Majambazi yavamia guest 2 na kupora Tsh 24,314,500/=

ntamaholo

JF-Expert Member
Aug 30, 2011
12,906
6,909
hi jf.
Nimepokea habari za kusikitisha kutoka sengerema inayoeleza kama ifuatavyo:-

huko kambi ya bugombe kata maisome tarafa kahunda (w) sengerema (m) mwanza.majambazi wapatao zaidi ya wawili wakiwa na silaha smg/sar na mapanga walivamia nyumba ya kulala wageni ya mandela na madini na kupora vitu mbalimbali vikiwa na thamani ya tsh.24,314,500/=

wageni katika nyumba hizo walikuwa wenyeji wa kutoka mikoa ya shinyanga, kigoma, bukoba na nchi ya jirani ya rwanda. Asilimia kubwa ya wageni hao ni wafanya biashara.

Hakuna aliyetiwa nguvuni na jeshi la polisi, na kila mwenye taarifa sahihi juu ya majambazi hawa asisite kuwasiliana na uongozi wa polisi wilaya ya sengerema au polisi mkoa wa mwanza.
 
Mwenye taarifa tafadhali asisite kutoa taarifa kituo cha polisi kilichokaribu naye.
kwani majambazi wengi, wakimaliza uharamia wao, huenda bar kujipongeza na wengine huanza kutamba.
ukipata taarifa, tOA KITUA KILICHO KARIBU NAWE
 
Polisi ifanye juu chini iwakamate majambazi hayo na kuyafikisha kwenye vyombo vya sheria.
 
Mwanza itapelekeshwa sana namajambazi kwa sababu majambazi mengi yameachiwa toka gerezani mengine yameshinda kesi ktk mazingira ya kutatanisha,pia kuna pesa za CAF money ambazo zinatakiwa wapewe raiawema watoa taarifa zinazohusu majambazi napia polisi hufanikiwa kukamata mpk silaha ila watoa taarifa hawapewi hata senti5,zinaliwa na polisi wenyewe.polisi mwanza wajipange na wajirekebishe.
 
mwanza itapelekeshwa sana namajambazi kwa sababu majambazi mengi yameachiwa toka gerezani mengine yameshinda kesi ktk mazingira ya kutatanisha,pia kuna pesa za caf money ambazo zinatakiwa wapewe raiawema watoa taarifa zinazohusu majambazi napia polisi hufanikiwa kukamata mpk silaha ila watoa taarifa hawapewi hata senti5,zinaliwa na polisi wenyewe.polisi mwanza wajipange na wajirekebishe.

ila kweli. Nakumbuka ilishawahi kutangazwa, ukitoa taarifa za kufanikisha kukamata majmbazi au silaha, zawadi yako nadhani ilikuwa laki tano. Cjui kama watu walipewa
 
ila kweli. Nakumbuka ilishawahi kutangazwa, ukitoa taarifa za kufanikisha kukamata majmbazi au silaha, zawadi yako nadhani ilikuwa laki tano. Cjui kama watu walipewa

usiende huko polisi wengine si waaminifu wanafichua siri kwa majambazi
 
Back
Top Bottom