Majambazi wawashangaa Police kwa kuwaacha wakiendelee kutesa tu

Kwa hali hii ya rushwa, kazi ipo. Polisi anapomfuata jambazi kwenda gawana ngawira na vilevile kumshauri apotee hadi hali itakapotulia, tumekwisha!!!! Waziri Masha upo!!!!???
 
mambo haya nimekuwa nikiona maigizo ya akina ze comedy, Onyango, vituko mahakamani, Ice Cube nk. kumbe huwa vinatokea mahakamani ki kweli kweli loh! mi ningekuwepo hapo mahakamani ingenilazimu kuondoka ili nisiwekwe ndani kwasababu ya kucheka kwa nguvu.
 
Huyo shahidi wa 25 mimi ningempa hata Uwaziri!! Kwa sababu ni mtu pekee aliyekubali kusema "mimi ni mwizi na nimekuwa nikiiba kwa miaka 10 na sitaacha daima"...
 
hii spirit isipite bila kupongezwa....! ushauri wangu ni kuwa na wengine ambao wametenda maovu (EPA,KIWIRA,RICHMOND,etc) waige mfano wa hawa nasi tuwapongeze na tusiwalaumu........!
"....... ITAFUTENI KWELI.....NAYO KWELI ......ITAWAWEKA HURU....."
ILA WASAIDIWE KUFUTA KAULI YAO KUWA HAWATAACHA WIZI......!
 
baadhi ya hao mashahidi wamenena, kwamba wamejisikia uchungu sana baada ya kuona wao ndiyo walioiba, lakini wameuliwa wengine, kwangu mimi ni kitendo cha kishujaa sana.hivi ni viongozi wangapi ambao wanaiba mapesa ya wananchi na wanauzulia katika misiba ya hao wananchi waliowibia pesa zao ambao wamekufa kwa kukosa ka panadol tu na hata aibu hawaoni?
 
Tanzania haina utawala wa sheria, inaumiza na ni mbaya lakini tulipofikishwa Watanzania bora na hili Jeshi la mafisadi nalo lingejaribu kuchukua nchi sote tukacharazwa viboko, wakianzwa watawala au viongozi wa mafisadi hata kwa miaka mitano tu ndio tutashika adabu nchi hii. Inauma lakini ni heri kuliko ilivyo
 
Huyo Mwizi/Shahidi naamini kama angekuwapo enzi za Yesu nadhani ni sawa na yule Mama Mgoni aliyekamatwa na kuletwa kwa Yesu au pia yule Mfarisayo aliyesimama nyuma kabisa ya sinagogi na kusema "mimi mdambi nihurumie".

Bottomline ni kuwa huyu bwana hajawa mnafiki.
 
Huyo shahidi kaamua kufa na Zombe maana lazima Zombe aliwanyanyasa sana kipindi akiwa madarakani. Yaani mnaiba, halafu polisi wanakuja mpaka nyumbani kisha mnagawana pesa, au wanachukua zote!!! Inatisha sana!! Halafu negotiations zilikuwa zinaruhusiwa, yaani kutoka shs. 350,000 mpaka shs. 40,000 kweli jeshi letu la polisi linatia kinyaaa!!!!
 
Hii story nimesoma nimecheka ile mbaya...haswa pale alipomfukuza yule polisi kwenye bar.Nakumbuka kuna wakati nilikuwa naongea na rafiki yangu mmoja polisi na akawa anasema kila akisikia kwenye radio call jambazi au majambazi wameuawa na polisi,wakifika kwenye tukio wanakuta wale majambazi mifuko yao iko inside out,yaani wamepekuliwa na polisi! Sasa hivi ndio naanza kujiuliza hivi wangapi kati ya hao walikuwa ni raia wema tu.
Lakini lazima tujiulize what the hell is going on! Mwizi anasema yeye ni mwizi na ataendelea kuwa mwizi...na huyu mizi polisi wanamjua na walimfuata na akawafukuza.Raia wema wameuawa kikatili na watu waliokula kiapo kuhahakisha usalama wao na mali zao!
 
Kwa hali hii ya rushwa, kazi ipo. Polisi anapomfuata jambazi kwenda gawana ngawira na vilevile kumshauri apotee hadi hali itakapotulia, tumekwisha!!!! Waziri Masha upo!!!!???

tatizo hapo mama mdogo ni mshahara mdogo wanao lipwa pamoja na nyumba chakavu wanazo ishi askari wetu.Hata ukiwa wewe huwezi kukataa fweza za ubwete 400000 wkt mshahara wako 90,000/= kwa mwezi na unafamilia ndani unasomesha ndugu kijijini wanakuangalia wewe hujavaa n.k lazima utapokea tu na kula deal la nguvu.
 
Kwa hali hii ya rushwa, kazi ipo. Polisi anapomfuata jambazi kwenda gawana ngawira na vilevile kumshauri apotee hadi hali itakapotulia, tumekwisha!!!! Waziri Masha upo!!!!???

Mama MDogo,

Na wezi wa EPA ndivo hivohivo waliambiwa
 
Nimeamini hakuna jiwe litakalo achwa bila kugeuzwa.Tukitaka kuiponya nchi yetu basi tuwe wakweli kama hawa jamaa,kwa ukweli huu nchi za wenzetu zingewapa ushauri maalumu ili waishi maisha safi.
Mimi nauliza swali,hawa polisi wa Kituo cha O`bay wanaposoma uoza huu bado wanaendelea kuvaa sare na kwenda kazini?
 
tatizo hapo mama mdogo ni mshahara mdogo wanao lipwa pamoja na nyumba chakavu wanazo ishi askari wetu.Hata ukiwa wewe huwezi kukataa fweza za ubwete 400000 wkt mshahara wako 90,000/= kwa mwezi na unafamilia ndani unasomesha ndugu kijijini wanakuangalia wewe hujavaa n.k lazima utapokea tu na kula deal la nguvu.


wanaipenda hiyo hali bwana, kama wangekuwa hawaipendi wasingekuwa wanawalinda hao viongozi wezi wao kazi yao kulala mika chini chini tuu... they should do something ili viongozi wajue wanachokitaka... we fikiria walipoifungua JF na walivosingizia kuwa ni magaidi... hapo utasema hawaipendi hali yao ya uchumi kweli
 
wanaipenda hiyo hali bwana, kama wangekuwa hawaipendi wasingekuwa wanawalinda hao viongozi wezi wao kazi yao kulala mika chini chini tuu... they should do something ili viongozi wajue wanachokitaka... we fikiria walipoifungua JF na walivosingizia kuwa ni magaidi... hapo utasema hawaipendi hali yao ya uchumi kweli

ndo hapo ninapo choka kwa hiyo wameridhika.Lakini wanapata fidia kwa kuwatorosha watuhumiwa namna hii kesho wewe au mm tukiibiwa sijui itakuwaje bila kukata cha mtu mtuhumiwa utamwona anadunda uswazi kama kawa.
 
ndo hapo ninapo choka kwa hiyo wameridhika.Lakini wanapata fidia kwa kuwatorosha watuhumiwa namna hii kesho wewe au mm tukiibiwa sijui itakuwaje bila kukata cha mtu mtuhumiwa utamwona anadunda uswazi kama kawa.

Hapo wanashangaa nini wananchi wanapochukua sheria mikononi
 
mh hapa huyu mwizi anatoa siri kwa sababu aliporwa pia na waporaji wa raia wa nchi hii.
Kinacho nishangaza ni usemi bila kificho kuwa amekuwa anaiba kwa miaka 10 na hataacha maisha yake yote???????!!!!!!! na hapa tumsaidie vipi? maana is a next victim wa kifo asipoacha wizi.
 
mwizi.jpg

Mmoja wa mashahidi katika kesi ya mauaji inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Abdallah Zombe na wenzake, Bw. Shaban Manyanya, akiwa katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam, baada ya kutoa ushahidi wake jana. (Picha na Peter Twite).

View attachment 1673
 
Kwa hali hii ya rushwa, kazi ipo. Polisi anapomfuata jambazi kwenda gawana ngawira na vilevile kumshauri apotee hadi hali itakapotulia, tumekwisha!!!! Waziri Masha upo!!!!???

Unamuuliza Masha juu ya hili wakati na yeye ana yake ? Ama umesahau kuna mjadala hapa ? Tofauti ni kwamba wale wanatumia silaha na hata kuua Masha anaua pole pole huku kavaa suti .Nina maana ya yeye na Kampuni kuwa katika ufisadi .By the way Masha kesha fungua ile kesi iliyo vuma hapa siku za nyuma kwamba anaenda kufungua ?
 
Kwa hali hii ya rushwa, kazi ipo. Polisi anapomfuata jambazi kwenda gawana ngawira na vilevile kumshauri apotee hadi hali itakapotulia, tumekwisha!!!! Waziri Masha upo!!!!???

waziri Masha atakuwepo naye yumo ndani ya chama cha mafisadi? Nchi haina mwenyewe!!! Inasikitisha sana.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom