Kwenye hii engua engua, tume iliwajazia form wagombea wa CCM.Mapingamizi asilimia 99% ni ya wagombea wa upinzani, ndio waliokosea kujaza form. Ndio wagombea pekee wenye mapungufu ya kibinaadamu (Na ndio wenye haki ya kufanyiwa figisu). Ila wagombea wa CCM kama vile walijaziwa fomu toka mbinguni (Hawana kasoro wala mapungufu).
Mgombea wa CCM anaruhusiwa kufanya kampeni kwa lugha ya kikabila, anaruhusiwa "KUTUFOKEA" na "KUTUTISHA" wananchi wapiga kura. Anaruhusiwa kutumia "MABAVU" dhidi ya wanaharakati, waandishi wa habari, raia wanaokosoa na wagombea wa upinzani.
CCM wajipange sana kisaikolojia, hawajui adha na matatizo yanayo wakumba raia, kampeni zinafanywa na LAND CRUISER VX zaidi ya 60 sambamba na helikopter.
Raia wameshachoka, hata wakilazimisha ushindi ila mwisho wao umekaribia.