Majambazi Wakenya Walivyotikisa na Kuweka Historia Kanda ya Kaskazini Nchini Tanzania

ijue historia

Member
Nov 10, 2021
9
100
Kitabu bora cha UJASUSI na USALAMA kiitwacho "IJUE HISTORIA" chenye kurasa 470 kinachoongelea historia za UJASUSI, UPELELEZI, SIRI ZA DUNIA, UGAIDI na UHALIFU kimeshatoka na kinapatikana kwa sh 25,000 tu.

Pia kundi la "ijuehistoria" (WhatsApp group) lipo kwa gharama ya sh 3000 kwa mwezi.

Namba za mawasiliano na malipo ni - TIGO 0679 95 93 08 (namba ya Whatsapp pia)


SEHEMU YA KWANZA

UJAMBAZI MKUBWA BENKI YA NMB KILIMANJARO

Na. COMRADE SABOUR/ G.H. MASHERETO (Ijue Historia)

Hii ni makala ya ujambazi inayoongelea moja ya ujambazi mkubwa na wa akili nyingi sana kuwahi kutokea katika ardhi ya taifa la TANZANIA na kuongelewa sana wakati wake tukio hili likiwa limetokea maana lilisimamisha taifa kwa muda na vyombo vya ulinzi na usalama kuhangaika kila kona kudili na ujambazi huu.

Ujambazi huu mkubwa na wa akili nyingi sana ulitokea mkoani KILIMANJARO wilayani MWANGA ambapo washiriki wa ujambazi huu walikuwa wanatokea mataifa mawili tofauti ambayo ni KENYA na TANZANIA na ijulikane mataifa haya ni jirani sana kwa kupakana.

Ujirani mwema na undugu wa mataifa haya ambao unajulikana umeimarishwa na waasisi wao kwa TANZANIA ni MWALIMU JULIUS NYERERE na KENYA ni bwana JOMO KENYATTA ulitumika vibaya na hawa majambazi kwa kushirikiana kupanga na kutekeleza ujambazi huu katika benki kubwa ya NMB.

Majambazi hawa walichofanya katika benki ya NMB wilayani MWANGA imebaki kuwa historia inayokumbusha kipindi cha matukio mengi ya ujambazi nchini TANZANIA ambayo yalianza mwisho mwa karne ya 20 [1990’s] kuingia karne ya 21 [2000’s].

Kiufupi kipindi cha utawala wa raisi BENJAMIN MKAPA na JAKAYA KIKWETE vitendo vya ujambazi na uhalifu kwa ujumla vilikuwa vimeshamiri sana nchini TANZANIA na viongozi hawa waliotawala vizuri TANZANIA huu udhaifu wa kushindwa kukabiliana na ujambazi ulioshamiri vipindi vyao vya utawala hawawezi kuukwepa.

Kwenye uongozi na siasa ni jambo la kawaida kwa kila utawala kuwa na mazuri na mabaya yake [uimara na udhaifu wake], sasa hawa majambazi waliokwenda kuweka historia katika ardhi ya WAPARE pale wilayani MWANGA kiongozi “mastermind” wao alikuwa ni MKENYA.

MKENYA huyu alikuwa akijulikana sana kwa jina lake la utani MACHO MBAYA [MACHO MABAYA, Kiswahili cha KIKENYA hakiko vizuri], kwa miaka ya 2000’s nchini KENYA ukisikia jambazi MACHO MBAYA na genge lake wamepiga sehemu tukio ujue haukuwa tu uwizi wa unyang’anyi kwa kutumia silaha tu bali ni vita.

MACHO MBAYA na genge lake ujambazi wao ulikuwa ni vita kutokana na kutumia silaha za kivita kama AK-47 na mabomu kitu ambacho sio cha kawaida na genge hili la MACHO MBAYA walikuwa wakifanya hivi ili wahanga wao na jeshi la polisi wawaogope kwa kuwaona kama ukoma.

MACHO MBAYA na genge lake walikuwa wanajua kuzitumia silaha ipasavyo utafikiri wamewahi kupitia jeshi lolote na kupata mafunzo, na ukiachana na uwezo mkubwa wa kutumia silaha hizo pia MACHO MBAYA yeye binfasi ni mzuri wa mapigano ya ngumi na alivyopanda juu [mrefu] ndo kunamuongezea uimara katika mapigano ya ngumi.

MACHO MBAYA kiufundi nchini KENYA alikuwa ameshindika na anatafutwa sana na vyombo vya ulinzi na usalama vya KENYA kwa kesi zake nyingi za mauaji na ujambazi maana yeye haoni shida kuua pale kunapotokea kiwingu cha kutaka kumkwamisha ujambazi wake.

Sasa baada ya kusumbua sana KENYA akahamia nchini TANZANIA na wakati huo kulikuwa na wimbi kubwa la majambazi wa KENYA kuja nchini TANZANIA kushirikiana na majambazi wazawa wa huko kutekeleza ujambazi wao katika taasisi za kifedha ambako ni uhakika kuna fedha za kutosha hakuna ubahatishaji.

Jambazi kama MACHO MBAYA na genge lake kuamua kuja TANZANIA kutekeleza matukio ya ujambazi ilikuwa habari mbaya sana na hawakuwa wamekuja kwaajili ya tukio moja la benki ya NMB bali kwa matukio mengi yani walikuja kuweka kambi ndo maana walipitisha mzigo mkubwa wa silaha na mabomu.

MACHO MBAYA na genge lake kwa ubora wao uliopelekea kushindikana nchini KENYA wakakutana na ubora wa jeshi la polisi la TANZANIA ambao ulisaidiwa na kauzembe kadogo walichoteleza wakina MACHO MBAYA na kupelekea “WAR IN ARUSHA”.

KUZALIWA KWA WAZO

Kabla ya kuelekea kuona wazo la ujambazi huu mkubwa wa benki ya NMB ulivyozaliwa kwanza kabisa tumjue MACHO MBAYA ni nani…? ambaye ndo “mastermind” wa ujambazi huu nchini TANZANIA na hata matukio mengine ya ujambazi huko nchini KENYA.

Kwanza ifahamike MACHO MBAYA kwa majina yake halisi anaitwa SAMUEL GITAU SAITOTI amezaliwa mwaka 1973 katika kaunti ya KAJIADO katika jimbo la RIFT VALLEY na wengi wanajua au kudhani MACHO MBAYA ni mzaliwa wa kaunti ya NAKURU.

Sababu inayopelekea kudhani MACHO MBAYA ni mzaliwa wa kaunti ya NAKURU ni maisha yake ya umaarufu kama jambazi hatari kuenea akiwa kaunti ya NAKURU na alipapenda sana na kuwa kitovu chake cha ujambazi yani eneo lake la kujidai akisifika na kutukuzwa kama shujaa fulani kumbe jambazi tu.

MACHO MBAYA kabila lake ni MKIKUYU halisi na kabila la WAKIKUYU ndo kabila kubwa na lenye nguvu nchini KENYA kwa kutawala nyanja mbalimbali kisiasa, kibiashara, kiuchumi, kielimu n.k na MACHO MBAYA wakati akikua katika kaunti ya KAJIADO alikuwa mtoto mtundu na mjanja sana.

MACHO MBAYA shule kwake ilikuwa kama kituo cha polisi na alikuwa akisoma ili mradi iende sababu ya kulazimishwa na wazazi/walezi wake, na akiwa kijana baada ya balehe alibadilika kutoka kuwa mtundu kwenda mdokozi/kibaka [mwizi wa vitu vidogo].

Safari yake ya kwenda kuwa jambazi hatari iianzia hapo na wakati akizidi kuwa kijana mkubwa kipindi hicho miaka ya mwanzoni mwa 1990’s nchini KENYA na barani AFRIKA kwa ujumla kulikuwa na genge hatari sana lijulikanalo kama MUNGIKI.

Genge la MUNGIKI asili yake ilikuwa ni kabila la WAKIKUYU ambalo ndo kabila la MACHO MBAYA, kwa genge hatari hili kujihusisha na kila aina ya uhalifu nchini KENYA sio uwizi, sio mauaji, sio ubakaji, sio uuzaji wa mihadarati, sio vurugu n.k yani kila takataka ya uvunjifu wa amani ilikuwa ikifanywa na genge hili la WAKIKUYU.

Vijana wengi nchini KENYA hasa WAKIKUYU ambao wameamua kujihusisha na mambo ya kihalifu walikuwa wanapenda kujiunga na kundi la MUNGIKI maana ilikuwa ndo kundi hatari linaloogopeka mpaka na serikali ya KENYA na vyombo vyake vya ulinzi na usalama.

Pia ilikuwa fahari kwa kijana kujulikana au kujitambulisha yeye ni mwanachama wa MUNGIKI na MACHO MBAYA alianzia hapa ila alikuwa wale wanakundi wa ngazi ya chini kabisa ambao ndo wanatumika na viongozi wa MUNGIKI kutekeleza uvunjifu wa amani nchini KENYA.

Kwa ngazi ya kina MACHO MBAYA walikuwa wanapewa silaha za jada kama mapanga, visu, mashoka n.k na rasmi akawa amehama nyumbani kwa kuishi kwenye makambi na maghetto ya wanachama wenzie wa MUNGIKI na utumiaji wa vilevi na mihadarati kama bangi ulianzia hapa.

Maghetto na makambi ya MUNGIKI kulikuwa na mafunzo ya mapigano na ikumbukwe MUNGIKI ilikuwa mpaka na wanachama kutoka vyombo vya ulinzi na usalama ambao walichangia sana kutisha kwa genge hili kwa kuwa wakufunzi kwa vijana wa MUNGIKI ili wawe hatari sana.

Ubora wa mapigano kwa MACHO MBAYA ulitengenezwa hapa akiwa mwanachama mdogo wa MUNGIKI na toka ajiunge genge hilo hakukaa sana yeye na vijana wengine walipangiwa kazi jijini NAIROBI [mji mkuu wa KENYA] ambako ndo kulikuwa kitovu cha genge la MUNGIKI.

Hapo jijini NAIROBI genge la MUNGIKI lilikuwa likikusanya kodi kwa wafanyabiashara, wakazi wa uswahilini, MATATUS [usafiri maarufu nchini KENYA] n.k kama vile wao ni serikali na asiyekubali kutoa hela kwa MUNGIKI basi cha mtema kuni atakipata na hana pa kwenda kulalamika maana walikuwa tishio nchini humo.

Genge la MUNGIKI walikuwa na utawala wao ndani ya utawala wa serikali ya KENYA na waliokuwa wanaumia ni wanachi sababu kodi ya serikali iko palepale kwahiyo kunalipwa kodi mara mbili na bora kodi ya serikali isilipwe kwa mlipaji kodi kufanya janja janja ila sio kodi ya MUNGIKI ambayo ni lazima na haitakiwi masihara kabisa.

Sasa MACHO MBAYA yeye jijini NAIROBI alikuwa amepangiwa kukusanya kodi kwa magari ya MATATUS akipozi kama mpigaji debe kwa kushinda kwenye vituo vikuu vya usafiri akifanya kazi ya genge lake na kipindi hicho hicho wamiliki na waendeshaji wa MATATUS walikuwa ni mamafia kwa kujihusisha na vitendo vya kihalifu.

Ndo maana leo hii ukipitia rekodi ya majambazi wakubwa na tishio katika historia ya taifa la KENYA unakuta wengi wao chimbuko lao walianzia kwenye familia kama wamiliki, madereva, makonda au wapigaji debe wa MATATUS na mfano ni jambazi hatari WACUCU n.k

MACHO MBAYA kutokana na kuwa karibu na jumuiya ya MATATUS alivutiwa na namna mamafia hao wanavyofanya uhalifu wao na baada ya hapo kila mtu anapata gawio lake huku wakiendelea na biashara ya usafiri huo tofauti naMUNGIKI jinsi ilivyokuwa ikijiendesha.

MUNGIKI waliokuwa wanafaidi ni viongozi wao wa chini wanatumika tu kuzalisha mapato kwaajili ya wakubwa zao na kubakia maskini maisha yao yote na ikitokea vurugu zozote wanatangulizwa wao kwa kukamatwa, kujeruhiwa au kuuliwa huku viongozi wanakula kuku kwa mrija.

Kwa MUNGIKI hakukuwa na usawa ila kwa MATATUS angalau kulikuwa na usawa na MACHO MBAYA akaona isiwe tabu akajihusisha na jumuiya ya MATATUS na kwa sifa zake za kimuonekano ziliwatia hamasa WANAMATATUS kumuona mali.

MUNGIKI walikuwa na utaratibu wa kuua wanachama wao wanaojitoa sababu sheria yao mtu akijiunga MUNGIKI kitakachomtenganisha na kundi hilo ni kifo na MACHO MBAYA alikuwa anajua hilo ila sheria hiyo ilikuwa ikitekelezeka kwa viongozi wa MUNGIKI hao wanachama wa chini mpaka awe msaliti na wajue ndo watamuua.

MACHO MBAYA alikuwa mwanachama wa chini hakuna anayemzingatia na akaachana na MUNGIKI kwa kujiunga na familia ya MATATUS ambapo alikabidhiwa basi na kuwa dereva na rasmi akawa mwanafamilia wa MATATUS kuweza sasa kuhusishwa na umafia wa familia hiyo ya usafiri maarufu nchini KENYA.

MACHO MBAYA alikuwa dereva na mhalifu hapo hapo na matumizi ya silaha za moto kama bunduki, mabomu alianza kujifunzia kutoka kwa familia yake mpya hiyo na pia alijifunza uwizi mkubwa zinafanyikaje huku kichwani mwake akiwa na ndoto siku aje kujitegemea kwa kuanzisha kundi lake binafsi.

MACHO MBAYA muda mfupi toka ajiunge na familia ya MATATUS alijiona kule MUNGIKI alikuwa akijichelewesha maana sasa anajua uhalifu ule ambao alikuwa akiutaka sio mambo ya vurugu kutawala sana, kusumbuana na kukusanya kodi n.k

MUNGIKI walikuwa wakifanya kila aina ya uvunjifu wa amani ila ya uwizi ilikuwa chini na matukio madogo yakulinganishwa na ukibaka sio wa kutekeleza matukio makubwa kama uwizi katika mabenki, utekaji magari, n.k ndo maana MUNGIKI walikuwa wakitegemea ukusanyaji wa kodi.

MACHO MBAYA akiwa anajifunza huku akijishughulisha na uhalifu wa maana sio wa ukibaka kulianza kutokea mzozo kati ya wamiliki na waendeshaji wa MATATUS dhidi ya MUNGIKI na kikubwa hapo ni wanafamilia wa MATATUS kuchoshwa na kodi wanazochajiwa na MUNGIKI halafu hapo hapo tena serikali nao wanawakamua.

Wanafamilia wa MATATUS wao ni mamafia sasa kwanini waendelea kuwachekea genge la MUNGIKI hata kama ni wazuri kwenye vurugu na uwingi wao, wanafamilia wa MATATUS wakasitisha kutoa chochote kwa genge la MUNGIKI na wako tayari kwa vita yoyote dhidi yao.

Mwaka 2002 vita waliyokuwa wako nayo tayari wanafamilia wa MATATUS ilianzishwa na MUNGIKI na ilikuwa hatari sana kwa kuuana, kujeruhiana na kukamatwa na polisi ambao walikuwa wakivamia kutuliza ghasia hizo sababu zilikuwa zinaathiri mpaka wananchi wa kawaida.

Vurugu hizi zilipelekea serikali ya KENYA na vyombo vyake vya ulinzi na usalama kuamka na hali ya amani ikawa chini maana operesheni kali iliendeshwa ya kukamata kwa malundo wanachama wa pande zote mbili na MACHO MBAYA akaona hali ishakuwa tete na kukimbilia kaunti ya NAKURU.

Hapo kaunti ya NAKURU alifikia mji wa NAVASHA na vurumai zilizotokea jijini NAIROBI kati ya MUNGIKI na wanafamilia wa MATATUS ilikuwa tiketi ya MACHO MBAYA kuanzisha utawala na genge lake mwenyewe kwa vijana wenzie kutokea pande zote mbili zilizokuwa zinagombana na kukimbia kama yeye kuwasajili na kuwa kiongozi wao.

Utawala wa kihalifu wa MACHO MBAYA ulianzia mwaka 2003 na aliweza kushawishi vijana wenzie kujiunga naye kutekeleza matukio ya kihalifu kwa kuachana na magenge ya wanafamilia wa MATATUS na MUNGIKI ambao wapo kwenye bifu kubwa sana.

Vijana waliokuwa tayari walimfuata MACHO MBAYA huku wengine walishindwa kushawishika naye sababu ya ugeni wake katika uongozaji wa kundi la kihalifu, MACHO MBAYA na genge lake walianza na uhalifu wa utekaji magari katika barabara kuu ya NAIVASHA-NAIROBI kujipatia fedha za kuweza kununua silaha zitakazotumika kwa ujambazi mkubwa.

Silaha za kufanyia uhalifu wao walikuwa wanazichukua kimagendo kutoka nchini SOMALIA ambako kulikuwa na migogoro na mapigano yasiyoisha toka mwaka 1991 na kupelekea uwepo wa silaha nyingi nchini humo na rahisi kwa wahalifu wa mataifa ya jirani kwenda kununua huko.

KENYA na SOMALIA ni nchi jirani na silaha huko nchini SOMALIA ni bei ya chini sana sababu zipo nyingi sana na muda mwingine wanunuzi wa silaha za kimagendo hizo wanabadilishana na vitu kama vyakula kwa silaha kutokana na hali ya njaa iliyopo nchini humo kwa WASOMALI kukosa muda wa kuzalisha chakula.

Hii sio SOMALIA tu ni mataifa yote ambayo yamegubikwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe kama BURUNDI, RWANDA, KONGO, SUDAN n.k kumekuwa na silaha bwelele na wahalifu wa mataifa jirani hutumia fursa kununua kutoka mataifa hayo kwa bei ya chini.

MACHO MBAYA soko rahisi la silaha nchini SOMALIA alilijua kupitia wanafamilia wa MATATUS kwa kujua wauzaji wa nchini SOMALIA, bei kwa kila aina ya silaha na mifereji ya kupitisha silaha hizo kutoka nchini SOMALIA kuja KENYA ambapo kulikuwa na mawakala rasmi wa kazi hiyo hupitisha silaha za wateja tofauti na wanajua ni vipi wanawapooza wanausalama na walinzi wa mpakani.

Kipindi hicho KENYA alikuwa hajaimarisha ulinzi na ukaguzi mkali mipakani mwa taifa lake na SOMALIA sababu AL-SHABAB ilikuwa haijazaliwa bado migogoro na mapambano yalikuwa hayahusishi makundi ya KIISLAMU yenye msimamo mkali kwahiyo uingizaji wa silaha ulikuwa sio mgumu kama miaka ya sasa.

MACHO MBAYA na genge lake mwaka huo huo 2003 wakiwa na silaha nzito baada ya mzigo kuwafikia kutoka nchini SOMALIA walianza utekelezaji wa ujambazi mkubwa wa pesa nyingi kwa kulenga taasisi za kifedha kama mabenki, maduka ya kubadilisha fedha n.k

Genge la MACHO MBAYA walianza na duka moja kubwa la kubadilisha fedha jijini MOMBASA liitwalo FORT JESUS na walichagua hili duka sababu ya kupatiwa taarifa kuwa linamzunguko mkubwa wa fedha kutokana na wateja wengi kubadilisha fedha zao dukani hapo.

Genge la MACHO MBAYA wakavamia duka hilo na kutekeleza ujambazi wao ambao ulifanikiwa na kuwa mwanzo mzuri kwa genge la MACHO MBAYA maana sasa wakawa na hela ya kutosha zaidi kuweza kuagiza mzigo mkubwa zaidi wa silaha na mambo mengine kama kula bata.

Kufikia mwaka 2005 genge la MACHO MBAYA lilikuwa hatari sana nchini KENYA na mtu ajulikanae MACHO MBAYA akawa midomoni mwa vyombo vya ulinzi na usalama huku wakiwa hawamjui sura yake bado ila jina lake walilisikia sana kama jambazi chipukizi hatari anayekuja kwa kasi ya 5G.

Nchini KENYA miaka hiyo ilikuwa kama TANZANIA kugubikwa na matukio makubwa ya kihalifu pamoja na majambazi sugu wenye majina yao na kwa mwaka 2005 jambazi MACHO MBAYA alikuwa akionekana kama jambazi sugu chipukizi maana kulikuwa na majambazi kama SILAS MUGENDI NJERU, GODFREY MULWA KITHEKA n.k

Na hao majambazi wakubwa waliokuwa na majina wakina SILAS MUGENDI NJERU walikuwa gerezani ila bado vitendo vya kihalifu vilikuwa vikishamiri na kuambiwa kuna jamaa mmoja anaitwa MACHO MBAYA ni hatari ndiye anayesumbua taifa la KENYA na genge lake kwa kupiga matukio ya kihalifu miji mbalimbali nchini humo.

MACHO MBAYA na genge lake kuwa hatari na tatizo jipya nchini KENYA mwaka huo huo 2005 walikwenda kuweka rekodi na kujisimika yeye na genge lake sio majambazi chipukizi tena bali majambazi sugu wanaotakiwa kuzimwa haraka na vyombo vya ulinzi na usalama nchini humo kwa usalama wa raia na mali zao.

Tukio hilo lilikuwa kwenda kuvamia gereza la EMBU GK na kutorosha wafungwa ambao ndani yake kulikuwa na vijana wake ambao walikuwa wamekamatwa na kuhifadhiwa humo na ndo hao baada ya kuhojiwa walimtaja kiongozi wao ni MACHO MBAYA na jina hilo kuanza kutamkwa sana midomoni mwa polisi wa KENYA.

Wazo la kuokoa vijana wake pamoja na wafungwa wengine gerezani EMBU GK halikuwa lake kwa yeye tayari kunyoosha mikono juu kuwa amepoteza hao vijana wake na anasajili vijana wengine kuziba mapengo yao kama vile magenge mengine ya kihalifu mwanachama akishatiwa nguvuni na vyombo vya ulinzi na usalama ndo basi hawamuhesabii tena labda aje kuachiwa kama hatafungwa kifungo cha maisha au kunyongwa.

Kwa kesi ya vijana wake MACHO MBAYA ilikuwa nitolee sababu walikuwa na mashtaka ya mauaji ya polisi na raia, wazo la kuvamia gereza lililetwa na jambazi sugu SILAS MUGENDI NJERU ambaye tarehe 22 juni 2005 na wenzie walitoroka gereza la SHIMO LA TEWA.

Wakina SILAS MUGENDI NJERU hawakutoroshwa na mtu ni wenyewe wakiwa gerezani walijipanga na kutoroka, na baada ya tukio hili jambazi sugu NJERU akataka kurudisha utawala wake wa ujambazi ila akakutana na ugumu wa genge lake kusambaratika kwa wengine kuwa magerezani na wengine wameanzisha magenge yao hawawezi tena kuwa chini yake.

Jambazi NJERU alionekana zama zake zimeshaisha baada ya kukamatwa na kufungwa gereza la SHIMO LA TEWA na sehemu ya watu wake wakina MBURU, WATHIGO, KARIUKU, n.k tayari walikuwa majambazi wa kimataifa hawashikiki.

Hao waliokuwa wanakundi wa jambazi NJERU mwaka 2004 walikuwa wametoka kufanya tukio la kihistoria nchini TANZANIA mkoani KILIMANJARO wilayani MOSHI katika benki ya NBC kwa kuiba kiasi kikubwa cha fedha katika historia ya taifa la TANZANIA ambacho kilikuwa shillingi bilioni 5.3.

Sasa majambazi wake wameshiriki katika uwizi mkubwa kama huo na wako vizuri kifedha waanze kumfikiria jambazi NJERU tena ambaye hapo alipo anatafutwa sana kwa kutoroka gerezani, ilikuwa ngumu sana kwa kuhesabika zilipendwa.

Jambazi NJERU akaona namna pekee ni kutorosha watu wake walioko magerezani kwa kuachana na hao ambao wameshaota mapembe na aliamini utawala wake utarudi sababu hao atakaowatorosha watamuona yeye kama Mungu mtu kuwaepusha na kifungo cha maisha au kunyongwa mpaka kufa kwa makosa yao ya ujambazi na mauaji.

Gereza ambalo lina watu wake lilikuwa EMBU GK na kuona hapo ndo pakuchorea mchoro kwenda kukomboa watu wake wawe huru tena na arudishe utawala wake wa ujambazi, na baada ya kulichagua gereza hilo ambalo ndo lenye majambazi wenzie wamefungwa akaona bado kuna shida moja ambayo ni hawezi mwenyewe kufanya tukio hilo kubwa ikizingatiwa na yeye ametoroka gerezani na anatafutwa sana na vyombo vya ulinzi na usalama.

Jambazi NJERU akamkumbuka jambazi MACHO MBAYA ambaye ndo alikuwa kwenye ubora wake na wanajuana kiasi fulani kwa kuweza kumshawishi washirikiane katika uvamizi huo gerezani EMBU GK na pia itakuwa fursa kwake MACHO MBAYA kutorosha vijana wake waliokamatwa na kufungwa gerezani humo.

Jambazi MACHO MBAYA kufuatwa na jambazi NJERU kuelezewa tukio hilo la uvamizi gerezani EMBU GK alikubali na kwa pamoja wakakaa chini kuandaa mchoro wa tukio hilo na uzoefu wa jambazi NJERU kukaa gerezani ulisaidia kuandaa mchoro mzuri kuhakikisha wanawakomboa majambazi wenzao.

Kila kitu kuwa sawa ikabaki kuvamia gereza la EMBU GK na mwezi agosti ndo ilikuwa utekelezaji wa mchoro wao na mashuhuda wa tukio hili wanasema ilikuwa kama wanaangalia filamu za HOLLYWOOD kumbe ndo uhalisia wenyewe na kuamini kinachoigizwa kwenye filamu za nje kinawezekana kutendeka.

Kwanza watekelezaji wakina MACHO MBAYA walikuwa na silaha za kutosha pamoja na mabomu kuhakikisha wanachopeleka gerezani EMBU GK ni vita kwa kujizungusha mikanda ya risasi ili wawe wanamimina tu na katika mchoro wao walishajua wanakamata wapi kuhakikisha gereza la EMBU GK linakuwa chini yao.

Grereza la EMBU GK ni kama magereza mengine duniani kwa askari magereza wanaoshika silaha za moto wanakuwa wale wa lango kuu la kuingilia gerezani pamoja na wale wa mnarani ila askari magereza wengine wanakuwa na silaha za jadi kama rungu, manati n.k ambazo hutumia kutuliza ghasia za wafungwa pale kunapotokea vurumai gerezani.

Ni sawa kuwa hivyo sababu ya mazingira ya gerezani kwa wafungwa kotukuwa na hatarishi yoyote kufanya askari magereza wote kutembea na silaha za moto na hiyo hali wakina MACHO MBAYA walitembea nayo wakijua nani anakuwa na silaha za moto kuweza kupambana naye kwanza na pia kuwahi kukimbilia ghala la silaha ili askari magereza wasikimbile kwenda kuchukua silaha .

Askari magereza wengi kutoshika silaha za moto haimaanishi hakuna silaha za moto za kutosha magerezani, na ikitokea kuna tukio kubwa limetokea gerezani linalohitaji silaha za moto kushikwa na askari wote basi haraka huelekee kwenye ghala lao la silaha ambako wanapewa silaha za moto hizo na huko ndo wakina MACHO MBAYA walipanga kupawahi kukamatwa wakishazama gerezani ili kujihakikishia hawapati upinzani wa ziada.

Siku ya tukio wakina MACHO MBAYA wakiwa na silaha wakafika gerezani EMBU GK wakiwa kamili na kufika getini ambako lazima ukaguzi ufanyike wakashuka na mitutu yao na kuanza kumimina kusafisha njia ili wazame gerezani ndani.

Wakina MACHO MBAYA walikuja kibabe hakuna stori wala kuchekeana ni wanamimina tu na polisi magereza mpaka wenye silaha walitupa na kukimbia kusikojulikana kwa wengine kujifungia majumbani mwao, wengine kuparamia ukuta na kutoroka n.k

Wakina MACHO MBAYA waliwasawazisha na sababu lilikuwa tukio lisilotegemewa kwa askari magereza ni walikuwa kama wamechanganyikiwa na ghala la silaha kama mchoro wao ulivyosema lilidhibitiwa na askari magereza aliyekuwa zamu ghalani hapo aliuliwa.

Wakina MACHO MBAYA hawakuhangaika na askari magereza waliokuwa wakikimbia kuokoa maisha yao sababu sio lengo lao, wenyewe walielekea moja kwa moja kwenye vyumba vya magereza kuwafungulia majambazi wenzao na wafungwa wengine waliobahatika.

Wafungwa waliokombolewa walikabidhiwa silaha hapo hapo kwaajili ya kujihami na wakateka magari ya askari magereza ili kuwapakia wenzao na kuondoka eneo la tukio wakiwa wameacha vifo vya watu wanne huku mmoja wao akiwa jambazi mwenzao waliyezama naye ndani.

Tukio hili lilikuwa aibu kwa taifa la KENYA na kuonesha majambazi wamewashindwa mpaka wanakuja kuwaokoa wenzao gerezani humo na mbaya zaidi matukio hayo ya wafungwa kutoroka mikononi mwa jeshi la magereza kwa kutoroka wenyewe au kutoroshwa na wenzao yalikuwa yamefuatana toka mwaka 2004 mpaka mwaka huo 2005 ila hakuna mabadiliko kwa vyombo vya ulinzi na usalama kuzuia matukio hayo ya aibu.

Mwaka 2004 kulitokea matukio mawili ya utorokaji wafungwa ambayo yalikuwa ya gereza la NAVASHA ambalo linahesabika ni gereza lenye ulinzi mkali zaidi ila wafungwa wapatao 28 walitoroka tena wale walioshindikana ambao ingekuwa hiari yao KENYA basi wangewaua ili roho zao zipumzike kuwa wasumbufu wao hawapo tena duniani.

Tukio la pili lilikuwa utoroshwaji wa wafungwa 29 wakiwa mahabusu ndogo ya mahakama ya MERU wakisubiria kesi zao kusikilizwa na wale wale wanaotoroshwa ni majambazi na wauaji ambao hawana la kupoteza sababu wanajua hata wakibaki mikononi mwa mamlaka za magereza vifungo vyao ni maisha jela au kunyongwa mpaka wafe.

Kwahiyo mwaka 2004 na 2005 nchini KENYA kuachana na matukio ya ujambazi yaliyokuwa yanaendelea pia mchezo wa wafungwa kutoroka au kutoroshwa ulikuwepo na habari tena ya raia wao kutekeleza uwizi wa kihistoria nchini TANZANIA pale benki ya NBC ulizidi kuwachanganya kuona wao sasa wamegeuka chuo cha ujambazi AFRIKA MASHARIKI NA KATI.

Sifa hiyo ya KENYA kuwa chuo cha ujambazi AFRIKA MASHARIKI NA KATI ilikuwa ya kweli maana sio TANZANIA tu hata UGANDA, KONGO, MSUMBIJI n.k kote huko wanalia na majambazi wa KENYA kuja kushirikiana na majambazi wa mataifa yao kutekeleza ujambazi mkubwa.

Hapo mwaka 2005 gereza la EMBU GK limeshavunjwa na kutoroshwa wafungwa miezi miwili mbele wale majambazi wake wa zamani NJERU ambao walihusika na ujambazi wa bilioni 5.3 NBC MOSHI TANZANIA walikwenda nchini MSUMBIJI kwaajili ya kuumiza na huko tena yani hawapoi wala kuridhika.

Hii tabia ya majambazi wa KENYA kutorosha wenzao magerezani au mahakamani walijaribu kuleta TANZANIA kuokoa majambazi WAKENYA wenzao kupitia vyoo vya mahakama wakidhani ni rahisi kama ilivyokuwa kwao kwa kusahau au kutojua vyombo vya ulinzi na usalama vya TANZANIA ni vinara wa ujasusi.

Vyombo vya ulinzi na usalama vya TANZANIA vilitoa funzo jinsi ya kudili na majambazi wanaotaka kujaribu visivyojaribika maana kitendo cha uwokozi wa wafungwa sugu walioshindikana ni hatari sana kwa usalama wa raia na mali zao, pia ni aibu kubwa sana isiyoelezeka ambayo kwa nchi zilizoendelea lazima viongozi wahusika watajiwashibisha wenyewe kupunguza aibu hiyo.

Kwa taifa la KENYA wahusika walikaa kimya kama hakujatokea jambo huku nguvu kubwa ikitumika kupoozesha tukio hilo la uvamizi gerezazi EMBU GK na KENYA walichofanya ndo mataifa mengi ya AFRIKA hufanya kwa kutotaka kuwajibika na badala yake huminya vyombo vya habari visieleze ukweli jamii ni kilitokea kwa undani na wapi uzembe ulifanyika.

Jambazi NJERU na MACHO MBAYA jambo lao lilitiki na kila mmoja aliendelea na mambo yake na watorokaji wake huku vyombo vya ulinzi na usalama vya KENYA vikiwa vimechachamaa kusaka wavamizi na watorokaji gerezani huku wakiwasihi wafungwa waliotoroka wajisalimishe wenyewe kabla nguvu kubwa haijatumika na kujitengenezea kesi nyingine mpya.

Kwenye utoroshaji wa wafungwa kuna wafungwa ambao hawakuwa kwenye orodha ya jambazi NJERU na MACHO MBAYA kutakiwa kutoroka, ni wenyewe walitumia nafasi ya sintofahamu iliyotokea gerezani baada ya uvamizi kutoroka kusikojulikana na hawakuangana na timu ya majambazi waliokuja kuvamia gereza la EMBU GK na ndo hao walikuwa wakishauriwa kujisalimisha ili kuwapunguzia kazi vyombo vya ulinzi na usalama wabaki kudili na masugu.

Vyombo vya ulinzi na usalama kwa tukio hili la uvamizi wa gereza la EMBU GK liliweza kumjua jambazi MACHO MBAYA vizuri mpaka muonekano wake na kuingizwa kwenye orodha ya watu wanaohitajika sana, na jeshi la polisi walikuwa wametangaza vita dhidi yake.

MACHO MBAYA kujua amewekwa kwenye orodha ya watu wanaohitajika sana hakujali hilo aliendelea na matukio yake ya ujambazi na pia aliona fahari kupata umaarufu hasi huo, na matukio yake mengine makubwa na maarufu aliyoyaongoza ni mwaka 2006 alifanya ujambazi jijini MOMBASA na kuua askari wawili.

Tukio hili la MOMBASA lilisikitisha na kukasirisha sana jeshi la polisi kwa kupoteza nguvu kazi yao kwa mtu hatari wanayehangaika kumtafuta usiku na mchana nchini humo, na MACHO MBAYA na genge lake walikuwa wanafanya kama kulipiza kisasi kutokana na polisi kuendesha operesheni ya kuua majambazi sugu yani hata wakiwa kwenye nafasi nzuri ya kuwakamata au kusalimu amri ni wanawaua.

Kipindi hicho KENYA ilikuwa ikisikika majambazi sugu yaliyoshindikana yameuwawa na sio kukamatwa hai na kupelekwa mahakamani, tukio lingine kubwa na maarufu MACHO MBAYA na genge lake walitekeleza mjini NJORO kaunti ya NAKURU tarehe 4 januari 2007.

Tukio lingine kubwa na maarufu zaidi ambalo lilikuwa la mwisho kwa MACHO MBAYA na genge lake nchini KENYA lilikuwa jijini MOMBASA katika benki ya HABIB tarehe 17 januari 2007 na ndo tukio la kihistoria kwa genge la MACHO MBAYA nchini KENYA.

Kihistoria kwa tukio hili, ni tukio la ujambazi ambalo genge la MACHO MBAYA waliiba fedha nyingi ambazo zilikuwa shillingi za kitanzania zaidi ya milioni 700 kwa kutowahi kuiba fedha nyingi kwa tukio moja toka kuanzisha utawala wake wa ujambazi mwaka 2003.

Tukio hili la ujambazi ndo tukio pekee kwa genge la MACHO MBAYA kutumia akili nyingi kuliko nguvu maana walikuwa na silaha ila hawakuzitumia na kuacha vyombo vya ulinzi na usalama kushindwa kung’amua akili kubwa iliyotumika na genge lake.

Tukio hili jambazi MACHO MBAYA alishirikiana na wafanyakazi ndani ya benki hiyo ambao ndo walimtaarifu tarehe 17 januari 2007 kuna fedha nyingi zinaletwa ndani ya benki hiyo jioni kabla ya benki kufungwa na wao wavizie muda huo kuondoka na mzigo mkubwa huo wa fedha.

Siku na muda kufika genge la MACHO MBAYA walifika eneo la tukio na wafanyakazi wa benki waliokula nao dili wakazima mfumo wa kamera ili tukio lisirekodiwe na muda mchache kabla ya benki kufungwa majambazi wawili wakaingia benki wakivizia kuwa wa mwisho ambapo benki huwa inafunga mlango kwa mteja mwingine yoyote asiingie ndani kwa wale wateja waliopo ndani ndo watahudumiwa wa mwisho na benki kwa siku hiyo itafungwa.

Walinzi wako nje hawajui kiendeleacho ndani na wanajua muda wa wateja kuruhusiwa kuingia benki umeisha wakawa hawana presha ya ulinzi na hali ya ulinzi mkali ikasizi huku wakisubiria kwa hamu gari la kubadilisha zamu kupita ili waondoke na wenzao wengine waingie lindo.

Sasa wakati majambazi wawili wako ndani huku nje majambazi wengine wawili kwa msaada wa wafanyakazi wa benki waliwachorea njia rahisi ya kuingilia mlango wa siri ambao unajulikana na benki ya HABIB pekee, na mlango huo unawapeleka kweye ushushaji wa fedha zilizoletwa ndani ya benki na huko kunaaminika usalama ni mkubwa sana kwahiyo hakuhitaji walinzi na mitutu yao.

Majambazi kufika kwenye ushushwaji wa fedha wakawadhibiti wahusika kimya kimya na kuchukua mzigo kiulaini na kuelekea eneo la kuhudumia wateja ambako waliwakuta wenzao wameshawaweka chini ya ulinzi watu wote waliobakia nao na kutoka wote kama wateja waliomaliza kupata huduma yao ndani na walinzi hawakuwahisi vibaya sababu wao tayari wanafikiria kuondoka majumbani kwao wakapumzike.

Tukio la ujambazi linakuja kushtukiwa tayari wakina MACHO MBAYA wameshapotea eneo la tukio bila ghasia yoyote na baadae uchunguzi kufanyika ndo vyombo vya ulinzi na usalama vikagundua genge la MACHO MBAYA limehusika na ujambazi huo kwa kushirikiana na wafanyakazi wa benki wasio waaminifu.

Jambazi MACHO MBAYA na genge lake baada ya kujulikana wamehusika tena na ujambazi mkubwa huo nguvu zaidi ziliongezwa na vyombo vya ulinzi na usalama vya KENYA kupambana na genge hilo na baadhi ya vijana wake MACHO MBAYA waliuliwa na kukamatwa maana msako ulikuw hatari sana.

Huku mlengwa mkuu hapo akiwa jambazi MACHO MBAYA ambaye ndo vyombo vya ulinzi na usalama vya KENYA vilikuwa vinamtamani sana wagawane mwili wake kutokana na jinsi alivyowatesa na kuwasumbua na matukio yake ya ujambazi.

MACHO MBAYA na genge lake ambao alibakia nao walikuwa wanahama miji leo NAIROBI, kesho KISERIAN, kesho kutwa MOMBASA n.k, ni hawatulii sehemu moja kuhofia kukamatwa au kuuliwa na wakati MACHO MBAYA na wenzie wanahama hama hivyo vichwani mwao kukazaliwa wazo kwanini wasihamishe harakati zao za ujambazi nchi jirani ambayo ni TANZANIA.

Pia matokeo mazuri ya matukio ya ujambazi yaliyokuwa yanafanywa na majambazi wenzao WAKENYA huko nchini TANZANIA kwa kushirikiana na wazawa wa huko walikuwa wakiyasikia sana yakitekelezwa na kufanikiwa katika mikoa ya ARUSHA, KILIMANJARO na DAR ES SALAAM, sasa wakaona kwanini na wao wasiwe sehemu ya historia hiyo ya majambazi WAKENYA kutekeleza na kufanikiwa matukio yao ya ujambazi nchini TANZANIA .

Wao wakina MACHO MBAYA walijua wakihamia huko watakuwa kama wamezaliwa upya sababu hawana rekodi yoyote ya ujambazi nchini TANZANIA wala kutafutwa na vyombo vya ulinzi na usalama vya TANZANIA, na hapa kuzaliwa wazo la kuhamia nchini TANZANIA ndo mwanzo wa kuzaliwa wazo la ujambazi mkubwa benki ya NMB wilayani MWANGA mkoani KILIMANJARO.

Wazo la kuhamia nchini TANZANIA limezaliwa ila kukubaliana kwa genge la MACHO MBAYA ilikuwa bado na nani atakuwa mwenyeji wao nchini TANZANIA ni moja ya swali gumu sana kwao maana majambazi wote wa KENYA wanaokuja kutekeleza matukio yao ya ujambazi nchini TANZANIA au mataifa mengine jirani lazima wawe na wenyeji.

Sio rahisi wao wenyewe waamke na kuhamia nchini TANZANIA au nchi nyingine na kujiongoza kutekeleza ujambazi sababu wanakuwa wageni na muda wa kukaa na kuzoe mazingira ili wawe wenyeji hawana sababu ya haraka kutaka kufanya matukio yao ya ujambazi au kuhofia kuhisiwa vibaya na vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi husika waliyokwenda.

Sababu bado genge la MACHO MBAYA hawajakubaliana kwahiyo swali gumu hilo la mwenyeji wao nchini TANZANIA kulipuuzia kwanza mpaka wazo lipitishwe na wote, genge la MACHO MBAYA wakakaa kikao kujadili wazo lililozaliwa kwa kuangalia faida na hasara za kuhamisha harakati zao za ujambazi nchini TANZANIA.

Pia kuangalia nchi mbadala kama TANZANIA itakuwa na hasara nyingi upande wao na kikao kizito kukaliwa na majadaliano ya hapa na pale kwa kila mwanagenge wa MACHO MBAYA kutoa uzoefu wake juu ya taifa la TANZANIA kwa namna anavyolijua basi mwishoe wazo likapitishwa kwa wote watahamia nchini TANZANIA kuwaletea vita maana ujambazi wao ni kama vita afe kipa afe beki
 
SEHEMU YA PILI

Wazo kupitishwa ndo mwanzo wa kurudi tena swali gumu lile la mwenyeji wao atakuwa nani nchini TANZANIA maana jamaa waliyemzoea na kufanya naye biashara za kihalifu nchini TANZANIA hakuwa duniani tena baada ya kuuliwa na polisi jijini ARUSHA.

Jambazi huyu alikuwa akijulikana kama FRANK LYATUU mkazi wa NGARAMTONI na mmoja wa majambazi sugu walioshindikana jijini ARUSHA na mhusika wa tukio kubwa la ujambazi jijini DAR ES SALAAM lililofanyika UBUNGO MATAA na kujulikana kama UWIZI MKUBWA UBUNGO MATAA.

UWIZI MKUBWA UBUNGO MATAA ni ule uwizi uliotokea tarehe 20 aprili 2006 pale kwenye makutano ya barabara ya MOROGORO na SAM NUJOMA jijini DAR ES SALAAM kwa fedha za benki ya NMB kuibiwa wakati zinasafirishwa kwenda mkoani MOROGORO (REJEA MAKALA YA UJAMBAZI MKUBWA UBUNGO MATAA)..

Sasa genge la MACHO MBAYA walikuwa wakishaiba magari nchini KENYA wana msogezea jambazi LYATUU jijini ARUSHA ayauze na hivyo hivyo magari yakiibiwa nchini TANZANIA yanasogezwa KENYA kwakina MACHO MBAYA kuuzwa, ni wanayavusha ili iwe ngumu kwa wamiliki walioibiwa au vyombo vya ulinzi na usalama kuyapata tena.

Kwenye nchi zote mbili za TANZANIA na KENYA kulikuwa na gereji ambazo kazi zake zilikuwa zinapokea magari ya uwizi na kuyabadilisha vitu muhimu kama rangi n.k ili yaingizwe sokoni na mmiliki wake akionyeshwa ndo hili gari lako anakataa sababu limebadilishwa na kuwa jipya machoni mwake.

Miaka ya nyuma kidogo uwizi wa magari ulishamiri sana na kuwa yanavushwa upande tofauti [KENYA au TANZANIA], sasa genge la MACHO MBAYA mshirika wao LYATUU hayupo ambaye ameuwawa mwaka 2006 katika zile operesheni za kutafuta majambazi wa UWIZI MKUBWA UBUNGO MATAA.

Kwahiyo wakina MACHO MBAYA wakaona hawawezi kukosa mshirika nchini TANZANIA na kuanza kumtafuta mtu wa kuaminika kama vile jambazi LYATUU, shida iliyokuwepo ni wakina MACHO MBAYA walikuwa wanataka mtu wa kuaminika sana kwaajili ya usalama wa shughuli zao za ujambazi nchini TANZANIA ila watu wanaofahamiana nao ni wengi sema ndo hawaaminiki sana.

Moja ya sababu zinazofelisha majambazi wengi na kuishia kukamatwa au kuuliwa ni washirika wao au wenyewe kwa wenyewe kukosa uaminifu hasa tamaa inapozalia baina yao na mwishoe wote wanaishi pabaya na kuwa wapotezaji.

Zoezi la kutafuta mshirika nchini TANZANIA lilifanyika kupitia wale watu wanaofahamiana nao ila ndo hawaamini kama vile walivyokuwa wanamuamini jambazi LYATUU ila inabidi waanze kuaminiana nao maana jambazi LYATUU kashauliwa hatarudi tena duniani na kikubwa ni kuwachambua na kuanza kuimarisha bondi [mahusiano] nao.

Washirika kutoka TANZANIA ambao waliona wanaweza kuchukua nafasi ya jambazi LYATUU ni bwana mdogo mmoja aitwaye SAMSON CHONJO aliyezaliwa mwaka 1981 na kipindi hicho mwaka huo 2007 alikuwa na umri wa miaka 26, ni kijana mdogo tu.

SAMSON CHONJO alikuwa ni mkazi wa NGULELO wilayani ARUMERU mkoani ARUSHA na kikazi alivyokuwa anatambulika ni dereva wa magari ya utalii na pia mwongoza watalii “TOUR GUIDE” sehemu za kutalii mkoani ARUSHA.

Mshirika mwingine wa pili alikuwa ni KALISTI JOSEPH KAMILI KISAMBU KANJE aliyezaliwa mwaka 1960 ambaye kipindi hicho mwaka huo 2007 alikuwa na umri wa miaka 47 na mkazi wa SANYA JUU wilayani SIHA mkoani KILIMANJARO akijishughulisha na biashara kwa kuwa mtu maarufu huko SIHA.

hawa wote walikuwa washirika wakuu wa genge la MACHO MBAYA na mawasiliano baina yao kuanza, na kitu kizuri sio wageni baina yao ni vile tu walikuwa hawaaminiki sana na genge la MACHO MBAYA na kama inavyojulikana uaminifu ndo nguzo kuu ya mafanikio yoyote kwenye shughuli zinazohusisha makundi na ikitokea mmojawapo ameharibu kwa kupoteza uaminifu basi kaua kundi nzima.

Mawasiliano baina ya genge la MACHO MBAYA na washirika wao nchini TANZANIA yalikuwa chanya kwa kukubaliana kufanya kazi na bwana KANJE kufurahishwa na jinsi genge la MACHO MBAYA lilivyojipanga akajitolea kuwa mfadhili wa shughuli za ujambazi zitakazofanywa na genge hilo la WAKENYA.

Bwana KANJE alicheza na fursa haraka kwa kupimia mbali kwamba akiwekeza kiasi fulani itajizalisha maradufu na kilichobakia kikawa ni genge la MACHO MBAYA kuhamia rasmi nchini TANZANIA na kazi ianze mara moja na kuna mambo makuu mawili genge la MACHO MBAYA lilikuwa limalizie hapo nchini KENYA ndo waanze safari.

Mambo hayo yalikuwa ni upatikanaji wa paspoti feki kwaajili ya MACHO MBAYA peke yake ambaye alikuwa kwenye orodha ya watu wanaotafutwa sana kwahiyo akitumia paspoti halali inayomtambulisha wasifu wake pamoja na picha yake basi atakuwa amekwisha.

Wanakundi wenzie ilikuwa haina shida sababu sio homa kwa vyombo vya ulinzi na usalama vya KENYA na hata hawajulikani kwa wenyewe kutembelea nyota ya MACHO MBAYA ambaye ndo kiongozi wao, na jambo lingine lilikuwa ni upatikanaji wa silaha pamoja na kuzivusha kuingia nchini TANZANIA.

Hayo mambo hawezi kuyafanya akiwa nchini TANZANIA na mara moja alianza kuyashughulikia kwa kutafuta paspoti feki kutoka kwa wataalamu wa kutengeneza nyaraka feki na kitu kizuri kipindi hicho hakukuwa na paspoti za kieletroniki ambazo zimesaidia sana kupunguza paspoti feki.

Suala la paspoti lilichukua muda mfupi sana likawa limekamilika na kuwa mkononi mwake MACHO MBAYA na suala la pili ambalo ni silaha likafuata kushughulikiwa na mfadhili bwana KANJE alianza ufadhili wake kuanzia hapo maana silaha hizo ndo zitakwenda kufanya kazi nchini TANZANIA.

Kwahiyo bwana KANJE alichotakiwa kufanya kama mfadhili akafanya na mfereji wa kuchukulia silaha ulikuwa ule ule wa SOMALIA na silaha zilikuwa za kivita kwa kuwepo silaha maarufu kama AK-47 pamoja na mabomu ambayo yalikuwa ya kurusha kwa mkono [mabomu ya kiazi].

Silaha zilikuwa mzigo mzito na nyongeza ya silaha zitaongezwa huko huko nchini TANZANIA kama zitahitajika kwa kutokea upungufu wa silaha, na silaha kuvushwa kuja nchini TANZANIA mpaka wa ROMBO ulionekana kuwa salama zaidi kuliko mipaka mingine ya KENYA na TANZANIA.

ROMBO ni wilaya ya mkoa wa KILIMANJARO kwahiyo mzigo wa silaha utaingilia mkoa wa KILIMANJARO na kuelekea mkoani ARUSHA ambako ndo MACHO MBAYA na genge lake walipachagua kuwa kitovu chao yani watahangaika mikoa mbalimbali kutekeleza ujambazi wao ila mwisho wa siku ARUSHA ndo kambi yao kuu kwa kupanga michoro yao ya ujambazi.

Faida ya mkoa wa ARUSHA kuwa kitovu chao ni ikitokea mambo yakivurugika rahisi kukimbia nchini TANZANIA kuelekea nyumbani kwao KENYA tofauti na kuweka kambi mikoa kama DAR ES SALAAM, DODOMA n.k lazima iwachukue muda na kuwa faida kwa vyombo vya ulinzi na usalama kuwadhibiti kwa kuwakamata au kuwaua.

Mpokeaji mzigo wa silaha ni wale washirika wao na kazi kama hii ndo faida ya kuwepo mwenyeji inaonekana na washirika wao walivyokwenda kupokea mzigo wa silaha walishangaa sana kuona mzigo mzito na kujua kweli wanaume wanakuja vitani na TANZANIA ijiandae nao.

Jambo la silaha kukamilika salama kwa kuvushwa na kufikishwa salama mkoani ARUSHA bila kujulikana ikawa imebaki genge la MACHO MBAYA kuanza safari kuja nchini TANZANIA na tarehe iliyopangwa ilikuwa 12 juni 2007 na hapo itakuwa imepita takribani miezi mitano toka ujambazi mkubwa wa mwisho nchini KENYA kufanywa na genge la MACHO MBAYA.

KENYA na TANZANIA wote hawajui genge la MACHO MBAYA linaelekea nchini TANZANIA na msako wa MACHO MBAYA nchini KENYA ulikuwa ukiendelea ila wanashindwa kumkamata ni anajua kuwakwepa vizuri ndo maana jina lake halitafutwa kwenye orodha ya majina ya majambazi wasumbufu kuwahi kutokea nchini humo.

KENYA waliunda mpaka kikosi maalumu ambacho kilikuwa na kazi moja tu ya kumkamata hai au mfu MACHO MBAYA na walikuwa wanausalama wabobezi ila alikuwa akiwapiga chenga ya mwili wao kikosi maalumu wakipata taarifa yuko sehemu fulani na wakifika haraka wanakuta ameshaondoka zamani.

MACHO MBAYA kama majambazi wengine wanahusishwa na imani za kishirikina kuwasaidia kuwa majambazi sugu walioshindikana kwa kila wanapokaribia kukamatwa kuna hisia zinawastua ambazo zinakuwa kama kuwashwa sehemu fulani, kubanwa na haja kubwa gafla n.k

Shida ni madai haya hayawezi kuthibitishwa ni yamekaa kiimani na bahati mbaya sana serikali zetu haziamini imani za kishirikina kwahiyo kitendo cha MACHO MBAYA kushindikana kukamatwa inahesabika anawazidi akili na sio uchawi unamsaidia.

Kipindi cha toka wazo la kwenda TANZANIA linazaliwa mpaka jambo la mwisho la mzigo wa silaha kuvushwa nchini TANZANIA kulitokea vifo vya wanagenge wa MACHO MBAYA katika ile operesheni ya jeshi la polisi kupambana na majambazi nchini humo.

Watu wake MACHO MBAYA muda mwingine walikuwa wakitekeleza ujambazi wao wenyewe na walikuwa huru kufanya hivyo sababu MACHO MBAYA kadri siku zilivyokuwa zikienda kasi yake ya kutafutwa ilikuwa ikiongezeka na kumfanya kupumzika kutekelea ujambazi akishughulikia mambo muhimu kabla hajahamia nchini TANZANIA.

Watu wake walikuwa hawako kwenye orodha ya watu wanaotafutwa sana kwahiyo waliendeleza ujambazi wa hapa na pale kuchangamsha miili yao isipoe pamoja na kupata fedha za kutanua mjini maana ndo ilikuwa kazi ya fedha zao hakuna cha kuwekeza biashara yoyote wala kujenga vibanda vya kujistiri.

Kwahiyo mpaka tarehe ya kusafiri kwenda nchini TANZANIA inafika MACHO MBAYA alikuwa na watu wake wawili tu ambao wako tayari kwenda naye ugenini na walikuwa ni PETER MBUGUA a.k.a NDUN’GU aliyezaliwa mwaka 1970 na mwaka huo 2007 alikuwa na miaka 37 na MICHAEL KIMANI PETER a.k.a KIM aliyezaliwa mwaka 1967 na mwaka huo 2007 alikuwa na miaka 40.

jambazi NDUN’GU na KIM wote ni wakazi wa jijini NAIROBI na walifahamiana na jambazi MACHO MBAYA kupitia kazi zao za kihalifu na kuamua kujiunga na genge la MACHO MBAYA, jambazi KIM kabla hajawa jambazi alikuwa dereva wa malori na baadae kuamua kuachana nayo kwa kuona inamchelewesha.

Hawa mapacha watatu kutoka KENYA ndo wanakwenda kusimamisha TANZANIA kwa kutangaza vita dhidi ya mali za WATANZANIA kuwa wanazitaka kwa nguvu na ukiwa mbishi hawacheki na wewe zaidi ya kukusafirisha kwa mola wako.

Tarehe 12 juni 2007 kufika MACHO MBAYA na genge lake walianza safari kuelekea nchini TANZANIA na walipanga kupitia mpaka maarufu wa NAMANGA ambao utawaingiza moja kwa moja nchini TANZANIA katika jiji lake la zuri na la kitalii yani ARUSHA.

Jambazi MACHO MBAYA sababu ya kuwa mtu anayetafutwa sana ilimpelekea muda wote wa safari mpaka hapo mpakani NAMANGA wanafika kuvalia koti lenye kofia “hood” na miwani nyeusi huku wenzie wamevalia kawaida kwa sura zao kuwa wazi hawana hofu yoyote.

Jambazi MACHO MBAYA na wenzie kukamilisha kila linalohitajika hapo mpakani NAMANGA kupitia ofisi za uhamiaji wakakutwa freshi na rasmi wakawa wamekanyaga ardhi ya TANZANIA, na MACHO MBAYA akavua koti lake na miwani nyeusi ili apumue kidogo na wakati huo mwenyeji wao bwana mdogo CHONJO alikuwa amefika mpakani hapo kuwapokea.

Genge la MACHO MBAYA na bwana mdogo CHONJO wakasalimiana na safari kuanza ambayo ilikuwa umbali wa kilomita 109.7, kuna mwendo kidogo mpaka kufika ARUSHA MJINI na njiani walikuwa wakipiga stori mbalimbali na moja ya stori ilikuwa mwenyeji wao kuwauliza wakina MACHO MBAYA kuhusu mzigo wa silaha mbona kuna mpaka mabomu.

MACHO MBAYA hakumjibu dogo kwa kuona anauliza maswali ya kijinga wakati wenzie wamejikoki kila idara sababu wanajua wamekuja vitani na hawatacheka na ngedere yoyote mbele yao atakayekuwa kiwingu, kama mtutu utamkosa basi bomu litamtawanya vipande vipande.

MACHO MBAYA alichofanya kwa mwenyeji wake kupotezea swali lake la kijinga ni kumuuliza ameshawatafutia watoto wazuri wa KIARUSHA wa kuburudika nao siku hiyo ili wapate joto murua la kukata baridi kali maana mwezi wa sita jijini ARUSHA ni kipindi cha baridi kali mwanzo mwisho.

Mwenyeji wake alimjibu MACHO MBAYA kuwa kwa hilo wasiwaze kabisa kila kitu kiko kwenye mstari mnyoofu ni wao tu kufurahia mabinti wazuri wa ARUSHA, na walipofika salama jijini ARUSHA wakina MACHO MBAYA walitaka kwanza kufika mahali mzigo wa silaha ulipohifadhiwa wauone ndo wapelekwe mahali pa kupumzika na kupata burudani za watoto wa KIARUSHA.

Wakina MACHO MBAYA kupitishwa kwenye maficho ya silaha hapo hapo ARUSHA MJINI na kuona ziko salama kama walivyozituma sasa wakawa tayari kuelekea kupumzika huku wakisubiri kesho yake kukuche na kazi iliyowaleta nchini TANZANIA kuianza mara moja.

Mwenyeji wao akawapeleka mpaka hotelini ambako tayari alishawasiliana na wadada poa [makahaba] kutangulia hotelini hapo katika vyumba husika ili wakina MACHO MBAYA wakifika waburudike, na hotelini watakaa kwa muda wakati nyumba inatafutwa ambayo ndo itakuwa kambi yao kuu.

Hotelini ni hatari kupanga mipango yao ya ujambazi, kuhifadhi fedha zao watakazoiba pamoja na silaha zao za kazi kwani wafanyakazi wa hoteli wanaweza kuwashtukia kwa kuona kitu kisicho cha kawaida vyumbani mwao na kutoa taarifa haraka kwa vyombo vya ulinzi na usalama na kukamatwa.

Wakina MACHO MBAYA hotelini kufika wakakuta walichoahidiwa na mwenyeji wao na siku ikaisha vizuri kwao na tabia yakina MACHO MBAYA hasa kiongozi wao mwenyewe MACHO MBAYA kupenda sana wanawake itakuja kumgharimu mbeleni.

MACHO MBAYA alikuwa akijiona ni masta wa kucheza na mabinti za watu bila kumgharimu kama alivyokuwa anafanya nchini KENYA kwa mitego ya mabinti aliyojaribiwa kuwekewa na kikosi maalumu kuchomoka na kusahau kila mjanja ana wajanja wake.

Kosa moja goli moja na hicho ndo kitamfundisha kitu kizuri MACHO MBAYA na genge lake, kukucha asubuhi wakina MACHO MBAYA wakaanza kazi ambayo ilikuwa ni kuweka mikakati ya kazi yao ya ujambazi nchini TANZANIA huku mikoa lengwa ya kwanza ikiwa ARUSHA na KILIMANJARO.

Mikoa ya ARUSHA na KILIMANJARO ilichaguliwa kwanza sababu ya ukaribu wa kutorokea nchini KENYA endapo mambo yakaenda kombo, sababu itakuwa ndo mara yao ya kwanza kufanya ujambazi nchini TANZANIA kwahiyo lazima wapime maji kwa kijiti na sio mguu kuona kina chake.

Mikakati ikipangwa huku wakitegemea muongozo wa washirika wao, huku nyuma utafutwaji nyumba ulikuwa ukiendelea kwani ulianza hata kabla wakina MACHO MBAYA hawajafika nchini TANZANIA sema shida ilikuwa hakujapatikana nyumba sahihi kulingana na kazi itakayokwenda kufanyika humo ndani.

Nyumba ilitakiwa maeneo ya hadhi ya juu [ushuani] kwamba kila mtu yuko ndani kwake hakuna uswahili sijui mtoto wa jirani amekwenda kucheza kwa watu au mama amina anagonga hodi ya kuomba chumvi na karaha zingine za uswahilini, na hii yote ni kuepusha watu wa nje wasijue kiendeleacho ndani.

Sehemu zilizopendekezwa na washirika wa genge la MACHO MBAYA zilikuwa ni NJIRO na UZUNGUNI kwa huko kuaminika ni ushuani kwenyewe kila mtu kwenye geti lake hajui jirani yake anaishiji zaidi ya kupishana barabarani kwa kila mmoja akiwa kwenye usafiri wake.

Sasa nani aliyepewa kazi ya kutafuta nyumba ya kuishi wakina MACHO MBAYA…? Kuna binti mmoja aitwaye ELIZABETH ELIAS MSANZE a.k.a BELLA ambaye alizaliwa mwaka 1983 kwa kipindi hicho mwaka huo 2007 kuwa na miaka 24 ndiye ambaye alikuwa na jukumu la kutafuta nyumba watakayokaa wakina MACHO MBAYA.

ELIZABETH MSANZE naye alikuwa mshirika wa wakina MACHO MBAYA ambaye aliongezwa na washirika wa kwanza wa wakina MACHO MBAYA kwa binti huyu kutofahamika na kina MACHO MBAYA awali ila baada ya kufika nchini TANZANIA watamfahamu.

Binti huyu ndo alikuwa akizunguka na madalali kutafuta nyumba maeneo ya kishua ya UZUNGUNI na NJIRO, binti huyu akishapata nyumba atatakiwa kukodisha kwa jina feki la bibi FRANCIS URASSA ikimaanisha binti huyo ni mke wa mtu kwa mumewe kuitwa FRANCIS URASSA.

Binti ELIZABETH MSANZE atajazia kuwa mumewe FRANCIS URASSA ni mfanyabiashara wa magari na nyumba hiyo wanataka kutumia kama ofisi na kuonesha wako “serious” watalipa kodi ya miezi sita ya nyumba hiyo itakayopatikana ili kuaminisha yeye na mumewe ni wafanyabiashara wa magari.

Sasa binti ELIZABETH MSANZE ndo anahangaika na madalali kufanikisha jambo lake sababu anajua ukweli wa nyumba hiyo inakwenda kufanyiwa nini na hana shida kwa hilo sababu yeye anachoangalia ni fedha tu maisha yasogee, hawa ndo wale mabinti wadogo ambao mtu unashangaa mbona anapendeza kwa mavazi ya gharama na anakula bata lisilo kuwa na mwisho kumbe nyuma ya pazia ndo mambo kama haya.

Kisheria hapo ELIZABETH MSANZE naye ni jambazi bila kujalisha atashiriki moja kwa moja kuiba au laa na ikitokea mauaji pia naye ni muuaji bila kujalisha alishiriki mauaji hayo moja kwa moja au laa, na hizo ndo gharama za vijana kupenda maisha ya mkato endapo mambo yakaenda ndivyo sivyo ila mambo yakitulia kwenye reli ni raha tu na kuvimbia vijana wenzako ukiwa maeneo kama “KIDIMBWI”.

Siku mbili baada ya wakina MACHO MBAYA kufika nchini TANZANIA binti ELIZABETH MSANZE alishtuliwa kwa njia ya simu na dalali mmoja wa kike jijini ARUSHA aitwaye LILIAN MUSHI kuwa nyumba yenye sifa zile anazotaka imepatikana eneo la NJIRO kituoni KONTENA huku dalali akimwaga sifa kedekede kwa nyumba hiyo ili kuhakikisha mteja hachomoki maana walimuona ana hela.

Nyumba inayoongelewa na dalali MUSHI ni ghorofa moja ambayo ni mali ya bwana MAKOYE NGERERE ambaye ni mhandisi wa shirika la umeme TANZANIA yani TANESCO na hivyo karibuni alikuwa amehamishwa kikazi kutoka jijini ARUSHA na kupelekwa makao makuu ya TANESCO jijini DAR ES SALAAM.

Nyumba hiyo ilikuwa nzuri na ya kifahari, ELIZABETH MSANZE baada ya simu hiyo alijongea kwa dalali wake na wote kuelekea eneo la tukio kuona nyumba hiyo nzuri na walivyofika kwenye nyumba yenyewe wakamkuta mlinzi wa nyumba hiyo aitwaye HAMISI KIRONGA.

HAMISI KIRONGA aliwaruhusu kuona nyumba hiyo sababu alikuwa anajua inatakiwa kupangishwa na ELIZABETH MSANZE akaridhika na nyumba hiyo kwa kuwa na zile sifa ambazo wanazitaka wao kwaajili ya majambazi wao wageni wakina MACHO MBAYA.

ELIZABETH MSANZE akamwambia dalali kuwa anachukua nyumba hiyo na kutaka kujua bei yake na dalali alimwambia kwa mwezi kodi ni shilingi 450,000 na ELIZABETH MSANZE akaanza kushushana naye bei dalali mpaka kufikia shilingi 400,000 kwa mwezi na kuahidi atalipa kodi ya miezi sita.

Biashara ya nyumba ikawa imesha kwa kupatikana na kulipiwa, na mkataba rasmi wa nyumba hiyo ulisainiwa tarehe 17 juni 2007 na ndo siku ambayo kodi ilianza kuhesabiwa na majambazi wakina MACHO MBAYA kuhamia hapo siku hiyo hiyo ambayo ilikuwa jumapili huku mlinzi HAMISI KIRONGA akiambiwa huduma yake haitajiki tena hapo.

Muda wote wakina MACHO MBAYA toka wamefika nchini TANZANIA walikuwa wanapanga mikakati yao wakisubiria nyumba ipatikane ili wawe huru sasa kuanza tukio la kwanza la ujambazi wao ugenini na mikoa iliyopangwa kuanzwa kushambuliwa nao ilibaki ile ile ARUSHA na KILIMANJARO.

Mzigo wa silaha nao ukahamishwa nyumbani NJIRO hapo sababu usalama ni asilimia 100, jambazi MACHO MBAYA na genge lake wakaanza hatua ya kwanza ya ujambazi wao ambao ni kutafuta taasisi gani ya kifedha wanakwenda kuitenda na mkoa gani.

Wakina MACHO MBAYA wao hawataki ujambazi wa kitoto ule wa kuvamia majumba ya watu na kuiba mali na fedha kidogo zinazokuwepo kwenye nyumba husika, wao wanataka kwenda kuiba sehemu ambazo fedha ni za kutosha hakuna kubahatisha na sehemu hizo zinakuwa taasisi za kifedha kama mabenki, maduka ya kubadilisha fedha n.k

Huko ni uhakika sababu biashara yao ni fedha, wakina MACHO MBAYA na washirika wao wakaanza kutafuta taasisi ya kifedha katika mikoa ya ARUSHA na KILIMANJARO ambayo itakuwa na faida upande wao katika utekelezaji wa ujambazi wao wa kwanza nchini TANZANIA.

Baada ya kuzunguka huku na kule katika mikoa ya ARUSHA na KILIMANJARO na ikumbukwe mikoa hii ni majirani kwa kufuatana, waliweza kuangukia kwenye taasisi moja ya kifedha ambayo ni benki ya NMB [NATIONAL MICROFINANCE BANK] wilayani MWANGA mkoani KILIMANJARO.

Kwanini benki ya NMB wilayani MWANGA mkoani KILIMANJARO…? Kwanza ifahamike benki ya NMB wilayani MWANGA iko moja tu wilaya nzima na ipo maeneo ya MWANGA mjini karibu na barabara kuu ya mkoani ambayo inakwenda mikoa mingine.

Benki ya NMB wilayani MWANGA iko katika ghorofa ambayo ofisi za benki na makazi ya wafanyakazi wa benki yako hapo hapo yani chini ni benki juu makazi ya wafanyakazi wa benki, hapo hapo tayari ni kosa kubwa sana kwa benki au taasisi yoyote ya kifedha kufanya hivyo.

Taasisi yoyote ya kifedha ambayo biashara yake kuu ni fedha haitakiwi eneo moja kukaa na wafanyakazi ni hatari kwa usalama wa fedha katika taasisi hiyo na pia huchanganya walinzi husika wanaolinda benki hiyo na hili litakuja kujidhihirisha kupitia tukio la ujambazi wa wakina MACHO MBAYA.

Benki ya NMB wilayani MWANGA walikosea sana maana hata hao wafanyakazi wanaweza kufanya yao na kuwa hasara kubwa kwa benki ambayo ingewezekana kuzuilika, sasa kitendo cha benki na makazi ya wafanyakazi wake kuwa sehemu moja ilikuwa na faida kulingana na mchoro wa MACHO MBAYA utakavyokuwa yani mbuzi kafia kwa muuza supu.

Ukiachana na sababu kuu hiyo iliyofanya wakina MACHO MBAYA kuchagua benki ya NMB wilayani MWANGA mkoani KILIMANJARO kuna sababu zingine mbili zinatajwa ambazo ni KONSTEBO NATHANIEL MANYAMA na bibie SALOME MATEMU.

Sababu ya kwanza ambayo ni KONSTEBO NATHANIEL MANYAMA, huyu alikuwa polisi mwenye cheo cha KONSTEBO mkazi wa MONDULI mkoani ARUSHA na ameshawahi kuwa lindo katika benki ya NMB wilayani MWANGA mkoani KILIMANJARO.

KONSTEBO NATHANIEL MANYAMA anatajwa kuwa mshirika mwingine aliyeongezwa katika ujambazi huu kwa kusaidia mchoro wa tukio la ujambazi katika benki hiyo ya NMB sababu ya kuwa mzoefu na mazingira ya benki hiyo kwa kujua nje ndani usalama wa benki hiyo pamoja na njia ambazo majambazi watatumia kutorokea eneo la tukio.

Sababu KONSTEBO MANYAMA alionekana hana hatia na uhusika wa ujambazi huu kupitia mahakama basi kwa heshima yake na jeshi la polisi maana tayari alishatia doa jeshi hilo hatutamchimba ila tukiachana na mambo ya sheria na mahakama kwa kutumia mahakama zetu za vichwa vyetu basi huyu askari tungemsukumia kwenye kundi moja na wakina MACHO MBAYA.

Tunasema mawakili wake walifanya kazi kubwa na nzuri kwa kucheza vizuri na sheria, sawa tu na vile ACP ABDALLAH ZOMBE jinsi mawakili wake walivyofanya kazi kubwa na nzuri kwa kucheza vizuri na sheria mwishoe naye akaonekana hana hatia.

Sababu ya pili ambayo ni bibie SALOME MATEMU ambaye huyu ni mfanyakazi wa benki ya NMB wilayani MWANGA mwenye cheo cha meneja operesheni naye anatajwa kuwa mshirika wa ujambazi huu wa benki ya NMB MWANGA kwa kuongezwa katika washirika wa genge la MACHO MBAYA.

Meneja operesheni SALOME MATEMU ndiye kiongozi wa kuba ya kuhifadhia fedha yani funguo na ruhusa ilikuwa katika mamlaka yake na kwa mustakabali huo alikuwa akijua kuba ya NMB MWANGA ina nini kwa kiasi gani, kuba ni sehemu ambayo inahifadhi vitu vya thamani vya benki/taasisi za kifedha kama fedha, madini n.k kutoka kwa wateja wao.

Meneja operesheni SALOME MATEU anatajwa kusaidia mchoro wakina MACHO MBAYA kuhusu benki ya NMB MWANGA na sababu alikuwa akiijua nje ndani akawasaidia, ila huyu bibie MATEU ni kama KONSTEBO MANYAMA alionekana hana hatia yoyote mbele ya mahakama ila kwa mahakama ya vichwa vyetu tusingemuacha tungemsukumia huko katika kundi la kina MACHO MBAYA.

Meneja operesheni SALOME MATEU kwa heshima yake na benki aliyokuwa anafanyia kazi yani NMB ambayo tayari alishaitia doa kwa namna ushahidi ulivyokuwa ukimtafutana na uhusika wa ujambazi huu naye hatutamchimba.

Sasa sababu zote hizo zilichangia MACHO MBAYA na genge lake kuchagua benki ya NMB MWANGA kufanya tukio la kwanza la ujambazi nchini TANZANIA na kwa kuwa benki ishapatikana kilichofuata sasa ni mchoro wa ujambazi kuandaliwa ili utekelezaji kuanza mara moja.

Wakati mambo ya mchoro wa ujambazi benki ya NMB unaanza yule binti ELIZABETH MSANZE alikuwa na ndugu zake watatu ambao ni DEVOTHA ELIAS MSANZE, JULIANA ELIAS MSANZE na NTABASILE ELIAS MSANZE na wote hawa kiumri ni wakubwa zaidi ya ELIZABETH ELIAS MSANZE.

ELIZABETH MSANZE na ndugu zake hao wakawa wapenzi wa genge la MACHO MBAYA na washirika wake na hili lilikuwa kosa la kwanza upande wakina MACHO MBAYA kwa kupindisha sheria yao waliojiwekea wenyewe toka wakiwa nchini KENYA.

Wakina MACHO MBAYA sheria yao waliojiwekea wenyewe ni kutokuwa na mpenzi wa kudumu hata siku mbili tatu yani wao walikuwa wakiishi katika ule msemo wa vijana wa mjini “hit n run” na hii iliwasaidia sana kukwepa mitego ya kile kikosi maalumu cha polisi nchini KENYA.

Wakina MACHO MBAYA waligundulika udhaifu wao ni mabinti na kikosi maalumu kutumia udhaifu huo kama wataweza kuwakamata ila mpaka wanahamia nchini TANZANIA walishindwa kuwakamata kwa mtego huo ila sasa nchini TANZANIA wanakwenda kuharibu kila kitu kwa kujisahau.

Maana kwao hao ndugu mapenzi yao yatakuwa “hit n stay” na makosa yake yatakuja kuonekana mbele, na katika kosa la kwanza hilo ndani yake kuna kosa lingine dogo ambalo lilikiuka sheria walizojiwekea wao wenyewe na kosa hilo ni kufanyia mambo yao humo humo ndani ya nyumba waliyopangisha NJIRO.

Wakina MACHO MBAYA wakiwa nchini KENYA walikuwa hawafanyi hivi kwa wanawake wanaokula nao raha sababu ni hatari kwa wanawake hao kubanwa au kuwa wametumwa na polisi kuwachunguza kuwaleta vyombo vya ulinzi na usalama wanapoishi na ikumbukwe wakina MACHO MBAYA hapo nyumba waliyokodisha ndo nyumbani na makao makuu yao kwa wakati wote watakaokuwa nchini TANZANIA.

Hao ndugu wakina MASANZE wakina MACHO MBAYA walitakiwa kula nao raha nje ya nyumba ya NJIRO ili wasijue wao wanaishi wapi ingawa kwa upande wa ELIZABETH MSANZE isingewezekana sababu ndiye aliyetafuta nyumba hiyo.

Mwisho wa siku kosa kubwa la kujihusisha nao kimapenzi ndo lilikuwa la kujiepusha nalo ili kusiwepo hilo kosa dogo ndani yake la kuwakaribisha hapo nyumbani NJIRO na binti ELIZABETH wangebaki washirika tu kwa kuheshimana kama walivyokuwa wanaheshimiana na washirika wao wengine.

Waswahili wanasema “NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE”, kwahiyo wakina MACHO MBAYA wakiendelea kula burudani na hao mabinti uanzaji wa mchoro nao ulianza na walikuwa wakishuhudia na kusikia kila kitu yani wakina MACHO MBAYA walijisahau sana.

Hao ndugu mpaka silaha walikuwa wanaziona na kuzichezea kama midoli, vichwa vikaanza kusuguliwa na wakina MACHO MBAYA huku wakipata ushirikiano wa washirika wao pale wanapohitaji taarifa zaidi ili watoe mchoro wenyewe kulingana na madhaifu ya benki ya NMB MWANGA.

Baada ya siku kadhaa ambapo ilikuwa mwanzoni kabisa mwa mwezi julai 2007 mchoro mzima ulikuwa umekamilika na kubakia utekelezaji tu na ulikuwa mchoro mzuri sana ambao ulionesha kweli wakina MACHO MBAYA walikuwa wamekuja kufanya kazi nchini TANZANIA.
 
Back
Top Bottom