Majibu ya Kikwete na BBC: Tumevuna tulichokipanda

Wakuu heshima mbele,
Yafuatayo ni mahojiano kati ya Rais Kikwete na Mwandishi wa BBC Bw. Omar Mutasa huko Afrika Kusini ambako Rais Kikwete alikuwa anaendelea na ziara yake ya Kiserikali.


BBC: Suala la Umeme Mheshimiwa Rais Kikwete ungependa kulizungumzia nini?

Rais Kikwete: Tatizo la umeme kimsingi ni suala la ukame tu. Kwa sababu mabwawa yetu ya kuzalisha umeme yanayotoa umeme karibu MW600 sasa hivi yanatoa umeme kidogo sana. Maji pungufu ndio maana kuna tatizo hilo.

BBC:Mheshimiwa, hili suala si la leo wala si la jana limekuwepo kwa muda mrefu, kwanini serikali haina njia mbadala ya kuweza kutatua suala hili? Tanzania ina raslimali nyingi mheshimiwa Kikwete!

Rais Kikwete: Kwanza, serikali haina uwezo wa kufanya mvua inyeshe, unajua unajua hivyo, Kwa sababu (kicheko) ingekuwa na uwezo wa kufanya mvua inyeshe mabwawa yale yangejaa.
Ni kweli kuwa Tanzania inazo raslimali za kutosha na katika kipindi hiki - toka wakati ule - sisi tulipoingia tumekuta suala la Ukame na mwaka 2007 tukapata matatizo ya kwanza.Baada ya pale tukafanya uamuzi kwamba sasa tuanze kuwekeza katika vyanzo vingine; tuongeze uzalishaji wa umeme kutoka vyanzo vingine. Tuongeze uzalishaji wa umeme kutoka vya vya kutumia gesi asilia twende kwenye makaa ya mawe. Kutoka vyanzo vya gesi asilia tayari tuna mtambo pale Ubungo, na toka mwaka 2009 mpaka sasa tumeshaongeza MW145, itakapofika Disemba tutakuwa tumeongeza MW160 nyingine. Tutakuwa tumeongeza MW300 siyo kidogo.

BBC: Mhe. Kikwete Mmoja katika wabunge Bw. John Mnyika ambaye ni Mbunge wa upinzani ambaye ni Waziri Kivuli wa Nishati amekuwa akilalamika na kwamba amewahi kusema kwamba hili tatizo ni tatizo linalowahusu Watanzania wote na amesema mje pamoja na kuona vipi mtakavyotatua tatizo hili. Na sasa hivi Bungeni wamesimamisha mswada, wa kutoa bajeti ya nishati ya Tanzania. Wewe unachukulia vipi matamshi kama haya kutoka kwa Wabunge?

Rais Kikwete: Mimi nasema hivi yeye si Mbunge atoe maarifa yake tu; anayo maarifa gani na anapendekeza kitu gani. Kwa sababu toka Uhuru mabwawa tuliyotengeneza ni Kidatu MW200, Mtera MW80, Kihansi MW 165 mimi nilipokuwa Waziri wa Nishati, pale Pangani tumeongeza.Sasa ufikirie kwamba toka Uhuru tumeweza kuzalisha umeme wa MW600, lakini toka 2009 mpaka Disemba mwaka huu tutakuwa tumeongeza MW300! Ni jitihada kubwa.
Mimi nasema kwamba usipozitambua hizo ni kwamba wewe mwenyewe siyo mkweli.Sasa ni hivi, unajua hii mitambo ya umeme si mitambo unaenda kununua kama unavyonunua jaketi lako hili. Ni kwamba ukitaka mitambo ya umeme, lazima uweke order wakutengenezee. Huu mtambo unaofika mwaka huu Disemba order tuliweka mwezi wa Juni mwaka jana. Inachukua muda huo kutengeneza. Sasa ingekuwa mnaenda kutafuta mitumba, mitumba ya mitambo tu ya kununua iko mingi kweli. Tukasema hatuwezi kufanya hivyo.Mimi nasema hivi, kitu kikubwa ni kuwa na subira. Tumefanya jitihada kubwa. Ni lazima watu watambue kuwa tumefanya jitihada kubwa katika miaka hii toka 2009 mpaka sasa hivi 2011 Disemba tutakuwa tumeongeza MW300 kulinganisha na MW600 ambazo tumeziongeza katika miaka yote hii. Nasema ni lazima watu watambue hivi. Sasa kama kuna mtu ana maarifa ya haraka zaidi nasema mtu atoe maarifa hayo na sisi kama yapo tutayafanyia kazi.

BBC: Kuna njia kama umeme wa jua, umeme wa kutokea ardhini wa mvuke, kwanini serikali haitafuti njia mbadala kuzalisha umeme kwa njia hizo?

Rais Kikwete: Nasema hivi, hata umeme wa jua lazima ujenge, umeme wa mvuke lazima ujenge, si kitu cha mwezi mmoja. Nasema huo ndio ukweli wenyewe na wakati mwingine na nyinyi mjifunze hayo mambo ya kitaalamu kulikoni kuuliza tu hivi hivi. Unajua ungekuwa na wewe unauliza kwa hoja - “unajua kwamba hiki kitu hiki ingekuwa umeme wa jua miezi miwili tu upo” - tungeweza kufanya hivyo.Sisi sasa hivi kwa mfano tunajiandaa kuzalisha umeme wa kutumia Upepo, pale Singida. Tuna mwaka wa tatu sasa tuna mipango na Wakorea wa Kusini, umeme haujakuwepo. Kwa hiyo nasema hayo ni maelezo rahisi. Wanasema “mbona jua lipo?” katengeneze umeme wa jua kama jua lipo! (kicheko).

BBC: Watanzania wamekuwa wakisema (mwisho kabisa) kwamba Tanesco ingebinafsishwa ili waweze kupata makampuni kufanya kazi hiyo ya umeme?

Rais Kikwete: Aah! Kwani ukitaifisha kesho ndio utapata mitambo kesho? Nasema hivi ni vizuri kuelewa tu - kwanza tatizo la msingi - ni maji kukauka kwenye mabwawa. Maji yasingekauka kwenye mabwawa tatizo hili halipo. Maji yamekauka kwenye mabwawa kwa sababu ya ukame. Hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzuia ukame usiwepo. Sasa hiki ndicho kiini cha tatizo. Sasa nasema sisi jitihada ambayo tumeifanya ni kupunguza sasa kutegemea umeme unaotakana na nguvu ya maji.Toka mwaka 2009 tumewekeza adi Disemba 2011 tutakuwa tumeongeza MW 310, yenyewe hiyo ni hitihada kubwa, ni vizuri ukaitambua jitihada hiyo. Kulikoni kusema kitu tu nasema hatakam huna majawabu rahisi utuambie tu.

MWISHO.
 
FaizaFoxy,

Miaka ya 80, hizo megawati 600 zilikuwa zinatutosha au hazitoshi? kulikuwa na watumiaji wangapi? Je umfactor kuwa kujenga hivo megawati 600 kuliendana na kujenga network ya kuusambaza umeme nchi nzima?

Kwa hilo la oda ya mitambo mipya, labda mwenzetu uko jikoni ukisaini tenda, mpaka Symbion na Jacobsen wamekuwa ndipo Serikali inaanza kudai mitambo itafika! Mwaka jana mwezi kama huu, tulikuwa na shida ya umeme, je walikuwa wapi kuagiza hiyo mitambo?

Jee mwaka 2006 walipoamua kuwapa Richmond na Dowans, kwa nini hawakuweka oda ya mitambo ili ikifika 2008 iwe imekamilika na ni mali ya Tanesco na iwe ya kuzalisha mw400 na si 50?

Just accept the fact that Jamaa anacheza bugi kila siku na ama hajui analofanya au ni kwa makusudi kabisa anafanya analofanya!


Miaka ya 80 (1980s)hatukuwa na megawati 600, uko wapi weyee? Nilichkueleza mimi ni jumla ya miaka themanini (80 Years)

Hakuna wakati wowote ambapo umeme umetutosha Tanzania na kabla hatujawa Tanzania. mpaka leo ni asilimia chini ya 15 inayopata umeme, Kikwete anakuambia atahakikisha ifike 50% kabla hajaondoka na hapo namuamini kwani anafanya kweli.

Megawati mia zinakuja mwezi huu na wa nane zilitiwa order June 2010. Wewe inaonesha uko "out of touch kabisa" bora ukae kimya tu maana huna hoja una viroja.
 
Mkandara kumbuka kuwa kwa miaka isiyopungua themanini, ndio 80, kabala ya Kikwete ni 600MW za umeme kwa miaka yote hiyo. Leo Kikwete kwa muda mfupi aliokuwepo, miaka 6 tu, kisha weka mikataba ya zaidi ya 700MW, ndio zaidi ya 700MW, na anaendelea.

Mfano, 100MW za kununua mitambo mipya order imetolewa June 2010 mitambo imeanza kufika mwezi huu, baada ya zaidi ya mwaka. Hiyo ndi hali halisi. Ulitaka afanye nini? Asisaini hata hiyo mikataba? Hao wenzake kabla yake walikuwa wapi? Walikuwa hawajapelekewa makadirio ya umeme na jinsi matumizi yanavyokuwa na upatikanaji wa mitambo huchukuwa muda? Walipelekewa na wakakaa kimya. Leo unataka kumlaumu anaetenda? Unanshangaza sana, au mlitaka akanunue mitumba? Kama ni mitumba hata ya kukodisha mliipigia kelele. Mnashangaza sana.

"Damned if you do, damned if yoo don't" ndio hukumu ya Kikwete kutoka kwa watu wa aina fulani na tunajua kwanini.
Hapana mkuu wangu unakosea sana na maelezo ya JK yanaonyesha ufinyu wake wa kufikiri..
labda nikueleze vizuri na kwa uhfasaha ambao JK anaukwepa.
Hadi kufikia miaka ya 80 uwezo wetu ktk kuzalsha umeme (vyanzo) ulikuwa zaidi ya MW 3,000 na sii 600 isipokuwa tulikuwa tukitumia MW 600 ambazo Tanesco walizitumia ktk usambazaji..

sasa JK anachozungumzia ni kuongezeka kwa generators kuzalisha MW 300 zaidi hali generator hizo zinatumia Gas! chanzo cha nguvu za umeme kinachotokana na gas ndicho muhimu zaidi ya mikataba ya wawekezaji wa Generators ambao wanatuumiza ktk malipo. Ujenzi wa gas ya Songos ili itumike kuzalisha umeme sio mkakati wa JK ameukuta. Hydro dams kazikuta na hata Kiwira hkaikuta lakini kashindwa ku zikarabati kwa njia moja ama nyingine kiasi kwamba demand ya Umeme imeongezeka lakini yeye anaendelea kujaza Magenerator..Vynzo vinakufa kama viwanda vya Nyerere na imefikia hadi vyanzo hivyo haviwezi tena kuzalisha zaidi ya tuseme MW 900 (generating capacity)..

Ni sawa na wewe kununua jiko la Umeme hali unajua kabisa kijijini kwenu hakuna Umeme, kisha unanunua generator wakati unajua hakuna Diesel..matatizo ni kuchukua maamuzi rahisi bila kuzingatia kwanza vyanzo vya kitu unachotaka kutumia. Na ndio sisi tunasema matatizo yetu ni ya kujitakia.

Toka JK ameingia madarakani anajua fika mwalimu alitumia MW 600 kwa sababu ndio ilikuwa mahitaji yetu wakati huo na kazi kubwa ilikuwa kusambaza umeme huo hadi vijijini, miji yote mikubwa yenye umeme haikupatwa na adha hizi za mgao, leo JK kenda sambaza umeme kwenye machimbo ya madini na kuita wawekezaji wa viwanda hali akijua fika hatuna vyanzo vya kutosheleza mahitaji hayo huoni kama huu ni Ujinga mkubwa!.. Mkuu wangu hata sisi wa uswahilini huwezi kualika watu kwenye Hitma wakati unajua fika huna gunia la mchele..maswala ya Sunna hayawezi kuondoa ukweli kwamba umewaweka watu njaa...

Ni majuzi tu ktk sakata la Dowans, niliwahi kusema wazi kwamba hata kama tutawachukua Diowans na hizo MW100 hazitoshi kulingana na mahitaji yetu kwa nini tuingie mkataba na shirika hili ama tukubali ufisadi wao kwa sababu ya shida wakati tunajua fika MW 100 haziwezi kuondoa tatizo la mgao hata kidogo..Lakini wamelazimisha kununuliwa kwa mtambo huo wakati wakijua fika kwamba tatizo kubwa ni uwezo wa bomba ya gas kuhudumia mitambo iliyopo.

Kwa hiyo mkuu wangu JK anachokifanya ni kununua mashangigi hali hatuna barabara na wewe unamsifia kwa kuongeza mashangingi zaidi ukashindwa kufikiria gharama za mafuta, maintanance na kadhalika..haya ndio yanatupata leo hii mkuu wangu Umeme umewekwa juu ya mawe!
 
Hapana mkuu wangu unakosea sana na maelezo ya JK yanaonyesha ufinyu wake wa kufikiri..
labda nikueleze vizuri na kwa uhfasaha ambao JK anaukwepa.
Hadi kufikia miaka ya 80 uwezo wetu ktk kuzalsha umeme (vyanzo) ulikuwa zaidi ya MW 3,000 na sii 600 isipokuwa tulikuwa tukitumia MW 600 ambazo Tanesco walizitumia ktk usambazaji..

sasa JK anachozungumzia ni kuongezeka kwa generators kuzalisha MW 300 zaidi hali generator hizo zinatumia Gas! chanzo cha nguvu za umeme kinachotokana na gas ndicho muhimu zaidi ya mikataba ya wawekezaji wa Generators ambao wanatuumiza ktk malipo. Ujenzi wa gas ya Songos ili itumike kuzalisha umeme sio mkakati wa JK ameukuta. Hydro dams kazikuta na hata Kiwira hkaikuta lakini kashindwa ku zikarabati kwa njia moja ama nyingine kiasi kwamba demand ya Umeme imeongezeka lakini yeye anaendelea kujaza Magenerator..Vynzo vinakufa kama viwanda vya Nyerere na imefikia hadi vyanzo hivyo haviwezi tena kuzalisha zaidi ya tuseme MW 900 (generating capacity)..

Ni sawa na wewe kununua jiko la Umeme hali unajua kabisa kijijini kwenu hakuna Umeme, kisha unanunua generator wakati unajua hakuna Diesel..matatizo ni kuchukua maamuzi rahisi bila kuzingatia kwanza vyanzo vya kitu unachotaka kutumia. Na ndio sisi tunasema matatizo yetu ni ya kujitakia.

Toka JK ameingia madarakani anajua fika mwalimu alitumia MW 600 kwa sababu ndio ilikuwa mahitaji yetu wakati huo na kazi kubwa ilikuwa kusambaza umeme huo hadi vijijini, miji yote mikubwa yenye umeme haikupatwa na adha hizi za mgao, leo JK kenda sambaza umeme kwenye machimbo ya madini na kuita wawekezaji wa viwanda hali akijua fika hatuna vyanzo vya kutosheleza mahitaji hayo huoni kama huu ni Ujinga mkubwa!.. Mkuu wangu hata sisi wa uswahilini huwezi kualika watu kwenye Hitma wakati unajua fika huna gunia la mchele..maswala ya Sunna hayawezi kuondoa ukweli kwamba umewaweka watu njaa...

Ni majuzi tu ktk sakata la Dowans, niliwahi kusema wazi kwamba hata kama tutawachukua Diowans na hizo MW100 hazitoshi kulingana na mahitaji yetu kwa nini tuingie mkataba na shirika hili ama tukubali ufisadi wao kwa sababu ya shida wakati tunajua fika MW 100 haziwezi kuondoa tatizo la mgao hata kidogo..Lakini wamelazimisha kununuliwa kwa mtambo huo wakati wakijua fika kwamba tatizo kubwa ni uwezo wa bomba ya gas kuhudumia mitambo iliyopo.

Kwa hiyo mkuu wangu JK anachokifanya ni kununua mashangigi hali hatuna barabara na wewe unamsifia kwa kuongeza mashangingi zaidi ukashindwa kufikiria gharama za mafuta, maintanance na kadhalika..haya ndio yanatupata leo hii mkuu wangu Umeme umewekwa juu ya mawe!

Hapo ndio umechemsha kabisa sina haja hata ya kumalizia kusoma mada yako. Mie naongelea jumla ya miaka 80 wewe unanipeleka 1980 ambapo hata chakula ilikuwa shida, kaya moja kilo moja kwa wiki ya sukari. Usinikumbushe.
 
Miaka ya 80 (1980s)hatukuwa na megawati 600, uko wapi weyee? Nilichkueleza mimi ni jumla ya miaka themanini (80 Years)

Hakuna wakati wowote ambapo umeme umetutosha Tanzania na kabla hatujawa Tanzania. mpaka leo ni asilimia chini ya 15 inayopata umeme, Kikwete anakuambia atahakikisha ifike 50% kabla hajaondoka na hapo namuamini kwani anafanya kweli.

Megawati mia zinakuja mwezi huu na wa nane zilitiwa order June 2010. Wewe inaonesha uko "out of touch kabisa" bora ukae kimya tu maana huna hoja una viroja.

Faiza,

Name us 5 major accomplishments done by 4th Government, and these accomplishments are project that they innitiated, planned and invest to the completion. Just 5 major projects!
 
Nchi inazidi kukumbwa na GIZA mtu anaendelea kusema JITIHADA KUBWA JITIHADA KUBWA!
 
Hapo ndio umechemsha kabisa sina haja hata ya kumalizia kusoma mada yako. Mie naongelea jumla ya miaka 80 wewe unanipeleka 1980 ambapo hata chakula ilikuwa shida, kaya moja kilo moja kwa wiki ya sukari. Usinikumbushe.
Sasa unaposema jumla ya miaka 80 unahesabu kitu gani? maanake nashindwa kukuelewa kwani hatujawa na Uhuru kwa miaka hiyo na hata ukizungumzia ukoloni inahusu vipi na uongozi wa JK?.

Na maajabu unakubali miaka ya 80 ambayo hatukuwa na chakula sijui kaya moja kilo moja kwa wiki lakini haya ya kukosa Umeme huyaoni tena una utetezi mkubwa wakati shida ni kubwa kuliko miaka 80 iliypita!. Wapi zamani mkuu...maanake mimi nakubali shida za miaka ya 80 lakini wewe unatetea ongezeko la umeme kwa miaka 80 wakati wananchi wanalia shida kuliko hata zile za miaka ya 80's au miaka 80 iliyopita. Kama hujichanganyi kitu gani mkuu wangu...

najua kweli JK ameweka mkataba na Warussi kujenga hydropower ya Mw 700 huko Iringa, lakini hii pia sio ujanja ikiwa yeye mwenyewe anakiri kwamba mvua hazileti yeye, na kwa nini asiende na geothermal au upepo? tukisema sisi mnasema tunamchukia JK. I mean mkuu wangu JK ktk utetezi wake hata angesema swala la ukosefu wa umeme tunalifanyia uchunguzi na zipo sababu akataja matatizo ya IPTL, Songos na kuwajaza ujinga wao kuliko kusingizia mvua kisha anakuwa mkali kwa ujinga na aibu alotuachia na zaidi ya yote JK anazidi kuweka mikataba ya ujenzi wa Dams kuzalisha umeme akitegemea mvua za Mungu...
Tena basi nasiki na Brazil nao wanapewa mradi wa 2bn kujenga nini - dam..
 
Kweli kama tuna machozi, basi tujililie wenyewe. Hamna wa kumlaumu mwenzake tujilaumu wenyewe
 
Ubabaishaji tu... tangu alipokuwa Waziri wa Nishati ni miaka mingapi imepita? Ukame ulikuwepo tangu 1974, 1984, 1994 nk... hata wangekuwa na mikakati imara tangu mwaka 2000 tu, kusingekuwa na tatizo la umeme mwaka 2011. Kwani mitambo ya umeme inahitajia karne nzima kutengenezwa? Asitubabaishe hapa!!!!!!!!!!!! Afrika Kusini walikuwa na tatizo la ghafla na wakalimaliza chini ya miezi miwili.
Halafu ufisadi wa mitambo ya Dowan, kama hiyo isingekuwa DEAL si angalau ingepunguza shida hizi?
Chad wameweza kutia taa za barabarani zinazotumia nguvu za jua katika mji mzima wa Abeche, na nusu ya mji wa Ndjamena kwa chini ya miezi sita! Sasa huu muda anaozungumza adhania watu wajinga? Ubaya wa Kikwete ni kuwa haoni haya kusema uongo. Badala ya kukiri uzembe na makosa aona afadhali aongopee. haoni kuwa tabia ya uongo ni tabia za kihuni za barabarani na kwamba unapokuwa kiongozi inabidi uepuke tabia hizo, au bado adhania yeye ni check bob?
 
Nasema hivi, ahadi zimekuwa nyingi na sisi tuko gizani. Hatutaki visingizio, miaka yote hiyo mmetawala ninyi CCM sasa leo unawaletea lawama wenzio as if you were not part of the system.
 
Hakuna kauli ya rais mkwele inayoniudhi na kunichefua siku nzima inayosema "serikali haina uwezo wa kufanya mvua inyeshe". Kwa maoni yangu binafsi kauli hiyo ndiyo inayopambanua waziwazi uwezo mdogo wa kikwete. Siju kama kuna chizi anayeweza kutamka maneno ya ajabu kama hayo.
 
Sasa unaposema jumla ya miaka 80 unahesabu kitu gani? maanake nashindwa kukuelewa kwani hatujawa na Uhuru kwa miaka hiyo na hata ukizungumzia ukoloni inahusu vipi na uongozi wa JK?.

Na maajabu unakubali miaka ya 80 ambayo hatukuwa na chakula sijui kaya moja kilo moja kwa wiki lakini haya ya kukosa Umeme huyaoni tena una utetezi mkubwa wakati shida ni kubwa kuliko miaka 80 iliypita!. Wapi zamani mkuu...maanake mimi nakubali shida za miaka ya 80 lakini wewe unatetea ongezeko la umeme kwa miaka 80 wakati wananchi wanalia shida kuliko hata zile za miaka ya 80's au miaka 80 iliyopita. Kama hujichanganyi kitu gani mkuu wangu...

najua kweli JK ameweka mkataba na Warussi kujenga hydropower ya Mw 700 huko Iringa, lakini hii pia sio ujanja ikiwa yeye mwenyewe anakiri kwamba mvua hazileti yeye, na kwa nini asiende na geothermal au upepo? tukisema sisi mnasema tunamchukia JK. I mean mkuu wangu JK ktk utetezi wake hata angesema swala la ukosefu wa umeme tunalifanyia uchunguzi na zipo sababu akataja matatizo ya IPTL, Songos na kuwajaza ujinga wao kuliko kusingizia mvua kisha anakuwa mkali kwa ujinga na aibu alotuachia na zaidi ya yote JK anazidi kuweka mikataba ya ujenzi wa Dams kuzalisha umeme akitegemea mvua za Mungu...
Tena basi nasiki na Brazil nao wanapewa mradi wa 2bn kujenga nini - dam..

Naona hujasoma vizuri post yangu, lakini nilifundishwa kuwa "Mwalim bora huwa hachoki kuelekeza" soma:

Miaka 40 ya Muingereza jumlisha miaka 20 ya Nyerere jumlisha miaka 10 ya Mwinyi jumlisha miaka 10 ya mkapa: awamu hizo zote zina jumla ya miaka 80. Jee, umefaham?

Na katika hiyo miaka 80 Kikwete kakuta jumla ya megawati 600 za umeme toka tulizorithi kwa mkoloni mpaka yeye anachukuwa nchi. Jee, umeelewa?

Sasa yeye Kikwete kwa muda wake mfupi, Kisha leta megawati 200 tayari, Kisha saini mikataba tofauti ya megawati zaidi ya 500 tayari. Kwa hiyo, Kikwete kawekeza kwenye umeme zaidi ya awamu zoooooote zilizowekeza kwenye umeme alioukuta. Umeelewa au hujaelewa?
 
personally nimemuelewa Mr. President sasa kama chadema wana alternatives hebu wauweke hapa tupime.
 
akijibu swali la omar mutasa wa bbc kuhusu kwanini hazitumiki njia mbadala wa kuzalisha umeme badala ya kutegemea maji ?
Kikwete alisema" umeme wa jua au mvuke siyo kitu cha mwezi mmoja au miwili " ameshasaau kuwa umeme wa mgao umeanza una zaidi
ya miaka 15. amefunika ufafanuzi wa swali la mtangazaji kwa kushindwa kufafanua juhudi za serikali ya ccm kuhusu njia mbadala za kuzalisha
umeme kwa zaidi ya miaka 10 iliyopita.majibu yake kwa BBC yamedhiirisha kuwa serikali haina comprehensive plan ya kutatua tatizo la umeme.
 
Rais wetu anajigamba na anafanya kosa kubwa sana kujisifia alichokifanya tofauti na wenzake waliomtangulia. Ni dalili ya kutokujiamini na kujitilia mashaka uwezo wake na inaelekea kana kwamba anataka apewe tukuzo na sifa wakati bado yupo madarakani kwa kazi ambayo matunda yake hayaonekani.

Nikirudi kwenye hizi megawati zake 300, sehemu kubwa ni kuwa tumejenga viwanda vya kufua umeme, lakini mitambo ya kuzalisha umeme si yetu. Pale Ubungo panapozalishwa mw 104, kuna IPTL (sina uhakika kama wanachangia sehemu), Symbion na sasa Jacobsen ambao mradi wao wa Dola milioni 125 za Kimarekani, sisi tumetoa asilimia 15 (15%) tuu kwa mradi mzima, na sehemu iliyobakia ni mikopo na ni Jacobsen na si Tanesco ndio inawezekana wakawa wamiliki wa mitambo.

Kuna hili jambo la umeme wa thermal na hiki kipande ni very interesting ukizingatia kuwa ni habari ya miaka miwili iliyopita na Tanesco hawajabadilisha walichoandika kwenye webusaiti yao. KIpande hiki, kinaonyesha mapungufu kwa vituo vinavyozalisha umeme kwa kutumia mafuta, na hovyo tukirudi kwemye majibu ya kudai mvuoa ndio chanzo, je hizi megawati nyingine zisizozalishwa kutokana na uchakavu wa mitambo ni nani alaumiwe?

Thermal Power Plant
TANESCO has been implementing power generation mix program, whereby a substantial amount of generation comes from thermal generation through own generation and independent power plants (IPPs). Own thermal generation comes from the Ubungo 100 MW gas-fired plant in Dar es Salaam. Another 45MW gas-fired power plant located at Tegeta in Dar es Salaam is expected to enter the grid system in September 2009.

There are also several diesel generating stations connected to the national grid in Dar es Salaam, Mwanza, Tabora, Dodoma, Musoma and Mbeya. These have installed capacity of 80 MW but the only operational grid diesel based station is Dodoma which contributes about 5 MW and the rest are due for disposal due to obsolescence and high maintenance costs. However a short term plan is being implemented to replace the retired capacity by a 60MW plant at Nyakato, Mwanza by 2011. The other regions, districts and townships namely, Kigoma, Mafia, Mpanda, Tunduru, Songea, Liwale, Ikwiriri, Masasi, Mbinga, Ludewa, Ngara, Bihalamulo, and Kilwa Masoko are dependent on isolated diesel – based generators with a total installed capacity of 31 MW. Mtwara and Lindi are supplied by M/S Artumas Group Ltd, an IPP based in Mtwara. The total capacity of Artumas power plant is 8MW using gas from Mnazi Bay gas wells in Mtwara.


Ama jedwali hili

New 100 MW Gas Based Power Plant at Ubungo, Dar es Salaam – New
Government of United Republic of Tanzania (GoT)
Ubungo, Ilala District - Dar es Salaam
To generate power using natural gas to increase generation capacity in the grid network, will be connected to the National Grid Control Center (GCC) at Ubungo, Dar es Salaam.
2011​
3
New 60 MW Heavy Fuel Oil Based (HFO) Power Plant at Nyakato, Mwanza – New
Government of United Republic of Tanzania (GoT)
Nyakato, Mwanza region
To generate 60 MW power using Heavy Fuel Oil (HFO) to increase generation capacity for in the grid network. This will also serve as base load in northern regions for load supply in the mining areas, will be connected to the National Grid Control at Nyakato substation, Mwanza.

na hili

1
Ubungo Gas Plant – 102.5 MW
Government of United Republic of Tanzania
Ubungo, Ilala district - Dar es Salaam
To generate power using natural gas to meet the growing power demands in Tanzania, Connected to the National Grid through Grid Control Center (GCC) Contributing to the National Grid System, injecting 102.5 MW
2007​
2
Tegeta 45MW Gas Based Power Plant
Government of United Republic of Tanzania (GoT) (50%)
and The Government of the Kingdom of the Netherlands under ORET/MILIEV program (50%)
Tegeta, Kinondoni District, Dar es Salaam
To generate power using natural gas to meet the growing power demands in Tanzania, Connected to the National Grid through Kunduchi substation, Contributing 42 MW of firm capacity.
2009​


na hii ambayo bado haijakamilika na iko chini ya wafadhili
Kiwira Coal to Electricity Project – Phase I-200MW, Phase II-200MW; Fuel from the Kabulo ridge Coal Reserves - New
Government of China
Financing Committed for Phase I of 200MW
Kyela, Rungwe and Mbeya Districts
The Mtwara – Mbamba Bay – Lake Tanganyika Development Corridor.
Kiwira Coal – to - Electricity power project involves expansion of the existing power facility, in Phase I & II up to 400MW, Construction of transmission line and the colliery redevelopment respectively, to meet the growing power demands in Tanzania, will contribute to the National Grid System, injecting 400 MW.

Phase I - 2011Phase II - 2014​

100MW Independent Power Tanzania Limited (IPTL) Power Plant - Conversion
World Bank - IDA
Tegeta, Kinondoni District, Dar es Salaam
To convert 100 MW IPTL plant from using expensive Heavy Fuel Oil (HFO) to using cheap natural gas.
2011​
10
Kinyerezi 240MW Gas Based Power Plant – New
African Development Bank (AfDB),
Tanzania Electric Supply Company Limited
Kinyerezi, Temeke District - Dar es Salaam
To generate power using natural gas to meet the growing power demands in Tanzania, will contribute to the National Grid System, injecting 240 MW.
2013​
11
Rumakali hydropower Plant - 222 MW (Expression of Interest - EoI)/ RFP
Word Bank
International Development Agency (IDA) Funds
Makete District, Iringa region
To generate power using Water (Hydro) to meet the growing power demands in Tanzania, will contribute to the National Grid System, injecting 222 MW.
2018​

So there goes mahesabu ya awamu yetu imefanya haya, in comparison to yaliyofanywa na awamu ya kwanza na ya pili.

TANESCO's generation system consists mainly of Hydro and Thermal based generation. Hydro contributes the largest share of TANESCO's power generation. The total generation from TANESCO own sources in 2008 was 2,985,275,264 kWh out of which 2,648,911,352 kWh (90%) was from Hydro Power Plants. Total country demand was 4,425,403,157 kWh, of which 33% was supplied by IPPs. The hydro-plants operated by TANESCO are all interconnected with the national grid system and their installed capacity for each station is as follows: Kidatu 204 MW; Kihansi 180 MW; Mtera 80 MW; Pangani 68 MW; Hale 21 MW; and Nyumba ya Mungu 8 MW totaling to 561 MW.
 
Tunataka umeme no more bla bla bla! Mnyika alipowaambia watangaze swala la umeme janga la kitaifa walimuona mpayukaji. Nadhani majibu wameyapata kwwenye bajeti na bado...Time will tell!!
 
Ukisoma vizuri between lines utagundua kuwa umeme anaofikiria Mh. rais ni umeme wa nguvu za maji tu.
 
kama unaelewa na kutafakari hii diologue utagundua hii issue imempanikisha,ata majibu yake yapaniki paniki,tulia kaa na wataalam tatua tatizo,kama mkuu wa kaya huwezi toa jibu eti hutengenezi mvua,so,ukame ukiendelea zaid miaka10 twafunga nchi!uongo
 
Back
Top Bottom