Maji yatakayojazwa Bwawa la Nyerere (JNHPP) yanaweza kuzalisha Umeme kwa mwaka mmoja bila kutegemea mvua

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,323
7,963
samia-pic.jpg
Akizungumza na waandishi wa habari kutoka eneo la mradi huo uliopo katika bonde la mto Rufiji, Waziri wa Nishati, January Makamba amesema mpaka sasa ujenzi wa bwawa hilo umefikia asilimia 78.68 ambayo ni hatua ya awali ya kuanza kujaza maji na inategemewa kuchukua misimu miwili ya mvua iliyo kamili.

"Wakati mradi unaanza kutekelezwa ili kujengwa handaki katikati ya mto ni lazima maji yachepushwe kwa njia nyingine ili yaendelee mbele yakupe nafasi ya sehemu kavu kujenga handaki hili lenye urefu wa mita 700 lenye gharama ya Tsh. Bilioni 235," alisema Makamba.

Ameongeza kuwa mageti ya kuziba mchepusho wa maji ya kujaza maji yamewasili na tayari yameshafungwa na ni miongoni mwa hatua tatu muhimu zilizofanyika katika utekelezaji wa mradi huo hivyo anaona fahari kuutangazia umma hatua hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme (TANESCO), Maharage Chande, amesema kuwa bwawa hilo linauwezo wa kuhifadhi lita bilioni 33.2 za maji na kama zikitumika na mitambo yote itaweza kuendesha mitambo kwa kipindi cha mwaka mmoja.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom