Maji ya bahari ya Hindi yaibukia Mjimkongwe Zanzibar na soko kuu la Darajani

Zurie

JF-Expert Member
Jul 6, 2014
1,743
4,272
itvdarajani.jpg


Katika hali isiyo ya kawaida na ya kuhatarisha jamii maji ya bahari ya Hindi yameibukia katika mitaro ya Mjimkongwe na eneo la soko kuu la Zanzibar na kuonekana kuwashangaza wananchi na kukumbwa na hofu.

ITV ilishuhdia maji hayo ya baharini yakiibukia katika mitaro ya soko kuu la Zanzibar liliko darajani na pia katika baadhi ya mitaa ya Mjimkongwe huku wananchi wakiendelea na shuguli zao kama kawaida ikiwemo biashara katika soko hilo, aidha baadhi ya mitaa ya Mjimkongwe yakionekana kujaa na kuzagaa maji hayo na usafiri wa abiria ukiendelea kama kawaida.

Wakizungumza na ITV baadhi ya wananchi na wafanyabiashara katika eneo hilo la darajani wameonekana kushangazwa na kuhofia hali ya hatari endapo maji hayo ya baharini yakizidi kasi na kiwango chake kuongezeka na kushauri serikali iliangalie suala hilo kwa maksudi na kuepukana na magonjwa.

Hata hivyo afisa uhuisano wa manispaa ya Zanzibar Mohamed Nassor Ali amesema hali hiyo ni ya kawaida na sio ya kutisha au hatari yeyote kwa wakazi wa maeneo hayo na maji hayo hujaa na kuizidi kiwango kwa muda mfupi tu.

Pamoja na kuwepo kwa uhakika wa manispaa, bado wakazi wengi wa Zanzibar wanaendelea kuwa na hofu ya maisha yao mbali ya kuona iko siku huenda samaki aina ya papa ataibukia hapo na maji hayo ya bahari yakazidi kasi na kubomoa mindombinu na kusababisha maisha ya watu kupotea.


Chanzo: itv
 
Ndio wajue muungano ni muhimu kwao, na kulinga na mabadiriko tabia nchi na hali ya joto duniania kuna hatari bahari kujaa na kuhatarisha visiwa
Tatizo ni bomba la kupitisha maji la huu mradi usiokamilika hapo uwanja wa mnazi mmoja(drainage project). Nyakati za high tide bomba lina rudisha maji uwanjani na kusababisha mafuriko hadi marikiti. Swali did project designers overlook the possibility of flow reversal during high tide?
 
Pamoja na hayo bado sisi ni ndugu majanga ya bara ni majanga ya zanziba na majanga ya zanzibar ni majanga ya bara tuachane na wanasiasa uchwara tuulinde muungano wetu sisi wote ni wamoja.
 
View attachment 347054 Maji ya bahari ya Hindi yaibukia Mjimkongwe Zanzibar na soko kuu la Darajani Chanzo: itv

Ni ya kawaida huko visiwani ila tuchukue tahadhari kama wasemavyo wasomi :-

The Economics of Climate Change inZanzibar http://www.economics-of-cc-in-zanzibar.org/images/Impacts_vulnerability_and_adaptation_vs_3.pdf

Kuna baadhi ya visiwa duniani vimeshapotea rasmi kama :-

Five Pacific islands lost to rising seas as climate change hits Five Pacific islands lost to rising seas as climate change hits

Sasa hawa wenzetu tumewatengea Bagamoyo, ila kama wabishi na hawataki muungano acha tuone..
 
  • Thanks
Reactions: bdo
Hao waandishi wa itv itakuwa ni mijitu ya bara na hawakuchukuwa fursa ya kuwauliza wenyeji kuhusu hali hiyo.

Hiyo ni hali ya kawaida sana Unguja wakati wa bamvua kubwa.

Kuna wakati barabara ya forodhani Unguja huwa haipitiki msimu wa bamvua kubwa.
Bamvua=mvua.
 
Tatizo ni bomba la kupitisha maji la huu mradi usiokamilika hapo uwanja wa mnazi mmoja(drainage project). Nyakati za high tide bomba lina rudisha maji uwanjani na kusababisha mafuriko hadi marikiti. Swali did project designers overlook the possibility of flow reversal during high tide?
Huyo project haina uhusiano na drainage system ya mji mkongwe. .....
 
Hao waandishi wa itv itakuwa ni mijitu ya bara na hawakuchukuwa fursa ya kuwauliza wenyeji kuhusu hali hiyo.

Hiyo ni hali ya kawaida sana Unguja wakati wa bamvua kubwa.

Kuna wakati barabara ya forodhani Unguja huwa haipitiki msimu wa bamvua kubwa.

Mvua
 
Bamvua ni hali ya kujaa na kupwa kwa maji ya baharini, hasa kujaa sana kuzidi usawa wa sakafu ya ardhi inayoungana na bahari. Mara nyingi neno hili hutumika na watu wa pwani na wavuvi wa pwani ya bahari ya Hindi. Kwa kawaida bamvua hutokea mara mbili kwa mwezi.

Bamvua inaonekana kutokana na hali ya mwezi kuwa ama mwezi mwandamo au mwezi mpevu na karibu na siku hizi bamvua inatokea.
Kutegemeana na tabia za pwani mara nyingi bamvua haionekani sana yaani maji hujaa sentimita chache juu ya uwiano wa kawaida. Lakini kwenye mlango wa bahari kwa mfano kati ya kisiwa na bara, au katika mdomo wa mto tofauti inaweza kuongezeka hasa ikiungana na upepo mkali wa kuelekea bara.
-Taarifa hii imepatikana kwa msaada wa Wikipedia
 
Hahaaaa... Kuna tofauti gani kati ya ba-mvua na ma-mvua kubwa.... Tudadavulie weee mswahili..

Au ndo matamvua ya samaki mkubwa;)
Hii post imenichekesha kweli, kwa jinsi ilivyojipinda. FaizaFoxy, twambie hiyo bamvua ni nini? Kama ni babake na mvua tujue. Huyo ndugu yako BAFA mwambie ajiangalie sana na hizo comment zake.

Nitashukuru ukinijuza maana ya bamvua.
 
Back
Top Bottom