manwest1
JF-Expert Member
- Apr 25, 2014
- 225
- 134
NI jambo la kusitisha sana hasa wakati kama huu ambao dunia nzima ipo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Covid- 19 mji kama Mtwara tena mjini maeneo mengi hayana maji kwa wiki mbili sasa.
Mkoa ambao umeonja shubiri kwa kuondokewa na mkuu wa wilaya haujabadilika kuhusu tahadhari ya kunawa mikono kila wakati. Binafsi naishi maeneo ya shangani na ni mteja mwaminifu wa MTUWASA lakini leo ni wiki ya pili maji hakuna watu wanahangaika kusaka maji kila kona.
Leo nilichukua hatua kufika MTUWASA wanachojitetea nacho ni kwamba umeme unakatika sana, wiki mbili kweli umeme? Mbona majumbani hatuoni kiasi hicho cha umeme kukatika?
MTUWASA tusaidieni maana ni agizo la wizara kwamba tunawe mikono mara kwa mara kuepuka kuambukizwa Covid-19.
Tafadhali tunaomba maji.
Mkoa ambao umeonja shubiri kwa kuondokewa na mkuu wa wilaya haujabadilika kuhusu tahadhari ya kunawa mikono kila wakati. Binafsi naishi maeneo ya shangani na ni mteja mwaminifu wa MTUWASA lakini leo ni wiki ya pili maji hakuna watu wanahangaika kusaka maji kila kona.
Leo nilichukua hatua kufika MTUWASA wanachojitetea nacho ni kwamba umeme unakatika sana, wiki mbili kweli umeme? Mbona majumbani hatuoni kiasi hicho cha umeme kukatika?
MTUWASA tusaidieni maana ni agizo la wizara kwamba tunawe mikono mara kwa mara kuepuka kuambukizwa Covid-19.
Tafadhali tunaomba maji.