kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 266
WATU wanaoaminika kuwa ni majambazi jijini Dar es Salaam, wamemuua kwa kumpiga risasi, mmoja kati ya watu wawili waliowavamia.
Tukio hilo la aina yake lilitokea juzi saa 3:30 usiku katika maeneo ya makutano ya Babara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na ile ya Sam Nujoma (Ubungo), baada ya majambazi hao kuvamia gari aina ya Mark II.
Gari hilo lililokuwa likiendeshwa na Pascal Wiliam wa Kiwanda cha MM, lilikuwa linatokea Mwenge kuelekea Mbezi ya Kimara.
Katika tukio hilo, dereva Wiliam alikufa katika eneo la tukio baada ya kupigwa risasi kichwani na kifuani wakati mtu mwingine alipigwa risasi mbili sehemu ya mbavu.
Habari ambazo gazeti hili ilizipata jana zilisema gari hilo lilikuwa linampeleka Mbezi mfanyabiashara mmoja wa eneo hilo, ambaye inasemekana kuwa katika tukio hilo alinusurika baada ya kujificha chini ya kiti cha gari.
Habari zilisema hata hivyo majambazi walimpiga risasi mbili mgeni wa mfanyabiashara huyo wa kike.
Kwa mujibu wa habari hiyo,majeruhi huyo sasa amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kwa matibabu.
Mwili wa marehemu Wiliam umesafirishwa kwenda Chalinze Msewe, kwa mazishi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Charles Kalinga alithibitisha habari kuhusu tukio hilo, lakini alisita hakulizungumzia kwa kina kwa maelezo kuwa taarifa zaidi ziko Kituo cha Polisi Urafiki.
Tukio hilo la aina yake lilitokea juzi saa 3:30 usiku katika maeneo ya makutano ya Babara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na ile ya Sam Nujoma (Ubungo), baada ya majambazi hao kuvamia gari aina ya Mark II.
Gari hilo lililokuwa likiendeshwa na Pascal Wiliam wa Kiwanda cha MM, lilikuwa linatokea Mwenge kuelekea Mbezi ya Kimara.
Katika tukio hilo, dereva Wiliam alikufa katika eneo la tukio baada ya kupigwa risasi kichwani na kifuani wakati mtu mwingine alipigwa risasi mbili sehemu ya mbavu.
Habari ambazo gazeti hili ilizipata jana zilisema gari hilo lilikuwa linampeleka Mbezi mfanyabiashara mmoja wa eneo hilo, ambaye inasemekana kuwa katika tukio hilo alinusurika baada ya kujificha chini ya kiti cha gari.
Habari zilisema hata hivyo majambazi walimpiga risasi mbili mgeni wa mfanyabiashara huyo wa kike.
Kwa mujibu wa habari hiyo,majeruhi huyo sasa amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kwa matibabu.
Mwili wa marehemu Wiliam umesafirishwa kwenda Chalinze Msewe, kwa mazishi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Charles Kalinga alithibitisha habari kuhusu tukio hilo, lakini alisita hakulizungumzia kwa kina kwa maelezo kuwa taarifa zaidi ziko Kituo cha Polisi Urafiki.