Majina Ya Viumbe Hai: wadudu, wanyama, ndege, mimea n.k.

Lakini nadhani pia anaitwa 'ugoko au ugoka' kwa Kiswahili, nadhani itakuwa hivyo maana Kibantu chetu kinafanana, na kule kanda ya ziwa wanatumia neno 'lugoka au logoka'.

SteveD.
 
Jama, na 'dragonfly' wanaitwa nini kwa kiswahili?

Najua jina la Kisukuma ni 'shilondela', direct translation is pursuer or chaser.

SteveD.
 
Jama, na 'dragonfly' wanaitwa nini kwa kiswahili?

Najua jina la Kisukuma ni 'shilondela', direct translation is pursuer or chaser.

SteveD.

Dragonfly wanaitwa 'Kereng'ende' kwa kiswahili
Jioni njema.
 
Dragonfly wanaitwa 'Kereng'ende' kwa kiswahili
Jioni njema.

Dah nilipokuwa shule ya msingi darasa la pili mwalimu alituuliza kwenye mtihani wa mwisho kuwa Kereng'ende huishi wapi?

Kila mtu alijibu kivyake, nakumbuka nilijibu anaishi kwenye maji nikakosa! Ila tatizo lilikuwa sio mahali anapoishi, ishu ilikuwa huyo kereng'ende ni mdudu gani!

Enzi hizo tunawaita kereng'ende Helicopter na panzi mkubwa barangulu!
 
ndiyo kuna senene, panzi, halafu wale wanaoliwa wako kama mchwa wanaitwaje, hasa kule kwenye "bomba hii, nyumba hii" wana mafuta hao!!
 
SteveD,
Kuhusu koboko na king cobra nadhani ni nyoka wawili tofauti kwa sababu:
Koboko (japo sijawahi kumuona kwa macho)nafahamu anapatikana sana maeneo ya msitu ya miombo hususan kule Kigoma na Tabora.Habari zinaeleza kuwa ana ushungi kama wa jogoo!! Kama umesikia juu ya nyoka anayevizia watu kwa kujificha kwenye matawi ya miti na kuwadonoa wapitapo chini. Pale Bulombora JKT tulipata sana habari kama hizi. Na namna ya kumtega na kumuua ni kwa wanawake kubeba mitungi yenye uji wa moto na kupita eneo aliloko huyu koboko, ambapo atajitumbukiza kichwa kichwa kwenye uji wa moto!
Cobra kwa upande mwingine, habari zinaeleza kuwa anapatikana zaidi Asia, hususan India na ana umbile la mashavu(?) makubwa ambayo hujivimbisha anapoghadhabika.
Hebu tupate maoni ya wengine wajuao zaidi labda.
 
Ngao you are right kwa koboko si King Cobra ila ni Black mamba ambaye rangi yake si mweusi ila kijani hafifu ila ndani ya mdomo ndiyo mweusi.King cobra wapo wa Asia na wa Misri wote wana vimbisha mashavu.
 
Hivyo Tanzania wapo Cobra? Halafu yule ndege anaitwa Dudumizi analo jina la kiingereza?

Halafu kuna vile vindege vidogo hupenda kuruka kwa makundi (siyo mbayuwayu) yaani ni vidogo kweli sijui vinaitwaje, nimekuwa nikitafuta jina lake kwa muda mrefu sasa.
 
Je, Koboko ndiyo king-cobra?!

Nadhani Cobra kwa Kiswahili anaitwa KIFUTU

Hivyo Tanzania wapo Cobra? Halafu yule ndege anaitwa Dudumizi analo jina la kiingereza?

Halafu kuna vile vindege vidogo hupenda kuruka kwa makundi (siyo mbayuwayu) yaani ni vidogo kweli sijui vinaitwaje, nimekuwa nikitafuta jina lake kwa muda mrefu sasa.

Nadhani Tanzania wapo Cobra. Nakumbuka nimeshawahi kumuona mtoto wa Cobra miaka mingi iliyopita. Labda macho yangu yawe yalindanganya akuwamdgo sana.

Kuna ndege wadogo warukao kwa makundi. Wana kelele sana, na vidari vyao ni vya njano. Wanaitwa USIGI. Sijui km ni hao uwazungumziao.
 
SteveD,
Kuhusu koboko na king cobra nadhani ni nyoka wawili tofauti kwa sababu:
Koboko (japo sijawahi kumuona kwa macho)nafahamu anapatikana sana maeneo ya msitu ya miombo hususan kule Kigoma na Tabora.Habari zinaeleza kuwa ana ushungi kama wa jogoo!! Kama umesikia juu ya nyoka anayevizia watu kwa kujificha kwenye matawi ya miti na kuwadonoa wapitapo chini. Pale Bulombora JKT tulipata sana habari kama hizi. Na namna ya kumtega na kumuua ni kwa wanawake kubeba mitungi yenye uji wa moto na kupita eneo aliloko huyu koboko, ambapo atajitumbukiza kichwa kichwa kwenye uji wa moto!
Cobra kwa upande mwingine, habari zinaeleza kuwa anapatikana zaidi Asia, hususan India na ana umbile la mashavu(?) makubwa ambayo hujivimbisha anapoghadhabika.
Hebu tupate maoni ya wengine wajuao zaidi labda.
Ngao, Take 5!! Yaani umenikumbusha mbali sana... ni kama vile tumekua pamoja toka utotoni. Hizo tales kuhusu jinsi ya kuua koboko ni sawa sawa kabisa na zile nilizosimuliwa mimi. Yaani ni kubeba uji wa moto kwenye chungu na kata nzito, uji uliomzito sana... ili akijilengesha tu na kudonyoa kichwani anajikuta kazamisha kichwa chake chenye ('usunzu'- in sukuma au 'cock-crown' kwa waingereza nadhani) ushungi kwenye uji.

Ulivyo watofautisha king cobra na koboko, sasa nimeanza kuona na kukumbuka tofauti zao. Ahsante.

Ngao, je unajua jinsi ya kumuua kenge au buru kenge (mburu in sukuma)?!.. nitajijibu: kuchemsha mayai kisha kuyatia kwenye maji baridi haraka haraka na kuyatega kwenye njia yake... kiini chake kinakuwa bado cha moto pale atakapofakamia na kuyameza, maana huwa wanameza mazima mazima na kuyapasulia kwenye koo!! (lakini nakusihi ndugu, usiongelee mambo haya huko ma-ulaya kwenu, nasikia kuna watu kibao wa RSPCA!! natumaini unajua kasheshe zao.... lol)!

Ngao you are right kwa koboko si King Cobra ila ni Black mamba ambaye rangi yake si mweusi ila kijani hafifu ila ndani ya mdomo ndiyo mweusi.King cobra wapo wa Asia na wa Misri wote wana vimbisha mashavu.

Mwenekapufi, mbona na kumbuka kuwa koboko ana rangi ya kijivu au ni jamii nyingine hii?! Halafu characteristic yake nyingine ni mbio... nadhani kwa simulizi nilizopatiwa mimi, ana mbio kupita nyoka wote kule kanda ya ziwa.

By the way wanaJF, natoa mifano mingi kutoka kanda ya ziwa kwani huku ndiyo nimekaa na kuona viumbe wengi zaidi, haswa aina za nyoka.

Hivyo Tanzania wapo Cobra? Halafu yule ndege anaitwa Dudumizi analo jina la kiingereza?

Halafu kuna vile vindege vidogo hupenda kuruka kwa makundi (siyo mbayuwayu) yaani ni vidogo kweli sijui vinaitwaje, nimekuwa nikitafuta jina lake kwa muda mrefu sasa.

Mkjj, hapa umenikumbusha ndege mmoja kule mwanza tulikuwa tuna mwita 'dodorima/dodolima'... this one I have seen it na nawajua kabisaa, wana rangi nyingi kama kasuku, ambao jina lao generic nadhani ni macaws (off course wapo species mbali mbali wa hawa). Hawa dodorima they are simply beautiful... lakini ni mbumbumbu kweli kweli... (no offence, lakini ni sawa na zile jokes za blondes, if you know what i mean!), hawa dodorima, hawana akili, kazi yao kusinzia tuuu... siongopi, yaani unaweza ukamkamata kwa mikono bila hata kuhangaika kumfukuza... kuna wimbo mmoja wa utotoni naukumbuka ulikuwa unaenda hivi:
#...dodorima sinzia
#...dodorima sinzia
#...mama yake....(sijui nini kilikuwa kinafata hapa, it's long time, can't remember)

Nikirudi kwa huyo dudumizi, nadhani amepewa jina hilo kutokana na kutoa sauti yake hiyo... yaani : duuduu... duudu-duuduu x2 !! Nikitaka kuwa describe kwa maisha ya kanda ya ziwa, ni kuwa, hawa wanapenda sana kuishi kwenye miti ya miembe... huwaoni, bali unasikia sauti yao tu hiyo wakiimba....hivyo jina ndiyo maana wanaitwa dudumizi. (naweza kuwa na describe ndege tofauti kabisa hapa, mtanisamehe). Na kwa nyongeza ni kuwa, hawa wanao kaa kwenye miembe, wanafanana sana na njiwa pori.

Mkjj, hao ndege wanao ruka kwenye makundi.. ni wale wenye speed kali sana kama vipanga, yaani wana madoido mengi utafikiri jet fighters... au hawa ndiyo mbayuwayu.. I'm confused, sijui yupi ni yupi..


Nadhani Cobra kwa Kiswahili anaitwa KIFUTU

Nadhani Tanzania wapo Cobra. Nakumbuka nimeshawahi kumuona mtoto wa Cobra miaka mingi iliyopita. Labda macho yangu yawe yalindanganya akuwamdgo sana.

Kuna ndege wadogo warukao kwa makundi. Wana kelele sana, na vidari vyao ni vya njano. Wanaitwa USIGI. Sijui km ni hao uwazungumziao.
T-1!
Za siku ndugu?!... hapa sina hakika kwa kweli, inawezekana you are right, lakini nadhani kifutu ni tofauti... kifutu kwa jinsi ninavyojua mimi ana rangi nyingi nyingi (kama za chatu hivi), na ni mfupi sana ila mnene. Sumu yake kwa wenye bahati mbaya ya kung'atwa naye nikuwa ina ozesha miguu au kiungo. Kwa hisia zangu mimi nafikiri kifutu ni rattle snake kama wale wa kule America. Kifutu hana hasira kama cobra.

Cobra ni mweusi na kule kanda ya ziwa tuna mwita Swila. Nadhani ulishawahi sikia hili. Na kama nilivyosema mwanzoni kabisa nadhani hili jina linaweza kunyambulishwa na kuwa neno la kiswahili. Jina swila linatokana na kutema mate, kama unavyojua, cobra are notorious kwa kutema mate, hence jina swila.
-----
Mkjj, Eeeh, kuna stori moja nikupe, unajua hawa kasuku wanaoimba nyimbo na kutamka maneno wanakamatika sana (off course wamepungua siku hizi) maeneo ya kanda za ziwa.... nakumbuka nikiwa mtoto, kuna jamaa kutoka Dar, ilikuwa ukifika tu msimu wa kuivisha na kuvuna mtama (nadhani inaitwa sogharm kwa kiingereza) na uwele (huu nao sijui ni jamii ya ulezi - i don't know!), walikuwa wanazingira vijiji kibao kwenye mashamba ya mazao haya. Walikuwa wanatumia ulimbo (watu wa dar na mijini kwingineko wanaweza wasijue haya -just ask me nyie watoto wa mijini... will describe the variety of this stuff.. lol), huo ulimbo ulikuwa unapakwa kwenye miti kibao kandokando ya mashamba hayo, maana ndege hutua kwenye miti hiyo kabla ya ku-swarm ndani ya shamba na kuanza kuteketeza nafaka... in a way, jamaa walikuwa wanasaidia wana kijiji, so to say, but nilibahatika kwenda dar na wakati fulani kwenda huko ulaya, ndiyo nilipoona hali halisi, yaani, kwanini jamaa walikuwa wanakamata ndege hao... they are dead expensive pets!! kumbe jamaa walikuwa wanakamata matenga na matenga ili kupeleka kuuza huko ulaya... duuh, i wish i knew this, nami ningelikuwa ka millionea fulani hivi labda hivi sasa... lol!


SteveD.
 
T-1!
Za siku ndugu?!... hapa sina hakika kwa kweli, inawezekana you are right, lakini nadhani kifutu ni tofauti... kifutu kwa jinsi ninavyojua mimi ana rangi nyingi nyingi (kama za chatu hivi), na ni mfupi sana ila mnene. Sumu yake kwa wenye bahati mbaya ya kung'atwa naye nikuwa ina ozesha miguu au kiungo. Kwa hisia zangu mimi nafikiri kifutu ni rattle snake kama wale wa kule America. Kifutu hana hasira kama cobra.

Cobra ni mweusi na kule kanda ya ziwa tuna mwita Swila. Nadhani ulishawahi sikia hili. Na kama nilivyosema mwanzoni kabisa nadhani hili jina linaweza kunyambulishwa na kuwa neno la kiswahili. Jina swila linatokana na kutema mate, kama unavyojua, cobra are notorious kwa kutema mate, hence jina swila.
SteveD.

SteveD,
Tupo, ndugu yangu! Hilo jina T-1 nimelipenda sana! Ni fupi na limetulia. I wish I could adapt it; need your advice.

Nimemkumbuka Kifutu baada ya kunitajia maumbile yake. I think I was wrong. Vilevile, niliwahi kusikia hilo jina "Swila" somewhere. Sikumbuki km muongeaji alikuwa mwenyeji wa kanda ya ziwa. What I want to say ni kwamba baadhi ya maneno ya Kiswahili yanaazimwa kutoka ktk lugha za makabila; hivyo, inawezekana hata hilo jina Swila likawa limeazimwa kutoka huko kanda ya ziwa, na kukubalika ktk Kiswahili. I'm not sure.

Nakumbuka kuwa rattle snake ni mrefu; kiasi cha kuweza kujivingirisha na sehemu ya mkia wake kuwa juu. Akiwa ktk hali hii, anauchezesha huo mkia ambao hutoa rattling sound (and hence the name) na kuwaonya viumbe wengine, hasa binadamu, kuwa "nipo hapa, angalia usinikanyage kwani nina sumu kali sana".

SteveD, hivi wale mijusi yenye rangi nyingi wanapatikana Mwanza tu? Au kanda ya ziwa tu? Wanaitwaje?

T-1
 
SWILA NI NYOKA MWEUSI na anatema mate(spitting cobra)KIFUTU NI NYOKA MFUPI NA MNENE ana rangi kama za chatu na ni mpole labda umkanyage ndiyo anauma. Ni kweli anaozesha muscles. Koboko ni kweli si wa kijani kabisa ila ni kati ya kijivu na kijani( Black mamba) black ina refer to the colour of its mouth. It is the fastest snake in the world and also the most poisonous.(3 minutes if not given aid you die) Njia ingine ya kumkamata au kumuua ni kupambana naye kwa kumtupia majani mabichi ya mkonge. Akiyauma yanakuka. So you throw mengi mpaka poison ina isha na jani kubakia bichi na la kijani.Kumbikumbi ni mchwa na kwetu tunawaita "NSWA" tulikua tuna export Zambia siku zileeeee.
 
ndiyo kuna senene, panzi, halafu wale wanaoliwa wako kama mchwa wanaitwaje, hasa kule kwenye "bomba hii, nyumba hii" wana mafuta hao!!

Mkuu, hao ni kumbikumbi. Ni watamu sana na wanaleta afya. Ni maarufu sana kule nyanda za juu Kusini kama unavyodai. Kuna picha za hao kumbi kumbi pale kwa Mjengwa ambazo alizipiga akiwa Sumbawanga wiki jana, unaweza kuchungulia!

Hivyo Tanzania wapo Cobra? Halafu yule ndege anaitwa Dudumizi analo jina la kiingereza?

Halafu kuna vile vindege vidogo hupenda kuruka kwa makundi (siyo mbayuwayu) yaani ni vidogo kweli sijui vinaitwaje, nimekuwa nikitafuta jina lake kwa muda mrefu sasa.


Mkuu, kuna dudumizi wa aina nyingi. Ila wale wakubwa huitwa "Giant hornbills" na wanasifika sana kwa sauti zao nzito wanapokuwa wanalia (au kuwika?). hupenda kula nyoka na mijuzi. Wakiwa wanatembea, mbawa zao ni nyeusi, ila wakiruka utaona rangi nyeupe chini ya mbawa.
Umenikumbusha mbali sanam big up sana.
Kuna kitabu maarufu sana cha ndege wa Afrika Mashariki na kinapatikana hapo US, kinaitwa "A Field Guide to Birds of East Africa",nimesahau mwandishi wake, ni kizuri sana, kitafute!
Kichungulie hapa, http://www.amazon.com/Field-Guide-Birds-East-Africa/dp/0856610798
 
SteveD,
Tupo, ndugu yangu! Hilo jina T-1 nimelipenda sana! Ni fupi na limetulia. I wish I could adapt it; need your advice.

Nimemkumbuka Kifutu baada ya kunitajia maumbile yake. I think I was wrong. Vilevile, niliwahi kusikia hilo jina "Swila" somewhere. Sikumbuki km muongeaji alikuwa mwenyeji wa kanda ya ziwa. What I want to say ni kwamba baadhi ya maneno ya Kiswahili yanaazimwa kutoka ktk lugha za makabila; hivyo, inawezekana hata hilo jina Swila likawa limeazimwa kutoka huko kanda ya ziwa, na kukubalika ktk Kiswahili. I'm not sure.

Nakumbuka kuwa rattle snake ni mrefu; kiasi cha kuweza kujivingirisha na sehemu ya mkia wake kuwa juu. Akiwa ktk hali hii, anauchezesha huo mkia ambao hutoa rattling sound (and hence the name) na kuwaonya viumbe wengine, hasa binadamu, kuwa "nipo hapa, angalia usinikanyage kwani nina sumu kali sana".

SteveD, hivi wale mijusi yenye rangi nyingi wanapatikana Mwanza tu? Au kanda ya ziwa tu? Wanaitwaje?

T-1

T-1, mijusi unaowasema nadhani unamaanisha wale wenye 'ku gonga gonga kichwa' kwa hasira au saa nyingine kwa dharau tuu!! Kwa kweli wana kitabia fulani hivi ukiwasoma kwa muda hutosita kusema ni 'kidharau' fulani hivi. Huwa wanagonga (node) kichwa kwa interval ya mara tatu tatu kwa jinsi ninavyokumbuka.

Kweli hawa wapo wengi sana kanda ya ziwa wanapenda kuishi kwenye mawe milimani. Lakini wanapatikana pia kwenye sehemu nyingi zenye mawe na milima, kama huku Iringa. Hawa rangi zao ni nyekundu nyekundu zaidi iliyochanganyika na kama mabaka meusi, na huwa wana ka-ushungi kichwani kwa madume yenye umri mrefu. Kule Mwanza jina lake la kisuma ni 'shigomola', meaning- head nodding.

Wale wengine wenye rangi rangi hivi zilizo fifia ambazo zina mistari iliyo nyooka toka kichwani hadi mkiani, na wanaonekana ni wapole wakati wote, hawa wanapatikana pande nyingi za Tanzania. Dar wapo wengi hawa na kule kanda ya ziwa wapo pia.

Kuna website hii http://www.faunaimportuk.com/photolizards2.htm ina onesha aina mbali mbali za mijusi.

Halafu nikupe stori, ina sikitisha kinamna, maana inaonesha ukatili nilio ufanya nikiwa mdogo. Nisameheni tu jamani....lol!
Basi, nilipokuwa mtoto nilikuwa naua sana mijusi, nilikuwa siwapendi ile kinoma. hasa hasa wale wanaokaa ndani ya nyumba wakati mwingine. Ambao wana rangi ya kijivu au saa nyingine wako colourless kabisa hadi utumbo wa ndani unaweza kuuona! Walikuwa wananitia kinyaa bana.... I don't know, but walikuwa target yangu kubwa ya utundu wa kikatili.

Nilikuwa natengeneza bunduki za risasi za chelewa...... natumaini wapo wana jf ambao wamefanya hivi pia... lol.. Hizi unachukua bomba fupi lenye tundu jembamba, kisha unaweka kwenye kitako cha bunduki cha ubao ulichochonga na kulifunga hilo bomba very tight na mipira ya matairi (kamba elastic). Kisha kutengeneza launcher ya chelewa kwa kutumia mipira (elastic rubber) ambayo inavutika mithili ya manati vile. Nilikuwa niko so soo deep katika hili, nakumbuka kuna wakati mpaka nilikuwa natengeneza automatic launchers za chelewa. T-1, utanisamehe, sitoelezea graphically yale yaliyotendeka baada ya kutengeneza bunduki hizo - CENSORED!!

Basi nilibahatika kwenda ulaya wakati fulani hivi. Nilikuwa naishi nyumba ya ku-share, na kulikuwa na dada mmoja wa kizungu alikuwa anaishi pale pia. Huyo dada alikuwa anafuga mjusi (pet animal wake), si unajua tena wenzetu jinsi walivyo, kila kitu kwao ni pet! Daah, mbona nilikuwa nateseka, maana kuna wakati ilikuwa inabidi anamtoa ili apate jua nje ya nyumba. Nami nikimwona tu kwenye kitenga change....mamaaaaaaaaaaaaaaaaa!!! uuwiiii, nilikuwa nakumbuka ile bunduki yangu ile mbaya!! Bahati sikuweza kuwa nayo tu..... nadhani police wangeitwa na hao RSPCA wa huko wangelijulishwa na mngeweza kumwona SteveD kwenye CBS na Foxnews zenu!!


Tanzania-1, T-1 iko poa pia. Nashukuru kwa kuniomba ushauri. OK, ningelikuwa wewe, ninge acha hilo jina la Tanzania -1 kama kitambulisho changu, maana ni rahisi mtu kujua uzalendo wako na wewe ni nani. Pia jina limetulia.
T-1, kwani nayo imetulia pia, hii unaweza kuiweka kwenye signature yako tu. Ili mtu anapo ona uvivu wa kutype mengi kama nilivo au kama anapenda kutype kwa kifupi jina la mtu kama jinsi mimi nilivo wakati mwingine, na aweze kufanya hivyo. Ukiiweka kwenye signature hivi sasa, itakatisha tamaa wale wengi wanaozidi kuongezeka wanaopenda 'kuiba' majina ya watu kwa kuyabadilisha badilisha kidogo......... :) :p


SteveD.
 
SWILA NI NYOKA MWEUSI na anatema mate(spitting cobra)KIFUTU NI NYOKA MFUPI NA MNENE ana rangi kama za chatu na ni mpole labda umkanyage ndiyo anauma. Ni kweli anaozesha muscles. Koboko ni kweli si wa kijani kabisa ila ni kati ya kijivu na kijani( Black mamba) black ina refer to the colour of its mouth. It is the fastest snake in the world and also the most poisonous.(3 minutes if not given aid you die) Njia ingine ya kumkamata au kumuua ni kupambana naye kwa kumtupia majani mabichi ya mkonge. Akiyauma yanakuka. So you throw mengi mpaka poison ina isha na jani kubakia bichi na la kijani.Kumbikumbi ni mchwa na kwetu tunawaita "NSWA" tulikua tuna export Zambia siku zileeeee.

Mwenekapufi,
Thanks a lot. Hiyo ya kurusha majani ya mkonge/katani nami naikumbuka haswaa!! Nakumbuka hizi simulizi, lakini sina uhakika nazo. Lakini niliambiwa wale wachezea nyoka wa asili kule Kanda ya ziwa (Wagobogobo) kama sijakosea, ndiyo huwa wanakamata nyoka kwa kutumia njia hiyoo. Infact, nyoka wengi wenye sumu ndiyo nasikia huwa wanakamatwa kwa njia hii. Halafu ndiyo wanawang'oa fangs zao ambazo huwa ndiyo chini yake iking'oka inakuwa ina hicho kifuko cha sumu. Hivyo kufanya hivyo ni kuzuia vifuko vya sumu kujitengeneza, wanafanya hivyo kwa interval za muda fulani (wiki moja au mbili kwa cobras - sina uhakika, nimesahau).

Kuhusu speed ya koboko, yaani wewe usiseme!! Nakumbuka wakati fulani hivi niko primary school, koboko alivamia shule.... aiseee... ilikuwa kasheshe tupu!! wanakijiji kibao walikuja kusaidia kumsaka. Nyoka anakimbia huyo usiombe... walahi tena, years gone by but i can still remember the incident!! Yaani anatimua hata kwenye mchanga utafikiri yuko majanini tu.. si unajua nyoka wengi hawawezi kukimbia kwenye mchanga au udongo...but that is not the case for koboko. Simply Amazing!
Wanakijiji, waalimu na wanafunzi walifanikiwa kumuua, baada ya simulizi zote, that was my first sight on the creature...... ukiondolea mambo ya Youtube siku hizi....lol :) !! Nikawa nimemwona, basi na kwa hilo naweza kusema kabisa kuwa, hiyo myth ya kuwa ana ushungi au kama nilivyo describe 'cock-crown' hapo awali, ni kuwa sidhani kama ni kweli... maana hakuwa nayo... or may be i am wrong and all, maana niliye mwona alikuwa amekufa tayari, na kwa maana hiyo some body organs zake zilikuwa tayari zimekwisha nguvu au kusinyaa. At the same time, naweza kuamini kuwa hawa nyoka wanaweza kuwa na ushungi kama wa jogoo, maana wana magamba, na kama unavyojua, nyoka, mijusi, na jamii nyingi za reptiles wakiwa na umri mwingi, haswa for male species, magamba yao yanabadilika rangi na kuwa makubwa na yakiwa kichwani, yanaweza kuonekana kama ushungi... so the myth could be factual in other sense.

By the way, Mwenekapufi, kuna nyoka nataka nimkumbuke sana jina lake lakini nashindwa... if you know can you help please, hata kama ni jina la Kisukuma au lugha yoyote nyingineyo ya nyumbani (and a latin name if possible).

Description: Anakaa kwenye maji, ni mrefu wasitani, ni mnene na ana rangi nyeusi tiii. Anakaa pembezoni mwa ziwa victoria (for what i remember), myths zipo kuwa, ukiwa na bahati mbaya ya kuumwa na nyoka huyo, usitoke majini, ni lazima utibiwa ukiwa majini, ukitoka- you are dead. Wako very poisonous. Pls help, i am very keen on remembering this one... the name doesn't seem to crop up! Thanks,

SteveD.
 
Back
Top Bottom