Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,399
Mimi ndio nazidisha imani kwamba CCM ni chama imara kwenye masuala ya propaganda na hizi ziara za Uchina ndio zinawanoa kisawasawa.
Mheshimiwa Samwel Sitta ni ndumilakuwili na ni wa kuogopewa sana maana ndie anaeonekana kuongoza kampeni ya kuwagawa wananchi kupitia vyombo fulani vya habari.
Juzijuzi alionyesha waziwazi kwamba ana ambition ya kuwa raisi na kwamba ana timu yake ya kumpa tafu. Kazi ya kuigawa CCM inamshinda na baada ya kupigwa mkwara ndio anakuja na hili.
Maslahi ya umma ni lazima siku zote yawekwe mbele na na vyombo vya habari vipo kwa ajili ya kuanika hizi propaganda na athari zake kwa demokrasia na mabadiliko ya kijamii.
Ni nani huyo ambae twaweza kusema kwamba kwa sasa ndie "spin doctor" au "senior propagandist?"
Mheshimiwa Samwel Sitta ni ndumilakuwili na ni wa kuogopewa sana maana ndie anaeonekana kuongoza kampeni ya kuwagawa wananchi kupitia vyombo fulani vya habari.
Juzijuzi alionyesha waziwazi kwamba ana ambition ya kuwa raisi na kwamba ana timu yake ya kumpa tafu. Kazi ya kuigawa CCM inamshinda na baada ya kupigwa mkwara ndio anakuja na hili.
Maslahi ya umma ni lazima siku zote yawekwe mbele na na vyombo vya habari vipo kwa ajili ya kuanika hizi propaganda na athari zake kwa demokrasia na mabadiliko ya kijamii.
Ni nani huyo ambae twaweza kusema kwamba kwa sasa ndie "spin doctor" au "senior propagandist?"