Maji ni Mtego wa Umasikini (poverty trap)

Asante sana mheshimiwa Zitto Kabwe kwa kulitazamia suala hili, binafsi ninaumizwa sana na tatizo la Maji kwa jinsi linavyotukumba nchi yetu ya Tanzania. Tanzania ni nchi yenye maziwa na mito mingi sana na ni kati ya Nchi inayozungukwa na Bahari ya Hindi lakini bado ni nchi yenye matatizo makubwa ya Maji -- Tunakwama wapi?
 
Binadamu hatuishi kulaumu na kulalama - Serikali imefanya makubwa - tatizo upofu wa kisiasa nao husababisha watu kutoona nini kimefanywa na Serikali
 
Binadamu hatuishi kulaumu na kulalama - Serikali imefanya makubwa - tatizo upofu wa kisiasa nao husababisha watu kutoona nini kimefanywa na Serikali
Nakubaliana na wewe pia naunga mkono heading ya mtoa post(tatizo la maji ni mtego wa umaskini).
 
Karibu Mh. Zitto,

Pili pokea salamu zangu maana nimekuwa mlevi wa Sera na aina siasa unazoziendesha!

Tatu, naomba nijikite kwenye hoja thabiti uliyokuja nayo , ni ukweli usiopingika kuwa maji yamekuwa mtego wa masikini hapa nchini kwetu tangu tupate Uhuru na mwarobaini wake haujapatikana!

Kwetu huko Singida hususan wilaya ya Manyoni tumekuwa tukihangaika na shida ya maj mpka tunajihisi sisi sio watanzania, huenda tulizaliwa Tanzania kwa bahati mbaya!

Wakati serikali hii iliyo madarakani ikijinasibu kuwa inatetea wanyonge, huku kwetu wanawake na Dada zetu bila kuwasahau wafugaji hawajui wanapata wapi maji! Nimeshukuru umeamua kuwaamsha wa Tanzania dira na kuelewa kuwa MAJI BADO NI MTEGO WA UMASIKINI HAPA TANZANIA!

HAPO nimejaribu kuelezea hali ilivyo katika vijiji vya kasanii, Chikola,mbugani, sasilo, kashangu, mamba, ukitoa sehemu kama HEKA, wao hawana shida kwani kanisa katoriki la Roma kupitia parokia yao ya heka wananeemeka na maji!

Mh Zitto, angalia wilaya ya Tarime, pamoja na utajiri mkubwa wa madini ya dhahabu yaliyoko wilayani humo, bado maji ni kitendawili kisicho na majibu! Nimekaa Tarime kwa zaidi ya miaka minne MAJI TARIME NI CHANGAMOTO KUBWA, hiyo ni research ndogo tu ambayo nimeifanya Mh Zitto!

Maswali yangu kwako na wanasiasa wengine:

Je, hawaoni kero hizi?

Je, hama hama za wanasiasa hizi zinatija gani kwa sasa tungali bado tunachangamoto nyingi za kushughulikia?

Chama chako kwa maana ya ACT, kilijipambanua vizuri hapo 2015, na niliamini kinakuja kuwa mbadala wa vyama vya upinzani tulivyo navyo maana havioneshi upinzani wa kweli, lkn sasa naona kinamegukameguk, je, utaweza kuyafanya haya uliyoweza kuyaandika? Au ni kuwahadaa wananchi tu?

Mwisho, japo chama chako kinazidi kumeguka, bado Nina imani na katiba ya chama chenu, natamani kukiona kinasonga mbele!

Wasaalam!
Kwenye para ya pili ondoa neno "millioni" kabla ya hizo "digits" ili usomeke vizuri.

Umechapia.
 
Inabidi waje mijini - Ila watapata taabu sana kwani hata mjini maji ni janga kubwa. Huna mia 5 hupati dumu la maji maeneo yetu
 
Katika ziara zake zote Magufuli watu waliomba ndege na matren ya umeme? Bado tu hajifunz? Bas tuko gizan
Barabara zina tija ila sio kutumia million 80 kujenga barabara ya Morocco to Mwenge, eneo hilo tayali lina barabara nzuri
 
Maji ni jambo lilopaswa kukamilika miongo mingi iliyopita.
 
Changamoto ya Maji inachangia sana kuwashikilia watu wa vijijini kwenye dimbwi la umasikini na kuongeza tofauti ya kipato Kati ya mijini na vijijini na kati ya wenye nacho na wasio nacho. Gharama za maji ni kubwa mno maeneo ya vijijini kiasi kwamba zinazidi wastani wa pato la mtu mmoja ( per capital income) kwa siku nchini Tanzania.

“Pato la Taifa mwaka 2016 lilikuwa shilingi milioni 103,744,606 kwa bei za mwaka husika. Aidha, idadi ya watu Tanzania Bara ilikadiriwa kuwa watu 48,676,698 mwaka 2016. Hivyo, Pato la wastani la kila mtu lilikuwa shilingi 2,131,299 mwaka 2016 ikilinganishwa na shilingi 1,918,897 mwaka 2015, sawa na ongezeko la asilimia 11.1. Pato la wastani kwa kila mtu katika Dola za Marekani liliongezeka kutoka Dola 967.5 mwaka 2015 hadi Dola 979.1 mwaka 2016 ikichangiwa na kupungua kwa kasi ya kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania. Mwaka 2015, shilingi ya Tanzania ilipungua thamani dhidi ya dola ya Marekani kwa asilimia 16.8 ikilinganishwa na asilimia 8.8 mwaka 2016.” Hali ya Uchumi wa Taifa Juni 30, 2017. Kwa kutumia takwimu hizi za Serikali Ina maana kila Mtanzania ana kipato cha wastani wa shilingi 2.1 milioni Sawa na USD 980 kwa mwaka.

Hanang wanatumia kipato chao kikubwa kununua Maji

Mwananchi wa kijiji cha Gehandu Huko Hanang Mkoa wa Manyara ananunua maji pipa moja la lita 200 kwa shilingi 7000 na familia moja inahitaji angalau pipa moja kwa siku kwa matumizi ya kujibana kabisa ya maji. Kwa hiyo mwananchi huyu atahitaji takribani shilingi 2.5 milioni kwa mwaka kwa ajili ya Maji tu ya kutumia yeye na familia yake. Kwa familia ya Watu 6, huu ni wastani wa 16% ya kipato cha kila mwanafamilia hata mtoto mdogo wa siku 1 kutumika kununua Maji.

Hivyo familia moja inatumia wastani wa kipato cha mtu mmoja kwa mwaka kwa ajili ya Maji tu. Lazima familia hii iendelee kushikwa kwenye mtego wa umasikini. Mwananchi mmoja kijijini Gehandu alitueleza kuwa bajeti yake yote inaishia kwenye maji wakati wa kiangazi. Alieleza kwa uchungu sana namna anaamka saa 10 alfajiri kufuata Maji kilometa 20 kutoka nyumbani kwake na huko huchukua muda mrefu kwani foleni ni kubwa sana. Hanang hutumia sana Punda kubeba Maji na hubidi wakati mwengine kuyafuata mpaka mkoa jirani wa Singida.

Mijini ni tofauti

Miji mingi nchini kwetu hupata maji kutoka mamlaka za Maji safi na salama. Wastani wa bei ya maji kwa pipa la lita 200 kwa mamlaka za maji nchini ni shilingi 300 tu. Mwananchi wa Uzunguni jijini Arusha au Mikocheni jijini Dar es Salaam au Shanty Town Manispaa ya Moshi au Capri Point jijini Mwanza hutumia wastani wa shilingi 108,000 kwa mwaka kama gharama za Maji kwa familia yake. Ikumbukwe kuwa maji yanayosambazwa na Mamlaka za Maji Mijini ni masafi, yana madawa ya kuua wadudu wanaosababisha magonjwa kama kuhara nk. Mtu wa mjini haoni mzigo mkubwa wa matumizi ya Maji kwenye kipato chake kwani ni chini ya 1% ya wastani wa kipato cha familia ( wastani wa familia 1 watu 6 ). Wakati kule Hanang familia itatumia kipato chote cha mwanafamilia mmoja kununua maji ya familia nzima, Arusha au Dar es Salaam familia itatumia 4% tu ya kipato cha mwanafamilia kugharamia maji ya familia nzima. Hii ni nchi moja yenye mataifa mawili!

Ni zaidi ya Maji

Kwa kuwa maji yanayotumiwa na watu wa vijijini si safi na salama, Wananchi hao hutumia fedha nyingine nyingi zaidi kwenye matibabu kutokana na magonjwa kama kuhara, kichocho, typhoid, amoebae na kadhalika. Serikali inaingia gharama kubwa kununua madawa ya kutibu magonjwa haya kwa watu wa vijijini pale ambapo dawa hizi zinapatikana. Lakini pia nguvu ya kufanya kazi za uzalishaji hupungua kwa sababu ya Watu kuwa na siha duni na hivyo mzunguko wa umasikini kuendelea kuzunguka. Kwa nchi ambayo haina Mfumo madhubuti wa Bima ya Afya kwa Wananchi wake, gharama za Afya kwa masikini ni kubwa mno.

Tufanye nini?

Serikali yeyote makini lazima ijikite kwenye kuboresha hali ya maisha ya Wananchi wake kwa kuwaondolea vikwazo vya Maendeleo na kuvunja mitego ya umasikini ( poverty traps ) inayowashika na kuwadidimiza kwenye umasikini. Maji safi na salama kwa gharama nafuu yaweza kuwa ni hatua kubwa ya kuwaondoa Wananchi kwenye mtego mmoja wapo wa umasikini ( water poverty trap ). Hivyo Serikali iwekeze vya kutosha kwenye usambazaji wa Maji vijijini.

Miradi ya Maji sio miradi rahisi sana hivyo kunahitajika fikra mpya Katika kupata fedha za kujenga miradi ya Maji, kutunza vyanzo vya maji na kuendesha miradi ya Maji. Katika kata ambazo ACT Wazalendo ina madiwani tumeona tufanye majaribio ya ushiriki wa Wananchi kupitia Jumuiya za watumiaji Maji na sekta binafsi Katika kusambaza maji na kuendesha miradi ya Maji. Tunafanya majaribio haya kata za Tomondo Morogoro, Gehandu Hanang na Sumbugu Misungwi. Kupitia majaribio haya tutaweza kuboresha na kushawishi sera ya Taifa ya Maji kutokana na ushahidi kwenye kata hizi.

Ni vizuri Serikali kutazama upya vipaumbele vyake vya kimaendeleo. Kwa mfano kuna tija kujenga barabara ya Morocco - Mwenge Kwa shilingi 80 bilioni wakati Wananchi wa Tomondo, Morogoro wanakunywa Maji na mifugo?

==========​
Tanzania tatizo siyo takwimu, tatizo ni CCM, wanatengeneza Sera ambazo hazina tija na unyumbu (ncertainty policies and herding behaviour'
 
86 Reactions
Reply
Back
Top Bottom