Maji ni Mtego wa Umasikini (poverty trap)

Salama,
Ni mambo yapi ambayo serikali inafanya hayana tija kwa wananchi? Bunge letu liko wapi? katika hayo mambo ambayo unaamini serikali inafanya hayana tija kwa wananchi wake?

shukrani!
Ujenzi wa uwanja wa ndege chato una tija gani kwa wananchi wa chato wakati hata traffic light walizowekewa hawajui matumizi yake kila mtu anajivukia barabara anavyojisikia
 
Ujenzi wa uwanja wa ndege chato una tija gani kwa wananchi wa chato wakati hata traffic light walizowekewa hawajui matumizi yake kila mtu anajivukia barabara anavyojisikia
Hilo jambo lishatolewa ufafanuzi. Kama ingekuwa ni ushabiki kama unavyonifikria basi bungeni hapo kungechimbika.
 
Kongole Ndg. ZZK kwa kuchokoza mada hii nyeti. Kwa maoni yangu, naona tatizo kubwa lipo kwenye mifumo yetu ya kiutendaji na aina ya wananchi tulionao. Mtu asiyejua kuwa ni wajibu wake na viongozi wake kuhakikisha anapata huduma msingi, ni kawaida sana kwake kuomba badala ya kudai serikali itekeleze wajibu wake.

Naunga mkono hoja yako kuwa tuanze na maji; baada ya hapo twende kwenye nishati, elimu, na afya.

Wanasiasa wetu wa dunia ya tatu wamekuwa wakitumia matatizo ya wananchi mf. maji kama mitaji yao ya kisiasa ili kupata kula. Siku zao zinahesabika.

Nawasilisha.
 
Hakuna ubishi kwamba maji ni muhimu. Labda swali kwa Mh. Zitto ni kwamba, analysis hiyo ya gharama ya maji kwa watu wa vijijini, ni kweli kwamba wananchi hao wanacho kipato cha kiasi hicho? Kama maji tu gharama yake ni hiyo, je, mahitaji mengine yanagharimu kiasi gani na kwa kipato kipi?

Aidha, tunapaswa kujiuliza, ni kwa nini vyanzo vya maji vilivyokuwa vinatiririsha maji siku za nyuma vimekauka na kupelekea kuzuka tatizo la maji vijijini?

Kuhusu miundo mbinu ya usafiri na usafirishaji ni muhimu pia kwa vile kutokuwa na ubora unaotakiwa, muda wa uzalishaji na namna ya kufikia masoko huathirika.

Hebu fikiria, kwa mfano; kuna kipindi watu walilalamikia foleni ya magari jijini Dar es Salaam kwamba ilikuwa inatia nchi hasara kwa vile muda mrefu ulikuwa ukitumika kwenye safari badala ya uzalishaji.

Inashangaza na kusikitisha mtu anapokebehi jitihada za kupunguza msongamano wa magari kwa jiji kama la Dar es Salaam.

Cha msingi, nafikiri, ni kuhakikisha kwamba tunatunza vyanzo vya maji na kuhakikisha kwamba miundo mbinu inayojengwa na serikali au wadau wengineo wa maji inajengwa kwa viwango na kulindwa na watumiaji wa maji na wananchi kwa ujumla. Namna nyingine ni kujenga utamaduni wa kuvuna maji ya mvua.

Kama wananchi wa vijijini wanao uwezo wa kutumia kiasi hicho kilichosemwa na Mh. Zitto kwenye kukabiliana na tatizo la maji, iweje wasiwe na uwezo wa kujenga au kununua matenki ili wayatumie kuvuna maji ya mvua? Au iweje halmashauri za Wilaya zisiwe na mkakati wa kujenga mabwawa ili kuvuna maji ya mvua vijijini?

Na leo hii tukisikia serikali inawahamisha watu wanaolima kwenye vyanzo vya maji, wanaolima na kujenga kwenye kuta za mto, wanasiasa na wananchi wanadai serikali haina huruma na wananchi wake, inawabomolea numba zao na kuwahamisha kwenye maeneo yao. Wananchi tujifunze kuyatunza hayo maji na vyanzo vyake.
 
Hili ni donda ndugu,nikirejea miaka ya sabini na themanini tuliahidiwa tatizo la maji kuisha miaka ya tisini,leo hii tuko pabaya zaidi,siasa imekuwa ni kila kitu na kila kitu kimekuwa ni siasa,miaka ya arobaini na saba utunzaji wa vyanzo vya maji wa wazazi wetu ulikuwa wa hali ya juu,leo hii kizazi chetu hatujali ni uharibifu kwa kwenda mbele,ole wetu
 
Umenena vyema ndugu Zitto ...wanasiasa wamekuwa wakitumia mwanya huo huo kuendelea kutukalia kwa laghai ya kututatulia kero za maji...
Si hilo tu nimekuwa nikiwaza ni vipi watawala wetu wanatuhadaa kwamba wana mpango wa kutukwamua ikiwa Afrika pekee wapo viongozi wa nchi 55 (wanaotambuliwa na UN) lakini kwa pamoja wamekosa kabisa hospitali yenye hadhi ya kuwatibia wala chuo kikuu chenye hadhi ya kutoa elimu kwa wanafamilia wao hadi kulazimu kutibiwa na kusomesha familia zao nje ya bara hili!
 
Tatizo kubwa letu Watanzania tunachenga chenga hoja za msingi. Tatizo la maji asilimia 75% ni tatizo la umeme. Hatuna tatizo la upatikanaji wa maji lakini tuna tatizo la maji kufikia wananchi. Ili maji yafikie wananchi yanahita mabomba ya kupeleka maji, matank ya kuweka maji, sehemu ya kusafisha na umeme wa kuvuta maji. Hivyo wakati tuna lalamikia maji ni lazima tujue kwamba maji yanakuja na upatikanaji wa umeme. Hii ndiyo sababu kubwa tunasema umeme utatoa umasikini ni kwasababu matatizo mengi sana sana yatatatuliwa na upatikanaji wa umeme hadi vijijini. Cha kuongeza tu umeme utasaidia kwenye Afya, Elimu na sehemu nyingine nyingi sana. Mfano kwenye elimu kama kuna umeme na mitandao kijijini ina maana mtoto wa kijijini anaweza kuingia kwenye Library yeyote Duniani na kusoma kitabu kwa bure.
 
Zitto muandish mzuri, Ila vitendo ni sifuri.. Zitto alikusanya wanamuziki wa kigoma akaunda kundi akadai watazunguka Tanzania na afrika
 
Changamoto ya Maji inachangia sana kuwashikilia watu wa vijijini kwenye dimbwi la umasikini na kuongeza tofauti ya kipato Kati ya mijini na vijijini na kati ya wenye nacho na wasio nacho. Gharama za maji ni kubwa mno maeneo ya vijijini kiasi kwamba zinazidi wastani wa pato la mtu mmoja ( per capital income) kwa siku nchini Tanzania.

“Pato la Taifa mwaka 2016 lilikuwa shilingi milioni 103,744,606 kwa bei za mwaka husika. Aidha, idadi ya watu Tanzania Bara ilikadiriwa kuwa watu 48,676,698 mwaka 2016. Hivyo, Pato la wastani la kila mtu lilikuwa shilingi 2,131,299 mwaka 2016 ikilinganishwa na shilingi 1,918,897 mwaka 2015, sawa na ongezeko la asilimia 11.1. Pato la wastani kwa kila mtu katika Dola za Marekani liliongezeka kutoka Dola 967.5 mwaka 2015 hadi Dola 979.1 mwaka 2016 ikichangiwa na kupungua kwa kasi ya kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania. Mwaka 2015, shilingi ya Tanzania ilipungua thamani dhidi ya dola ya Marekani kwa asilimia 16.8 ikilinganishwa na asilimia 8.8 mwaka 2016.” Hali ya Uchumi wa Taifa Juni 30, 2017. Kwa kutumia takwimu hizi za Serikali Ina maana kila Mtanzania ana kipato cha wastani wa shilingi 2.1 milioni Sawa na USD 980 kwa mwaka.

Hanang wanatumia kipato chao kikubwa kununua Maji

Mwananchi wa kijiji cha Gehandu Huko Hanang Mkoa wa Manyara ananunua maji pipa moja la lita 200 kwa shilingi 7000 na familia moja inahitaji angalau pipa moja kwa siku kwa matumizi ya kujibana kabisa ya maji. Kwa hiyo mwananchi huyu atahitaji takribani shilingi 2.5 milioni kwa mwaka kwa ajili ya Maji tu ya kutumia yeye na familia yake. Kwa familia ya Watu 6, huu ni wastani wa 16% ya kipato cha kila mwanafamilia hata mtoto mdogo wa siku 1 kutumika kununua Maji.

Hivyo familia moja inatumia wastani wa kipato cha mtu mmoja kwa mwaka kwa ajili ya Maji tu. Lazima familia hii iendelee kushikwa kwenye mtego wa umasikini. Mwananchi mmoja kijijini Gehandu alitueleza kuwa bajeti yake yote inaishia kwenye maji wakati wa kiangazi. Alieleza kwa uchungu sana namna anaamka saa 10 alfajiri kufuata Maji kilometa 20 kutoka nyumbani kwake na huko huchukua muda mrefu kwani foleni ni kubwa sana. Hanang hutumia sana Punda kubeba Maji na hubidi wakati mwengine kuyafuata mpaka mkoa jirani wa Singida.

Mijini ni tofauti

Miji mingi nchini kwetu hupata maji kutoka mamlaka za Maji safi na salama. Wastani wa bei ya maji kwa pipa la lita 200 kwa mamlaka za maji nchini ni shilingi 300 tu. Mwananchi wa Uzunguni jijini Arusha au Mikocheni jijini Dar es Salaam au Shanty Town Manispaa ya Moshi au Capri Point jijini Mwanza hutumia wastani wa shilingi 108,000 kwa mwaka kama gharama za Maji kwa familia yake. Ikumbukwe kuwa maji yanayosambazwa na Mamlaka za Maji Mijini ni masafi, yana madawa ya kuua wadudu wanaosababisha magonjwa kama kuhara nk. Mtu wa mjini haoni mzigo mkubwa wa matumizi ya Maji kwenye kipato chake kwani ni chini ya 1% ya wastani wa kipato cha familia ( wastani wa familia 1 watu 6 ). Wakati kule Hanang familia itatumia kipato chote cha mwanafamilia mmoja kununua maji ya familia nzima, Arusha au Dar es Salaam familia itatumia 4% tu ya kipato cha mwanafamilia kugharamia maji ya familia nzima. Hii ni nchi moja yenye mataifa mawili!

Ni zaidi ya Maji

Kwa kuwa maji yanayotumiwa na watu wa vijijini si safi na salama, Wananchi hao hutumia fedha nyingine nyingi zaidi kwenye matibabu kutokana na magonjwa kama kuhara, kichocho, typhoid, amoebae na kadhalika. Serikali inaingia gharama kubwa kununua madawa ya kutibu magonjwa haya kwa watu wa vijijini pale ambapo dawa hizi zinapatikana. Lakini pia nguvu ya kufanya kazi za uzalishaji hupungua kwa sababu ya Watu kuwa na siha duni na hivyo mzunguko wa umasikini kuendelea kuzunguka. Kwa nchi ambayo haina Mfumo madhubuti wa Bima ya Afya kwa Wananchi wake, gharama za Afya kwa masikini ni kubwa mno.

Tufanye nini?

Serikali yeyote makini lazima ijikite kwenye kuboresha hali ya maisha ya Wananchi wake kwa kuwaondolea vikwazo vya Maendeleo na kuvunja mitego ya umasikini ( poverty traps ) inayowashika na kuwadidimiza kwenye umasikini. Maji safi na salama kwa gharama nafuu yaweza kuwa ni hatua kubwa ya kuwaondoa Wananchi kwenye mtego mmoja wapo wa umasikini ( water poverty trap ). Hivyo Serikali iwekeze vya kutosha kwenye usambazaji wa Maji vijijini.

Miradi ya Maji sio miradi rahisi sana hivyo kunahitajika fikra mpya Katika kupata fedha za kujenga miradi ya Maji, kutunza vyanzo vya maji na kuendesha miradi ya Maji. Katika kata ambazo ACT Wazalendo ina madiwani tumeona tufanye majaribio ya ushiriki wa Wananchi kupitia Jumuiya za watumiaji Maji na sekta binafsi Katika kusambaza maji na kuendesha miradi ya Maji. Tunafanya majaribio haya kata za Tomondo Morogoro, Gehandu Hanang na Sumbugu Misungwi. Kupitia majaribio haya tutaweza kuboresha na kushawishi sera ya Taifa ya Maji kutokana na ushahidi kwenye kata hizi.

Ni vizuri Serikali kutazama upya vipaumbele vyake vya kimaendeleo. Kwa mfano kuna tija kujenga barabara ya Morocco - Mwenge Kwa shilingi 80 bilioni wakati Wananchi wa Tomondo, Morogoro wanakunywa Maji na mifugo?

Iko siku tutafika mheshimwa
 
kiongozi ukizungumzia maji nakuelewa sana kiongozi wangu. namimi napenda niongeze mchango wangu japo kidogo kuhusiana na mada hii.
naaamini tatizo la maji kama yalivyo matatizo mengine mengi sana yanahitaji mabadiliko ya jinsi ya kufikiri. natamani sana tungetathimini ni kiasi gani cha maji tunayapoteza kabla ya kufikiri ni jinsi gani serikali inavyo weza kusambaza maji kwa kuwekeza kwenye miradi hii mikubwa tunayo izungumza.
hivi ni maji kiasi gani ya mvua tunayaacha yanapotea ardhini? au tutajitetea kuyavuna haya maji ni gharama sana? kama mtu anatumia 7000 kwa ajili ya maji kwa siku kijijini, maana yake anatumia 2,555,000 kwa mwaka, hivi hawa wanakijiji wanashindwaje kujenga visima vikubwa vikubwa vya maji ya mvua. nguvu kazi ya kuchimba wanayo wenyewe na visima vya kuchimba chini kwaajili ya kuvuna maji ya mvua gharama yake si kubwa sana, wanashindwaje kufanya hivi? wanashindwaje kuunganisha nguvu na kutatua tatizo dogo kama hili. tuseme wameshindwa sawa, hawa watu 2020 wanaenda kumchagua mbunge wanashindwaje kukaa kikao na kujadili sifa ya kumpitisha mbunge ni lazima nusu ya mshahara wake utumike kuchimba visima vya maji vya kutosha katika vijiji vyao. nguvu kazi ni wao wenyewe mshahara wa mbunge utumike kununua vifaa tuu. ni rahisi sana tubadilishe jinsi ya kufikiri na tujifunze kutatua matatizo yetu wenyewe. japo tusiache kuikumbusha serikali pale tunapoona kuna umuhimu wa kuikumbusha kutimiza wajibu wake.
haya ni mawazo yangu tu
 
Changamoto ya Maji inachangia sana kuwashikilia watu wa vijijini kwenye dimbwi la umasikini na kuongeza tofauti ya kipato Kati ya mijini na vijijini na kati ya wenye nacho na wasio nacho. Gharama za maji ni kubwa mno maeneo ya vijijini kiasi kwamba zinazidi wastani wa pato la mtu mmoja ( per capital income) kwa siku nchini Tanzania.

“Pato la Taifa mwaka 2016 lilikuwa shilingi milioni 103,744,606 kwa bei za mwaka husika. Aidha, idadi ya watu Tanzania Bara ilikadiriwa kuwa watu 48,676,698 mwaka 2016. Hivyo, Pato la wastani la kila mtu lilikuwa shilingi 2,131,299 mwaka 2016 ikilinganishwa na shilingi 1,918,897 mwaka 2015, sawa na ongezeko la asilimia 11.1. Pato la wastani kwa kila mtu katika Dola za Marekani liliongezeka kutoka Dola 967.5 mwaka 2015 hadi Dola 979.1 mwaka 2016 ikichangiwa na kupungua kwa kasi ya kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania. Mwaka 2015, shilingi ya Tanzania ilipungua thamani dhidi ya dola ya Marekani kwa asilimia 16.8 ikilinganishwa na asilimia 8.8 mwaka 2016.” Hali ya Uchumi wa Taifa Juni 30, 2017. Kwa kutumia takwimu hizi za Serikali Ina maana kila Mtanzania ana kipato cha wastani wa shilingi 2.1 milioni Sawa na USD 980 kwa mwaka.

Hanang wanatumia kipato chao kikubwa kununua Maji

Mwananchi wa kijiji cha Gehandu Huko Hanang Mkoa wa Manyara ananunua maji pipa moja la lita 200 kwa shilingi 7000 na familia moja inahitaji angalau pipa moja kwa siku kwa matumizi ya kujibana kabisa ya maji. Kwa hiyo mwananchi huyu atahitaji takribani shilingi 2.5 milioni kwa mwaka kwa ajili ya Maji tu ya kutumia yeye na familia yake. Kwa familia ya Watu 6, huu ni wastani wa 16% ya kipato cha kila mwanafamilia hata mtoto mdogo wa siku 1 kutumika kununua Maji.

Hivyo familia moja inatumia wastani wa kipato cha mtu mmoja kwa mwaka kwa ajili ya Maji tu. Lazima familia hii iendelee kushikwa kwenye mtego wa umasikini. Mwananchi mmoja kijijini Gehandu alitueleza kuwa bajeti yake yote inaishia kwenye maji wakati wa kiangazi. Alieleza kwa uchungu sana namna anaamka saa 10 alfajiri kufuata Maji kilometa 20 kutoka nyumbani kwake na huko huchukua muda mrefu kwani foleni ni kubwa sana. Hanang hutumia sana Punda kubeba Maji na hubidi wakati mwengine kuyafuata mpaka mkoa jirani wa Singida.

Mijini ni tofauti

Miji mingi nchini kwetu hupata maji kutoka mamlaka za Maji safi na salama. Wastani wa bei ya maji kwa pipa la lita 200 kwa mamlaka za maji nchini ni shilingi 300 tu. Mwananchi wa Uzunguni jijini Arusha au Mikocheni jijini Dar es Salaam au Shanty Town Manispaa ya Moshi au Capri Point jijini Mwanza hutumia wastani wa shilingi 108,000 kwa mwaka kama gharama za Maji kwa familia yake. Ikumbukwe kuwa maji yanayosambazwa na Mamlaka za Maji Mijini ni masafi, yana madawa ya kuua wadudu wanaosababisha magonjwa kama kuhara nk. Mtu wa mjini haoni mzigo mkubwa wa matumizi ya Maji kwenye kipato chake kwani ni chini ya 1% ya wastani wa kipato cha familia ( wastani wa familia 1 watu 6 ). Wakati kule Hanang familia itatumia kipato chote cha mwanafamilia mmoja kununua maji ya familia nzima, Arusha au Dar es Salaam familia itatumia 4% tu ya kipato cha mwanafamilia kugharamia maji ya familia nzima. Hii ni nchi moja yenye mataifa mawili!

Ni zaidi ya Maji

Kwa kuwa maji yanayotumiwa na watu wa vijijini si safi na salama, Wananchi hao hutumia fedha nyingine nyingi zaidi kwenye matibabu kutokana na magonjwa kama kuhara, kichocho, typhoid, amoebae na kadhalika. Serikali inaingia gharama kubwa kununua madawa ya kutibu magonjwa haya kwa watu wa vijijini pale ambapo dawa hizi zinapatikana. Lakini pia nguvu ya kufanya kazi za uzalishaji hupungua kwa sababu ya Watu kuwa na siha duni na hivyo mzunguko wa umasikini kuendelea kuzunguka. Kwa nchi ambayo haina Mfumo madhubuti wa Bima ya Afya kwa Wananchi wake, gharama za Afya kwa masikini ni kubwa mno.

Tufanye nini?

Serikali yeyote makini lazima ijikite kwenye kuboresha hali ya maisha ya Wananchi wake kwa kuwaondolea vikwazo vya Maendeleo na kuvunja mitego ya umasikini ( poverty traps ) inayowashika na kuwadidimiza kwenye umasikini. Maji safi na salama kwa gharama nafuu yaweza kuwa ni hatua kubwa ya kuwaondoa Wananchi kwenye mtego mmoja wapo wa umasikini ( water poverty trap ). Hivyo Serikali iwekeze vya kutosha kwenye usambazaji wa Maji vijijini.

Miradi ya Maji sio miradi rahisi sana hivyo kunahitajika fikra mpya Katika kupata fedha za kujenga miradi ya Maji, kutunza vyanzo vya maji na kuendesha miradi ya Maji. Katika kata ambazo ACT Wazalendo ina madiwani tumeona tufanye majaribio ya ushiriki wa Wananchi kupitia Jumuiya za watumiaji Maji na sekta binafsi Katika kusambaza maji na kuendesha miradi ya Maji. Tunafanya majaribio haya kata za Tomondo Morogoro, Gehandu Hanang na Sumbugu Misungwi. Kupitia majaribio haya tutaweza kuboresha na kushawishi sera ya Taifa ya Maji kutokana na ushahidi kwenye kata hizi.

Ni vizuri Serikali kutazama upya vipaumbele vyake vya kimaendeleo. Kwa mfano kuna tija kujenga barabara ya Morocco - Mwenge Kwa shilingi 80 bilioni wakati Wananchi wa Tomondo, Morogoro wanakunywa Maji na mifugo?
Kwa kweli suala la maji baada ya miaka kadhaa ijayo itakuwa ni vita nyingine kubwa ambayo mwisho wake hutaweza kuamlika kirahisi
 
nafikiri kwa nyinyi wasomi inatakiwa muandike haya kila zikku lengo liwe kuikumbusha serikali wajibu wake lakini kukebehi ujenzi wa Barbara sioni kama ni sahihi
 
Daah umeelezea vizuri sana. Kijijini wanapata shida sana ya maji.
Inabdi ianzishwe program ya maji vijijini kama ile ya umeme (REA). Itasaidia sana hakika.
 
Changamoto ya Maji inachangia sana kuwashikilia watu wa vijijini kwenye dimbwi la umasikini na kuongeza tofauti ya kipato Kati ya mijini na vijijini na kati ya wenye nacho na wasio nacho. Gharama za maji ni kubwa mno maeneo ya vijijini kiasi kwamba zinazidi wastani wa pato la mtu mmoja ( per capital income) kwa siku nchini Tanzania.

“Pato la Taifa mwaka 2016 lilikuwa shilingi milioni 103,744,606 kwa bei za mwaka husika. Aidha, idadi ya watu Tanzania Bara ilikadiriwa kuwa watu 48,676,698 mwaka 2016. Hivyo, Pato la wastani la kila mtu lilikuwa shilingi 2,131,299 mwaka 2016 ikilinganishwa na shilingi 1,918,897 mwaka 2015, sawa na ongezeko la asilimia 11.1. Pato la wastani kwa kila mtu katika Dola za Marekani liliongezeka kutoka Dola 967.5 mwaka 2015 hadi Dola 979.1 mwaka 2016 ikichangiwa na kupungua kwa kasi ya kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania. Mwaka 2015, shilingi ya Tanzania ilipungua thamani dhidi ya dola ya Marekani kwa asilimia 16.8 ikilinganishwa na asilimia 8.8 mwaka 2016.” Hali ya Uchumi wa Taifa Juni 30, 2017. Kwa kutumia takwimu hizi za Serikali Ina maana kila Mtanzania ana kipato cha wastani wa shilingi 2.1 milioni Sawa na USD 980 kwa mwaka.

Hanang wanatumia kipato chao kikubwa kununua Maji

Mwananchi wa kijiji cha Gehandu Huko Hanang Mkoa wa Manyara ananunua maji pipa moja la lita 200 kwa shilingi 7000 na familia moja inahitaji angalau pipa moja kwa siku kwa matumizi ya kujibana kabisa ya maji. Kwa hiyo mwananchi huyu atahitaji takribani shilingi 2.5 milioni kwa mwaka kwa ajili ya Maji tu ya kutumia yeye na familia yake. Kwa familia ya Watu 6, huu ni wastani wa 16% ya kipato cha kila mwanafamilia hata mtoto mdogo wa siku 1 kutumika kununua Maji.

Hivyo familia moja inatumia wastani wa kipato cha mtu mmoja kwa mwaka kwa ajili ya Maji tu. Lazima familia hii iendelee kushikwa kwenye mtego wa umasikini. Mwananchi mmoja kijijini Gehandu alitueleza kuwa bajeti yake yote inaishia kwenye maji wakati wa kiangazi. Alieleza kwa uchungu sana namna anaamka saa 10 alfajiri kufuata Maji kilometa 20 kutoka nyumbani kwake na huko huchukua muda mrefu kwani foleni ni kubwa sana. Hanang hutumia sana Punda kubeba Maji na hubidi wakati mwengine kuyafuata mpaka mkoa jirani wa Singida.

Mijini ni tofauti

Miji mingi nchini kwetu hupata maji kutoka mamlaka za Maji safi na salama. Wastani wa bei ya maji kwa pipa la lita 200 kwa mamlaka za maji nchini ni shilingi 300 tu. Mwananchi wa Uzunguni jijini Arusha au Mikocheni jijini Dar es Salaam au Shanty Town Manispaa ya Moshi au Capri Point jijini Mwanza hutumia wastani wa shilingi 108,000 kwa mwaka kama gharama za Maji kwa familia yake. Ikumbukwe kuwa maji yanayosambazwa na Mamlaka za Maji Mijini ni masafi, yana madawa ya kuua wadudu wanaosababisha magonjwa kama kuhara nk. Mtu wa mjini haoni mzigo mkubwa wa matumizi ya Maji kwenye kipato chake kwani ni chini ya 1% ya wastani wa kipato cha familia ( wastani wa familia 1 watu 6 ). Wakati kule Hanang familia itatumia kipato chote cha mwanafamilia mmoja kununua maji ya familia nzima, Arusha au Dar es Salaam familia itatumia 4% tu ya kipato cha mwanafamilia kugharamia maji ya familia nzima. Hii ni nchi moja yenye mataifa mawili!

Ni zaidi ya Maji

Kwa kuwa maji yanayotumiwa na watu wa vijijini si safi na salama, Wananchi hao hutumia fedha nyingine nyingi zaidi kwenye matibabu kutokana na magonjwa kama kuhara, kichocho, typhoid, amoebae na kadhalika. Serikali inaingia gharama kubwa kununua madawa ya kutibu magonjwa haya kwa watu wa vijijini pale ambapo dawa hizi zinapatikana. Lakini pia nguvu ya kufanya kazi za uzalishaji hupungua kwa sababu ya Watu kuwa na siha duni na hivyo mzunguko wa umasikini kuendelea kuzunguka. Kwa nchi ambayo haina Mfumo madhubuti wa Bima ya Afya kwa Wananchi wake, gharama za Afya kwa masikini ni kubwa mno.

Tufanye nini?

Serikali yeyote makini lazima ijikite kwenye kuboresha hali ya maisha ya Wananchi wake kwa kuwaondolea vikwazo vya Maendeleo na kuvunja mitego ya umasikini ( poverty traps ) inayowashika na kuwadidimiza kwenye umasikini. Maji safi na salama kwa gharama nafuu yaweza kuwa ni hatua kubwa ya kuwaondoa Wananchi kwenye mtego mmoja wapo wa umasikini ( water poverty trap ). Hivyo Serikali iwekeze vya kutosha kwenye usambazaji wa Maji vijijini.

Miradi ya Maji sio miradi rahisi sana hivyo kunahitajika fikra mpya Katika kupata fedha za kujenga miradi ya Maji, kutunza vyanzo vya maji na kuendesha miradi ya Maji. Katika kata ambazo ACT Wazalendo ina madiwani tumeona tufanye majaribio ya ushiriki wa Wananchi kupitia Jumuiya za watumiaji Maji na sekta binafsi Katika kusambaza maji na kuendesha miradi ya Maji. Tunafanya majaribio haya kata za Tomondo Morogoro, Gehandu Hanang na Sumbugu Misungwi. Kupitia majaribio haya tutaweza kuboresha na kushawishi sera ya Taifa ya Maji kutokana na ushahidi kwenye kata hizi.

Ni vizuri Serikali kutazama upya vipaumbele vyake vya kimaendeleo. Kwa mfano kuna tija kujenga barabara ya Morocco - Mwenge Kwa shilingi 80 bilioni wakati Wananchi wa Tomondo, Morogoro wanakunywa Maji na mifugo?

Uko sahihi kabisa Brother ,Tuendelee kuwaonesha Watanzania kwa kutumia namba pengine watalewa zaidi.
 
Back
Top Bottom