuma, mpaka makabila yote ya Tanzania tutayamaliza.

Mwenye ujuzi wowote anakaribishwa kuchangia
 
Jamani nahitaji shule juu ya historia ya Wanyakyusa. Wapo mpakani na nchi nyingi, kwa nini wanaitwa Wanyakyusa na sio Wanyakoma au Wanyandosya? Au Wanakipesile, Wanyakitwange Wanyakyembe, Wanyangosi......?

Kuna uhusiano gani kati ya Wandali na Wanyakyusa? Najua humu ndani kuna watu wamebobea katika hili, kuna vitabu adimu sana vinavyosemekana kuongelea habari hizi, isitoshe vitabu hivyo vinaelekea kutokana na tafiti za thesis za wajerumani wa enzi za kijerumani. Havipatikani tena sokoni.

Leka
 
Au wangonde na wanyakyusa jaribu kutembbelea www.nyakyusa.com
Lol ngumbwike akapote,amapenenga,ikimpumu,ifwefwe,ehndingala,ikitumbwike,ubusipa,imbasa and imbagala,haa Kubinika kupata historia huenda unende vijijini wilaya za Rungwe na Kyela kama unabahati unaweza kuwakuta wazee wakakupa akasumo ingawa kwa kweli wengi wametangulia mbele ya haki,kwa kweli inasikitisha Wanyakyusa hatuna historia yoyote wala kumkumbu ya utamaduni wa Wanyakyusa.Nasikia chanzo chetu ni Mahenge sehemu za Mwaya pia inahisiwa kuwa tuna nasaba na Nguni a.k.a Ngonis
 
Niliambiwa kuwa wanataokea bondeni uko kwa mzee madiba then wakaja mpaka maeneo ya morogoro wakasetle kidogo then wakashuka mpaka Tukuyu then baadae wengine wakashuka Kyela.
Wandali ni wanyakyusa ila tofauti ni kuwa wakati wenzao walipita shortcut kuja mbeya wenyewe wakapita njia ndefu ie Ndali
 
mnanitia aibu jamani... Wanyakyusa hawana asili ya Afrika Kusini...

........Kama unajua ni vema ungetujulisha asili ya hawa Wasokile.

Kwa upekuzi wangu nimeona wametokana na Malkia wa Kinubi aliyeitwa Nyanseba. Huyu malkia alikuwa Malawi, lakini je huko Malawi ndio kuna hawa wanyasa, na kama tujuavyo asili ya wanyasa ni kama wangoni. Ndio tutakapokuja sema asili ya nyakyusa ni africa kusini.
 
Looks like many of you never heard of, or been at kwa Kabale, history starts there, there's pre and post ofcourse!
 
mnanitia aibu jamani... Wanyakyusa hawana asili ya Afrika Kusini...
Wabantu wote asili yao Matebeleland kando ya Zambezi river. Hujui kwamba lugha ya makabila mengi ya Nigeria inayo maneno yanayofanana na ya Afrika Mashariki achilia mbali Afrika kusini? Unajitia aibu mwenyewe, wanakupatia shule hapo.Amanyisye na Amanyisye, Amunike na Amulike, Mandela na Mwandela

Lekaga
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom