simon james
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 283
- 140
Viongozi wakimila walianza kwa kumsimika Rasmi Ole Milya kuwa mkombozi maeneo ya Umasaini na baada ya Kiapo alikabidhiwa Kirungu na kutakiwa asiwe Kinyonga kwani akikiuka makubwa yatampata. Baada ya hapo zoezi la kukabidhi kadi lilianza ambapo mabalozi wa ccm, wenyeviti wa vitongoji, madiwani na wanachama wengine wa CCM zaidi ya elfu walitupa kadi zao kwenye Dustbeen maalum na kukabidhiwa kadi za Chadema. OLEMILYA alihutubia mkutana na kuwataka wa tz wawapuuze wana CCM wanao muita yeye Gamba huku akisema wanachosubiri ndani ya CCM nikupewa nafasi za uongozi kama shukrani. Aidha aliapa kuzunguka maeneo yote umasaini na kuhakikisha anavuna wamasai wote na mwisho aliapa kuwafanyia kitu kibaya wana CCM wanao mchafua Kamanda mbowe amewatuliza wananchi waliokuwa wanashaka na Olemilya na amesema kuwa CDM ni Chama makini kwahiyo kitamuadilisha Ole milya na wote wanaovua magamba na kuhamia CDM. Mbowe amesema kuwa hata baadhi ya wabunge wa CDM walihamia toka CUF, TLP, CCM lakin waliweza kuwafunza, alitoa mfano wa Wenje kuwa alitoka CCM. Kuhusu Usukaj wa Baraza la Mawazir Kamanda Mbowe amesema kuwa J.k amevunja katiba na kulidharau bunge baada ya kuteua wabunge na muda mchache kuwapa uwaziri na kuwataka waanze kazi bila kula kiapo Cha ubunge. MBOWE ameahidi kuwa atapanga upya baraza lake ili wakiingia bungeni wapinge uvunjaji huo wa katiba aliofanya J.K. Katika hatua nyingine kamanda wa anga alitoa taarifa kuwa wapo wabunge wa CCM 70 Walio mfuata kufanya booking ya nafasi za uongozi na hata katika baraza jipya linalo apishwa juma tatu Takribani mawaziri 9 wamemfuata wakitaka kufanya booking. Mwisho kamanda mbowe alifanya harambee na akakusanya zaid ya mil 1 ambayo itatumika kuendeleza Mv4change Umasaini. Kwa upande wa Nassari aliwataka wamachinga kuendelea na biashara zao bila kuogopa vitisho vya halmashauri kuwataka jumatatu waondoke mitaani. Nassari alisema Atatoa Amri ya kumzuia J.K Kukatiza Arusha kwani yeye Ni Raisi wa Arusha Na Lema ni Waziri Mkuu.