Majambazi Wakenya Walivyotikisa na Kuweka Historia Kanda ya Kaskazini Nchini Tanzania

Tukio la Njiro nalikumbuka vyema Maana nilikuwa miongoni mwa wananchi waliojaa kushuhudia. Ni kweli DC alikuwa Kepten Evans Balama na Mkuu wa mkoa alikuwa Ndomba ambaye baadaye akateuliwa kuwa mnadhimu wa JWTZ.
Ila siku Ile kulikuwa na weaknesses kwa vikosi vyetu hasa decisions nini kifanyike..
Hasa baada ya kufika JWTZ wao walitaka tuu kulipua nyumba na hizo rpg..
Naelewa huyu anasema hiki, huyu vile, wananchi kelele, mzazi wa binti yowe, DC, Rc... Kulikuwa na sintofahamu kidogo Maana tukio lilikuwa sio la kawaida.
Ila at the end hekima ndio ilishinda mpaka kuwatoa humo ndani wakiwa hai.

Hongera sana vyombo vya ulinzi na usalama kwa ku risk maisha kiasi kile.
Mkuu hizi kaz ni ngumu sana yan mtu ajitolee maisha yake kwa ajili ya wengnr.

Tanzania tumewah pitia vipind vigumu sanaaa.

Ila Mungu kajalia yote yalipita
 
Kitabu bora cha UJASUSI na USALAMA kiitwacho "IJUE HISTORIA" chenye kurasa 470 kinachoongelea historia za UJASUSI, UPELELEZI, SIRI ZA DUNIA, UGAIDI na UHALIFU kimeshatoka na kinapatikana kwa sh 25,000 tu.

Pia kundi la "ijuehistoria" (WhatsApp group) lipo kwa gharama ya sh 3000 kwa mwezi.

Namba za mawasiliano na malipo ni - TIGO 0679 95 93 08 (namba ya Whatsapp pia)


SEHEMU YA KWANZA

UJAMBAZI MKUBWA BENKI YA NMB KILIMANJARO

Na. COMRADE SABOUR/ G.H. MASHERETO (Ijue Historia)

Hii ni makala ya ujambazi inayoongelea moja ya ujambazi mkubwa na wa akili nyingi sana kuwahi kutokea katika ardhi ya taifa la TANZANIA na kuongelewa sana wakati wake tukio hili likiwa limetokea maana lilisimamisha taifa kwa muda na vyombo vya ulinzi na usalama kuhangaika kila kona kudili na ujambazi huu.

Ujambazi huu mkubwa na wa akili nyingi sana ulitokea mkoani KILIMANJARO wilayani MWANGA ambapo washiriki wa ujambazi huu walikuwa wanatokea mataifa mawili tofauti ambayo ni KENYA na TANZANIA na ijulikane mataifa haya ni jirani sana kwa kupakana.

Ujirani mwema na undugu wa mataifa haya ambao unajulikana umeimarishwa na waasisi wao kwa TANZANIA ni MWALIMU JULIUS NYERERE na KENYA ni bwana JOMO KENYATTA ulitumika vibaya na hawa majambazi kwa kushirikiana kupanga na kutekeleza ujambazi huu katika benki kubwa ya NMB.

Majambazi hawa walichofanya katika benki ya NMB wilayani MWANGA imebaki kuwa historia inayokumbusha kipindi cha matukio mengi ya ujambazi nchini TANZANIA ambayo yalianza mwisho mwa karne ya 20 [1990’s] kuingia karne ya 21 [2000’s].

Kiufupi kipindi cha utawala wa raisi BENJAMIN MKAPA na JAKAYA KIKWETE vitendo vya ujambazi na uhalifu kwa ujumla vilikuwa vimeshamiri sana nchini TANZANIA na viongozi hawa waliotawala vizuri TANZANIA huu udhaifu wa kushindwa kukabiliana na ujambazi ulioshamiri vipindi vyao vya utawala hawawezi kuukwepa.

Kwenye uongozi na siasa ni jambo la kawaida kwa kila utawala kuwa na mazuri na mabaya yake [uimara na udhaifu wake], sasa hawa majambazi waliokwenda kuweka historia katika ardhi ya WAPARE pale wilayani MWANGA kiongozi “mastermind” wao alikuwa ni MKENYA.

MKENYA huyu alikuwa akijulikana sana kwa jina lake la utani MACHO MBAYA [MACHO MABAYA, Kiswahili cha KIKENYA hakiko vizuri], kwa miaka ya 2000’s nchini KENYA ukisikia jambazi MACHO MBAYA na genge lake wamepiga sehemu tukio ujue haukuwa tu uwizi wa unyang’anyi kwa kutumia silaha tu bali ni vita.

MACHO MBAYA na genge lake ujambazi wao ulikuwa ni vita kutokana na kutumia silaha za kivita kama AK-47 na mabomu kitu ambacho sio cha kawaida na genge hili la MACHO MBAYA walikuwa wakifanya hivi ili wahanga wao na jeshi la polisi wawaogope kwa kuwaona kama ukoma.

MACHO MBAYA na genge lake walikuwa wanajua kuzitumia silaha ipasavyo utafikiri wamewahi kupitia jeshi lolote na kupata mafunzo, na ukiachana na uwezo mkubwa wa kutumia silaha hizo pia MACHO MBAYA yeye binfasi ni mzuri wa mapigano ya ngumi na alivyopanda juu [mrefu] ndo kunamuongezea uimara katika mapigano ya ngumi.

MACHO MBAYA kiufundi nchini KENYA alikuwa ameshindika na anatafutwa sana na vyombo vya ulinzi na usalama vya KENYA kwa kesi zake nyingi za mauaji na ujambazi maana yeye haoni shida kuua pale kunapotokea kiwingu cha kutaka kumkwamisha ujambazi wake.

Sasa baada ya kusumbua sana KENYA akahamia nchini TANZANIA na wakati huo kulikuwa na wimbi kubwa la majambazi wa KENYA kuja nchini TANZANIA kushirikiana na majambazi wazawa wa huko kutekeleza ujambazi wao katika taasisi za kifedha ambako ni uhakika kuna fedha za kutosha hakuna ubahatishaji.

Jambazi kama MACHO MBAYA na genge lake kuamua kuja TANZANIA kutekeleza matukio ya ujambazi ilikuwa habari mbaya sana na hawakuwa wamekuja kwaajili ya tukio moja la benki ya NMB bali kwa matukio mengi yani walikuja kuweka kambi ndo maana walipitisha mzigo mkubwa wa silaha na mabomu.

MACHO MBAYA na genge lake kwa ubora wao uliopelekea kushindikana nchini KENYA wakakutana na ubora wa jeshi la polisi la TANZANIA ambao ulisaidiwa na kauzembe kadogo walichoteleza wakina MACHO MBAYA na kupelekea “WAR IN ARUSHA”.

KUZALIWA KWA WAZO

Kabla ya kuelekea kuona wazo la ujambazi huu mkubwa wa benki ya NMB ulivyozaliwa kwanza kabisa tumjue MACHO MBAYA ni nani…? ambaye ndo “mastermind” wa ujambazi huu nchini TANZANIA na hata matukio mengine ya ujambazi huko nchini KENYA.

Kwanza ifahamike MACHO MBAYA kwa majina yake halisi anaitwa SAMUEL GITAU SAITOTI amezaliwa mwaka 1973 katika kaunti ya KAJIADO katika jimbo la RIFT VALLEY na wengi wanajua au kudhani MACHO MBAYA ni mzaliwa wa kaunti ya NAKURU.

Sababu inayopelekea kudhani MACHO MBAYA ni mzaliwa wa kaunti ya NAKURU ni maisha yake ya umaarufu kama jambazi hatari kuenea akiwa kaunti ya NAKURU na alipapenda sana na kuwa kitovu chake cha ujambazi yani eneo lake la kujidai akisifika na kutukuzwa kama shujaa fulani kumbe jambazi tu.

MACHO MBAYA kabila lake ni MKIKUYU halisi na kabila la WAKIKUYU ndo kabila kubwa na lenye nguvu nchini KENYA kwa kutawala nyanja mbalimbali kisiasa, kibiashara, kiuchumi, kielimu n.k na MACHO MBAYA wakati akikua katika kaunti ya KAJIADO alikuwa mtoto mtundu na mjanja sana.

MACHO MBAYA shule kwake ilikuwa kama kituo cha polisi na alikuwa akisoma ili mradi iende sababu ya kulazimishwa na wazazi/walezi wake, na akiwa kijana baada ya balehe alibadilika kutoka kuwa mtundu kwenda mdokozi/kibaka [mwizi wa vitu vidogo].

Safari yake ya kwenda kuwa jambazi hatari iianzia hapo na wakati akizidi kuwa kijana mkubwa kipindi hicho miaka ya mwanzoni mwa 1990’s nchini KENYA na barani AFRIKA kwa ujumla kulikuwa na genge hatari sana lijulikanalo kama MUNGIKI.

Genge la MUNGIKI asili yake ilikuwa ni kabila la WAKIKUYU ambalo ndo kabila la MACHO MBAYA, kwa genge hatari hili kujihusisha na kila aina ya uhalifu nchini KENYA sio uwizi, sio mauaji, sio ubakaji, sio uuzaji wa mihadarati, sio vurugu n.k yani kila takataka ya uvunjifu wa amani ilikuwa ikifanywa na genge hili la WAKIKUYU.

Vijana wengi nchini KENYA hasa WAKIKUYU ambao wameamua kujihusisha na mambo ya kihalifu walikuwa wanapenda kujiunga na kundi la MUNGIKI maana ilikuwa ndo kundi hatari linaloogopeka mpaka na serikali ya KENYA na vyombo vyake vya ulinzi na usalama.

Pia ilikuwa fahari kwa kijana kujulikana au kujitambulisha yeye ni mwanachama wa MUNGIKI na MACHO MBAYA alianzia hapa ila alikuwa wale wanakundi wa ngazi ya chini kabisa ambao ndo wanatumika na viongozi wa MUNGIKI kutekeleza uvunjifu wa amani nchini KENYA.

Kwa ngazi ya kina MACHO MBAYA walikuwa wanapewa silaha za jada kama mapanga, visu, mashoka n.k na rasmi akawa amehama nyumbani kwa kuishi kwenye makambi na maghetto ya wanachama wenzie wa MUNGIKI na utumiaji wa vilevi na mihadarati kama bangi ulianzia hapa.

Maghetto na makambi ya MUNGIKI kulikuwa na mafunzo ya mapigano na ikumbukwe MUNGIKI ilikuwa mpaka na wanachama kutoka vyombo vya ulinzi na usalama ambao walichangia sana kutisha kwa genge hili kwa kuwa wakufunzi kwa vijana wa MUNGIKI ili wawe hatari sana.

Ubora wa mapigano kwa MACHO MBAYA ulitengenezwa hapa akiwa mwanachama mdogo wa MUNGIKI na toka ajiunge genge hilo hakukaa sana yeye na vijana wengine walipangiwa kazi jijini NAIROBI [mji mkuu wa KENYA] ambako ndo kulikuwa kitovu cha genge la MUNGIKI.

Hapo jijini NAIROBI genge la MUNGIKI lilikuwa likikusanya kodi kwa wafanyabiashara, wakazi wa uswahilini, MATATUS [usafiri maarufu nchini KENYA] n.k kama vile wao ni serikali na asiyekubali kutoa hela kwa MUNGIKI basi cha mtema kuni atakipata na hana pa kwenda kulalamika maana walikuwa tishio nchini humo.

Genge la MUNGIKI walikuwa na utawala wao ndani ya utawala wa serikali ya KENYA na waliokuwa wanaumia ni wanachi sababu kodi ya serikali iko palepale kwahiyo kunalipwa kodi mara mbili na bora kodi ya serikali isilipwe kwa mlipaji kodi kufanya janja janja ila sio kodi ya MUNGIKI ambayo ni lazima na haitakiwi masihara kabisa.

Sasa MACHO MBAYA yeye jijini NAIROBI alikuwa amepangiwa kukusanya kodi kwa magari ya MATATUS akipozi kama mpigaji debe kwa kushinda kwenye vituo vikuu vya usafiri akifanya kazi ya genge lake na kipindi hicho hicho wamiliki na waendeshaji wa MATATUS walikuwa ni mamafia kwa kujihusisha na vitendo vya kihalifu.

Ndo maana leo hii ukipitia rekodi ya majambazi wakubwa na tishio katika historia ya taifa la KENYA unakuta wengi wao chimbuko lao walianzia kwenye familia kama wamiliki, madereva, makonda au wapigaji debe wa MATATUS na mfano ni jambazi hatari WACUCU n.k

MACHO MBAYA kutokana na kuwa karibu na jumuiya ya MATATUS alivutiwa na namna mamafia hao wanavyofanya uhalifu wao na baada ya hapo kila mtu anapata gawio lake huku wakiendelea na biashara ya usafiri huo tofauti naMUNGIKI jinsi ilivyokuwa ikijiendesha.

MUNGIKI waliokuwa wanafaidi ni viongozi wao wa chini wanatumika tu kuzalisha mapato kwaajili ya wakubwa zao na kubakia maskini maisha yao yote na ikitokea vurugu zozote wanatangulizwa wao kwa kukamatwa, kujeruhiwa au kuuliwa huku viongozi wanakula kuku kwa mrija.

Kwa MUNGIKI hakukuwa na usawa ila kwa MATATUS angalau kulikuwa na usawa na MACHO MBAYA akaona isiwe tabu akajihusisha na jumuiya ya MATATUS na kwa sifa zake za kimuonekano ziliwatia hamasa WANAMATATUS kumuona mali.

MUNGIKI walikuwa na utaratibu wa kuua wanachama wao wanaojitoa sababu sheria yao mtu akijiunga MUNGIKI kitakachomtenganisha na kundi hilo ni kifo na MACHO MBAYA alikuwa anajua hilo ila sheria hiyo ilikuwa ikitekelezeka kwa viongozi wa MUNGIKI hao wanachama wa chini mpaka awe msaliti na wajue ndo watamuua.

MACHO MBAYA alikuwa mwanachama wa chini hakuna anayemzingatia na akaachana na MUNGIKI kwa kujiunga na familia ya MATATUS ambapo alikabidhiwa basi na kuwa dereva na rasmi akawa mwanafamilia wa MATATUS kuweza sasa kuhusishwa na umafia wa familia hiyo ya usafiri maarufu nchini KENYA.

MACHO MBAYA alikuwa dereva na mhalifu hapo hapo na matumizi ya silaha za moto kama bunduki, mabomu alianza kujifunzia kutoka kwa familia yake mpya hiyo na pia alijifunza uwizi mkubwa zinafanyikaje huku kichwani mwake akiwa na ndoto siku aje kujitegemea kwa kuanzisha kundi lake binafsi.

MACHO MBAYA muda mfupi toka ajiunge na familia ya MATATUS alijiona kule MUNGIKI alikuwa akijichelewesha maana sasa anajua uhalifu ule ambao alikuwa akiutaka sio mambo ya vurugu kutawala sana, kusumbuana na kukusanya kodi n.k

MUNGIKI walikuwa wakifanya kila aina ya uvunjifu wa amani ila ya uwizi ilikuwa chini na matukio madogo yakulinganishwa na ukibaka sio wa kutekeleza matukio makubwa kama uwizi katika mabenki, utekaji magari, n.k ndo maana MUNGIKI walikuwa wakitegemea ukusanyaji wa kodi.

MACHO MBAYA akiwa anajifunza huku akijishughulisha na uhalifu wa maana sio wa ukibaka kulianza kutokea mzozo kati ya wamiliki na waendeshaji wa MATATUS dhidi ya MUNGIKI na kikubwa hapo ni wanafamilia wa MATATUS kuchoshwa na kodi wanazochajiwa na MUNGIKI halafu hapo hapo tena serikali nao wanawakamua.

Wanafamilia wa MATATUS wao ni mamafia sasa kwanini waendelea kuwachekea genge la MUNGIKI hata kama ni wazuri kwenye vurugu na uwingi wao, wanafamilia wa MATATUS wakasitisha kutoa chochote kwa genge la MUNGIKI na wako tayari kwa vita yoyote dhidi yao.

Mwaka 2002 vita waliyokuwa wako nayo tayari wanafamilia wa MATATUS ilianzishwa na MUNGIKI na ilikuwa hatari sana kwa kuuana, kujeruhiana na kukamatwa na polisi ambao walikuwa wakivamia kutuliza ghasia hizo sababu zilikuwa zinaathiri mpaka wananchi wa kawaida.

Vurugu hizi zilipelekea serikali ya KENYA na vyombo vyake vya ulinzi na usalama kuamka na hali ya amani ikawa chini maana operesheni kali iliendeshwa ya kukamata kwa malundo wanachama wa pande zote mbili na MACHO MBAYA akaona hali ishakuwa tete na kukimbilia kaunti ya NAKURU.

Hapo kaunti ya NAKURU alifikia mji wa NAVASHA na vurumai zilizotokea jijini NAIROBI kati ya MUNGIKI na wanafamilia wa MATATUS ilikuwa tiketi ya MACHO MBAYA kuanzisha utawala na genge lake mwenyewe kwa vijana wenzie kutokea pande zote mbili zilizokuwa zinagombana na kukimbia kama yeye kuwasajili na kuwa kiongozi wao.

Utawala wa kihalifu wa MACHO MBAYA ulianzia mwaka 2003 na aliweza kushawishi vijana wenzie kujiunga naye kutekeleza matukio ya kihalifu kwa kuachana na magenge ya wanafamilia wa MATATUS na MUNGIKI ambao wapo kwenye bifu kubwa sana.

Vijana waliokuwa tayari walimfuata MACHO MBAYA huku wengine walishindwa kushawishika naye sababu ya ugeni wake katika uongozaji wa kundi la kihalifu, MACHO MBAYA na genge lake walianza na uhalifu wa utekaji magari katika barabara kuu ya NAIVASHA-NAIROBI kujipatia fedha za kuweza kununua silaha zitakazotumika kwa ujambazi mkubwa.

Silaha za kufanyia uhalifu wao walikuwa wanazichukua kimagendo kutoka nchini SOMALIA ambako kulikuwa na migogoro na mapigano yasiyoisha toka mwaka 1991 na kupelekea uwepo wa silaha nyingi nchini humo na rahisi kwa wahalifu wa mataifa ya jirani kwenda kununua huko.

KENYA na SOMALIA ni nchi jirani na silaha huko nchini SOMALIA ni bei ya chini sana sababu zipo nyingi sana na muda mwingine wanunuzi wa silaha za kimagendo hizo wanabadilishana na vitu kama vyakula kwa silaha kutokana na hali ya njaa iliyopo nchini humo kwa WASOMALI kukosa muda wa kuzalisha chakula.

Hii sio SOMALIA tu ni mataifa yote ambayo yamegubikwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe kama BURUNDI, RWANDA, KONGO, SUDAN n.k kumekuwa na silaha bwelele na wahalifu wa mataifa jirani hutumia fursa kununua kutoka mataifa hayo kwa bei ya chini.

MACHO MBAYA soko rahisi la silaha nchini SOMALIA alilijua kupitia wanafamilia wa MATATUS kwa kujua wauzaji wa nchini SOMALIA, bei kwa kila aina ya silaha na mifereji ya kupitisha silaha hizo kutoka nchini SOMALIA kuja KENYA ambapo kulikuwa na mawakala rasmi wa kazi hiyo hupitisha silaha za wateja tofauti na wanajua ni vipi wanawapooza wanausalama na walinzi wa mpakani.

Kipindi hicho KENYA alikuwa hajaimarisha ulinzi na ukaguzi mkali mipakani mwa taifa lake na SOMALIA sababu AL-SHABAB ilikuwa haijazaliwa bado migogoro na mapambano yalikuwa hayahusishi makundi ya KIISLAMU yenye msimamo mkali kwahiyo uingizaji wa silaha ulikuwa sio mgumu kama miaka ya sasa.

MACHO MBAYA na genge lake mwaka huo huo 2003 wakiwa na silaha nzito baada ya mzigo kuwafikia kutoka nchini SOMALIA walianza utekelezaji wa ujambazi mkubwa wa pesa nyingi kwa kulenga taasisi za kifedha kama mabenki, maduka ya kubadilisha fedha n.k

Genge la MACHO MBAYA walianza na duka moja kubwa la kubadilisha fedha jijini MOMBASA liitwalo FORT JESUS na walichagua hili duka sababu ya kupatiwa taarifa kuwa linamzunguko mkubwa wa fedha kutokana na wateja wengi kubadilisha fedha zao dukani hapo.

Genge la MACHO MBAYA wakavamia duka hilo na kutekeleza ujambazi wao ambao ulifanikiwa na kuwa mwanzo mzuri kwa genge la MACHO MBAYA maana sasa wakawa na hela ya kutosha zaidi kuweza kuagiza mzigo mkubwa zaidi wa silaha na mambo mengine kama kula bata.

Kufikia mwaka 2005 genge la MACHO MBAYA lilikuwa hatari sana nchini KENYA na mtu ajulikanae MACHO MBAYA akawa midomoni mwa vyombo vya ulinzi na usalama huku wakiwa hawamjui sura yake bado ila jina lake walilisikia sana kama jambazi chipukizi hatari anayekuja kwa kasi ya 5G.

Nchini KENYA miaka hiyo ilikuwa kama TANZANIA kugubikwa na matukio makubwa ya kihalifu pamoja na majambazi sugu wenye majina yao na kwa mwaka 2005 jambazi MACHO MBAYA alikuwa akionekana kama jambazi sugu chipukizi maana kulikuwa na majambazi kama SILAS MUGENDI NJERU, GODFREY MULWA KITHEKA n.k

Na hao majambazi wakubwa waliokuwa na majina wakina SILAS MUGENDI NJERU walikuwa gerezani ila bado vitendo vya kihalifu vilikuwa vikishamiri na kuambiwa kuna jamaa mmoja anaitwa MACHO MBAYA ni hatari ndiye anayesumbua taifa la KENYA na genge lake kwa kupiga matukio ya kihalifu miji mbalimbali nchini humo.

MACHO MBAYA na genge lake kuwa hatari na tatizo jipya nchini KENYA mwaka huo huo 2005 walikwenda kuweka rekodi na kujisimika yeye na genge lake sio majambazi chipukizi tena bali majambazi sugu wanaotakiwa kuzimwa haraka na vyombo vya ulinzi na usalama nchini humo kwa usalama wa raia na mali zao.

Tukio hilo lilikuwa kwenda kuvamia gereza la EMBU GK na kutorosha wafungwa ambao ndani yake kulikuwa na vijana wake ambao walikuwa wamekamatwa na kuhifadhiwa humo na ndo hao baada ya kuhojiwa walimtaja kiongozi wao ni MACHO MBAYA na jina hilo kuanza kutamkwa sana midomoni mwa polisi wa KENYA.

Wazo la kuokoa vijana wake pamoja na wafungwa wengine gerezani EMBU GK halikuwa lake kwa yeye tayari kunyoosha mikono juu kuwa amepoteza hao vijana wake na anasajili vijana wengine kuziba mapengo yao kama vile magenge mengine ya kihalifu mwanachama akishatiwa nguvuni na vyombo vya ulinzi na usalama ndo basi hawamuhesabii tena labda aje kuachiwa kama hatafungwa kifungo cha maisha au kunyongwa.

Kwa kesi ya vijana wake MACHO MBAYA ilikuwa nitolee sababu walikuwa na mashtaka ya mauaji ya polisi na raia, wazo la kuvamia gereza lililetwa na jambazi sugu SILAS MUGENDI NJERU ambaye tarehe 22 juni 2005 na wenzie walitoroka gereza la SHIMO LA TEWA.

Wakina SILAS MUGENDI NJERU hawakutoroshwa na mtu ni wenyewe wakiwa gerezani walijipanga na kutoroka, na baada ya tukio hili jambazi sugu NJERU akataka kurudisha utawala wake wa ujambazi ila akakutana na ugumu wa genge lake kusambaratika kwa wengine kuwa magerezani na wengine wameanzisha magenge yao hawawezi tena kuwa chini yake.

Jambazi NJERU alionekana zama zake zimeshaisha baada ya kukamatwa na kufungwa gereza la SHIMO LA TEWA na sehemu ya watu wake wakina MBURU, WATHIGO, KARIUKU, n.k tayari walikuwa majambazi wa kimataifa hawashikiki.

Hao waliokuwa wanakundi wa jambazi NJERU mwaka 2004 walikuwa wametoka kufanya tukio la kihistoria nchini TANZANIA mkoani KILIMANJARO wilayani MOSHI katika benki ya NBC kwa kuiba kiasi kikubwa cha fedha katika historia ya taifa la TANZANIA ambacho kilikuwa shillingi bilioni 5.3.

Sasa majambazi wake wameshiriki katika uwizi mkubwa kama huo na wako vizuri kifedha waanze kumfikiria jambazi NJERU tena ambaye hapo alipo anatafutwa sana kwa kutoroka gerezani, ilikuwa ngumu sana kwa kuhesabika zilipendwa.

Jambazi NJERU akaona namna pekee ni kutorosha watu wake walioko magerezani kwa kuachana na hao ambao wameshaota mapembe na aliamini utawala wake utarudi sababu hao atakaowatorosha watamuona yeye kama Mungu mtu kuwaepusha na kifungo cha maisha au kunyongwa mpaka kufa kwa makosa yao ya ujambazi na mauaji.

Gereza ambalo lina watu wake lilikuwa EMBU GK na kuona hapo ndo pakuchorea mchoro kwenda kukomboa watu wake wawe huru tena na arudishe utawala wake wa ujambazi, na baada ya kulichagua gereza hilo ambalo ndo lenye majambazi wenzie wamefungwa akaona bado kuna shida moja ambayo ni hawezi mwenyewe kufanya tukio hilo kubwa ikizingatiwa na yeye ametoroka gerezani na anatafutwa sana na vyombo vya ulinzi na usalama.

Jambazi NJERU akamkumbuka jambazi MACHO MBAYA ambaye ndo alikuwa kwenye ubora wake na wanajuana kiasi fulani kwa kuweza kumshawishi washirikiane katika uvamizi huo gerezani EMBU GK na pia itakuwa fursa kwake MACHO MBAYA kutorosha vijana wake waliokamatwa na kufungwa gerezani humo.

Jambazi MACHO MBAYA kufuatwa na jambazi NJERU kuelezewa tukio hilo la uvamizi gerezani EMBU GK alikubali na kwa pamoja wakakaa chini kuandaa mchoro wa tukio hilo na uzoefu wa jambazi NJERU kukaa gerezani ulisaidia kuandaa mchoro mzuri kuhakikisha wanawakomboa majambazi wenzao.

Kila kitu kuwa sawa ikabaki kuvamia gereza la EMBU GK na mwezi agosti ndo ilikuwa utekelezaji wa mchoro wao na mashuhuda wa tukio hili wanasema ilikuwa kama wanaangalia filamu za HOLLYWOOD kumbe ndo uhalisia wenyewe na kuamini kinachoigizwa kwenye filamu za nje kinawezekana kutendeka.

Kwanza watekelezaji wakina MACHO MBAYA walikuwa na silaha za kutosha pamoja na mabomu kuhakikisha wanachopeleka gerezani EMBU GK ni vita kwa kujizungusha mikanda ya risasi ili wawe wanamimina tu na katika mchoro wao walishajua wanakamata wapi kuhakikisha gereza la EMBU GK linakuwa chini yao.

Grereza la EMBU GK ni kama magereza mengine duniani kwa askari magereza wanaoshika silaha za moto wanakuwa wale wa lango kuu la kuingilia gerezani pamoja na wale wa mnarani ila askari magereza wengine wanakuwa na silaha za jadi kama rungu, manati n.k ambazo hutumia kutuliza ghasia za wafungwa pale kunapotokea vurumai gerezani.

Ni sawa kuwa hivyo sababu ya mazingira ya gerezani kwa wafungwa kotukuwa na hatarishi yoyote kufanya askari magereza wote kutembea na silaha za moto na hiyo hali wakina MACHO MBAYA walitembea nayo wakijua nani anakuwa na silaha za moto kuweza kupambana naye kwanza na pia kuwahi kukimbilia ghala la silaha ili askari magereza wasikimbile kwenda kuchukua silaha .

Askari magereza wengi kutoshika silaha za moto haimaanishi hakuna silaha za moto za kutosha magerezani, na ikitokea kuna tukio kubwa limetokea gerezani linalohitaji silaha za moto kushikwa na askari wote basi haraka huelekee kwenye ghala lao la silaha ambako wanapewa silaha za moto hizo na huko ndo wakina MACHO MBAYA walipanga kupawahi kukamatwa wakishazama gerezani ili kujihakikishia hawapati upinzani wa ziada.

Siku ya tukio wakina MACHO MBAYA wakiwa na silaha wakafika gerezani EMBU GK wakiwa kamili na kufika getini ambako lazima ukaguzi ufanyike wakashuka na mitutu yao na kuanza kumimina kusafisha njia ili wazame gerezani ndani.

Wakina MACHO MBAYA walikuja kibabe hakuna stori wala kuchekeana ni wanamimina tu na polisi magereza mpaka wenye silaha walitupa na kukimbia kusikojulikana kwa wengine kujifungia majumbani mwao, wengine kuparamia ukuta na kutoroka n.k

Wakina MACHO MBAYA waliwasawazisha na sababu lilikuwa tukio lisilotegemewa kwa askari magereza ni walikuwa kama wamechanganyikiwa na ghala la silaha kama mchoro wao ulivyosema lilidhibitiwa na askari magereza aliyekuwa zamu ghalani hapo aliuliwa.

Wakina MACHO MBAYA hawakuhangaika na askari magereza waliokuwa wakikimbia kuokoa maisha yao sababu sio lengo lao, wenyewe walielekea moja kwa moja kwenye vyumba vya magereza kuwafungulia majambazi wenzao na wafungwa wengine waliobahatika.

Wafungwa waliokombolewa walikabidhiwa silaha hapo hapo kwaajili ya kujihami na wakateka magari ya askari magereza ili kuwapakia wenzao na kuondoka eneo la tukio wakiwa wameacha vifo vya watu wanne huku mmoja wao akiwa jambazi mwenzao waliyezama naye ndani.

Tukio hili lilikuwa aibu kwa taifa la KENYA na kuonesha majambazi wamewashindwa mpaka wanakuja kuwaokoa wenzao gerezani humo na mbaya zaidi matukio hayo ya wafungwa kutoroka mikononi mwa jeshi la magereza kwa kutoroka wenyewe au kutoroshwa na wenzao yalikuwa yamefuatana toka mwaka 2004 mpaka mwaka huo 2005 ila hakuna mabadiliko kwa vyombo vya ulinzi na usalama kuzuia matukio hayo ya aibu.

Mwaka 2004 kulitokea matukio mawili ya utorokaji wafungwa ambayo yalikuwa ya gereza la NAVASHA ambalo linahesabika ni gereza lenye ulinzi mkali zaidi ila wafungwa wapatao 28 walitoroka tena wale walioshindikana ambao ingekuwa hiari yao KENYA basi wangewaua ili roho zao zipumzike kuwa wasumbufu wao hawapo tena duniani.

Tukio la pili lilikuwa utoroshwaji wa wafungwa 29 wakiwa mahabusu ndogo ya mahakama ya MERU wakisubiria kesi zao kusikilizwa na wale wale wanaotoroshwa ni majambazi na wauaji ambao hawana la kupoteza sababu wanajua hata wakibaki mikononi mwa mamlaka za magereza vifungo vyao ni maisha jela au kunyongwa mpaka wafe.

Kwahiyo mwaka 2004 na 2005 nchini KENYA kuachana na matukio ya ujambazi yaliyokuwa yanaendelea pia mchezo wa wafungwa kutoroka au kutoroshwa ulikuwepo na habari tena ya raia wao kutekeleza uwizi wa kihistoria nchini TANZANIA pale benki ya NBC ulizidi kuwachanganya kuona wao sasa wamegeuka chuo cha ujambazi AFRIKA MASHARIKI NA KATI.

Sifa hiyo ya KENYA kuwa chuo cha ujambazi AFRIKA MASHARIKI NA KATI ilikuwa ya kweli maana sio TANZANIA tu hata UGANDA, KONGO, MSUMBIJI n.k kote huko wanalia na majambazi wa KENYA kuja kushirikiana na majambazi wa mataifa yao kutekeleza ujambazi mkubwa.

Hapo mwaka 2005 gereza la EMBU GK limeshavunjwa na kutoroshwa wafungwa miezi miwili mbele wale majambazi wake wa zamani NJERU ambao walihusika na ujambazi wa bilioni 5.3 NBC MOSHI TANZANIA walikwenda nchini MSUMBIJI kwaajili ya kuumiza na huko tena yani hawapoi wala kuridhika.

Hii tabia ya majambazi wa KENYA kutorosha wenzao magerezani au mahakamani walijaribu kuleta TANZANIA kuokoa majambazi WAKENYA wenzao kupitia vyoo vya mahakama wakidhani ni rahisi kama ilivyokuwa kwao kwa kusahau au kutojua vyombo vya ulinzi na usalama vya TANZANIA ni vinara wa ujasusi.

Vyombo vya ulinzi na usalama vya TANZANIA vilitoa funzo jinsi ya kudili na majambazi wanaotaka kujaribu visivyojaribika maana kitendo cha uwokozi wa wafungwa sugu walioshindikana ni hatari sana kwa usalama wa raia na mali zao, pia ni aibu kubwa sana isiyoelezeka ambayo kwa nchi zilizoendelea lazima viongozi wahusika watajiwashibisha wenyewe kupunguza aibu hiyo.

Kwa taifa la KENYA wahusika walikaa kimya kama hakujatokea jambo huku nguvu kubwa ikitumika kupoozesha tukio hilo la uvamizi gerezazi EMBU GK na KENYA walichofanya ndo mataifa mengi ya AFRIKA hufanya kwa kutotaka kuwajibika na badala yake huminya vyombo vya habari visieleze ukweli jamii ni kilitokea kwa undani na wapi uzembe ulifanyika.

Jambazi NJERU na MACHO MBAYA jambo lao lilitiki na kila mmoja aliendelea na mambo yake na watorokaji wake huku vyombo vya ulinzi na usalama vya KENYA vikiwa vimechachamaa kusaka wavamizi na watorokaji gerezani huku wakiwasihi wafungwa waliotoroka wajisalimishe wenyewe kabla nguvu kubwa haijatumika na kujitengenezea kesi nyingine mpya.

Kwenye utoroshaji wa wafungwa kuna wafungwa ambao hawakuwa kwenye orodha ya jambazi NJERU na MACHO MBAYA kutakiwa kutoroka, ni wenyewe walitumia nafasi ya sintofahamu iliyotokea gerezani baada ya uvamizi kutoroka kusikojulikana na hawakuangana na timu ya majambazi waliokuja kuvamia gereza la EMBU GK na ndo hao walikuwa wakishauriwa kujisalimisha ili kuwapunguzia kazi vyombo vya ulinzi na usalama wabaki kudili na masugu.

Vyombo vya ulinzi na usalama kwa tukio hili la uvamizi wa gereza la EMBU GK liliweza kumjua jambazi MACHO MBAYA vizuri mpaka muonekano wake na kuingizwa kwenye orodha ya watu wanaohitajika sana, na jeshi la polisi walikuwa wametangaza vita dhidi yake.

MACHO MBAYA kujua amewekwa kwenye orodha ya watu wanaohitajika sana hakujali hilo aliendelea na matukio yake ya ujambazi na pia aliona fahari kupata umaarufu hasi huo, na matukio yake mengine makubwa na maarufu aliyoyaongoza ni mwaka 2006 alifanya ujambazi jijini MOMBASA na kuua askari wawili.

Tukio hili la MOMBASA lilisikitisha na kukasirisha sana jeshi la polisi kwa kupoteza nguvu kazi yao kwa mtu hatari wanayehangaika kumtafuta usiku na mchana nchini humo, na MACHO MBAYA na genge lake walikuwa wanafanya kama kulipiza kisasi kutokana na polisi kuendesha operesheni ya kuua majambazi sugu yani hata wakiwa kwenye nafasi nzuri ya kuwakamata au kusalimu amri ni wanawaua.

Kipindi hicho KENYA ilikuwa ikisikika majambazi sugu yaliyoshindikana yameuwawa na sio kukamatwa hai na kupelekwa mahakamani, tukio lingine kubwa na maarufu MACHO MBAYA na genge lake walitekeleza mjini NJORO kaunti ya NAKURU tarehe 4 januari 2007.

Tukio lingine kubwa na maarufu zaidi ambalo lilikuwa la mwisho kwa MACHO MBAYA na genge lake nchini KENYA lilikuwa jijini MOMBASA katika benki ya HABIB tarehe 17 januari 2007 na ndo tukio la kihistoria kwa genge la MACHO MBAYA nchini KENYA.

Kihistoria kwa tukio hili, ni tukio la ujambazi ambalo genge la MACHO MBAYA waliiba fedha nyingi ambazo zilikuwa shillingi za kitanzania zaidi ya milioni 700 kwa kutowahi kuiba fedha nyingi kwa tukio moja toka kuanzisha utawala wake wa ujambazi mwaka 2003.

Tukio hili la ujambazi ndo tukio pekee kwa genge la MACHO MBAYA kutumia akili nyingi kuliko nguvu maana walikuwa na silaha ila hawakuzitumia na kuacha vyombo vya ulinzi na usalama kushindwa kung’amua akili kubwa iliyotumika na genge lake.

Tukio hili jambazi MACHO MBAYA alishirikiana na wafanyakazi ndani ya benki hiyo ambao ndo walimtaarifu tarehe 17 januari 2007 kuna fedha nyingi zinaletwa ndani ya benki hiyo jioni kabla ya benki kufungwa na wao wavizie muda huo kuondoka na mzigo mkubwa huo wa fedha.

Siku na muda kufika genge la MACHO MBAYA walifika eneo la tukio na wafanyakazi wa benki waliokula nao dili wakazima mfumo wa kamera ili tukio lisirekodiwe na muda mchache kabla ya benki kufungwa majambazi wawili wakaingia benki wakivizia kuwa wa mwisho ambapo benki huwa inafunga mlango kwa mteja mwingine yoyote asiingie ndani kwa wale wateja waliopo ndani ndo watahudumiwa wa mwisho na benki kwa siku hiyo itafungwa.

Walinzi wako nje hawajui kiendeleacho ndani na wanajua muda wa wateja kuruhusiwa kuingia benki umeisha wakawa hawana presha ya ulinzi na hali ya ulinzi mkali ikasizi huku wakisubiria kwa hamu gari la kubadilisha zamu kupita ili waondoke na wenzao wengine waingie lindo.

Sasa wakati majambazi wawili wako ndani huku nje majambazi wengine wawili kwa msaada wa wafanyakazi wa benki waliwachorea njia rahisi ya kuingilia mlango wa siri ambao unajulikana na benki ya HABIB pekee, na mlango huo unawapeleka kweye ushushaji wa fedha zilizoletwa ndani ya benki na huko kunaaminika usalama ni mkubwa sana kwahiyo hakuhitaji walinzi na mitutu yao.

Majambazi kufika kwenye ushushwaji wa fedha wakawadhibiti wahusika kimya kimya na kuchukua mzigo kiulaini na kuelekea eneo la kuhudumia wateja ambako waliwakuta wenzao wameshawaweka chini ya ulinzi watu wote waliobakia nao na kutoka wote kama wateja waliomaliza kupata huduma yao ndani na walinzi hawakuwahisi vibaya sababu wao tayari wanafikiria kuondoka majumbani kwao wakapumzike.

Tukio la ujambazi linakuja kushtukiwa tayari wakina MACHO MBAYA wameshapotea eneo la tukio bila ghasia yoyote na baadae uchunguzi kufanyika ndo vyombo vya ulinzi na usalama vikagundua genge la MACHO MBAYA limehusika na ujambazi huo kwa kushirikiana na wafanyakazi wa benki wasio waaminifu.

Jambazi MACHO MBAYA na genge lake baada ya kujulikana wamehusika tena na ujambazi mkubwa huo nguvu zaidi ziliongezwa na vyombo vya ulinzi na usalama vya KENYA kupambana na genge hilo na baadhi ya vijana wake MACHO MBAYA waliuliwa na kukamatwa maana msako ulikuw hatari sana.

Huku mlengwa mkuu hapo akiwa jambazi MACHO MBAYA ambaye ndo vyombo vya ulinzi na usalama vya KENYA vilikuwa vinamtamani sana wagawane mwili wake kutokana na jinsi alivyowatesa na kuwasumbua na matukio yake ya ujambazi.

MACHO MBAYA na genge lake ambao alibakia nao walikuwa wanahama miji leo NAIROBI, kesho KISERIAN, kesho kutwa MOMBASA n.k, ni hawatulii sehemu moja kuhofia kukamatwa au kuuliwa na wakati MACHO MBAYA na wenzie wanahama hama hivyo vichwani mwao kukazaliwa wazo kwanini wasihamishe harakati zao za ujambazi nchi jirani ambayo ni TANZANIA.

Pia matokeo mazuri ya matukio ya ujambazi yaliyokuwa yanafanywa na majambazi wenzao WAKENYA huko nchini TANZANIA kwa kushirikiana na wazawa wa huko walikuwa wakiyasikia sana yakitekelezwa na kufanikiwa katika mikoa ya ARUSHA, KILIMANJARO na DAR ES SALAAM, sasa wakaona kwanini na wao wasiwe sehemu ya historia hiyo ya majambazi WAKENYA kutekeleza na kufanikiwa matukio yao ya ujambazi nchini TANZANIA .

Wao wakina MACHO MBAYA walijua wakihamia huko watakuwa kama wamezaliwa upya sababu hawana rekodi yoyote ya ujambazi nchini TANZANIA wala kutafutwa na vyombo vya ulinzi na usalama vya TANZANIA, na hapa kuzaliwa wazo la kuhamia nchini TANZANIA ndo mwanzo wa kuzaliwa wazo la ujambazi mkubwa benki ya NMB wilayani MWANGA mkoani KILIMANJARO.

Wazo la kuhamia nchini TANZANIA limezaliwa ila kukubaliana kwa genge la MACHO MBAYA ilikuwa bado na nani atakuwa mwenyeji wao nchini TANZANIA ni moja ya swali gumu sana kwao maana majambazi wote wa KENYA wanaokuja kutekeleza matukio yao ya ujambazi nchini TANZANIA au mataifa mengine jirani lazima wawe na wenyeji.

Sio rahisi wao wenyewe waamke na kuhamia nchini TANZANIA au nchi nyingine na kujiongoza kutekeleza ujambazi sababu wanakuwa wageni na muda wa kukaa na kuzoe mazingira ili wawe wenyeji hawana sababu ya haraka kutaka kufanya matukio yao ya ujambazi au kuhofia kuhisiwa vibaya na vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi husika waliyokwenda.

Sababu bado genge la MACHO MBAYA hawajakubaliana kwahiyo swali gumu hilo la mwenyeji wao nchini TANZANIA kulipuuzia kwanza mpaka wazo lipitishwe na wote, genge la MACHO MBAYA wakakaa kikao kujadili wazo lililozaliwa kwa kuangalia faida na hasara za kuhamisha harakati zao za ujambazi nchini TANZANIA.

Pia kuangalia nchi mbadala kama TANZANIA itakuwa na hasara nyingi upande wao na kikao kizito kukaliwa na majadaliano ya hapa na pale kwa kila mwanagenge wa MACHO MBAYA kutoa uzoefu wake juu ya taifa la TANZANIA kwa namna anavyolijua basi mwishoe wazo likapitishwa kwa wote watahamia nchini TANZANIA kuwaletea vita maana ujambazi wao ni kama vita afe kipa afe beki
Na serikali yetu ipo tu, sie walalahoi tukiiba mihogo tunakamatwa ila majambazi wanaachiliwa tu wakipeta.
 
Back
Top Bottom