Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,396
IJUE SHERIA YA VYAMA VYA SIASA:
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ana jukumu la kusimamia chaguzi za ndani za vyama vya siasa na kuhakikisha ziko huru na haki
Ofisi hiyo inapaswa kutuoa muongozo na taratibu za mapato na matumizi ya fedha ndani ya vyama vya siasa
Kutoa elimu kuhusu Demokrasia, sheria zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa
Kuishauri Serikali kuhusu mambo yote yanayohusiana na siasa vyama vya siasa pamoja na kuwezesha mawasiliano mazuri kati ya Vyama vya Siasa na Serikali
====
MAJUKUMU YA OFISI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imejikita katika usimamizi wa Sheria ya Vyama vya Siasa Na 5 ya mwaka 1992 na Sheria ya Gharama za uchaguzi ya mwaka 2010 ili kuhakikisha uwepo na ukuaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini
Majukumu ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ni kusajili chama cha siasa kinachokidhi vigezo vya usajili kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992, ikiwamo kufuta chama chenye usajili wa muda au kudumu ambacho kwa mujibu wa sheria kimepoteza sifa ya usajili
Msajili amepewa mamlaka ya kusajili na kuvifuta vyama vinavyokiuka masharti ya usajili kwa mujibu wa sheria
Majukumu mengine ni kuratibu shughuli za Baraza la vyama vya siasa, kufuatilia mapato na matumizi ya vyama vya siasa katika uchaguzi kwa mujibu wa Sheria ya gharama za uchaguzi ya mwaka 2010
Kufuatilia utendaji wa vyama vya siasa kwa mujibu wa sheria, kugawa ruzuku kwa vyama vya siasa vyenye sifa, kuwa kiungo kati ya serikali na vyama vya siasa nchini. Pia, kutoa elimu kwa umma kwa vyama vya siasa na wadau wa vyama vya siasa
Kwa mujibu wa tovuti ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, kuna vyama 19 vyenye usajili wa kudumu
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ana jukumu la kusimamia chaguzi za ndani za vyama vya siasa na kuhakikisha ziko huru na haki
Ofisi hiyo inapaswa kutuoa muongozo na taratibu za mapato na matumizi ya fedha ndani ya vyama vya siasa
Kutoa elimu kuhusu Demokrasia, sheria zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa
Kuishauri Serikali kuhusu mambo yote yanayohusiana na siasa vyama vya siasa pamoja na kuwezesha mawasiliano mazuri kati ya Vyama vya Siasa na Serikali
====
MAJUKUMU YA OFISI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imejikita katika usimamizi wa Sheria ya Vyama vya Siasa Na 5 ya mwaka 1992 na Sheria ya Gharama za uchaguzi ya mwaka 2010 ili kuhakikisha uwepo na ukuaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini
Majukumu ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ni kusajili chama cha siasa kinachokidhi vigezo vya usajili kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992, ikiwamo kufuta chama chenye usajili wa muda au kudumu ambacho kwa mujibu wa sheria kimepoteza sifa ya usajili
Msajili amepewa mamlaka ya kusajili na kuvifuta vyama vinavyokiuka masharti ya usajili kwa mujibu wa sheria
Majukumu mengine ni kuratibu shughuli za Baraza la vyama vya siasa, kufuatilia mapato na matumizi ya vyama vya siasa katika uchaguzi kwa mujibu wa Sheria ya gharama za uchaguzi ya mwaka 2010
Kufuatilia utendaji wa vyama vya siasa kwa mujibu wa sheria, kugawa ruzuku kwa vyama vya siasa vyenye sifa, kuwa kiungo kati ya serikali na vyama vya siasa nchini. Pia, kutoa elimu kwa umma kwa vyama vya siasa na wadau wa vyama vya siasa
Kwa mujibu wa tovuti ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, kuna vyama 19 vyenye usajili wa kudumu