Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
Salaam Jenerali,
Kabla sijasema neno kuhusu mada nina angalizo kwenye kichwa cha habari cha mada iliyozaa mjadala ninaoanzisha, "Jenerali...umewaacha mashabiki wako njia panda. Kwa mtazamo wangu mtu anayeshabikia kitu ni kutokana na sababu fulani, na kwa bahati mbaya ni ngumu kubadili 'ushabiki'. Kwa mfano, ukiniuliza kwa nini mpaka leo nashangilia Liverpool FC sina jibu! Matatizo ninayoyapata kwa kufungwa na timu za ajabu, uchungu anaopata mtoto wangu mwenye umri wa miaka 10! kwa kuona Liverpool inafungwa si mdogo! Namhurumia kwa nini amekuwa mshabiki kwa sababu tu baba yake na yeye ni mshabiki wa timu inayofungwa!
Mbaya zaidi, sijawahi kufikiria 'kuhama' Liverpool na kushabikia timu inayoshinda ingawaje mtoto wangu wa kumzaa anataeseka nayo, mimi nateseka kwa kero za kusemwa na mashabiki wa Man U, Chelsea, Arsenal etc!! Cha kushangaza wachezaji wanahama, na wao ndio wanalipwa! Makocha wanahama, na hao ndio wanaolipwa! Wakichemsha wanafukuzwa!! Mashabiki hawalipwi, hawahami, hawafukuzwi!
Napata tatizo kuwafikiria mashabiki wa Jenerali Ulimwengu walio njia panda! Je ni kina nani? Wana hali gani? Furaha? Huzuni? hawalipwi, sina uhakika kama watahama, ila wanafukuzwa kama hoja zenyewe ndio hizi!! Huo ndio ushabiki! Sasa naomba tulitafakari neno ushabiki kwa muda wetu wa baadae ili tuone je ni lazima kumshabikia mtu?
Nikirudi kwenye barua ya Jenerali. Kuna wengine wanaiona nzuri. Labda wako wengi. Kuna wengine inachefua. Na wenyewe wako wengi. Mimi imenikera. Imenikera sana.
Imenikera sio tu kwa sababu ni ndefu na Raisi hataisoma, ni kwa sababu Jenerali analijua hilo lakini kwa makusudi ameamua kutupotosha. Sana sana labda Raisi atasomewa na kama watamsomea wataruka yale ambayo hawataki Raisi ayasikie (kama yapo)
Kwa kuangalia baadhi ya mistari naomba kuonyesha sababu za kero zangu kwa kutumia mistari ilimo kwenye barua hiyo ili kuepuka kukurupuka!! nitarudia maneno yalimo kenye barua hiyo (kwa rangi)
Pili, napenda kukupongeza kwa ushindi uliopata katika uchaguzi uliopita, ushindi uliodhirisha kwa mara nyingine tena jinsi ambavyo wewe kama mwanasiasa unakubalika machoni mwa Watanzania.
Umekuwa ushindi unaodhihirisha imani iliyojengeka katika nyoyo za Watanzania kwamba wewe, Jakaya, utawaongoza vyema ili waondokane na adha zilizowazingira, hususan ufukara uliokithiri na unaoendelea kujijenga kila siku miongoni mwao bila ya kuwapo kwa ishara kwamba viongozi wao wanajua au kujali hali zao.
Anachosema (na anachoamini) Ulimwengu ni kwamba;
i) Ushindi ni ishara ya kukubalika kwa JK.
iii) JK anakubalika machoni mwa watanzania.
Na anaendelea na imani yake;
i) Ushindi wa JK unadhihirisha imani
ii) Imani ya watanzania
iii) Imani kwamba JK ataongoza vyema
iv) Watanzania wana adha hususan ufukara
v) Ufukara umekithiri
vi) Ufukara unaendelea kujijenga kila siku
vii) Hakuna ishara kwamba viongozi wanajua au kujali hali hiyo.
Mosi, Jenerali, ni watanzania wapi unawaongelea? Unataka tuamaini kwamba binadamu wote ni sawa kwa hiyo watanzania wote wanamkubali JK? Au ni watanzania waliomchagua? Hivi unataka tuamini kwamba watanzania tunafanana sio tu mawazo pia hali zetu za maisha? Na waliokuwa wanamkubali Dr Slaa na Prof Lipumba ni wakenya?? Walikuwa wanasafirishwa kutoka sehemu nyingine kuhudhuria mikutano ya Dr na Prof? na waliopiga kura kwa Dr na Prof wameonyesha ishara gani? Kumkubali JK?
Hii ndio hoja yako?
Sawa, hayo ni mawazo yako Jenerali na haki yako ya Kikatiba kuwaza. Lakini,
Unakubali kwamba watanzania wana adha ya ufukara (ingawaje hoja yako inatujumuisha wewe na mimi (watanzania) eti tuna adha ya ufukara!! Huoni tatizo hapo??). Tuendelee, umesema 'ufukara huo unaendelea kujijenga kila siku'. Kwa hiyo unakubali na kulitambua hilo. Sasa Jenerali, ina maana unakubali ufukara umeendelea kujijenga kila siku ikiwa ni pamoja na 2005 mpaka leo!! JK bado hajaingia madarakani? Hiyo imani ya watanzania imejengeka lini? 2005 au 2010? Nadhani, kwa maneno yako, ni 2010 na watanzania tumeonyesha ishara kwa kumpa ushindi!!
Ni sababu ipi imekufanya usidiriki kusema moja kwa moja kwa 'mkombozi' haoni ufukara unakua na ni yeye kama kiongozi haonyeshi ishara ya kujali? Au unaongea kwa mafumbo? Kama ulikuwa unamfumba, ili nini?
Unaendelea,
hamasa na mapenzi waliyoonyesha Watanzania kwako tena ni kielelezo kwamba wanayo imani kuwa bado unaweza kuwa mkombozi wao
Jenerali, unataka tuamini kwamba hamasa na mapenzi yanayoonyeshwa kwenye kampeni za uchaguzi ni kielelezo cha imani? Kwa hiyo wanaopewa fedha, ahadi za kufaidi baada ya uchaguzi, nafasi za kuteuliwa kama ahsante, kofia, kanga, sabuni, sukari etc wanasukumwa na imani ya kutaka mkombozi!! Huyo ni wewe kweli au kivuli chako?
Kwa nini wanaamini hivyo, mimi sijui, lakini ukweli ni kwamba hivyo ndivyo wanavyoamini.
Huu ukweli umeupata wapi Jenerali? Umewahi kuniuliza kama naamini hivyo? Unafikiri Sitta anaamini hivyo? Mama Kilango anaamini hivyo? Ni nani anaamini hivyo? Unadai ni watanzania!! Umeongea nao?? Ishara zako unatoa wapi? Kwa kuangalia hamasa na mapenzi wakati wa kampeni za uchaguzi!!?
Jenerali unataka mtu ambaye ni Raisi wa nchi aamini hivyo? Hiyo ndiyo unaita kweli?? Na umeweka wazi tusome ili tujue unachomwambia Raisi! Akikusikiliza sitashangaa ila nitamuachia Mungu.
Ni kwa nini umerudia hiyo barua? Huku ukijua kabisa umeirudia, umeandika kama vile JK ameingia madarakani kwa mara ya kwanza. Hivi kabla ya kuwa Raisi JK alikuwa si kiongozi? Hakuwa waziri? Wakati nchi ilipozama JK alikuwa wapi? Unasema amerithi mzigo, maneno hayo yanatoka moyoni mwako??
Hoja yangu Jenerali
a) JK alikuwa kiongozi kabla ya mwaka 2005. Alikuwa ni waziri. Na kama ulivyosema alianza kusafiri nje ya nchi toka mwaka 1974 mlivyokutana Bulgaria na bado anasafiri!!! Nchi imeanza kuzama lini? Tuambie!!
b) Ufukara haujaanza leo wala jana. Ulipoanzia JK alikuwepo kama kiongozi mwenye nafasi ya kuupunguza hata kama hakuwa Raisi au alikuwa ni mmoja wa waliosabanisha ufukara huo na alikuwa anaona nchi ikizama. Akaacha izame leo hii anataka kuitoa ilipozama!! Kama ni kwenye maji hata akiitoa si itakuwa na kutu na injini haifanyi kazi? Ni sawa na kwenda kuitoa MV Bukoba ziwani sasa hivi wakati uliicha ikzame! Kwa nini hakuzuia isizame? Huoni kwamba angekuwa ni shujaa badala ya mkombozi? Tunataka shujaa na siyo mkombozi!! Usinikwaze na kunisabisha nikatenda dhambi! angeanza na ushujaa ndio atukomboe
c) Chama kilichomlea JK na watangulizi wake ni kile kile kinacholaumiwa kusababisha ufukara huo! Na umekubali unajijenga kila siku (hata ile miaka ambayo JK amekuwa Raisi. Labda kwako miaka 5 sio mingi, lakini kwa mtu asiye na ada ya mtoto, asiye na uhakika wa mlo, asiye na nyumba bora, asiye na uwezo wa kuvaa mavazi mazuri, asiyejua mimi na wewe tunaongea nini hapa kwa sababu hajui kusoma, hana internet au computer, umeme nk. Miaka mitano no mingi sana! Sana! Unawazungumzia imani yao na unaifikisha kwa Raisi yule yule aliyekuwepo miaka 5 iliyopita! Utasema ni kukumbushana??
Unamkumbusha jina lake au nini? Hivi naweza kukumbusha wewe unaitwa Jenerali Ulimwengu?? Miaka yote umeitwa hivyo iweje umesahau jina lako? Ina maana JK anaweza kusahau shida za watanzania au majukumu ya kiongozi wa nchi umeamua kumkubusha??
d) Imani ya kwamba JK ni mkombozi ni potofu. Umeileta wewe. Huna mamlaka yoyote ya kuwazungumzia watanzania. Huwezi ukawaongelea watanzania kwa upotoshaji mkubwa kama huo. Huo ni ushabiki! Na nimesema kuhusu tatizo la ushabiki. Unajua wazi kabisa JK amekuwepo siku zote kama kiongozi katika nchi hii. Serikali zote mbili zilizopita alikuwepo. Alifanya nini? Labda umkumbushe hayo mazuri aliyoyafanya na utukumbushe na sisi!
e) Kwa nini usimkumbushe Raisi mazuri au mabaya aliyoyafanya badala ya kutuletea porojo na kutusababishia hasira na kututendesha dhambi?? Kama kweli unaweza kusimamia ukweli ungemwambia Raisi haya yafuatayo;
i) Miaka 5 ya uongozi wake ameshindwa kutekeleza majukumu yake kama ilivyotarajiwa kama Raisi.
ii) Kwa miaka 5 ameendelea kutokujali ufukara ambao umeendelea kujengeka. Hii hoja ungeiweka wazi bila kumumunya maneno na kuficha ficha!
iii) Baraza la mawaziri lililopita lilikuwa hovyo na halikumsaidia katika utendaji.
Kwa sasa inatosha kusema kwamba mawaziri utakaowateua, na watendaji wengine wengi unaoruhusiwa kuwateua, hao ndio watakaounda timu yako. Hawa wote ni wachezaji; wewe ndiye kocha au meneja. Timu ikicheza vibaya, ikafungwa wewe ndiye wa kulaumiwa. Ikicheza vizuri ikashinda, wewe ndiye wa kusifiwa.
Hukuwa na sababu ya kuongelea mawaziri wapya kabla hujasema tatizo la waliopita ambao wengine atawarudisha!! Kwa nini unaongelea timu ikicheza wakati imeshacheza?? Si utumie mfano uliopo badala ya abstracts!! alishateua mawaziri kabla kuwa mkweli na useme walifanya vizuri au vibaya! Mwambie asikie!
iv) Kujuana kulikuwa kwingi katika nafasi zote za utendaji. Watu wengine waliteuliwa ili kuondoa mipasuko na kuvunja makundi. Siasa!! Hao wamemponza sana.
v) Amezungukwa na watu kama wewe. Kusema ukweli wanaanza na maneno mengi ya kupaka mafuta, wanazunguka weeee, wanaremba remba maneno na kumuaminisha kwamba tatizo si yeye ila ni wengine!! Hawamwambii ukweli kama ulivyo kwa kuogopa kwamba Raisi atajisikia vibaya!
Ni vyema ukasema ukweli na ukausimamia kama ulivyo. Maneno yako;
Lakini ninaamini kwamba unanijua vyema na unaelewa kwamba kujadili masuala kama haya ni sehemu ya jinsi nilivyo. Iwapo kati ya mambo nitakayoyasema katika waraka huu yatakuudhi, natanguliza kuomba radhi; na iwapo yatakuchosha, naomba uyatupilie mbali.
Sio tu tuishie kwenye kujadili, ni lazima tuishi tunayoyazungumza!! Sioni ni kwanini Raisi ataudhika na uliyoyasema. Hakuna jipya, ingekuwa hivyo angeudhika kila siku akiangalia maisha ya wananchi wengi fukara na masikini! ndio hali halisi.
Angeudhika kwa kuangalia picha za maelfu ya wananchi waliokuwa wakihudhuria mikutano ya Dr na Prof huku wakitoa hisia zao! Angeudhika kwa kuangalia wabunge wa CCM walioangushwa kwa aibu au waliozomewa na wananchi mbele yake.
Angeudhika na upuuzi unaofanywa na baadhi ya maofisa wa juu wenye kutegemewa katika taifa ambao wanakurupuka wanatoa taarifa za kupotosha bila kufikiria athari zake. Kwa mfano Jeshi wakati wa uchaguzi, PCCB wakati wa kumsafisha Chenge hayo ni maudhi!! Lakini sijaona kama yamemuudhi Raisi wetu ndio maana unaona mpaka sasa wanaendelea na maisha yeye unamshauri aendelee kutabasamu na asikunje sura!! Mungu anatuona!!
Angalizo: kumuachia Mungu ni kwa sababu sijaona mtu mwingine wa kumuachia! Yeye pekee ndie tegemeo letu kwa hapa tulipofika, samahani, tulipofikishwa!!!
Wasalaam.
Kabla sijasema neno kuhusu mada nina angalizo kwenye kichwa cha habari cha mada iliyozaa mjadala ninaoanzisha, "Jenerali...umewaacha mashabiki wako njia panda. Kwa mtazamo wangu mtu anayeshabikia kitu ni kutokana na sababu fulani, na kwa bahati mbaya ni ngumu kubadili 'ushabiki'. Kwa mfano, ukiniuliza kwa nini mpaka leo nashangilia Liverpool FC sina jibu! Matatizo ninayoyapata kwa kufungwa na timu za ajabu, uchungu anaopata mtoto wangu mwenye umri wa miaka 10! kwa kuona Liverpool inafungwa si mdogo! Namhurumia kwa nini amekuwa mshabiki kwa sababu tu baba yake na yeye ni mshabiki wa timu inayofungwa!
Mbaya zaidi, sijawahi kufikiria 'kuhama' Liverpool na kushabikia timu inayoshinda ingawaje mtoto wangu wa kumzaa anataeseka nayo, mimi nateseka kwa kero za kusemwa na mashabiki wa Man U, Chelsea, Arsenal etc!! Cha kushangaza wachezaji wanahama, na wao ndio wanalipwa! Makocha wanahama, na hao ndio wanaolipwa! Wakichemsha wanafukuzwa!! Mashabiki hawalipwi, hawahami, hawafukuzwi!
Napata tatizo kuwafikiria mashabiki wa Jenerali Ulimwengu walio njia panda! Je ni kina nani? Wana hali gani? Furaha? Huzuni? hawalipwi, sina uhakika kama watahama, ila wanafukuzwa kama hoja zenyewe ndio hizi!! Huo ndio ushabiki! Sasa naomba tulitafakari neno ushabiki kwa muda wetu wa baadae ili tuone je ni lazima kumshabikia mtu?
Nikirudi kwenye barua ya Jenerali. Kuna wengine wanaiona nzuri. Labda wako wengi. Kuna wengine inachefua. Na wenyewe wako wengi. Mimi imenikera. Imenikera sana.
Imenikera sio tu kwa sababu ni ndefu na Raisi hataisoma, ni kwa sababu Jenerali analijua hilo lakini kwa makusudi ameamua kutupotosha. Sana sana labda Raisi atasomewa na kama watamsomea wataruka yale ambayo hawataki Raisi ayasikie (kama yapo)
Kwa kuangalia baadhi ya mistari naomba kuonyesha sababu za kero zangu kwa kutumia mistari ilimo kwenye barua hiyo ili kuepuka kukurupuka!! nitarudia maneno yalimo kenye barua hiyo (kwa rangi)
Pili, napenda kukupongeza kwa ushindi uliopata katika uchaguzi uliopita, ushindi uliodhirisha kwa mara nyingine tena jinsi ambavyo wewe kama mwanasiasa unakubalika machoni mwa Watanzania.
Umekuwa ushindi unaodhihirisha imani iliyojengeka katika nyoyo za Watanzania kwamba wewe, Jakaya, utawaongoza vyema ili waondokane na adha zilizowazingira, hususan ufukara uliokithiri na unaoendelea kujijenga kila siku miongoni mwao bila ya kuwapo kwa ishara kwamba viongozi wao wanajua au kujali hali zao.
Anachosema (na anachoamini) Ulimwengu ni kwamba;
i) Ushindi ni ishara ya kukubalika kwa JK.
iii) JK anakubalika machoni mwa watanzania.
Na anaendelea na imani yake;
i) Ushindi wa JK unadhihirisha imani
ii) Imani ya watanzania
iii) Imani kwamba JK ataongoza vyema
iv) Watanzania wana adha hususan ufukara
v) Ufukara umekithiri
vi) Ufukara unaendelea kujijenga kila siku
vii) Hakuna ishara kwamba viongozi wanajua au kujali hali hiyo.
Mosi, Jenerali, ni watanzania wapi unawaongelea? Unataka tuamaini kwamba binadamu wote ni sawa kwa hiyo watanzania wote wanamkubali JK? Au ni watanzania waliomchagua? Hivi unataka tuamini kwamba watanzania tunafanana sio tu mawazo pia hali zetu za maisha? Na waliokuwa wanamkubali Dr Slaa na Prof Lipumba ni wakenya?? Walikuwa wanasafirishwa kutoka sehemu nyingine kuhudhuria mikutano ya Dr na Prof? na waliopiga kura kwa Dr na Prof wameonyesha ishara gani? Kumkubali JK?
Hii ndio hoja yako?
Sawa, hayo ni mawazo yako Jenerali na haki yako ya Kikatiba kuwaza. Lakini,
Unakubali kwamba watanzania wana adha ya ufukara (ingawaje hoja yako inatujumuisha wewe na mimi (watanzania) eti tuna adha ya ufukara!! Huoni tatizo hapo??). Tuendelee, umesema 'ufukara huo unaendelea kujijenga kila siku'. Kwa hiyo unakubali na kulitambua hilo. Sasa Jenerali, ina maana unakubali ufukara umeendelea kujijenga kila siku ikiwa ni pamoja na 2005 mpaka leo!! JK bado hajaingia madarakani? Hiyo imani ya watanzania imejengeka lini? 2005 au 2010? Nadhani, kwa maneno yako, ni 2010 na watanzania tumeonyesha ishara kwa kumpa ushindi!!
Ni sababu ipi imekufanya usidiriki kusema moja kwa moja kwa 'mkombozi' haoni ufukara unakua na ni yeye kama kiongozi haonyeshi ishara ya kujali? Au unaongea kwa mafumbo? Kama ulikuwa unamfumba, ili nini?
Unaendelea,
hamasa na mapenzi waliyoonyesha Watanzania kwako tena ni kielelezo kwamba wanayo imani kuwa bado unaweza kuwa mkombozi wao
Jenerali, unataka tuamini kwamba hamasa na mapenzi yanayoonyeshwa kwenye kampeni za uchaguzi ni kielelezo cha imani? Kwa hiyo wanaopewa fedha, ahadi za kufaidi baada ya uchaguzi, nafasi za kuteuliwa kama ahsante, kofia, kanga, sabuni, sukari etc wanasukumwa na imani ya kutaka mkombozi!! Huyo ni wewe kweli au kivuli chako?
Kwa nini wanaamini hivyo, mimi sijui, lakini ukweli ni kwamba hivyo ndivyo wanavyoamini.
Huu ukweli umeupata wapi Jenerali? Umewahi kuniuliza kama naamini hivyo? Unafikiri Sitta anaamini hivyo? Mama Kilango anaamini hivyo? Ni nani anaamini hivyo? Unadai ni watanzania!! Umeongea nao?? Ishara zako unatoa wapi? Kwa kuangalia hamasa na mapenzi wakati wa kampeni za uchaguzi!!?
Jenerali unataka mtu ambaye ni Raisi wa nchi aamini hivyo? Hiyo ndiyo unaita kweli?? Na umeweka wazi tusome ili tujue unachomwambia Raisi! Akikusikiliza sitashangaa ila nitamuachia Mungu.
Ni kwa nini umerudia hiyo barua? Huku ukijua kabisa umeirudia, umeandika kama vile JK ameingia madarakani kwa mara ya kwanza. Hivi kabla ya kuwa Raisi JK alikuwa si kiongozi? Hakuwa waziri? Wakati nchi ilipozama JK alikuwa wapi? Unasema amerithi mzigo, maneno hayo yanatoka moyoni mwako??
Hoja yangu Jenerali
a) JK alikuwa kiongozi kabla ya mwaka 2005. Alikuwa ni waziri. Na kama ulivyosema alianza kusafiri nje ya nchi toka mwaka 1974 mlivyokutana Bulgaria na bado anasafiri!!! Nchi imeanza kuzama lini? Tuambie!!
b) Ufukara haujaanza leo wala jana. Ulipoanzia JK alikuwepo kama kiongozi mwenye nafasi ya kuupunguza hata kama hakuwa Raisi au alikuwa ni mmoja wa waliosabanisha ufukara huo na alikuwa anaona nchi ikizama. Akaacha izame leo hii anataka kuitoa ilipozama!! Kama ni kwenye maji hata akiitoa si itakuwa na kutu na injini haifanyi kazi? Ni sawa na kwenda kuitoa MV Bukoba ziwani sasa hivi wakati uliicha ikzame! Kwa nini hakuzuia isizame? Huoni kwamba angekuwa ni shujaa badala ya mkombozi? Tunataka shujaa na siyo mkombozi!! Usinikwaze na kunisabisha nikatenda dhambi! angeanza na ushujaa ndio atukomboe
c) Chama kilichomlea JK na watangulizi wake ni kile kile kinacholaumiwa kusababisha ufukara huo! Na umekubali unajijenga kila siku (hata ile miaka ambayo JK amekuwa Raisi. Labda kwako miaka 5 sio mingi, lakini kwa mtu asiye na ada ya mtoto, asiye na uhakika wa mlo, asiye na nyumba bora, asiye na uwezo wa kuvaa mavazi mazuri, asiyejua mimi na wewe tunaongea nini hapa kwa sababu hajui kusoma, hana internet au computer, umeme nk. Miaka mitano no mingi sana! Sana! Unawazungumzia imani yao na unaifikisha kwa Raisi yule yule aliyekuwepo miaka 5 iliyopita! Utasema ni kukumbushana??
Unamkumbusha jina lake au nini? Hivi naweza kukumbusha wewe unaitwa Jenerali Ulimwengu?? Miaka yote umeitwa hivyo iweje umesahau jina lako? Ina maana JK anaweza kusahau shida za watanzania au majukumu ya kiongozi wa nchi umeamua kumkubusha??
d) Imani ya kwamba JK ni mkombozi ni potofu. Umeileta wewe. Huna mamlaka yoyote ya kuwazungumzia watanzania. Huwezi ukawaongelea watanzania kwa upotoshaji mkubwa kama huo. Huo ni ushabiki! Na nimesema kuhusu tatizo la ushabiki. Unajua wazi kabisa JK amekuwepo siku zote kama kiongozi katika nchi hii. Serikali zote mbili zilizopita alikuwepo. Alifanya nini? Labda umkumbushe hayo mazuri aliyoyafanya na utukumbushe na sisi!
e) Kwa nini usimkumbushe Raisi mazuri au mabaya aliyoyafanya badala ya kutuletea porojo na kutusababishia hasira na kututendesha dhambi?? Kama kweli unaweza kusimamia ukweli ungemwambia Raisi haya yafuatayo;
i) Miaka 5 ya uongozi wake ameshindwa kutekeleza majukumu yake kama ilivyotarajiwa kama Raisi.
ii) Kwa miaka 5 ameendelea kutokujali ufukara ambao umeendelea kujengeka. Hii hoja ungeiweka wazi bila kumumunya maneno na kuficha ficha!
iii) Baraza la mawaziri lililopita lilikuwa hovyo na halikumsaidia katika utendaji.
Kwa sasa inatosha kusema kwamba mawaziri utakaowateua, na watendaji wengine wengi unaoruhusiwa kuwateua, hao ndio watakaounda timu yako. Hawa wote ni wachezaji; wewe ndiye kocha au meneja. Timu ikicheza vibaya, ikafungwa wewe ndiye wa kulaumiwa. Ikicheza vizuri ikashinda, wewe ndiye wa kusifiwa.
Hukuwa na sababu ya kuongelea mawaziri wapya kabla hujasema tatizo la waliopita ambao wengine atawarudisha!! Kwa nini unaongelea timu ikicheza wakati imeshacheza?? Si utumie mfano uliopo badala ya abstracts!! alishateua mawaziri kabla kuwa mkweli na useme walifanya vizuri au vibaya! Mwambie asikie!
iv) Kujuana kulikuwa kwingi katika nafasi zote za utendaji. Watu wengine waliteuliwa ili kuondoa mipasuko na kuvunja makundi. Siasa!! Hao wamemponza sana.
v) Amezungukwa na watu kama wewe. Kusema ukweli wanaanza na maneno mengi ya kupaka mafuta, wanazunguka weeee, wanaremba remba maneno na kumuaminisha kwamba tatizo si yeye ila ni wengine!! Hawamwambii ukweli kama ulivyo kwa kuogopa kwamba Raisi atajisikia vibaya!
Ni vyema ukasema ukweli na ukausimamia kama ulivyo. Maneno yako;
Lakini ninaamini kwamba unanijua vyema na unaelewa kwamba kujadili masuala kama haya ni sehemu ya jinsi nilivyo. Iwapo kati ya mambo nitakayoyasema katika waraka huu yatakuudhi, natanguliza kuomba radhi; na iwapo yatakuchosha, naomba uyatupilie mbali.
Sio tu tuishie kwenye kujadili, ni lazima tuishi tunayoyazungumza!! Sioni ni kwanini Raisi ataudhika na uliyoyasema. Hakuna jipya, ingekuwa hivyo angeudhika kila siku akiangalia maisha ya wananchi wengi fukara na masikini! ndio hali halisi.
Angeudhika kwa kuangalia picha za maelfu ya wananchi waliokuwa wakihudhuria mikutano ya Dr na Prof huku wakitoa hisia zao! Angeudhika kwa kuangalia wabunge wa CCM walioangushwa kwa aibu au waliozomewa na wananchi mbele yake.
Angeudhika na upuuzi unaofanywa na baadhi ya maofisa wa juu wenye kutegemewa katika taifa ambao wanakurupuka wanatoa taarifa za kupotosha bila kufikiria athari zake. Kwa mfano Jeshi wakati wa uchaguzi, PCCB wakati wa kumsafisha Chenge hayo ni maudhi!! Lakini sijaona kama yamemuudhi Raisi wetu ndio maana unaona mpaka sasa wanaendelea na maisha yeye unamshauri aendelee kutabasamu na asikunje sura!! Mungu anatuona!!
Angalizo: kumuachia Mungu ni kwa sababu sijaona mtu mwingine wa kumuachia! Yeye pekee ndie tegemeo letu kwa hapa tulipofika, samahani, tulipofikishwa!!!
Wasalaam.