Majenerali Wamgeuka Yahya Jammeh, sasa kwenda uhamishoni

Brigedia Chan-ocha

JF-Expert Member
Mar 7, 2014
1,353
2,842
Jenerali MUSA SAVAGE na Jenerali Badjie wamemgomea Rais wa Gambia Bwana Yahya Jammeh, wakisema tarahe 19 January 2017 wataanza kumtii Rais mteule ADAMA Barrow, linataarifu Gazeti la FREEDOM la Nchini humo.

Taarifa zinasema, Jana Alhamis Ikulu ya Gambia kulikuwa na Kikao cha " SECURITY BRIEFING" ambapo Rais Yahya Jammeh ametaarifiwa kuwa wakuu wa Battalions zote wamekubaliana kutoruhusu Jeshi kupigana ikiwa itatokea uvamizi wa Nchi za ECOWAS ili kumuondoa madarakani.

Jenerali MUSA SAVAGE tayari amewaarifu wenzake kuwa hataruhusu Battalion yake ipigane na kwamba ni lazima maamuzi ya wananchi wa GAMBIA yaheshimiwe.

Hali ilibadilika jana ndani ya ikulu punde baada ya Yahya Jammeh kuarifiwa hivyo ambapo alibadilika na kuondoka ndani ya kikao asiamini kile alichoelezwa na mtu wake wa karibu Jenerali Badjie.

Taarifa mpya zinasema, Tayari mazungumzo yameanza ili Rais Yahya Jammeh aende uhamishoni katika moja ya nchi za AMERICA KUSINI ambapo nchi hizo hazina utaratibu wa kutekeleza amri za ICC za kumsalimisha mtu kwenye mahakama hiyo.
 
Huyo jamaa amesema kasikia ,kwahiyo hana uhakika na hiyo taarifa

Tetesi so hopefully ziwe za kweli

Maana juzi huyo Badjie alivaa combat yenye picha ya Jammeh na alisema atapigana kwajili ya Jammeh

Lakini lazima ujue ECOWAS wakiongozwa na Senegal wanafua misuli kwa ajili ya kumtia adabu, kwa jiografia ya Gambia mpiganaji yeyote mwenye akili lazima ajue kitakachofuata baada ya vita kuanza kwani uwezi jua Senegal wataanzia pembe ipi. Hivyo uki geu geu nautegemea sana
 
Ni vzr kuona makamanda wa ngazi za juu wakisimamia UKWELI na kuheshimu maamuzi ya wananchi ,huo ndio uzalendo wa kweli na sio unafiki
 
Jenerali MUSA SAVAGE na Jenerali Badjie wamemgomea Rais wa Gambia Bwana Yahya Jammeh, wakisema tarahe 19 January 2017 wataanza kumtii Rais mteule ADAMA Barrow, linataarifu Gazeti la FREEDOM la Nchini humo, Taarifa zinasema, Jana Alhamis Ikulu ya Gambia kulikuwa na Kikao cha " SECURITY BRIEFING" ambapo Rais Yahya Jammeh ametaarifiwa kuwa wakuu wa Battalions zote wamekubaliana kutoruhusu Jeshi kupigana ikiwa itatokea uvamizi wa Nchi za ECOWAS ili kumuondoa madarakani, Jenerali MUSA SAVAGE tayari amewaarifu wenzake kuwa hataruhusu Battalion yake ipigane na kwamba ni lazima maamuzi ya wananchi wa GAMBIA yaheshimiwe, hali ilibadilika jana ndani ya ikulu punde baada ya Yahya Jammeh kuarifiwa hivyo ambapo alibadilika na kuondoka ndani ya kikao asiamini kile alichoelezwa na mtu wake wa karibu Jenerali Badjie.

Taarifa mpya zinasema, Tayari mazungumzo yameanza ili Rais Yahya Jammeh aende uhamishoni katika moja ya nchi za AMERICA KUSINI ambapo nchi hizo hazina utaratibu wa kutekeleza amri za ICC za kumsalimisha mtu kwenye mahakama hiyo.

Maamuzi mazuri kabisa kwa jeshi lenye nidhamu na utii wa sharia za kikatiba. Naomba majeshi mengine yote ya Africa yajifunze kwa hilo maana itasaidia sana kuepusha vita, vifo na mahangaiko ya raia pasipo sababu za msingi. Hongereni sana Makamanda wa Gambia kwa kutetea uamuzi wa wananchi wenu.
 
Kuna watu wanafikiri nchi ni miliki zao na familia zao.
Hao majenerali wameonyesha uzalendo wa kweli kwa nchi yao.
 
Back
Top Bottom