Majina ya Wabunge Viti Maalum hadharani: CCM-64, CHADEMA-36, CUF-10

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
attachment.php
attachment.php
attachment.php

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) leo imetangaza idadi ya wabunge wa viti maalumu ambao vyama vya CCM, CHADEMA na CUF vimepata baada ya kupata angalau asilimia 5 ya kura zote halali za wabunge nchi nzima.

Mwenyekiti wa tume hiyo Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema chama cha CCM ambacho kilipata jumla ya kura milioni 8.3 kimepata wabunge 64 wakati chama cha CHADEMA ambacho kilipata kura milioni 4.7 kimepata wabunge 36

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), leo imetangaza idadi ya Wabunge wa Viti Maalum, ambao vyama vya CCM, Chadema na CUF vimewapata baada ya kupata asilimia zote halali za wabunge nchini.

Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu, Damian Lubuva, amekaririwa na FikraPevu akisema Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho kilipata jumla ya kura milioni 8.3 kimepata wabunge 64, wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambacho kilipata kura milioni 4.7 na sasa kimepata wabunge 36, huku Chama Cha Wananchi (CUF) kilichopata kura milioni 1.2 kikipata wabunge 10.

Aidha, amebainisha kuwa wabuge wa viti maalumu vya ubunge ni viti 113, wakati viti 5 vitatoka baraza la Wawakilishi Zanzibar.

Jaji Mstaafu Lubuva, ameeleza kuwa majina ya wabunge hao yatapatikana kwenye Ofisi za vyama husika.

Hata hivyo, amesema kutokana na kuwepo kwa majimbo 8 ambayo hayakufanya uchaguzi, mgawanyo wa viti maalumu, kwa sasa ni 110 ambapo viti 3 vilivyobaki vitagawanywa baada ya kufanyika kwa uchaguzi katika majimbo hayo.


Soma zaidi =>
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yatangaza idadi ya Wabunge wa Viti Maalum
 

Attachments

  • vt1.jpg
    vt1.jpg
    84.3 KB · Views: 28,479
  • vt2.jpg
    vt2.jpg
    91.2 KB · Views: 27,650
  • vt3.jpg
    vt3.jpg
    50.1 KB · Views: 26,912
Sasa majina yako wapi? Mleta uzi ungetulia maana hata hiyo asilimia ya chadema uliyoandika siyo
 
Hivi chama kama NLD kilikuwa na msaada gani kwenye kampeni
za uchaguzi mkuu huu hasa kwa kundi la UKAWA..??
Ndo maana hata NEC hawajawapa hata kiti kimoja tu
kwani wameonekana kama best looser of the game.
 
Hapa wanaifurahia hadi tume.....ila ukirudi kwenye urais tu tayari inakua vita ya betina na zena wa sani.

Chadema hawajielewi!
Taarifa hii ya tume wameshaifanyia kazi na watapeleka majina, ila raisi hawamtambui kwa kuwa tume haiko huru!
Inahitaji kujitoa ufahamu ili uwaelewe chadema.
 
Hao 36 wametokana na ukawa kati yao cuf nld na nccr watapewa vingapi?
 
90% wa chama fulani watatoka kaskazini wakiwamo pia ndugu,wake na vimada wa viongozi
Viti maalum CCM utasikia dada mkubwa wa mgimwa ndani, mke wa Kigoda ndani, my wife wa nape ndani, nyumba ndogo ya nchimbi ndani, shemeji yake sitta, binamu wa mama salma, dada yake msukuma, mama masaburi, dada mdogo wa dialo, ex wa bulembo, ex wa mzee lofa, shemeji ya makamba dah shida tupu.
 
Back
Top Bottom