Maji ni Mtego wa Umasikini (poverty trap)

Ni sahihi sana, haiwezekani serikali ikawekeza ama kuanza na vipaumbele ambavyo havina manufaa kwa kiasi kikubwa kwa taifa. Na badala yake kusahau sekta muhimu kama ya maji.

Hata mheshimiwa Lema ashawahi kuliongea hili na kuishauri serikali, kuhusu umuhimu wa maji na kusema kuwa maji ni bidhaa muhimu, hivyo serikali inatakiwa ifanye bidii kufikisha maji maeneo mengi ya nchi yetu ili wananchi wasipate adha ya kufata maji umbali mrefu, na badala yake wajikite katika uzalishaji zaidi.
 
Ukweli utaendelea kuwa ukweli.

Hakuna sababu ya kununua ndege nyingi na kwa mbwembwe, zikaishia kushikiriwa wakati wananchi hawana maji, barabara, elimu,umeme etc.
 
Zitto,

Tija ya kujenga barabara wewe huioni? Bora ungesema ile midege isiyo na tija au ile SGR isiyo na tija yoyote..
 
CCM wana macho lakini hawaoni, wana masikio lakini hawasikii. Hela zimeelekezwa kwenye chaguzi za marudio na kununua madiwani na wabunge.
 
Mheshimiwa Zitto, ungeanza na sisi hapa Ujiji maana kimsingi hatupaswi kulilia maji zile posho unazogomea Bungeni tumia kutuletea maji BURE toka hapo Tanganyika, utakuwa mbunge wetu milele.
 
Utawala wa CCM umelaaniwa.

Wewe angalia maeneo ya Temeke, Mbagala, Mkuranga kuna shida kubwa ya maji lakini toka Mbagala hadi mto Rufiji ni kama kilometers 100 tu, lakini serkali za CCM zimeshindwa kuvuta maji toka mto rufiji kuja mkuranga, Mbagala na Temeke.

Watu maeneo hayo wanakunywa maji ya visima vya mavi, lakini mamilioni ya lita za maji ya mto Rufiji yanamiminikia baharini kila siku.

Bomba la gesi limeweza kutoka Mtwara hadi Dar wanashindwaje kuchukua maji Rufiji kuleta Dar?
Kujenga bomba la maji sambamba na lile la gesi kwa wakati mmoja na kutumia mkandarasi huyo huyo kungepunguza gharama sana.

Tatizo kubwa serikalini wanapanga jambo moja moja na huchukua muda mrefu kutekeleza, pengine hata technology hubadilika kabla ya utekelezaji.
 
Mh. Zitto, kama ulivyo hitimisha kwa swali zuri. Tatizo la hii nchi ni priority!! (vipaumbele!), katika suala la maji hii nchi tumelaliwa kuwa na vyanzo vingi lakini ni kama hatuna macho.

Mfano, Mji wa dodoma na wilaya zake zingeweza kupatiwa maji kwa kujenga mabwawa badala ya kufikiria kusafirisha maji kutoka ziwa victoria. Tuna hazina kubwa ya maji ya chini ya ardhi! Lakini hayatumiki ipasavyo. Mimi nakuunga mkono kwamba tukiboresha huduma za upatikanaji wa maji hasa vijijini tutajikwamua kama nchi kutoka wenye umaskini japo kwa kiasi fulani.
Ni vyema unapotoa hoja uwe unaweka tarakimu.

Mfano. Hiyo akiba kubwa ya maji chini ya ardhi ni kiasi gani na ipo maeneo yapi? Na je yana ubora upi? Umewahi kuyatumia maji ya visima maeneo ya Dar. Dodoma na Manyara? Ubora wake ukoje?

Je. Dodoma wajenge mabwawa eneo gani yaani kwenye mto upi na bwawa litakuwa na uwezo wa kutoa maji kiasi gani?

Hasara ya kutoa maji ziwa victoria badala ya kujenga mabwawa kwa ajili ya mji wa dodoma ni ipi?
 
Everything is a trap in this country.
Lack of water is a trap....lack of electricity is a trap....poor roads is a trap....poor healthcare is a trap.....don't even mention the education system!
All one vicious cycle designed to keep us perpetually deprived
Kwahiyo ni sahihi kuanza kuondoa mtego wa barabara kabla ya hiyo mitego mingine ikiwemo maji elimu umeme nk.
 
Huwa nashangaa sana Tanga jiji kupata maji toka Muheza mto Zigi,cha ajabu pale Muheza maji yanakotoka kuna shida ya maji ni balaa,nadhani tumekosa vipaumbele kama nchi.
Hili ni tatizo la kimfumo. Kwamba katika kugawa maji kunakuwa na mamlaka za mijini ambako maji yanauzika, na mamlaka za vijijini ambako maji hayana bei.

Kama mradi wa kupeleka maji Tanga mjini ungezingatia maeneo yote ya jirani kusingeanzishwa mradi mwingine wa kupeleka maji muheza.

Mhe. Zito mweleze waziri wa maji aache kuwa na discrete projects kwa kila eneo. Nchi hii ni kubwa inahitaji miradi mikubwa ili kusambaza maji kila mahala kwa gharama nafuu.

Mfani ni mitadi kama ya kuleta maji jijini Dar iliyozingatia miji ya Kibaha na Bagamoyo. Na miradi ya kitaifa kama ule wa mugango au wa wang'ing'ombe. Mambo ya vidima kila kijiji ni siasa.
 
Serikali yetu vipaumbele vyake having mantiki na inataka ionekane kuwa INA uwezo wakati wananchi ndio tunaumia. Mfano kila siku inajisifu kununua bombardier wakati hatuna Maji. Bombardier moja ingeweza kuwekeza miradi zaid ya 1000 ya maji
 
gfsonwin,

Pole kwa kuchoka.

Sera ya maji ya mwaka 2002 imeainisha vipaumbele vya kugawa maji. Kwanza ni maji kwa ajili ya binadamu yaani kunywa kuoga msalani kupikia nk. Pili ni maji kwa ajili ya MAZINGIRA na mwisho ni MATUMIZI MENGINEYO yaani matumizi ya kiuchumi.

Hapo kwenye matumizi mengineyo ni kwamba wadau wanatakiwa wakae pamoja wagawane maji yaliyobaki baada ya maji ya binadamu na mazingira kutengwa pembeni kutoka kwenye chanzo husika.

Bodi za maji za mabonde ndizo zenye jukumu la kuyagawa maji hayo na kila mtumiaji anatakiwa awe na KIBALI CHA KUTUMIA MAJI.
 
Barabara zina tija ila sio kutumia million 80 kujenga barabara ya Morocco to Mwenge, eneo hilo tayali lina barabara nzuri
Hujawahi kukutana na msongamano wa pale wewe, yaan unaweza kusema magari yote Tanzania yapo hicho kipande, halafu haikuwa milioni 80, ilikuwa bilioni 2 nadhani.., na japo barabara zilikuwa nzuri ila zilikuwa nyembamba hivyo wakaona wapanue..
 
SGR ina tija kuliko barabara
TAZARA ilikuaje kwani? Wafanyabiashara wanaona tija kutumia barabara kuliko reli, nyinyi mnalazimisha na hilo li-SGR, unajua ni kwanini malori yanafurika Zambia highway ilihali TAZARA ipo?
 
chambimagaka,

Wale jamaa hata uvute maji toka ziwa victoria, mto kirumi bado watakata mabomba....pale Nyamongo walivutiwa maji toka mgodini usiku wanakata mabomba wanaenda kuuza Kenya. Baadae mwekezaji akaweka water tanks points akawa anapitisha maji asubuhi anajaza kwenye tanks hizo kwa matumizi ya binadamu...ili wana Nyamongo waje wachote bado wale jamaa wakawa wakimaliza kuchota wanaiba koki za maji....wao walikuwa wanataka waachiwe sehemu wakavune dhahabu sio huduma za kijamii.

Pili....Ruzuku anayo toa mwekezaji....ingekuwa inatumika vyema Tarime ingekuwa na maji toka 2008. Matumizi mabaya ya ruzuku ni changamoto....zile hela zingetumika kwanza na vipaumbile kama hivyo tatizo hilo lingekuwa historia kwa sasa na pengine na matatizo mengine mengi yangekuwa historia....tatizo ni culture ya watu wale.

Ila kwa sasa naona mambo yamebadilika baada ya umeme kufika nyamongo....ustaarabu umeanza kuwaingia....na udhibiti mkubwa uliowekwa wa kuchukua mchanga wa dhahabu umefanya vijana kuanza kuwaza njia mbadala ya kupata kipato.

Mwita Mwita.
 
Back
Top Bottom