Majizo, Kusaga na Regina watumie njia gani nyingine ili wamuangushe Diamond na kundi lake? Kwanini wanashindwa? Tuwasaidie

Umaarufu alioupata Dai kipindi kile umemsaidia aendelee ila hakuna atakaempeleka mbele kinidhamu kimafanikio na kiubunifu zaidi ya hapo alipofika.
Endelea kupiga ramli tu lkn jamaa anazidi kujenga CV,mpaka sasa ana show 30 booked,jana katangaza show Ethiopia,mwezi ujao Malawi,ana show Madagascar miji mitatu,ana show za One Africa (Dubai,New York na London),bado hapo anashow za Wasafi festival Wadhamini wa kumwaga,juzi South Africa album yake ya A boy from Tandale imechukua tuzo.

Manake mnasema Youtube ananunua views lkn boomplay upande wa Tanzania anakimbiza miezi miwili wa 4 na watano (Refer Boomplay insta account).

Alafu mbona kuna wasanii kibao walikuwa maarufu huko nyuma,lkn hata show hawapati pamoja na kutoa nyimbo.
 
Diamond hawezi kufa kwa kuwa Kuna team Mond hao ni die hard fans. .ni kama Simba na Yanga..Msondo na Sikinde. .ndio maana ngumu msanii mpya kutamba. .Kuna manyumbu yameshajitune
 
Endelea kupiga ramli tu lkn jamaa anazidi kujenga CV,mpaka sasa ana show 30 booked,jana katangaza show Ethiopia,mwezi ujao Malawi,ana show Madagascar miji mitatu,ana show za One Africa (Dubai,New York na London),bado hapo anashow za Wasafi festival Wadhamini wa kumwaga,juzi South Africa album yake ya A boy from Tandale imechukua tuzo.

Manake mnasema Youtube ananunua views lkn boomplay upande wa Tanzania anakimbiza miezi miwili wa 4 na watano (Refer Boomplay insta account).

Alafu mbona kuna wasanii kibao walikuwa maarufu huko nyuma,lkn hata show hawapati pamoja na kutoa nyimbo.
Hakuna atakaempeleka mbele zaidi kinidhamu, kimafanikio na kiubunifu
 
kuna watu wanasema kashashuka kimataifa amebaki east Africa tu..kashaondoka kwenye ligi na kina davido SO what?? umefaidika nini tangu diamind aporomoke kwenye hizo ligi?? kama kuna ulipofaidika chochote nadhani una haki zaidi ya kufurahia anguko lake hata hapa Nchini maana utafaidika mara dufu...
Takwimu zinaonesha kwa Afrika Mashariki. Tz tunaongoza kwa imani za kishirikina. Si ajabu humu jf kuwa wachawi nguli.

Maana wivu wa kipumbavu ni sifa kongwe ya mchawi.
 
Kwan bro Una mwona Diamond ni yule yule,Diamond cyo msanii wa kushushwa bin vuu inahitaji muda,zile views za you tube zisiwadang'anye Watz ila Diamond kashashuka amebaki anatamba hapa hapa nchin na Kenya,Siyo diamond tu kashuka Bali mziki wetu wa kibongo umebaki unapumlia mipira kwenye soko la kimataifa.
Kwa hiyo hapo sasa nafsi yako imepata tulizo baada ya Diamond kushuka ?
 
Hakuna atakaempeleka mbele zaidi kinidhamu, kimafanikio na kiubunifu
Angekuwa hana nidhamu na ubunifu asingefika pale na bado anaisimamisha WCB kama kampuni,si swala dogo ndani ya WASAFI kuna Wasafi media,Wasafi Label na Wasafi Festival so bila kuwa na nidhamu na ubunifu leo hii asingeweza kumiliki vitu hivyo.
 
Youtube,insta et al,bado unategemea radio imuinue ama kumuangusha mtu ?Hiyo ilikuwa kabla ya 2014 Kabla mchina hajaleta smartphones
Hao walioenda kupiga magoti Clouds unadhan hawajui Kuna YouTube na Insta au kwa nini Diamond kaanzisha Radio station wakati YouTube ndo inatake over
 
Angekuwa hana nidhamu na ubunifu asingefika pale na bado anaisimamisha WCB kama kampuni,si swala dogo ndani ya WASAFI kuna Wasafi media,Wasafi Label na Wasafi Festival so bila kuwa na nidhamu na ubunifu leo hii asingeweza kumiliki vitu hivyo.
Muulize wasanii wangapi wenye majina makubwa wenye projects kubwa au zaidi ya hizo za Diamond?
 
Hao walioenda kupiga magoti Clouds unadhan hawajui Kuna YouTube na Insta au kwa nini Diamond kaanzisha Radio station wakati YouTube ndo inatake over
Kutokujiamini ni ugonjwa wa watanzania wengi wakiwemo hao waliokwenda kupiga magoti.
 
Angekuwa hana nidhamu na ubunifu asingefika pale na bado anaisimamisha WCB kama kampuni,si swala dogo ndani ya WASAFI kuna Wasafi media,Wasafi Label na Wasafi Festival so bila kuwa na nidhamu na ubunifu leo hii asingeweza kumiliki vitu hivyo.
Nidhamu aliokua nayo na ubunifu aliokuwa anapewa ndio imemsaidia hayo mafanikio zaidi ya hapo hatakua na zaidi
 
Vituo binafsi vya watu kutopiga nyimbo za msanii ni adhabu?
Wasalaam wanaJF,

Msanii Diamond ambaye ukweli ulio wazi ni msanii nambari moja hapa Tanzania
Msanii Diamond bado anapitia kwenye adhabu isiyo na kikomo ambayo amepewa na wamiliki wa EATV,efm na Clouds fm.

Adhabu hii inalenga kuhakikisha Diamond anapotea kwenye ramani ya Muziki na ikiwezekana asinyanyuke tena.

Lakini adhabu ya kutocheza nyimbo zake ilikwenda mbele zaidi na kuwafata wasanii wake wakina Harmonize,Rich Mavoko,Lavalava na Mboso na Queen Doreen nao wamefungiwa kutochezwa nyimbo zao kwenye vituo vya mabosi hao tajwa.

Lakini pamoja na kutocheza nyimbo za wasanii wote wa WCB bado wasanii hao wamezidi kung'ara kila kona na nyimbo zao zinapigwa kila kona na bila shaka na wao hao maboss wa hivyo vituo wanazisikia kila kona na hilo jambo linawatesa sana maana lengo la kumuangusha Diamond limekuwa gumu sana maana sasa Diamond ameshazaa wakina Diamond wengi kama Harmonize,Mboso na Lavalava.

Sasa Diamond amekuwa kama ni tatizo kubwa zaidi maana ameshazaa vidaimond vingine ambavyo kwakweli kuvizuia itakuwa ngumu sana na watapoteza lengo na ni wazi inakuwa ngumu sana kujua ni wapi sahihi kwa kupiga je ni kwa Diamond au kwa vidaimond.

Rich Mavoko wamemsamehe baada ya kujitoa WCB.

Hawa watanzania wenzetu wana lengo jema sana la kuhakikisha Diamond na vidiamond vyake viaanguka na vinakufa kabisa lakini kila kukicha vinazidi kunawiri moboss wameshindwa kabisa kumuangusha Diamond na wanaendelea kujaribu lakini wanashindwa na ni vyema wakasaidiwa kufanikisha lengo lao hili jema hata la mawazo.

Watumie njia gani mbadala?
Wafanye nini?
Wana kwama wapi?
 
Na kwa sasa hatutaweza pata mtu aliewaunganisha wasanii wakawa wanasikika karibia wote na kutoboa kimafanikio kama wakati Ruge yupo ulikua unaweza msikia Mwasiti katoa wimbo, Chege katoa wimbo, Shilole, Ney wa mitego na zikawa zote zinafanya vizuri na kualikwa kufanya show kila mahali lakin wakati huu watasikia wcb tu hata watoe mabata madogo hutaweza sikia wimbo unahit zaid yao ndipo tunasema bongo music inapotea
 
ukifattilia chanzo cha ugomvi utagundua kuwa hizo media zilitaka Diamond aperfom bure bila malipo kwenye matamasha yao ila jamaa akavunga sababu ya kujitambua yeye ni nani kwenye game, na wao wanajitetea kuwa wamechangia kumkuza kwenye muziki hivyo wana haki zote za kumpigisha shows bure eti dah! wengine wanaenda mbali zaidi kwa kusema "Ataona" >> source planet bongo dulla na jr. Dunia ya sasa imebadilika mnoooo watu hawasubiri kutoka kwa media wanatoka kwenye digital platforms na sosho mediaaaaa!!! Alafu akishakufa watakuwa wa kwanza kutangaza kifo chake kinafiki na kucheza nyimbo zake ilhali ameshafumba macho na hasikii masikiniiii!
 
Diamond alinitoka siku ile aliokuwa akimsalimia dingi wake studio, yaani mzee kajishusha lakini dogo hata heshima imemruka.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️

Utakuwa Mke wake Alikiba ww sio bure...hiyo chuki sio ya ya Kitanzania kabsaaa.
 
Back
Top Bottom