nderingosha
JF-Expert Member
- Mar 20, 2011
- 4,281
- 3,243
- Ndugu zangu sijui ni wangapi mnafatilia yanayojiri toka Davos kwa World Economic Forum (WEF)?
au tukishaambiwa na watu wa ikulu kuwa JK kaondoka basi
.hatuoji tena nini anafanya huko alikokwenda au nini kimejiri huko?...nashangaa sana hata vyombo vyetu vya habari (hasa hizi tv)vinakuwa shallow sana kufatilia hizi safari za JK na anachofanya anapokuwa huko nje
..tunabaki tu kehesabu tumeliwa kiasi gani na hizi safari zake
..
- Nimeanza hivi nikitaka kuleta moja ya hoja muhimu haswa kwenye discussions za next bunge session.Kama tunafatilia tutakuwa na taarifa kuwa hivi karibuni serikali ya JK waliandika barua IMF kuwataarifu juu ya mipango yao ya kupunguza bajeti ya serikali katika kukabiliana na athari za euro zone economic crisis.Katika andishi lao,serikali wamesema hatua za kupunguza bajeti zitaathiri miradi ya maendeleo jambo ambalo linapingwa vikali na wachumi ikizingatiwa kuwa jambo hili litaathiri ukuaji wa uchumi ambao tayari ni legelege Kinachoshauriwa kikiwa kupunguza matumizi ya serikali yasiyo na tija e.g posho etc.......
- Katika kile kinachoonekana kuwa ni majibu ya msingi kwa hoja hii kwa seriakali ya JK kutoka kwa wakubwa wa uchumi wa dunia Mkurugenzi wa IMF (Christine Lagarde), Rais wa bank ya dunia(Robert Zoellick)na Rais wa WTO(Pascal Lamy)wote kwa pamoja wamesema juhudi za serikali zozote za kupunguza matumizi lazima zilenge kukuza uchumi na kuongeza ajira na si kuupunguza :Nanukuu:-`The International Monetary Fund's managing director and top global finance officials are urging the world's political leaders to avoid budget cuts that would hinder economic growth. Christine Lagarde said in a statement that government spending cuts and other fiscal austerity measures should ``promote rather than reduce prospects for growth and employment.''Akamalizia kwa kusema kwamba haya ni matamshi yake na wenzake niliowataja hapo juu na wote kwa pamoja wakatia saini statement yao.Nanukuu:- World Bank President Robert Zoellick and Director-General Pascal Lamy of the World Trade Organization signed onto the statement.
- (Source:Christine Lagarde joins call for growth, economic reform - The Economic Times).
- Nadhani hili litakuwa jibu zuri la food for thought kwa kina mh.Zitto watakapokuwa wanajadili masuala ya kupunguzwa kwa bajeti ya serikali yatakapoletwa na serikali katika bunge session next week.Angalizo: serikali ipunguze matumizi yake kwenye issue kama hizi safari za JK zisizo na tija,magari ya serikali,mawizara yasiyo na kazi, mikoa na mawilaya feki etc etc ..na kamwe wasiguse bajeti ya maendeleo ambayo wala hatuyaoni .tunachoona ni safari,posho na mawizara yakilipa watu mishahara bure .
- Katika hali ya kusikitisha nimeshangaa kuona JK akiongea jambo la ajabu sana (uongo)kwenye plenary session ya Afrika pale Davos ..plenary ilihusisha waziri mkuu Raila, Zenawi,marais makini Chonde(Guinea)na Zuma(SA) .wenzake walijikita kwenye mikakati ya kukuza uchumi wa Africa kwa kujenga ushirikiano .yeye JK akawaambia eti kupambana na ufisadi ndio issue kubwa (as if yeye anafanya hivyo) cha kuuzunisha akamaliza kwa kusema kitu cha kwanza kwenye kupambana na ufisadi ni kuwa na uwazi(transparency) na eti yeye kwenye nchi yake(TZ) sasa wana publish mikataba ya madini (wanaweka wazi mikataba)kama new mining code!!! Nanukuu:- However tackling the problem of corruption was still a "major issue", said Tanzanian President Jakaya Kikwete."The first thing to fight against corruption is transparency," he said, adding that his country was now publishing all mining contracts as part of a new mining code. "The best guarantee for an investor is transparency."
Is this a joke jamani!!!! Hizi ndizo tija tunazopata watanzania kwa huyu rais wetu anaposafiri nje amazing eh!!