Majibu ya Zitto kwa JK yaleta utata mwingine

calmdowndear

JF-Expert Member
Jul 12, 2011
605
273
Haya ndio majibu ya Zitto kwa Profesa KIKWETE:

10689636_811943778826321_562774869891451206_n.jpg




Zitto kaanza kwa kusema hivi:

Our Leaders Must move away from culture of denials, cover-ups and proxies and deal honesty, sincerely and transparently with Tanzanians to regain their trust and confidence.

Tanzanians are no fools, they can see, they can hear, they can talk among themselves, they can think and they can act in the interest of their country.

[ largely borrowed from General Obasanjo's letter to President Jonathan of Nigeria ]. Found the words very relevant at the current circumstances in Tanzania

Kisha akaendelea kwa kusema hivi:

Nimemsikiliza Mhe Rais.
Ninachoweza kusema ni kwamba maazimio yale hayakuwa ya Zitto Kabwe, PAC, CAG au PCCB. Yalikuwa ni maamuzi ya Bunge zima. Bunge la vyama vyote kikiwamo chama cha Rais Kikwete yaani CCM. Sisi kama Bunge tulitoa maazimio yale kwa maridhiano, uzalendo na bila kutaka kumuonea mtu yeyote.

Suala hili sasa naliacha kwa wananchi. Bunge limefanya kazi yake na Serikali ambayo ndiyo tulikuwa tunasubiri maamuzi yake imeamua hivyo. Wananchi wataamua wenyewe.

Kuweka rekodi sawa:

1. PAP ( sio IPTL ) wamelipwa tshs 306 bilioni.

2. Alizosema Rais ni zile zilizokuwa Benki kama taslimu na dhamana za Serikali.

3. Ambazo hakusema ni zile ambazo zililipwa na TANESCO baadaye.

4. Ifahamike hadidu rejea ( Terms of References ) kwa CAG kufanya uchunguzi zilitolewa na PAC, hivyo PAC ndio yenye mamlaka ya kuzisemea, kuzielezea na kuzitolea ufafanuzi.

5. Kwenye eneo hili Rais hakuwa sahihi na Ikulu inapasa kurekebisha. Jumla ya fedha ambayo PAP wamelipwa kutoka akaunti ya TegetaEscrow Ni tshs 306 bilioni.

Muhimu sana Mamlaka ya Kutafsiri Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali haipo kwa mkaguliwa ( Serikali ) Bali kwa Bunge. Bunge hufanya kazi hiyo kupitia Kamati ya PAC.
 
Zitto na PAC yake walifanya makosa kuficha sehemu ya ukweli wanaoujua kwa kumsitiri huyu baba.
Hivyo Zitto na yeye anabeba laana ya kuliangamiza taifa hili kwa kumjua mwizi mkuu na kumfumbia macho.

Ni kweli tutaamua wenyewe ila kwa hili la kuficha ushiriki wa mkuu wa kaya mmetuangusha na kwa hali ya sasa,nchi hii inahitaji viongozi na wananchi jasiri kuliko Zitto na wenzie.
 
Huyu mtoto wa mama naye hana jipya kanafanya mambo ya kitoto tu bora kanyamaze tu.
 
Why kati ya maazimio yote 8. Hakuna hata moja amelikubali na kulitolea maamuzi?

1-8 ameweka porojo na vitisho na mbwembwe tu.

Mikataba kuwa wazi kutafukuza uwekezaji?
Kutaifisha mitambo ya tapeli kutafukuza wawekezaji?

Why ame-deal na Tiba wakati kuna watu walioidhinisha ufisadi wa escrow?

Maadili ni kwa Tibaijuka pekee na siyo Chenge and the team?.
 
Zitto na PAC yake walifanya makosa kuficha sehemu ya ukweli wanaoujua kwa kumsitiri huyu baba.
Hivyo Zitto na yeye anabeba laana ya kuliangamiza taifa hili kwa kumjua mwizi mkuu na kumfumbia macho.

Ni kweli tutaamua wenyewe ila kwa hili la kuficha ushiriki wa mkuu wa kaya mmetuangusha na kwa hali ya sasa,nchi hii inahitaji viongozi na wananchi jasiri kuliko Zitto na wenzie.


JK anasema wawezekaji hawataki mikataba iwe wazi. Lakini wawekezaji wanaituhumu serikali kuficha mikataba maana wao wanataka iwe wazi.
 
Haya majibu ya jumla jumla kwa Jambo moja moja ni hatari,kufanya mzaha kwa kutumia kigezo cha ufinyu wa uelewa wa wazee na kwa nini haya hakuyasema kwa wanahabari na aulizwe maswali?

Mlisema mkulu akiguswa nchi itayumba na haya isiyumbe lol
 
Zitto Kabwe
Shujaa wa skandali ya Goldenberg: David Munyakei
March 2014
Nchi ya Kenya iligubikwa na kashfa kubwa sana ya
ufisadi iliyoitwa Goldenberg Scandal katika miaka ya
mwanzo ya 1990. Kashfa ile ilihusu uporaji wa zaidi ya
dola za kimarekani bilioni moja ( shilingi trilioni moja
za kitanzania kwa bei za sasa). Ulikuwa ni wakati wa
utawala wa Daniel Arap Moi kama Rais wa Kenya. Ni
ufisadi ambao unaendelea kupigiwa mfano mpaka sasa
katika medani za kimataifa. Raia wa Kenya aitwaye
David Munyakei ndio shujaa wa kashfa hiyo ya
Goldernberg. Kitabu cha hadithi ya kweli ya David
Munyakei kinaelezea namna shujaa huyu alivyoibua
kashfa hiyo na namna maisha yake yalivyoisha katika
hali ya uduni mkubwa licha ya kupata tuzo mbalimbali
za kupambana na ufisadi. Mwandishi Billy Kahora
kupitia Kwani Series ndio ameandika kitabu hiki. Ni
kitabu cha kurasa 135 tu lakini kimesheheni masuala
mazito kuhusu mtu mmoja aliyeibua kashfa kubwa
nchini Kenya na kunusuru uchumi wa nchi hiyo. Kashfa
hiyo ilihusu uuzaji nje wa dhahabu na almasi ili kukuza
mauzo nje ya nchi.
David Sadera Munyakei alikuwa karani wa Benki Kuu
ya Kenya na alianza kugundua nyaraka zinazoonyesha
masuala mbalimbali ya kifedha ambayo yalikuwa
yanatia shaka na kutoa taarifa kwa mabosi wake,
mabosi walidharau taarifa zake. Aliamua kwa ushujaa
kabisa kutoa taarifa kwa wabunge wa upinzani nchini
Kenya, Paul Muite na Profesa Anyang’ Nyong’o ambao
waliibua kashfa hii bungeni na kuanza kuandikwa na
vyombo vya habari kama gazeti la Nation. Baadaye
Munyakei alikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa
kutoa siri za Serikali, kisha akaachiwa lakini akapoteza
kazi yake na kuamua kuhama jijini Nairobi na kwenda
kuishi mjini Mombasa ambapo alibadili dini kuwa
muislam, kuoa binti wa wa kibajuni na kubadili kabisa
maisha yake. Hata hivyo maisha ya Mombasa
yalimshinda na kuamua kurudi kijijini kwao Olokurto
katika wilaya ya Narok. Alipokimbilia Mombasa alibeba
nyaraka zote za kashfa ya Goldenberg na kwenda
nazo huko, akazificha chini ya ardhi. Nyaraka hizo
zilitumika miaka kumi baadaye katika uchunguzi wa
Tume ya Goldenberg iliyoundwa na Rais wa Tatu wa
Kenya Mheshimiwa Mwai Kibaki.
David Munyakei aliajiriwa na Benki Kuu ya Kenya
mwaka 1991alipomaliza elimu ya sekondari kama
karani kwa ahadi ya kupelekwa kwenye masomo ya
ziada ya Chuo Kikuu. Mwenyewe alikuwa na ndoto ya
kusoma mpaka kufikia elimu ya kiwango cha Shahada
ya Uzamivu (PHD). Alipangiwa idara ya maendeleo na
baada ya miezi kadhaa aligundua kuwa mambo
hayaendi sawa katika nyaraka alizokuwa anafanyia
kazi. “niligundua kuwa mambo hayapo sawa na hivyo
kumwambia rafiki yangu Onyango Jamasai ambaye
alikuwa mkubwa zaidi kazini kwangu” alinukuliwa
akihadithia David Munyakei. Aliendelea “Haya mambo
sio sawa kabisa, hizi dhahabu na almasi zinatoka pande
gani ya Kenya kupelekea mamilioni haya ya fedha
kulipwa”. Hata hivyo mabosi wa Munyakei hawakuwa
tayari kushughulikia maangalizo ya David Munyakei.
“ilikuwa ni ufisadi wa wazi wazi”. Munyakei alipoona
hali inazidi kuwa mbaya na uporaji wa mabilioni ya
fedha unafanyika aliamua kuwaeleza wabunge ili
waweze kulisema jambo hilo bungeni na kwenye vyombo
vya habari. “nilimwambia Anyang’ Nyong’o na Paul
Muite nini kilikuwa kinatokea, ilichukua miezi mitatu
tangu niwaambie na kuanza kuona habari hiyo kwenye
vyombo vya habari”. “ nilipoona habari imetoka kwenye
vyombo vya habari nilifurahi sana na nikabeba gazeti
kwenda kuwaonyesha wafanyakazi wenzangu”. Huo ndio
ulikuwa mwisho wa David kazini kwake kwani alifuatwa
na askari wa polisi wa Kenya na kumweka ndani kwa
makosa ya kutoa siri za ofisi.
Kukamatwa kwa David kulileta madhara makubwa sana
kwa familia yake kwani mama yake mzazi alipata
mshtuko mkubwa sana kusikia mtoto wake
amekamatwa na kuwekwa ndani. Mama ya David
alikuwa mfanyakazi wa Magereza nchini Kenya na
hakupenda kabisa kuona mwanae akiwa mfungwa.
Mama huyu alipatwa na shinikizo la moyo na kufariki
dunia mwezi mmoja baada ya David kukamatwa. Hata
hivyo David hakukutwa na hatia yeyote na aliachiliwa
huru. Benki Kuu ya Kenya ilimwachisha kazi kwa kwa
sababu ‘haina imani naye’. David alihamia Mombasa
ambapo alifanya kazi ya kuuza matangazo katika
gazeti la Standard na kisha lile na Nation. Baadaye
alimwoa Mariam Ali Hani kutoka kabila la Bajuni la
Pwani ya Kenya. Maisha yalipomshinda huko Mombasa,
David alirudi kijijini kwao Olokurto.
Baada ya Rais Mwai Kibaki kushika madaraka kutoka
kwa Daniel Arap Moi, aliunda Tume ya Goldenberg
kufanya uchunguzi dhidi ya ufisadi mkubwa sana wa
uliotokea katika historia ya nchi ya Kenya. David
aliamua yeye mwenyewe bila kuombwa na mtu yeyote
kupanda matatu na kutoa ushahidi wake katika Tume
hii. Alikwenda Mombasa kufukua nyaraka alizoficha
huko na kutoa ushahidi wenye vielelezo vyote kwa
Tume. David akawa mtu maarufu na shujaa nchini
Kenya. David akapewa tuzo mbalimbali ikiwemo Tuzo
ya Uadilifu na Tuzo ya Firimbi. Aliahidiwa kuwa
atarejeshwa kazini kwake na kulipwa mishahara yake
yote tangu aondolewe kazini. Hakuna ahadi kwa David
iliyotekelezwa. Alikufa masikini kwa kukosa dawa ya
gharama ndogo sana. Aliacha mjane na watoto bila
msaada wowote ule.
Hiki ni kitabu cha mafunzo makubwa ya namna ya
kuwaenzi mashujaa wetu, watu wanaoamua kujitoa
muhanga kutoa habari za kifisadi ili kukomesha
vitendo hivyo katika nchi. Ni kweli David alipata tuzo
mbalimbali lakini tuzo hizo hazikuwa na maana yeyote
katika maisha yake na familia yake. David katika
maisha yake ya mwisho alijikuta anavunja misingi ile ile
aliyojiwekea kwa kuanza kuona fedha ni bora kuliko
utu. Tukiwaenzi mashujaa wetu vizuri tutapata
mashujaa wengi zaidi. Hivi hapa Tanzania tunajua
shujaa wa EPA? Tunamjua shujaa wa Buzwagi? Sio
wanasiasa waliopewa hoja na kwenda kuzisema bungeni,
bali wananchi waliojitoa muhanga kutoa taarifa hizi
kwa wanasiasa. Kuna mtu amewahi kuthubutu kujiuliza
mashujaa hawa wapo wapi?
Nashauri upate kitabu hiki “The true story of David
Munyakei”
 
walichofanya kamati ya akina Zitto kwenye sakata la Escrow ndicho walichokifanya kamati ya akina mwakyembe kwenye sakata la Richmond,tuliambiwa kwamba ukimgusa Rais nchi itayumba, kumbe daima WIZI umekuwa bora na unalindwa kuliko maslah mapana ya nchi yetu,Watanzania tunafanyiwa usanii na mwiz anajulikana alafu mbuzi wa kafara wanakuwa akina Tibaijuka,Sasa tumeaminishwa na Rais kuwa ni bora kuumia kuliko kuondoa jinamiz la IPTL kama mwekezaji,Rais anaongea kana kwamba Tanesco haijui na ni shirika la Kenya au Uganda.Ni hasara Kuwa na viongoz kama Jk wasioguswa na mateso ya watanzania.Kama Urais utaendelea kubakwa namna hii nchi haina mud a mrefu itasambaratika.
 
Zitto na PAC yake walifanya makosa kuficha sehemu ya ukweli wanaoujua kwa kumsitiri huyu baba.
Hivyo Zitto na yeye anabeba laana ya kuliangamiza taifa hili kwa kumjua mwizi mkuu na kumfumbia macho.

Ni kweli tutaamua wenyewe ila kwa hili la kuficha ushiriki wa mkuu wa kaya mmetuangusha na kwa hali ya sasa,nchi hii inahitaji viongozi na wananchi jasiri kuliko Zitto na wenzie.

Maamuzi hayakuwa ya Zitto na PAC peke yake, bali yalikuwa maamuzi ya Bunge zima.
Ova
 
Why kati ya maazimio yote 8. Hakuna hata moja amelikubali na kulitolea maamuzi?

1-8 ameweka porojo na vitisho na mbwembwe tu.

Mikataba kuwa wazi kutafukuza uwekezaji?
Kutaifisha mitambo ya tapeli kutafukuza wawekezaji?

Why ame-deal na Tiba wakati kuna watu walioidhinisha ufisadi wa escrow?

Maadili ni kwa Tibaijuka pekee na siyo Chenge and the team?.
Chenge hakuwemo kwenye mapendekezo ya Bunge. labda tuwaulize wabunge kwa nn hawakumuweka
 
Back
Top Bottom