simba45 mkali
JF-Expert Member
- Oct 15, 2012
- 1,980
- 1,879
Mkuu point yako ya mwisho ndio kiini cha tatizo ata mwigulu nchemba hivi karibuni alishawahi kutoa kauli kama hiyo na kushauri polisi wasitumie nguvu nyingi katika kupambana na mambo yasiokuwa na umuhimu watumie nguvu nyingi kupambana na majambazi hapo wananchi watawaelewa. Ukweli lazima usemwe ili kurekebisha palipo na madhaifu turekebishe na kusonga mbele. Uchelewi kuitwa mchochezi wa kuvuruga amani kama utakosoa pale panapowagusa wale miungu watu.Kwa hilo Tanzania tukijifunza Rwanda sio mbaya. Mfano Kigali mjini ni vigumu sana kufanya uhalifu na kukimbia zaidi ya meter 50 kabla hujakamatwa ukiwa hai au maiti. Wao jukumu la kulinda usalama ndani ya nchi linafanywa ni vikosi vyote vya ulinzi na usalama, (Army, Police and Local defence). Tatizo letu tumewaachia Police pekeake ambao ni wachache, hawana uwezo na vifaa vya kutosha kwa ajili ya kuzuia uhalifu. Bahati mbaya sana nguvu kubwa imeelekezwa katika kupambana na wanasiasa.