MAJIBU YA MAWAZIRI WA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TNZANIA DHIDI YA KERO ZA WANANCHI
- Swali alilouliza mbunge ni kweli lipo na serikali ina taarifa nalo
- Suala hili ni nyeti na hasa kwa usalama wa nchi yetu
- Hata hivyo katika ziara yake Mh. Rais ameonana na wafadhili na kufanya nao mazungumzo na wameahidi kutusaidia
- Lipo kwenye sera ya chama
- Serikali ni sikivu
- Mchakato utakapokamilika litatatuliwa na litakuwa historia kwa wananchi wetu
- Kama ilivyotolewa ufafanuzi kwenye jibu la msingi, upembuzi yakinifu umekamilika
- Utekelezaji unategemea fedha za wafadhili
- Kadiri fedha zitakavyotolewa na wafadhili
- Waheshimiwa muwe wavumilivu naamini kabla ya mwaka 2015 mradi utakuwa umekamilika
- Nashangaa watu wanaobeza jitihada za serikali
- Kwenye mwaka huu wa fedha ni mradi uliotengewa bilioni .... za fedha
- Kufanya tathmini upya ya wananchi watakaofidiwa na fedha hii inategemea kutolewa na wafadhili na serikali ya ...... (marekani) imekubali kutoa hela
- Kutambua nchi hii ni kubwa na vipaumbele ni vingi
- Serikali inafikiri kabla ya kuanza ..... tunahitaji kupitia sheria zetu na kuona namna ya kulitekeleza
- Serikali haina taarifa nalo
- Ikibanika serikali itachukua hatua kali
- Serikali inafikiria ni namna gani ya kuwasiliana na wadau wake kuona namna gani
- Mchakato wa katiba mpya
- Ni kati ya vitu ambavyo ni vya kujivunia ambavyo serikali yetu imevifanya
- Wananchi wapewe fursa bila kuingiliwa
- Kabla ya uchaguzi mkuu ujao
- Ni tuhuma za uchochezi dhidi ya serikali yetu
- Suala hili liko mahakamani na haturuhusiwi kuingila uhuru wa mahakama
- Lipo kwenye ilani ya CCM
- Kwenye hotuba ya Mh. Rais kwenye hotuba ya ufunguzi wa bunge
- Kujitafutia umaarufu wa kisiasa
- Kwa majibu haya kero za wananchi wetu zitatatuliwa?
- Wanafunzi wetu wakitumia mtindo huu mashuleni tutegemee kuwa na kizazi gani?
- Je nchi za wenzetu hasa Afrika Mashariki majibu yanayotolewa na mawaziri wao yanalingana na haya ya mawaziri wetu?
- Umakini wa serikali yetu katika kutatua kero za wananchi unaweza kupimwa na viongozi waliopo katika serikali hii kwa majibu haya?
- Ukitathimini majibu haya unapata picha gani?