Majaliwa: Kumejitokeza tabia ya Watu kutumia vibaya Uhuru wa kutoa Mawazo kwenye Mitandao

Yaani hawa viongozi wanataka kufanya uhuru wa kujieleza kuwa ni dhambi. Kana kwamba wao wenyewe tu ndo wenye haki ya kusema kuhusu mambo yanayoendelea nchini. Wakae wakitambua kuwa kwasasa teknolojia haiepukiki, wamepambana nayo ilikuzuia watu wasijieleze ila mpaka sasa bila bila. Waelekeze nguvu zao kwenye kutumikia wananchi na kutatua shida zao, wala hawatasikia 'wakisemwa vibaya'.

Teknolojia imeleta usawa na kumruhusu mwananchi wakawaida kutoa maoni kuhusu mambo yanayoendelea nchini, na akasikia, kwahiyo teknolojia inabidi ilindwe na sio kuanza kupambana nayo. Kweli Tanzania kuna ombwe la uongozi. Tuna safari ndefu sana.
 
Mbona sasa hamtaki Mkiti wetu wa kudumu akosolewe kama mnajua hilo? Maana akiguswa huyo lazima mporomoshe matusi ya nguoni
Mpenda haki ni rafiki ya mpenda haki na hawezi kuwa rafiki na asiyeamiki katika haki,tofauti iko hapo.
 
Mpenda haki ni rafiki ya mpenda haki na hawezi kuwa rafiki na asiyeamiki katika haki,tofauti iko hapo.
Kwa mtazamo wangu siasa za TZ hazijawahi kuwa na uadui mkubwa sanaa, Ila hii miaka 5 ya jamaa ilikuwa na ukakasi sana, and bahati mbaya kuna watu walinogewa na ile miaka 5, ndiyo hao wanataka Mother aende njia hiyo, but hadi muda huu Mother kaonesha ukomavu kwenye mambo kadhaa, nafikiri hata zile kelele za anaweza or hawezi kwa sasa hazipo tena! Tumpe kamuda kidogo
 
Ndugu sowey ni mmoja wa unaoamini katika ubabe na uvunjifu wa Katiba,kiasi cha kuugeuza uhuru wa maoni kuwa ni hatia kwakuwa ni wapenda maovu na hamtaki kuambiwa mnapo kosea.
Hawa ndiyo wale walikuwa brain washed na jamaa, sijawahi kumkubali jamaa, na sitokuja mkubali kamwee!!
 
Kwa mtazamo wangu siasa za TZ hazijawahi kuwa na uadui mkubwa sanaa, Ila hii miaka 5 ya jamaa ilikuwa na ukakasi sana, and bahati mbaya kuna watu walinogewa na ile miaka 5, ndiyo hao wanataka Mother aende njia hiyo, but hadi muda huu Mother kaonesha ukomavu kwenye mambo kadhaa, nafikiri hata zile kelele za anaweza or hawezi kwa sasa hazipo tena! Tumpe kamuda kidogo
Shida iko hivi ,viwango vya unafiki katika taifa hili ni vya juu mno. Hasa kwa wale wanufaikao na maovu wafanyayo.
 

Majaliwa amesema "Hivi karibuni kumejitokeza tabia ya baadhi ya watu kutumia vibaya haki ya uhuru wa mawazo. Matumizi mabaya ya mitandao yamesababisha kusambazwa kwa taarifa za upotoshaji na wakati mwingine kudhalilisha Watu, vikundi ama Viongozi"
Hakuna jambo lililomwondolea heshima Majaliwa kama ile kauli ya kusema Magufuli anachapa kazi, huku akijua Magufuli anapambana na kifo wakati akiyasema hayo!
 
..wanasoma mijadala kwenye ma space na club house Kama za kina Maria sarungi zinawauma...wanaona mijadala ya kina kule ni tishio kwao...maana inahusisha vijana wasomi wa vyuo vikuu ambao hawana pa kusemea issue za nchi ..sasa wanataka kuanza kuidhibiti..maana kina lissu wanatoa madini adimu kule club house..
 
Ndugu sowey ni mmoja wa unaoamini katika ubabe na uvunjifu wa Katiba,kiasi cha kuugeuza uhuru wa maoni kuwa ni hatia kwakuwa ni wapenda maovu na hamtaki kuambiwa mnapo kosea.
Si kweli mkuu,Mimi ni moja ya watu wanaoamini katika utawala wa Sheria,
 
Mitandao ya kijamii kuwa jukwaa la kutolea maoni kwa Sasa ni Jambo halikwepeki Mana hata yeye ndo anaitmia. Muhimu ajue Kuna mahalo Kuna ombwe linalopelekea hayo malalamiko yake
Absolutely !! Hoja hujibiwa kwa hoja unless otherwise kuwe kuna upotoshaji.
 
Back
Top Bottom