Majambazi wajeruhi na kupora Ngara

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,395
Majambazi wameteka eneo la mpaka wa Tanzania na Rwanda kijiji cha Benako Wilaya ya Ngara wamejeruhi mmoja na kupora fedha kwenye maduka.

Chanzo: ITV

==========

Michango ya Wachangiaji wengine....

Si kweli kwamba Majambazi wameteka Kijiji, Wala si kweli kwamba Majambazi walipambana na vyombo vya Usalama.

Usahihi ni;

Benaco ni Centre ya Biashara iliyopo Kijiji cha Kasulo Kata Kasulo baada ya kugawanywa. Zamani ilukuwa ya Rusumo Wilaya ya Ngara Mkoani Kagera. Majambazi Waliovamia walikua Wawili wenye Bunduki. Walivamia Kibanda cha M Pesa cha Mfanyabiashara aitwaye Niko na kufanikiwa Kupora Pesa za wateja waliokuwepo na Mfanya biashara mwenyewe.

Walijeruhi Mtu Mmoja aliyejaribu kukimbia. Dakika kumi Baada ya Majambazi kuondoka, Ndipo Polisi walifika na kuanza kufyatua risaisi Hewani. KUtokea sehemu ya tukio hadi kituo cha Polisi ni umbali wa KM 1 tu, lakini Polisi walichelewa. Majambazi walitumia kama dakika 10 tu wakaondoka.

Pesa iliyoibiwa haijafahamika kwani alikuwa bado hajafunga Mahesabu. Ila Mteja mmoja mwenyeji wa Rusumo alikua katoa Mil 1 ambayo Majambazi waliondoka nayo.
 
Tanzania bana Askari wanakaa Tu badala ya kuwaweka wakae Doria maeneo hatari Rwanda tembea hata saa 8 ucku Doria IPO ya Kutosha
 
Watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wameteka kijiji cha benako wilayani ngara mkoani kagera na kupora fedha kwa zaidi ya masaa 3.

Taarifa iliokuja kama breaking news kupitia kituo cha ITV kinasema kuwa kuwa majambazi hao wameteka kijiji huku wakiwa na silaha za kivita na kuzunguka kijiji kizima ikiwepo kituo cha polisi kilichopo hapo hapo. kijiji hicho ambacho kina njia tatu za kuingia kilizingirwa na majambazi hao.

Polisi wanaelezwa kuchelewa kufika eneo la tukio ambalo limefanyika usiku wa kuamkia leo na kupelekea mashambulizi kudumu kwa masaa 3. ikumbukwe kuwa kijiji hicho kipo karibu na mpaka na rwanda na Tanzania ambapo magari makubwa ya mizigo na biashara mbalimbali zinafanyika.

Mpaka sasa hakuna taharifa yoyote ya kifo japo wapo watu walio jeruhiwa na tukio hilo,,, mpaka sasa vyombo vya usalama ikiwemo jeshi la wananchi wa Tanzania, polisi, usalama wa Taifa na uhamiaji wamejaa eneo la tukio,

Taarifa za awali hakuna jambazi yeyote alie kamatwa mpaka sasa,, pia kituo cha polisi cha eneo hilo kilizingirwa na majambazi hao na polisi kutegemea kutoka wilayani.

Waandishi wa habari wamezuiwa kukaribia eneo hilo la karibu kwani kuna msako wa hali ya juu.

SOURCE; ITV BREAKING NEWS
 
56b9f36010376f032c591b1a5389918d.jpg
 
unaambiwa ukitoka tu unarushiwa grenade mbili , mtu ana silaha ya kivita na wanatembea nyumba hadi nyumba ssa uyo polisi na kiSMG atafanya nini uku washikaji wamebeba rocket mgongoni
 
Watu wanaozaniwa kuwa majambazi wenye siraha wameteka kijiji cha Benako, wilayani Ngara, mkoa wa Kagera kwa takriban saa tatu leo, na kupora fedha kwa wanakijiji na kujeruhi wengne kwa risasi.
source; ITV breaking news.
 
Polis walikua wap?? Masaa matatu du!! Poor my country
kaka hata ungekua wewe ni polisi usingeenda kwa sababu jamaa walikua na grenade za kutosha mifukoni na ukitoa pua tu wanakurushia ufe nalo, hata miki nisingeenda hata iweje
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom